Jinsi Putin alivyoibadilisha Urusi kuwa na nguvu ya kibabe ulimwenguni

Jinsi Putin alivyoibadilisha Urusi kuwa na nguvu ya kibabe ulimwenguni

It's untested because of there quality since it create fear to the enemies......

Mfano ....Saud Arabia walinunua mifumo ya ulinzi wa anga kwa USA ambayo iliaminika kuwa Bora .......lakin.

Drone za waasi wa Yemen .....ziliangamiza vituo vya mafuta .....lkn Iran haijapigwa kutokana na ubora wa hiyo mitambo
Syria wanayo hayo mapipa lakini wanadundwa kila siku na IDF.
 
Putin awekeze kuinua wananchi wake kiuchumi aachane na mambo ya Kununua silaha za kivita, huwezi amini Canada yenye watu million 30+ imewapita Russia kwa GDP yenye watu million 130+
Hii comment kila sehemu ihusuyo URUSI unaiweka.
 
Hii comment kila sehemu ihusuyo URUSI unaiweka.
Ndo maana yake mkuu maana ya nguvu ni ipi kama wananchi wako wanaishi kwa shida, Russia angekua vizuri kiuchumi asingetumia nguvu kubwa kumshawishi Ukraine kuwa upande wake
 
Putin awekeze kuinua wananchi wake kiuchumi aachane na mambo ya Kununua silaha za kivita, huwezi amini Canada yenye watu million 30+ imewapita Russia kwa GDP yenye watu million 130+
Wananunua silaha au wanatengeneza?
 
Russia ni nchi ingetakiwa iwe mbali sana Wana resources nyingi Ila ndo hivyo nchi za kijamaa zinawekeza sana kwenye jeshi

Russia ni wapili kuwa viwanda vya silaha baada ya marekani
Kwani Marekani ni nchi ya kijamaa! Urusi siyo nchi ya kijamaa! Au una maanisha USSR? Urusi na USSR ni vitu tofauti!
 
Nchi inaheshimika kwa kuwa na uchumi imara na wala sio una Nuclear Warheads ngapi.

Leo hii China, Japan na South Korea zinaheshimika zaidi duniani kwa kuwa na uchumi mkubwa na wala sio kwa kujilimbikizia silaha nyingi na itakumbukwa kwamba miaka 40 iliyopita Urusi ilikuwa mbele ya hayo mataifa kiuchumi lakini leo yameiacha Russia mbali kwa sababu Russia haijui vipa umbele vyake ni nini.

Wao wangejishughulisha na maendeleo ya watu wao wakaachana na ndoto za kutafuta umaarufu wa kuuza silaha kwa sababu hiyo ndiyo imewafanya leo hii wawe maskini pamoja na akili nyingi walizonazo.
Hivi uliyo andika una uhakika nayo? Miaka 40 uliyo sema mbona Russia haikuwa nchi kamili - palikuwapo USSR! Wewe utaambiwa ukajilishe kwanza kama walivyo ambiwa waKenya! Yaani mtanzania anasema Russia ni masikini? Wonders will never end! Mtanzania eti!
 
...Russia haijawahi kuitawala Africa kwa Mabavu, hawajawahi kuiba rasilimali zetu, kutesa babu zetu na pia hawajawahi kuivamia Africa kwa vifaru na Mabomu kama NATO na Mataifa ya Ulaya. Napenda Demokrasia ila sipendi Demokrasia inayoenezwa kwa Mtutu wa Bunduki.

Sent from my SM-A022F using JamiiForums mobile app
 
Hivi ikatokea wasimame wawili tu Russia na USA bila washirika nani atashinda?
 
Unazima moto wa msitu, lakini bado unawaka," yalisoma maandishi juu ya picha ya mwanamke mchanga wa Kirusi, akitabasamu huku akiwa nusu uchi. Kama hii, picha zingine 11 zenye maneno ya kuudhi zilitengeneza kalenda ya mwaka 2011 iliyohusisha wanafunzi wa uandishi wa habari wa Chuo Kikuu cha Moscow na kuitolea kwa sanamu yao.

Kiongozi wa kisiasa wa Urusi Vladimir Putin, ambaye katika majira ya joto ya mwaka 2010, alikuwa ameongoza binafsi helikopta ya zima moto ili kukabiliana na moto huo uliokuwa umeutishia mji wa Moscow.

Zawadi za kupendeza za kuadhimisha siku ya kuzaliwa ya Putin, ambaye amekuwa madarakani nchini Urusi kwa zaidi ya miongo miwili, ni sehemu moja tu ya utekelezaji kimila wa umma wa sifa ya kiongozi huyo wa Urusi.

