Jinsi nilivyotapeliwa na mtu niliyedhani ni mhitaji kumbe ni tapeli

Jinsi nilivyotapeliwa na mtu niliyedhani ni mhitaji kumbe ni tapeli

at leas
Umenikumbusha mbali sana!!mwaka jana kama mwez wa pili hv!!Mafuriko yalipiga sana pande zetu!!ikatokea mkulima mmoja mhamiaji tena ngosha ana wake wawili na amebomokewa nyumba hz za udongo !!akawa amepata hifadhi kwa mtu tena chumba kimoja akadai hakitoshi ana wake wawili na watoto karibu sita!nikaamua kumpa akae nyumba yangu ya vyumba viwili na sebule!!!sasa akanipigisha stori za biashara za samaki tukafikia mwafaka tufanye kazi sasa nikatoa mtaji na yeye akawa anabanika samaki!!samaki walipokauka tu!akasema soko zuri lipo kahama !akaenda kuwauza!!alipopata hela akaitumia hela familia yke kimya kimya na wakatoroka hadi leo sijawaona tena!!!!LAKINI CHA AJABU MAISHA YANGU YA KIFEDHA YALIBADILIKA SANA KUANZIA PALE!YAANI HADI LEO FAMILIA YANGU INAINGIZA PESA NYINGI AMBAZO HATA MWANZO NILIKUWA ZISIPATI!!HADI NASHANGAA HADI LEO AISEEH!!!
JAMAA ALIKUWA ANATIA HURUMA HUKU AKIWA NA WATOTO WADOGO CHINI YA MIAKA MIWILI NA WALIKUWA WANALALA CHINI TENA KUMELOWA MAJI!!LAKINI NILIWA NYUMBA YENYE KITANDA NA KILA KITU!!!
NADHANI MUNGU ALITUBARIKI KWASABB YA WALE WATOTO!!!
UKITAKA KUWA TAJIRI JIFUNZE KUTOA TU HASA PALE UNAPOKUWA NA AMANI MOYON.I MWAKO!HUWEZ JUA KWANN ANAKUDANGANYA UJUE ANA SHIDA KUBWA!!!
NIKUTIE MOYO SANA MAN!!WE ENDELEA TU!!!
at least I hear something positive maana kusaidiaga matapeli siwez
 
Pole sana, watu hawa ndio husababisha hadi wale wenye shida kweli washindwe kusaidiwa, maana mtu akikuleza shida yake unaona kama ni utapeli mtupu..
 
