Davidmmarista
JF-Expert Member
- Apr 11, 2024
- 1,367
- 2,451
Hello waungwana wa jamiiforums Naitwa, Davidmmarista. Mimi ni kijana mjasiriamali, programmer, na mkulima. Hii ni stori yangu ya mafanikio katika biashara ya chakula, na jinsi nilivyoweza kufikia hatua ya kutengeneza milioni tano kwa mwezi.
Kila kitu kilianza kwa maamuzi yangu ya kuwekeza mtaji mdogo wa milioni moja. Nilijua kabisa kwamba ni lazima niwe na malengo na kuwa na mikakati madhubuti. Kwa hiyo, nilianza kwa kununua vyombo muhimu vya biashara, ambavyo vilikamilisha kiasi cha shilingi 400,000. Baada ya hapo, nilijua kuwa ili biashara yangu iweze kufanikiwa, lazima nimpate mwenye eneo ambapo ningeanzisha biashara yangu. Nilitembelea maeneo mbalimbali, na baada ya uchambuzi kidogo, nilikubaliana na mwenye frame moja kwenye maeneo ya Mwenge kwa shilingi 200,000 kwa mwezi wa kuanzia.
Baada ya kuhakikisha kuwa nipo katika eneo sahihi, nilijua sasa nilihitaji kuajiri mfanyakazi ambaye alikuwa na ujuzi katika upishi wa chakula bora. Niligundua kuwa kuwa na mfanyakazi bora upishi kunaweza kuleta faida kubwa kwa biashara yangu. Kwa hiyo, nilimpata mdada mmoja kutoka Tanga ambaye alikuwa na vizuri kwenye kupika. Tulikubaliana kumlipa shilingi 70,000 kwa mwezi, na alikubali. Alianza kazi na haraka sana alionyesha uwezo wa kujituma sana.
Nilijua kuwa ili biashara yangu iweze kuwa na mafanikio, lazima nisimamie kila kitu mwenyewe. Hii ilikuwa ni kazi kubwa, lakini nilikuwa tayari kufanya juhudi zote. Mwaka jana, mwezi wa 6, nilielekea sokoni Mabibo nikaenda kununua vyakula vya kutosha pamoja na viungo mbalimbali ili niweze kuanzisha maandalizi ya chakula. Nilikuwa na mtaji kidogo, lakini kwa akili yangu na mikakati bora, niliweza kununua samaki wazuri na dagaa kutoka kwa dada mmoja anayeitwa Tricy Dagaa yupo Twitter(X). Hali ya kupata pweza pia ilikamilika, na nilikuwa na uhakika wa kupata bidhaa za ubora.
Kila jioni, nilikuwa na supu ya pweza ambayo iliuzwa sana, na pia chips zilikuwa ni bidhaa maarufu. Wateja walikuwa wanarudi tena na tena kwa supu nzuri ya pweza na chips za kufurahisha. Kila asubuhi, tuliandaa uji maridadi na supu iliyovutia wateja wengi. Nilijua kuwa kila sehemu ya biashara inahitaji kuwekwa kwa umakini, hivyo nikawekeza kwa kiasi cha shilingi 300,000 kwa viungo vyote. Nilikuwa na mtungi wa gesi, hivyo nilikuwa na uhakika wa kuwa na gesi ya kutosha. Nilijua kuwa ni muhimu kuwa na jiko la mkaa na vifaa vingine vya kupikia ili biashara yangu iweze kutimiza malengo yangu.
Nikiwa na viti vizuri, sehemu ya kupumzika kwa wateja, na bango kubwa lililobeba jina langu, biashara yangu ilianza kuwa maarufu. Kila asubuhi, wateja walijaa, na chakula kilikamilika kwa haraka. Supu ya pweza ilikuwa ni maarufu sana, na wateja walikuwa wanapenda bei nafuu. Supu ilikuwa shilingi 1500, donati ilikuwa 500, na maandazi yalikuwa shilingi 200. Kila asubuhi, tulikuwa na chai ya kupendeza na kahawa nzuri. Vyakula vyetu vilikuwa ni vya bei nafuu na vilikuwa bora kwa afya ya watu. Kuanzia saa 11 asubuhi hadi saa 4, biashara ilikuwa inaenda vizuri, na namshukuru Mungu kwa juhudi zote.
Mwisho wa mwezi, nilikagua hesabu yangu. Nilijua kuwa ningeweza kupata faida kubwa, lakini nilikuwa na shaka kidogo kwa kuwa siyo kila biashara inaweza kuwa na mafanikio makubwa. Lakini, nilikuwa na furaha kubwa nilipoona kuwa nilikuwa na kiasi cha shilingi milioni 5 na laki 7. Hii ilikuwa ni zaidi ya nilivyokuwa na matarajio. Nilijivunia sana na kutambua kuwa mimi ni mjasiriamali aliyejenga biashara kutoka chini na kufanikiwa.
Pamoja na mafanikio yangu, nilianza kuhamasika zaidi na kuongeza watu wawili wa kusaidia katika biashara yangu. Hii iliwezesha kazi kufanyika kwa haraka na vyakula vyetu kuwa bora zaidi. Tulianza kupata oda nyingi kutoka Kariakoo na maofisini mbalimbali. Ili kuendelea kuwa na ubora wa bidhaa, tuliongeza chakula zaidi kama pilau, wali, ndizi, ugali wa samaki, dagaa, nyama, na mboga za majani. Pia, tuliendelea na chips, na tukaanza kutoa full diet ya matunda.
Kwa kweli, nilijifunza jambo muhimu sana katika biashara hii: "A better service, a better income (and vice versa)." Hii ni kanuni niliyoiweka katika biashara yangu. Kutokana na ubora wa huduma, wateja walirudi na kurudia tena. Hata sasa, biashara yangu inashika kasi, na inatambuliwa kwa ubora wake. Siku moja, naamini nitaweza kuwa na biashara kubwa
kama Macdonalds.