Putin amekuwa kielelezo cha ubabe na kuwatia moyo wanasiasa duniani kote, kama vile Mmarekani Donald Trump, Mhungari Viktor Orban na Mbrazil Jair Bolsonaro, ambaye aliondoka Jumatatu wiki hii kwenda Moscow kwa lengo la kukutana na rais huyo wa Urusi.

Mbali na kipindi cha helikopta ya zima moto, Putin tayari amejiruhusu kupigwa picha katika mfululizo wa hali za kiume. Aliwaangusha wapinzani kwenye mkeka katika mechi za judo. Alichunguza meno ya dubu katika Aktiki na chui huko Siberia, wote wawili wakiwa wamelala.

Aliendesha nyambizi na mashua. Alipiga picha akiwa na bunduki mkononi (na bila shati) alipokuwa akiwinda Siberia. Aliibuka akiwa utupu akiwa amepanda farasi na kuvua samaki. Alijionesha na bastola kwenye safu ya risasi. Au tu alionekana akiwa amevalia mavazi ya michezo alipokuwa akifanya mazoezi ya misuli ya kifua chake kwenye ukumbi wa mazoezi.

'Nguvu za ubabe duniani'

Baada ya kuingia madarakani mwishoni mwa miaka tisini, Putin alichukua uongozi wa nchi inayojaribu kuinuka kutoka kwa vifusi vya Umoja wa Kisovieti. Umoja wa Kisovieti ulikuwa umesambaratika mwaka wa 1991, na Warusi walikabiliwa na maswali ya utambulisho, wakilazimika kuzoea ubepari, kushughulikia mgawanyiko wa eneo na upotezaji wa hadhi ya nguvu ya ulimwengu.

"Kulikuwa na hali ya kushindwa kwa ujumla, kuyumba kwa uchumi, na kushuka kwa thamani ya sarafu ya Urusi, na kushindwa katika Vita Baridi. Udhaifu huo ulionekana wazi zaidi kati ya wazazi wa Urusi, watu wa miaka 30, 40 na 50 ambao walipoteza maisha yao, akiba na kazi, kwamba hawangeweza tena kutunza familia zao huku akashuhudia vijana wakitajirika katika biashara mpya, na kwamba alikuwa mlengwa wa kukosolewa waziwazi, kwa kutokuwepo kwake katika maisha ya familia, kwa unyanyasaji wa nyumbani na kwa shida kama vile ulevi, anasema Amy Randall, profesa wa historia katika Chuo Kikuu cha Santa Clara huko California na mhariri wa toleo maalum "Masculinities Soviet" wa jarida la Masomo ya Historia ya Kirusi.

Kwa mujibu wa Randall, udhalilishaji na aibu ya Kirusi kwa ulimwengu katika miaka ya 1990 iliishia kufananishwa na kiongozi wa nchi hiyo wakati huo, Boris Yeltsin, alinaswa akiwa amelewa na katika mitazamo ya aibu katika hafla za kimataifa. Hata alijifanya kuongoza orchestra kwenye sherehe ya kijeshi na kutoa taarifa juu ya tamaa ya kutokomeza silaha za nyuklia za Kirusi baada ya kulewa.

Bila kujulikana kwa umma, Putin anaonekana kwenye uwanja wa kisiasa wa Urusi mikononi mwa Yeltsin, ambaye alikuja kumrithi. "Putin anawapa Warusi picha ya ajenti mkali wa sanaa ya kijeshi kutoka KGB (shirika la ujasusi la Soviet). Anasema Sperling.

Chini ya amri yake, jeshi la Urusi lilipata tena udhibiti wa Chechnya, lilivamia Georgia na kuteka Crimea. Sasa nchi inakabiliana na uwezekano wa mzozo wa silaha na Ukraine. Tangu mwishoni mwa mwaka jana, Putin ameweka zaidi ya wanajeshi 100,000 kwenye mpaka kati ya nchi hizo mbili na akitaka Ukraine isiingizwe kwenye Jumuiya ya kujihami ya nchi za magharibi, NATO, muungano wa kijeshi unaoongozwa na Marekani na Ulaya Magharibi ambao Putin anaona kama tishio kwa usalama wa nchi yake.