Umenikumbusha miezi miwili iliyopita nikiwa pale studio nasubiri daladala niende kariakoo akaja kaka mmoja mdogo mdgo umri kati ya miaka 17-19. Akaniambia dada samahani mimi naulizia machinga complex ipo wapi, mimi nikasahau ilipo nikamwambia mh hata sikumbuki ipo wapil akasema yeye ametoka singida huku amekumbatia begi lake kama wa bush haswa aliepewa story dar kuna matapeli, akaniambia ni wachimbaji wadogo wa madinj hivyo wamepata na yeye ameambia aje huku auze maana wananunua kwa bei nzuri huko machinga complex,
Ikabidi nianze kumshauri.kwanza nikamwambia mimi machinga complex sipakumbuki ipo wapi ila ukiwa unamuuliza mtu usipende kumueleza shida yako yote sababu hujui yupi atakua mwema kwako na yupi mbaya. Basi ikabidi nimpigie mume wangu kumuuliza hivi machanga complex ipo wapi, huku napiga kuna baba yupo pembeni yangu mtu mzima yule kijana akaanza kumuuliza tena yule baba machinga xomplex ni wapi na akaanza kumuelezea habari ya yeye kuja kuuza haya madini, ikabidi nimvute yule kaka nimkumbushe awe makini asubiri mme wangu apokee sim anielekeze ni wapi na asirudie tena kuwaambia watu kila kitu kuhusu yeye. Bas yule baba akaamuelekeza machinga ni wapi, huku bado nasubiri daladala yule kaka akaanza kuniambia dada nisaidie nisije nkatapeliwa na bla bla nyingi, kilichokuja nitokea hata sielewi nilijikuta science sina simu wala pesa , ikabidi niombe msaada wa nauli nirudi nyumban.
Mpak leo naomba Mungu amuongoze yule kaka, unajitoa kumsaidia mtu kwa moyo kumbe ni tapeli.
Niliapa sitosaidia tena wapita njia lkn bado najiuliza kila mtu akila hiki kiapo tutaishi vipi maana na mimi nilisaidiwa nauli ya kurudi kwangu.
Kubwa ni kuwa makini matapeli ni wengi sana na sijui wengine wanatumia dawa gani maana niliumwa almost wiki nzima na nikawa napoteza kumbukumbu
Kukwambia ana madini hyo ni chambo ya kukuvuta😀matapeli wana mbinu nyingi sna, shukuru mungu wamekuacha salama kuna dada mmoja alikutana na hao matapeli anasema aliongozana nao kutoka posta hadi kimara nyumban kwake na akawakaribisha ndani walikomba kila kitu kilichokuwa rahisi kuhamishika. Baada ya kupata fahamu amekuta nyumba nyeupe kuuliza majirani wanasema walikuwa wanajua anahama nyumba mana wale matapeli walisema ni ndugu yao wamekuja kumuhamisha kwenda nyumba nyingine na kwa vile aliingia nao ndani hawakuwa na hofu nao...baada ya dada kupoteza faham ndani jamaa walileta Fuso wakaanza kuhamisha vitu. Dada anasema hajui alifikaje nyumbani kwake mda ule mana yeye alitoka ofisin alikuwa anaenda lunch ndio akakutana na hao watu. Tuwe makini jamani
 
Kukwambia ana madini hyo ni chambo ya kukuvuta[emoji3]matapeli wana mbinu nyingi sna, shukuru mungu wamekuacha salama kuna dada mmoja alikutana na hao matapeli anasema aliongozana nao kutoka posta hadi kimara nyumban kwake na akawakaribisha ndani walikomba kila kitu kilichokuwa rahisi kuhamishika. Baada ya kupata fahamu amekuta nyumba nyeupe kuuliza majirani wanasema walikuwa wanajua anahama nyumba mana wale matapeli walisema ni ndugu yao wamekuja kumuhamisha kwenda nyumba nyingine na kwa vile aliingia nao ndani hawakuwa na hofu nao...baada ya dada kupoteza faham ndani jamaa walileta Fuso wakaanza kuhamisha vitu. Dada anasema hajui alifikaje nyumbani kwake mda ule mana yeye alitoka ofisin alikuwa anaenda lunch ndio akakutana na hao watu. Tuwe makini jamani
Hivi hao huwa wanatumia dawa kukulaghai au ni lugha tu?
 
Sipati picha na Mimi ungekuja kuniomba nauli nisingekuamini. by the way ni kweli I don't fuckn trust no body in this world especially wanaoombaomba
Ni kweki ingekua ngumu kunisaudia kwa namna nilivyo vaa alafu nlikua naomba mia tu ya kuongezea nauli maana kweny pochi ilibaki 300 na 60000 imechukuliwa pamoja na simu
 
Kukwambia ana madini hyo ni chambo ya kukuvuta[emoji3]matapeli wana mbinu nyingi sna, shukuru mungu wamekuacha salama kuna dada mmoja alikutana na hao matapeli anasema aliongozana nao kutoka posta hadi kimara nyumban kwake na akawakaribisha ndani walikomba kila kitu kilichokuwa rahisi kuhamishika. Baada ya kupata fahamu amekuta nyumba nyeupe kuuliza majirani wanasema walikuwa wanajua anahama nyumba mana wale matapeli walisema ni ndugu yao wamekuja kumuhamisha kwenda nyumba nyingine na kwa vile aliingia nao ndani hawakuwa na hofu nao...baada ya dada kupoteza faham ndani jamaa walileta Fuso wakaanza kuhamisha vitu. Dada anasema hajui alifikaje nyumbani kwake mda ule mana yeye alitoka ofisin alikuwa anaenda lunch ndio akakutana na hao watu. Tuwe makini jamani
Du mtihani kwa kweli. Yan aliniumiza kwa kua very kind to him, imagine nampigia hadi mme wangu aniambie machinga ni wapi sema hakupokea simu,
 
