Jinsi Putin alivyoibadilisha Urusi kuwa na nguvu ya kibabe ulimwenguni

Jinsi Putin alivyoibadilisha Urusi kuwa na nguvu ya kibabe ulimwenguni

Hii barabara ni kama Arusha-Moshi, hamna tofauti. Eti hii ndio Highway na hawa ndio wanawakomalia nchi za magharibi.

Hii ndio shida ya nchi zinazotawaliwa kidikteta na ndio kielelezo tosha cha kutuonyesha kwamba maendeleo hayawezi kuletwa kwa ubabe kwa sababu hii ndio nchi inayoongoza duniani kwa kuwa na rasilimali nyingi za asili lakini hii ndio taswira yake kamili..😛😛😛
[emoji23][emoji23][emoji134],US roads
mqdefault.jpg
102851537-GettyImages-465172040-1.jpg
10.jpg
 
Helcopters, bunduki, etc
Marekani ina soko kubwa la uuzaji silaha na ukiona wanaagiza silaha kutoka Russia basi ujue waagizaji ni private sector na hizo silaha are not meant for the use by the US military but purely for civilian use.

Serikali za Marekani na Russia hawana utaratibu wa kuuziana silaha kwa matumizi ya kijeshi.
 
wala uchumi sio kil kitu kwenye kuifanya nchi ama taifa fulani liwe upande fulani kama unavyodai mbona CUB VENEZEVUELA wapo karibu na US ila wapo upande wa RUSSIA?
mmemezeshwa prooaganda[emoji23][emoji23][emoji23]
Kabisa
 
Sasa Venezuela si sawa na somalia Hana faida yeyote yaan sio potential
Hamnaga taifa ambalo sio potential mkuu.........kibiashara hilo ndio Lina fulsa kubwa .......refer ...chanzo cha Iran kuanza kupeleka shehena za mafuta kule
 
sasa mkuu,kati ya nchi ulizotaja ukilinganisha na russia nani anaheshimika na kuogopwa zaidi,mipaka yako ni muhimu sana..
Kabsa mkuu ...pamoja na China kuwa na uchumi mkubwa......but alikuwa ananyayaswa na Jimbo lake la ndani ......HONKONG......hadi pale alipo amua kufuata ubabe

Now .....bado .... Taiwan....inamzingua
 
Angekuwa amejenga taifa lenye nguvu angekuwa haogopi Ukraine kujiunga na EU na NATO. Halafu maisha ya watu ni ya hali ya chini sana; kuna matajiri wachache tu. Alipopota mafuta na gesi, pesa yote akapeleka kwenye jeshi. Nchi haina barabara za maana za kuunganisha miji. Ni sehemu chache tu zilizoko Magharibi maneo ya Moscow na St Petersbug ndiko kuna maisha; ukishafika Ufa kutokea Mosco unakutana na barabara za hovyo sana kuliko hata za Burundi. Kwa mfano angalia hizi Highway za kutoka Ufa kwenda sehemu nyingine ispokuwa kwenda Moscow.

View attachment 2125684

View attachment 2125687
Hapo hujatumia akili mkuu .....yani Ukubwa wa urusi .....unaifananisha na Burundi kweli ..Russia ilibidi liwe bara........Ukubwa wa nchi unapelekea connectedness ya n hi kuwa ndogo
 
Ndiyo utasema iliyumba kipindi cha Boris Yeltsin kwa vile yule hakuwa na muelekeo wo wote na kuna wakati fulani Georgia ilikuwa na nguvu sana lakini sasa kimya.
Yaaaah....ni kweli
 
Yaani hao warusi ni watu bure kabisa yaani barabara zao hamna tofauti na za kwetu na ndio wanang'ang'ania eti kupambana na nchi za magharibi, hawa jamaa wana akili kweli..!!

Hawa watu kumbe tatizo lao ni sawa na sisi, kukosa uongozi. Nchi kubwa yenye watu wenye akili na rasilimali lukuki kama Russia ndio inakuwa na barabara feki hivyo eti ndio Highway....!!

Kwa hali hii hawa jamaa wana safari ndefu sana kuja kufikia hatua ya maendeleo iliyokwisha fikiwa na nchi za magharibi labda wana karne mbili mbele au wapate viongozi wenye maono tofauti na walionao sasa kwani watawala walionao sasa hawana tofauti na akina Kim Jong Un.
Nchi ni kubwa Sana ile ......Tz inaweza kuingia Mara 300.....so kuwa connected with quality infrastructures itachukua miaka 300
 
Hii barabara ni kama Arusha-Moshi, hamna tofauti. Eti hii ndio Highway na hawa ndio wanawakomalia nchi za magharibi.

Hii ndio shida ya nchi zinazotawaliwa kidikteta na ndio kielelezo tosha cha kutuonyesha kwamba maendeleo hayawezi kuletwa kwa ubabe kwa sababu hii ndio nchi inayoongoza duniani kwa kuwa na rasilimali nyingi za asili lakini hii ndio taswira yake kamili..😛😛😛
Kwani mmechunguza barabara zote

Acheni kuwa na HALLO EFFECTS
 
Marekani ina soko kubwa la uuzaji silaha na ukiona wanaagiza silaha kutoka Russia basi ujue waagizaji ni private sector na hizo silaha are not meant for the use by the US military but purely for civilian use.

Serikali za Marekani na Russia hawana utaratibu wa kuuziana silaha kwa matumizi ya kijeshi.
Ila Russia Wana mifumo bora ya ulinzi wa anga than USA ........refer to s _ 300
 
Tangiapo US wananunua silaha za mrusi
US hainunui silaha kutok urusi. Zamani sana wakati wa utawala wa Reagan kabla na baada ya USSR kuvunjika, kulikuwa na kampuni fulani ya watu waliokuwa na connection kwenye serikali ya Reagan kupitia mgongo wa james baker ilikuwa na contract ya kuwa inanunua silaha kutoka Belarus kisiri na kuzipeleka Nicaragua kusaidia waasi wa Contra. Vile vile CIA ilikuwa inanunua silaha za Urusi na Korea ya kaskazini kwa siri kwa ajili ya kutathmini ubora wake ikiwa ni pamoja na kutafuta mbinu za kuzijam, lakini siyo kwa matumizi ya kijeshi. Wakati huo kituo chao cha kufanyia utafiti wa silaha hizo kilikuwa Ujerumani; siku hizi hawafanyi hivyo tena.
 
Hapo hujatumia akili mkuu .....yani Ukubwa wa urusi .....unaifananisha na Burundi kweli ..Russia ilibidi liwe bara........Ukubwa wa nchi unapelekea connectedness ya n hi kuwa ndogo
Mbona marekani imeunganishwa yote; kusini mpaka kasikazini na kutokea magaharibi hadi mashariki. Hizo highway za urusi, ni barabara za vijijini kwenye mashamba ya wakulima wa marekani; siyo hata za serikali ya mtaa.

hii ni Highway A6 kutoka Tanga (urusi) kwenda Chita (urusi). Ndiyo barabara pekee inayounganisha majiji ya Irkutsk na Vladvostock

1645456556273.png
 
Kwani mmechunguza barabara zote

Acheni kuwa na HALLO EFFECTS
barabara nzuri Urusi ziko maeneo ya Magharibi tu: Kuanzia Ufa kurudi hadi Moscow na St Pettersberg. Eneo lote kutokea Ufa hadi vlavodostock ni barabara mbovu sana ispokuwa chache chache za mijini.
 
Back
Top Bottom