Kila kitu kilianza kwa maamuzi yangu ya kuwekeza mtaji mdogo wa milioni moja. Nilijua kabisa kwamba ni lazima niwe na malengo na kuwa na mikakati madhubuti. Kwa hiyo, nilianza kwa kununua vyombo muhimu vya biashara, ambavyo vilikamilisha kiasi cha shilingi 400,000. Baada ya hapo, nilijua kuwa ili biashara yangu iweze kufanikiwa, lazima nimpate mwenye eneo ambapo ningeanzisha biashara yangu. Nilitembelea maeneo mbalimbali, na baada ya uchambuzi kidogo, nilikubaliana na mwenye frame moja kwenye maeneo ya Mwenge kwa shilingi 200,000 kwa mwezi wa kuanzia.
Baada ya kuhakikisha kuwa nipo katika eneo sahihi, nilijua sasa nilihitaji kuajiri mfanyakazi ambaye alikuwa na ujuzi katika upishi wa chakula bora. Niligundua kuwa kuwa na mfanyakazi bora upishi kunaweza kuleta faida kubwa kwa biashara yangu. Kwa hiyo, nilimpata mdada mmoja kutoka Tanga ambaye alikuwa na vizuri kwenye kupika. Tulikubaliana kumlipa shilingi 70,000 kwa mwezi, na alikubali. Alianza kazi na haraka sana alionyesha uwezo wa kujituma sana.
Nilijua kuwa ili biashara yangu iweze kuwa na mafanikio, lazima nisimamie kila kitu mwenyewe. Hii ilikuwa ni kazi kubwa, lakini nilikuwa tayari kufanya juhudi zote. Mwaka jana, mwezi wa 6, nilielekea sokoni Mabibo nikaenda kununua vyakula vya kutosha pamoja na viungo mbalimbali ili niweze kuanzisha maandalizi ya chakula. Nilikuwa na mtaji kidogo, lakini kwa akili yangu na mikakati bora, niliweza kununua samaki wazuri na dagaa kutoka kwa dada mmoja anayeitwa Tricy Dagaa yupo Twitter(X). Hali ya kupata pweza pia ilikamilika, na nilikuwa na uhakika wa kupata bidhaa za ubora.
Kila jioni, nilikuwa na supu ya pweza ambayo iliuzwa sana, na pia chips zilikuwa ni bidhaa maarufu. Wateja walikuwa wanarudi tena na tena kwa supu nzuri ya pweza na chips za kufurahisha. Kila asubuhi, tuliandaa uji maridadi na supu iliyovutia wateja wengi. Nilijua kuwa kila sehemu ya biashara inahitaji kuwekwa kwa umakini, hivyo nikawekeza kwa kiasi cha shilingi 300,000 kwa viungo vyote. Nilikuwa na mtungi wa gesi, hivyo nilikuwa na uhakika wa kuwa na gesi ya kutosha. Nilijua kuwa ni muhimu kuwa na jiko la mkaa na vifaa vingine vya kupikia ili biashara yangu iweze kutimiza malengo yangu.
Nikiwa na viti vizuri, sehemu ya kupumzika kwa wateja, na bango kubwa lililobeba jina langu, biashara yangu ilianza kuwa maarufu. Kila asubuhi, wateja walijaa, na chakula kilikamilika kwa haraka. Supu ya pweza ilikuwa ni maarufu sana, na wateja walikuwa wanapenda bei nafuu. Supu ilikuwa shilingi 1500, donati ilikuwa 500, na maandazi yalikuwa shilingi 200. Kila asubuhi, tulikuwa na chai ya kupendeza na kahawa nzuri. Vyakula vyetu vilikuwa ni vya bei nafuu na vilikuwa bora kwa afya ya watu. Kuanzia saa 11 asubuhi hadi saa 4, biashara ilikuwa inaenda vizuri, na namshukuru Mungu kwa juhudi zote.
Mwisho wa mwezi, nilikagua hesabu yangu. Nilijua kuwa ningeweza kupata faida kubwa, lakini nilikuwa na shaka kidogo kwa kuwa siyo kila biashara inaweza kuwa na mafanikio makubwa. Lakini, nilikuwa na furaha kubwa nilipoona kuwa nilikuwa na kiasi cha shilingi milioni 5 na laki 7. Hii ilikuwa ni zaidi ya nilivyokuwa na matarajio. Nilijivunia sana na kutambua kuwa mimi ni mjasiriamali aliyejenga biashara kutoka chini na kufanikiwa.
Pamoja na mafanikio yangu, nilianza kuhamasika zaidi na kuongeza watu wawili wa kusaidia katika biashara yangu. Hii iliwezesha kazi kufanyika kwa haraka na vyakula vyetu kuwa bora zaidi. Tulianza kupata oda nyingi kutoka Kariakoo na maofisini mbalimbali. Ili kuendelea kuwa na ubora wa bidhaa, tuliongeza chakula zaidi kama pilau, wali, ndizi, ugali wa samaki, dagaa, nyama, na mboga za majani. Pia, tuliendelea na chips, na tukaanza kutoa full diet ya matunda.
Kwa kweli, nilijifunza jambo muhimu sana katika biashara hii: "A better service, a better income (and vice versa)." Hii ni kanuni niliyoiweka katika biashara yangu. Kutokana na ubora wa huduma, wateja walirudi na kurudia tena. Hata sasa, biashara yangu inashika kasi, na inatambuliwa kwa ubora wake. Siku moja, naamini nitaweza kuwa na biashara kubwa
kama Macdonalds.