Hivi hao huwa wanatumia dawa kukulaghai au ni lugha tu?
I think dawa ina husika sababu baada ya siku ile nilikua nikiumwa kichwa sana na kupoteza kumbukumbu ktk baadhi ya nyakati ndani ya wiki
 
Unasaidiaje mtu usiyemjua pesa? Binafsi hii kitu sifanyi tangu 2009 hadi leo hii. Na hili jambo niliambiwa na jamaa mmoja ni mchungaji ilikuwa ni semina akasema hili jambo.

Tangu kipindi kile hadi leo pesa ni kitu nisichokitoa kama sadaka popote. Nikikutana na mtu hivyo kama ni hela ya kula naenda mnunulia mwenyewe na njiani sitaki stori naye.

Unaweza kutoa hiyo pesa ukanunua matatizo makubwa zaidi, wanadamu si wema kabisa.
 
Habari ndugu wapendwa na natumaini sote tu wazima wa afya na walio na mitihani ya maradhi au changamoto mbali mbali Mungu awapiganie ili sote tuishi kwa raha na kukiri utukufu wa Mungu.

Nimeamua kuileta habari hii ambayo ilinitokea mimi mwenyewe ili iwe kama funzo kwa wengine wenye mioyo ya kusaidia wanadamu wenzao wenye uhitaji lakini badala yake wanakutana na matapeli.

Nakumbuka siku fulani miezi kadhaa nyuma nilipanda dala dala kituo cha Mwembechai nikiwa naelekea Sinza, pembeni yangu alikuwa ameketi kijana mmoja wa makamo hivi huku mkono wake wa kulia akiwa ameushikilia huku akigugumia kwa maumivu makali.

Kilio chake kilivuta hisia zangu kama mwanadamu na kutaka kujua zaidi alipatwa na jambo gani, basi katika maelezo yake machache na alinifunulia kile kiganja kilichokuwa kimevimba kwa kutunga usaha mzito huku akisema kuwa hana msaada wowote nikadhamiria kumsaidia.

Alisema kuwa alikuwa anahitaji kiasi kama 15,000/= ili akapasuliwe ule uvimbe na kusafishwa kidonda. Yeye alisema ni dereva wa magari madogo ya mizigo na maskani yake ni pale Manzese Bakhresa kwa hali hiyo anashindwa kufanya shughuli zake za udereva hivyo kukosa kipato na kupelekea kudhoofu kutokana na lishe duni, pale nilimpatia kiasi kama 20,000/= ili akajitibie na nikampatia mawasiliano yangu ili awe ananipa maendeleo ya kidonda chake na kwa msaada zaidi.

Baada ya pale tukawa tunawasiliana na yule kijana kuhusu maendeleo ya kidonda chake na nikawa kila siku namtumia 7,000/= kwa ajili ya kujikimu huku akijiuguza kidonda chake, baada ya masiku kadhaa nikamuuliza wewe unatokea mkoa gani akaniambia anatokea mkoa wa Tanga. Nikamwambia kwanini nisimpe nauli arudi Tanga kwa wazazi kupumzika akijiuguza taratibu mpaka atakapotengemaa ndipo arejee mjini maana kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba hata pakulala hana maana alifukuzwa baada ya kushindwa kulipia pango, basi tukakubaliana kesho yake ajiandae ili nimtumie nauli ili aende nyumbani kupumzika, kesho yake nikamtumia 50,000/= nikiamini itamtosha nauli ya Tanga na hela kidogo ya kujikimu.

