Jinsi nilivyotapeliwa na mtu niliyedhani ni mhitaji kumbe ni tapeli

Mimi nilikutana na mzee maeneo ya kanisani magomeni na yeye akainiomba nauli..wakati narudi namwona kajibanza sehemu anahesabu hela nyingi🀣
 
Tunatakiwa tufkirie Mara mbili mbili kabla hatujasaidia watu

Inatakiwa ukae chini ufkirie Kama unachoambiwa na muomba msaada Kina ukweli
 
Umenikumbusha mbali sana!!mwaka jana kama mwez wa pili hv!!Mafuriko yalipiga sana pande zetu!!ikatokea mkulima mmoja mhamiaji tena ngosha ana wake wawili na amebomokewa nyumba hz za udongo !!akawa amepata hifadhi kwa mtu tena chumba kimoja akadai hakitoshi ana wake wawili na watoto karibu sita!nikaamua kumpa akae nyumba yangu ya vyumba viwili na sebule!!!sasa akanipigisha stori za biashara za samaki tukafikia mwafaka tufanye kazi sasa nikatoa mtaji na yeye akawa anabanika samaki!!samaki walipokauka tu!akasema soko zuri lipo kahama !akaenda kuwauza!!alipopata hela akaitumia hela familia yke kimya kimya na wakatoroka hadi leo sijawaona tena!!!!LAKINI CHA AJABU MAISHA YANGU YA KIFEDHA YALIBADILIKA SANA KUANZIA PALE!YAANI HADI LEO FAMILIA YANGU INAINGIZA PESA NYINGI AMBAZO HATA MWANZO NILIKUWA ZISIPATI!!HADI NASHANGAA HADI LEO AISEEH!!!
JAMAA ALIKUWA ANATIA HURUMA HUKU AKIWA NA WATOTO WADOGO CHINI YA MIAKA MIWILI NA WALIKUWA WANALALA CHINI TENA KUMELOWA MAJI!!LAKINI NILIWA NYUMBA YENYE KITANDA NA KILA KITU!!!
NADHANI MUNGU ALITUBARIKI KWASABB YA WALE WATOTO!!!
UKITAKA KUWA TAJIRI JIFUNZE KUTOA TU HASA PALE UNAPOKUWA NA AMANI MOYON.I MWAKO!HUWEZ JUA KWANN ANAKUDANGANYA UJUE ANA SHIDA KUBWA!!!
NIKUTIE MOYO SANA MAN!!WE ENDELEA TU!!!
 
Wewe utalipwa kwa kumsaidia na yeye atalipwa kwa kukutapeli
 
kuna kibabu huwa kila ijumaa anapita ofisini kwangu kuomba nampa jero au buku!!
siku hiyo sikumuona kama kawaida yake ya kupita mchana siku ya ijumaa!
badala yake akapitia jioni na akanikuta ofisini!!
nikamwambia leo sina kitu mzee umechelewa nimewapa wenzio...
akaanza kulalamika leo hali mbali toka asubuhi hadi jioni hajapata vile amezoea kupata!!
nikamuuliza kiutani kwani mzee umepata sh ngapi leo??!!
elfu 48 mwanangu yaani leo ni nuksi tupu!hadi leo omba omba pita hivi usinisogelee.

mwingine huwa anatembea kwenye mahospitali na hotpot na chupa ya chai..
anasema mtoto wake kalazwa amekataa kula hvyo anaomba ela kdgo ajaribu kumnunulia mtori au supu
 
Mkuu kama una amani nafsini uwe unatoa tu!nafsi ndio mwalimu mzuri wa kila jambo!!!we fanya kile nafsi ina kwambia tu!!
 

Huyu nilikutana nae Manzese kwenye Zebra pale machale yakanicheza nikamkata jicho nikapanda bajaji nikaondoka zangu
Ila hadithi ni Kama hii hii
 
[emoji23][emoji23]mimi hawa wanaotembezwa wameshikwa mikono,sio vipofu bali ni mbibi wa 70 na mdada kama wa 25 hivi.

ninaposhinda kuna vibanda vya jamaa wakala mwingine anaingiza nyimbo,vimegawanywa na barabara kimoja huko kingine huku,wakaja nimekaa na mshikaji wakaniomba nikawapa 2000,baadae nikahamia upande wa pili kwa yule wakala,wakanikuta wakiwa wanarudi wakaniomba tenaa.nikajua kumbe akikugeuzia mgongo tu na habari yako imeisha,hata akikukuta sehemu unapigwa mawe hatakumbuka.
 
Usijali kilichopotea, kama ulitoa kwa nia njema basi subiri.
 
mimi sikupi pole, ila nakupa hongera kwa kujali na kuwajibika ipasavyo; kimsingi binadamu tunapaswa kusaidiana kama hivyo kwa sababu ni kweli kuna wenye uhitaji huko mtaani......ni hawa waharifu wachache ndiyo wanaharibu na kuwaharibia wenzao wenye uhitaji wa kweli. kwa upande wako we umeshinda, tena sana tu. kinachopatikana hapo ni zaidi ya kile ambacho kingepatikana kwa aliye na shida kweli kweli. kitakachokosekana kwa tapeli huyo ni kikubwa sana hapo baadae.
 
Huyu nilikutana nae Manzese kwenye Zebra pale machale yakanicheza nikamkata jicho nikapanda bajaji nikaondoka zangu
Ila hadithi ni Kama hii hii
Nilikuja kuammbiwa wapo wengi wa design hii
 
πŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“ŒπŸ“Œ
 
Mtoa mada tegemea baraka zaidi kurudi kwako....endelea kutoa hata kama ni kibaka ww toa...ni hazina hiyo
 
Aisee kwa hiyo jamaa ameamua kutembea na mkono wenye usaha ili apige pesa tu, akicheza huo usaha utamuozesha mkono mwishowe utakatwa.
 
Aiseee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…