"Chini ya uongozi wa Putin, Urusi imejiimarisha kama nguvu ya uanaume duniani, ikionyesha nguvu zake za kisiasa, kujitegemea kiuchumi, na uwezo wake wa kiteknolojia na kijeshi. Putin anatumia umaarufu wake na uwezo kubaki madarakani kwa muda mrefu , mifumo kama vile utaifa wake wa kiume, nia yake ya kuifanya Urusi kuwa kubwa tena, matumizi yake ya maadili ya mfumo dume na dhana ya tofauti katika majukumu ya kijamii kati ya jinsia, pamoja na chuki ya wazi ya jinsia moja", anasema Randall, ambaye Trump pia alipata msukumo wa Kirusi kwa kauli mbiu yake ( "ifanye Marekani kuwa kubwa tena") na sio tu mtangulizi wake Ronald Reagan.

'Sifa bora za kiume'

Ilikuwa kutoka kwa mtazamo huu ambapo Putin alisema, mnamo Novemba 2020, kwamba Jair Bolsonaro alikuwa na "sifa bora za kiume" kwenye usukani wa Brazil. Pongezi hizo zilikuja wakati wa hotuba ya rais wa Urusi kwenye mkutano wa BRICS, kundi linaloundwa na Brazil, Urusi, India, Uchina na Afrika Kusini, na kurejelea jinsi Bolsonaro alishughulikia janga la covid-19.

"Hata wewe binafsi uliambukizwa na ugonjwa huu na ulistahimili mtihani huo kwa ujasiri mkubwa. Najua wakati huo lazima haukuwa rahisi, lakini ulikabiliana nao kama mwanaume halisi na ulionyesha sifa bora za kiume, kama vile nguvu na utayari", Putin ilisema kulingana na nakala ambayo serikali ya Brazil yenyewe ilichapisha.

Wiki moja iliyopita, Putin alivutia hisia za ulimwengu kwa taarifa ambayo alimsuta Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, mkosoaji wa makubaliano ya amani ya Minsk.

"Upende usipende, mrembo wangu, lazima uvumilie," Putin alisema, akitumia msemo wa kike kuhutubia kiongozi wa Ukraine. Bolsonaro, katika kilele cha majadiliano yake na Rais Emmanuel Macron kuhusu moto katika Amazon mnamo 2020, alichapisha tena chapisho ambalo lililinganisha Mama wa Taifa Michelle Bolsonaro, 39, na Brigitte Macron, 68. Chapisho hilo lilisema:

"Unaelewa sasa kwa nini Macron unamtesa Bolsonaro?" Na rais mwenyewe akatoa maoni yake "Usidhalilishe jamani lol".

Mbinu nyingine ya kawaida ni kufanya "utani" kuhusu ubakaji na chuki dhidi ya wanawake. Mnamo 2014, katika majadiliano na mwenzake wa PT Maria do Rosário, naibu Jair Bolsonaro alisema kuwa "Sitakubaka kamwe, kwa sababu haustahili." Bolsonaro alielezea kuwa Rosário atakuwa mbaya sana kwa yeye kumpenda.

Putin, mwaka wa 2006, aliripotiwa kumwambia mwandishi wa habari wa Israel, kuhusu tuhuma za ubakaji dhidi ya Rais wa wakati huo wa Israel Moshe Katsav: "Msalimie rais wako. Alitokea kuwa kijana mwenye nguvu sana. Alibaka wanawake kumi, sote tunashangaa, sote tunamuonea wivu." Baada ya msukosuko wa kipindi hicho, Kremlin ililaumu dosari katika tafsiri.

Mnamo 2014, wakati Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Merika Hillary Clinton alilinganisha uvamizi wa Crimea na shambulio la Mjerumani Adolf Hitler dhidi ya Poland, Putin alisema kwa ufupi: "Bora hata usibishane na wanawake." Pia alisema kuwa maoni ya Hillary yalifichua "udhaifu".

Na kwamba "udhaifu sio lazima liwe jambo baya kwa wanawake". Bolsonaro, mnamo mwaka 2017, alisema kuhusu binti yake Laura: ""Nina watoto watano kuna wanaume wanne, kisha katika mtoto wa tano nilikuwa na udhaifu na mwanamke akakuja".

Tofauti na Brazili, nchini Urusi ndoa ya watu wa jinsia moja ni kinyume cha sheria. Wanandoa wa jinsia moja hawawezi kuasili watoto pamoja. Ikiwa itafanywa, itasajiliwa kwa jina la mmoja tu wa wazazi.

Kuhusu suala la mizozo nyumbani, nchini Brazili, Sheria ya Maria da Penha ilikamilisha miaka 15. Katika Urusi, unyanyasaji dhidi ya wanawake ulikataliwa mwaka 2017.