Baada ya masaa kama 7 nikiamini ameshaondoka mjini kwenda Tanga, akanipigia Simu kwa namba ya mtu mwingine maana yeye hakuwa na simu, aliniambia kuwa ameshafika Stendi Kange lakini amepungukiwa na nauli maana amebakiwa na 5,000/= hivyo mpaka afike kwao hiyo hela haitoshi. Kuanzia hapo akili yangu ikawa na mashaka kwa kuwa Tanga napafahamu inawezekana vipi kutoka Dar mpaka Tanga atumie 45,000/= ? Sikumtumia hela nilimwambia nipo bize kidogo.

Baada kama dakika 10 nikatumia namba nyingine kumpigia yule aliyenipigia nilimpa msichana aongee naye ili nijue yupo wapi, ikagundua kuwa yule alikuwa Manzese darajani na hakuwa Tanga, nikawapigia watu waliokuwa wanampa simu niongee naye na nilipokuwa nawatumia kumtumia hela, wote wakanithibitishia kuwa yule jamaa yupo Pale pale Dar na alikuwa ni muokota makopo ya plastiki maarufu na pia mtumiaji mkubwa dawa za kulevya hata wakati namtumia fedha walijua mimi ni ndugu yake na mara nyingi anautumia mkono wake uliojaa usaha kujipatia kipato huo ndio ukawa mwisho wa mimi na yeye, na yote niliyomsaidia nikamwachia Mungu.

Nb;
Tuwe macho na tunaodhania wanahitaji misaada.

Hahaaa! Endelea na moyo huo huo nawe utalipwa na Maulana!
 
Mi huwa natoaga tu msaada ata kuchunguza huwa sichunguz km ni wa kweli au lah. Ila sadaka ina baraka na mafanikio mbele yako. Hao inawezekana ni Wana shida kweli lkn njia zao wanazotumia ni mbaya na zisizo stahili. Kwa uluchokitoa ww ata usilalamike ww jihesabie tu kwamba unapokea baraka kutokn na moyo mzuri uliouonyesha kwa huyo muhitaji. Usijutie kwa uluchokitoa bali mshukuru Mungu kwa moyo huo mwema aliokugea.
Wanashida ya kutokufanya kazi
 
Umenikumbusha miezi miwili iliyopita nikiwa pale studio nasubiri daladala niende kariakoo akaja kaka mmoja mdogo mdgo umri kati ya miaka 17-19. Akaniambia dada samahani mimi naulizia machinga complex ipo wapi, mimi nikasahau ilipo nikamwambia mh hata sikumbuki ipo wapil akasema yeye ametoka singida huku amekumbatia begi lake kama wa bush haswa aliepewa story dar kuna matapeli, akaniambia ni wachimbaji wadogo wa madinj hivyo wamepata na yeye ameambia aje huku auze maana wananunua kwa bei nzuri huko machinga complex,
Ikabidi nianze kumshauri.kwanza nikamwambia mimi machinga complex sipakumbuki ipo wapi ila ukiwa unamuuliza mtu usipende kumueleza shida yako yote sababu hujui yupi atakua mwema kwako na yupi mbaya. Basi ikabidi nimpigie mume wangu kumuuliza hivi machanga complex ipo wapi, huku napiga kuna baba yupo pembeni yangu mtu mzima yule kijana akaanza kumuuliza tena yule baba machinga xomplex ni wapi na akaanza kumuelezea habari ya yeye kuja kuuza haya madini, ikabidi nimvute yule kaka nimkumbushe awe makini asubiri mme wangu apokee sim anielekeze ni wapi na asirudie tena kuwaambia watu kila kitu kuhusu yeye. Bas yule baba akaamuelekeza machinga ni wapi, huku bado nasubiri daladala yule kaka akaanza kuniambia dada nisaidie nisije nkatapeliwa na bla bla nyingi, kilichokuja nitokea hata sielewi nilijikuta science sina simu wala pesa , ikabidi niombe msaada wa nauli nirudi nyumban.
Mpak leo naomba Mungu amuongoze yule kaka, unajitoa kumsaidia mtu kwa moyo kumbe ni tapeli.
Niliapa sitosaidia tena wapita njia lkn bado najiuliza kila mtu akila hiki kiapo tutaishi vipi maana na mimi nilisaidiwa nauli ya kurudi kwangu.
Kubwa ni kuwa makini matapeli ni wengi sana na sijui wengine wanatumia dawa gani maana niliumwa almost wiki nzima na nikawa napoteza kumbukumbu
Pole Sana, mama angu pia aliwahi kutapeliwa kwa njia hiyo
 