Kuanzia wakati huo, unyanyasaji tu wa waume ambao husababisha madhara makubwa ya mwili kwa wake zao ndio wanakabiliwa na adhabu ya kisheria. Mabadiliko ya sheria yaliwakilisha faida kwa serikali ya Putin, ambayo imekuwa ya kihafidhina zaidi kwa miaka.

"Putin na Bolsonaro wanatazamana na kwa pamoja wanaimarisha hisia hii ya kujivunia uanaume. Bolsonaro amejaribu kwa uwazi kumuiga Putin katika misimamo yake ya chuki dhidi ya wanawake na ushoga, na katika makabiliano yake na uongozi wa Ulaya na wa kimataifa. Anamwona wazi Putin kuwa mtu mwenye nguvu na picha hii ya mtu mwenye nguvu imekuwa maarufu zaidi na imeenea ulimwenguni nyakati hizi, "anasema Randall

Source bbc news

View attachment 2123944
Mambo ya vita ya zamani sana anaonekana kichaa tu .kwanza vita yenyewe inamshinda hajachukua major city mpaka Sasa .Ukraine wanapigania nchi Yao .Putin si mtu wa kumchezea ni shetani dunia mpya Hii
 
Nchi inaheshimika kwa kuwa na uchumi imara na wala sio una Nuclear Warheads ngapi.

Leo hii China, Japan na South Korea zinaheshimika zaidi duniani kwa kuwa na uchumi mkubwa na wala sio kwa kujilimbikizia silaha nyingi na itakumbukwa kwamba miaka 40 iliyopita Urusi ilikuwa mbele ya hayo mataifa kiuchumi lakini leo yameiacha Russia mbali kwa sababu Russia haijui vipa umbele vyake ni nini.

Wao wangejishughulisha na maendeleo ya watu wao wakaachana na ndoto za kutafuta umaarufu wa kuuza silaha kwa sababu hiyo ndiyo imewafanya leo hii wawe maskini pamoja na akili nyingi walizonazo.
Unachekesha kweli.
So wewe ndio unajua vipaumbele vya Urusi Ila wao hawajui?

Taifa zima la watu 130+ M hawajitambui Ila wewe hapo Vingunguti ndio unajua wafanye nini.
Jinga sana wewe.
 
Nikuulize, hivi wewe uliyepo hapo Chamazi ndio unajua umuhimu wa uchumi wa Urusi kuliko wao Wenyewe.

Hivi nchi kubwa vile hadi ilipofikia hapo kwamba hawajui wanachokifanya, then mtu wa gezaulole ndie anataka kuwashauri.

Huu ujuaji wetu nadhani tunaweza Kuwakosoa hata wanasayansi wa NASA wanavyotuma chombo Mars
Hivi amewahi jiuliza kwamba sisi pamoja na gas na oil deposits bado tunatumia kuni kupikia chakula sasa anavuka nchi na bahari kwenda kuilaumu russian na akati hapa tz kwetu mikoa yenye madini kama shinyanga ndiko hali ngumu wabibi na wamayo macho mekundu kisa moshi wa kuni hadi wanakula mapanga kusingiziwa uchawi
 
Putin awekeze kuinua wananchi wake kiuchumi aachane na mambo ya Kununua silaha za kivita, huwezi amini Canada yenye watu million 30+ imewapita Russia kwa GDP yenye watu million 130+
Kweli wewe ni kapuku wa fikra
 
Putin awekeze kuinua wananchi wake kiuchumi aachane na mambo ya Kununua silaha za kivita, huwezi amini Canada yenye watu million 30+ imewapita Russia kwa GDP yenye watu million 130+
Pambania nchi yako yenye watu mili9n 58 afu mnazidiwa na kenya
 
Nchi inaheshimika kwa kuwa na uchumi imara na wala sio una Nuclear Warheads ngapi.

Leo hii China, Japan na South Korea zinaheshimika zaidi duniani kwa kuwa na uchumi mkubwa na wala sio kwa kujilimbikizia silaha nyingi na itakumbukwa kwamba miaka 40 iliyopita Urusi ilikuwa mbele ya hayo mataifa kiuchumi lakini leo yameiacha Russia mbali kwa sababu Russia haijui vipa umbele vyake ni nini.

Wao wangejishughulisha na maendeleo ya watu wao wakaachana na ndoto za kutafuta umaarufu wa kuuza silaha kwa sababu hiyo ndiyo imewafanya leo hii wawe maskini pamoja na akili nyingi walizonazo.
Sizitaki mbichi hizi


Uwezo mkubwa wa kijeshi ndio unaamua pia uwezo wako wa uchumi
 
Back
Top Bottom