Umenikumbusha mbali sana!!mwaka jana kama mwez wa pili hv!!Mafuriko yalipiga sana pande zetu!!ikatokea mkulima mmoja mhamiaji tena ngosha ana wake wawili na amebomokewa nyumba hz za udongo !!akawa amepata hifadhi kwa mtu tena chumba kimoja akadai hakitoshi ana wake wawili na watoto karibu sita!nikaamua kumpa akae nyumba yangu ya vyumba viwili na sebule!!!sasa akanipigisha stori za biashara za samaki tukafikia mwafaka tufanye kazi sasa nikatoa mtaji na yeye akawa anabanika samaki!!samaki walipokauka tu!akasema soko zuri lipo kahama !akaenda kuwauza!!alipopata hela akaitumia hela familia yke kimya kimya na wakatoroka hadi leo sijawaona tena!!!!LAKINI CHA AJABU MAISHA YANGU YA KIFEDHA YALIBADILIKA SANA KUANZIA PALE!YAANI HADI LEO FAMILIA YANGU INAINGIZA PESA NYINGI AMBAZO HATA MWANZO NILIKUWA ZISIPATI!!HADI NASHANGAA HADI LEO AISEEH!!!
JAMAA ALIKUWA ANATIA HURUMA HUKU AKIWA NA WATOTO WADOGO CHINI YA MIAKA MIWILI NA WALIKUWA WANALALA CHINI TENA KUMELOWA MAJI!!LAKINI NILIWA NYUMBA YENYE KITANDA NA KILA KITU!!!
NADHANI MUNGU ALITUBARIKI KWASABB YA WALE WATOTO!!!
UKITAKA KUWA TAJIRI JIFUNZE KUTOA TU HASA PALE UNAPOKUWA NA AMANI MOYON.I MWAKO!HUWEZ JUA KWANN ANAKUDANGANYA UJUE ANA SHIDA KUBWA!!!
NIKUTIE MOYO SANA MAN!!WE ENDELEA TU!!!
Niliwahi kukaa na dogo mmoja hivi hakua na mwelekeo, maisha yake yalikua magumu Sana lakini yangu uhakika wa kula ulikuwepo, siku moja nimeenda kwenye mihangaiko nilipoludi sikuamini kabeba nguo zangu zote, na uwezo wa kununua hata nguo ckuanao, Mungu mkubwa hazikuisha wiki mbili niliingiza mil. 9 cash
 
Kuna jamaa alinisimamisha njiani akalalama sana kwamba yeye ni mwalimu anatoka mkoa A kwenda B, siku hiyo amelala guest hata hela ya chumba hana na ana familia akadai nimsaidie hela ya chumba tu kuhusu kuondoka atajua mwenyewe, hapo tulipokutana alikuwa na kandambili za guest zimekatwa kwa mbele akasema amedanganya anakwenda benki kuwachukulia hela lakini kiukweli hana hela yoyote benki hivyo anafedheheka nimsaidie aepuke fedheha inayomkabili

Mimi kama mwanaume ikanigusa kwamba mwanaume mwenzangu anafedheheka wacha nimsaidie, haikuwa kubwa sana ilikuwa kama elfu 12 tu nikamwambia twende benki tulipofika karibu na benki akabaki njiani akasema ntamkuta nikamtolea hela nikampa akachukua na namba yangu

Baadae nikaja kugundua alikuwa tapeli ndio maana aliogopa kuongozana na mimi mpaka benki alijua nimemshtukia ntamkamatisha kwa askari wa benki

Hela haikuniuma ila nilichukia kudanganywa/kutapeliwa.
Nikawaza hawa matapeli ndio wanafanya tusisaidiane, kila mmoja unamuona tapeli kumbe wengine wana shida kweli
 
Back
Top Bottom