Jinsi Tundu Lissu Alivyojikaanga Kwa "Mafuta ya Taaluma Yake!!"

Jinsi Tundu Lissu Alivyojikaanga Kwa "Mafuta ya Taaluma Yake!!"

Sitabomoa hiyo nyumba, yaani kwa upande wa Muungano sitauvunja bali "nitapigilia msumari!" Kwa "Mwanasheria Nguli" atakuambia hiyo nyumba ni BATILI tuivunje!

Unamuweka Lissu maneno mdomoni? Kuwa na serikali tatu ndio kuuboresha muungano wenyewe... acheni kujifanya hamna akili...
 
Inamaana wewe haujawahi kuona trafic anakamata gari kwa kosa la eidha kuzidisha mzigo,bovu,gari la wizi,kukosa fire exstinguisher au linaendeshwa bila leseni ya barabara n.k! Lakini na yeye ANAPANDA GARI HILOHILO ili akupeleke polisi central!.
 
Sasa kama ameyatambua hayo leo hii mnataka asiyaseme ili kulinda ubunge wake? amesema ukweli alioutambua. Kitakachofuata ni taratibu za kurekebisha mambo ili tuwe na uhalali wa huu muungano, sio lazima aachie ubunge au chochote. Tujenge utamaduni wa kuusema ukweli bila kujali maslahi binafsi.
 
Mbona mna papara? Subirini asubuhi ya tarehe 14/4/2014 saa 3 kwa saa za Afrika mashariki kupitia TBC majibu yote ya maswali yenu mtajibiwa na Tundu Lissu ugomvi wa nini? Hivi sasa usalama wanajuta kwa nini walishinikiza matangazo ya katwe maana sasa nchi nzima inasubiri kwa hamu kumsikia Lissu tofauti na jumamosi ambapo wengi hawakuwa na habari.
Tanesco tumesikia wanampango wa kuhakikisha hakuna umeme zaidi ya nusu ya nchi kwa wakati huo ili tusisikie.
Sijui inawezekana wakikata umeme tutake tena mwongozo ili siku inayofata Lissu arudie tena kwa sababu zile zile za Mhe Sitakuwa ni muhimu Watanzania wote wasikie kisemwacho bungeni.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Mkuu Pasco,
Heshima kwako! Nakubaliana na hoja zako kimsingi ila ujue sio kila kitu lazima kiharamishwe na mahakama ndio kiitwe HARAMU! Mtu binafsi naye ana uhuru wa kutoa mawazo yake na yakakubalika katika jamii! After all mahakama zenyewe ni creation ya Muungano, na zenyewe uhalali wake ni questionable!
Hoja za kisheria, zinahitaji ufumbuzi wa kisheria!.

Mfano ndoa ni muungano wa ridhaa wa watu wawili!, lakini ikiisha kuwa kisheria, wawili hawa hawawezi tena kuridhia kuachana kwa ridhaa zao tena, kwa sababu uhusiano wao unakuwa binding kwenye sheria!. Hata wachokane vipi na kukubalia wenyewe kuwa hakuna ndoa, hata iliyofungwa msikitini, kanisani au kwa DC, zote zinaweza kuvunjwa mahali pamoja tuu, not msikitini, not kanisani not kwa DC bali ni mahakamani tuu!.

Ni mahakama pekee tuu ndio yenye uwezo wa kutangaza ubatili wa mkata kisheria, ila hata kama mahakama haijatangaza, kupiga kelele kuhusu muungano batili ruksa, ila hizo ni kelele tuu, za kujifurahisha!.

Makubaliano ya muungano hayakusema chochote kuhusu mambo ya muungano kisheria, ila katiba ya JMT ya mwaka 1977 iliweka provision ya kuundwa kwa mahakama ya katiba!, but it has never been constituted!, hivyo hiyo taarifa ya Lisu kuhusu muungano batili nayo ni kelele tuu kama ambazo tumekuwa tukizipiga humu!.
Pasco.
 
Mkuu The Boss, umeona ehe!. Tangu alipowaingiza Chaka Chadema kwa kutoa go ahead ya kuipitisha sheria ya mabadiliko ya katiba badala ya kuizuia, nilimface head on face to face na kumuuliza kwanini alitoa maoni ya kammbi ya upinzani badala ya kuwasilisha pingamizi rasmi, alinijibu kwenye maoni yale, last line alisema wanapinga!. Nilichoka, maoni yale ni go ahead ya sheria ile kupita ambayo sasa ndio hii inayotuletea madudu yote haya!, maoni ni maoni, na pingamizi ni pingamizi!,
[h=2]Search Results[/h]
  1. [h=3]Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!.[/h]Pasco

Pasco,

Unaongea kama mtu asiyefaham hila za ccm na jinsi watanzania walivyofichwa kuhusu muungano. Ukifanya mambo kisa tu kuna ukweli bila kuangalia nyakati yaweza kuwa mwisho wako au wa taasisi

1. Lissu na Chadema wangefanya hicho unachokisema wakati ule isingewezekana na wangeishia kuonekana wapiga kelele kama wazanzibar na zaidi wavunja muungano na wahatarishi wa amani
a/ Wakati ule hakuna aliyekuwa anafaham kilichopo kwenye kijikaratasi cha makubaliano ya muungano
b/ hakuna aliyekuwa anafaham kufojiwa kwa signature

2. Unachokiona kama mtazamaji ni tofauti wanaocheza ngoma yenyewe(field)
a/ lazima ujue kurudisha majeshi nyuma kama alivyowahi kusema Mbowe ujipange,
b/ lazima u balance kinachotakiwa kufanywa na situation ya wakati(je mazingira,hali ya hewa) inawa favour kufikia lengo na
c/ lazima ukubali chance kupotea ukiombea nafasi nyingine ijitokeze au kwa calculations(wacheza draft) usubiri wakati wa kusukuma kete fulani

Siasa ni calculated move, unaacha favourable conditions zikiwepo una attack
 
Katiba za Tanganyika na Zanzibar hazikuruhusu marais kuingiza nchi katika mikataba ya kimataifa?
 
..na huko kwenye BLW itakuwaje?

..je, wata-ratify bila kupata ridhaa ya wananchi wa Znz, au baada ya kupata ridhaa ya wananchi kupitia kura ya maoni?

cc Buchanan
Mkuu JK, hili nalo neno!.

Kwa maoni yangu,
  1. Makubaliano ya Muungano ya tarehe 22/04/1964, Mwal. Nyerere na timu yake, walitoka Dar na kutua Zanzibar, zilisainiwa hati mbili ya kwake na ya Karume, baada ya hapo, zote mbili zilikusanywa, wakarudi nazo Dar!.
  2. Yale makubaliano halisi yaliweka kipindi cha mpito ni hadi mwaka 1965 na hapo itungwe katiba ya kudumu ya JMTZ!.
  3. Kulikuwa na kipengele cha trial period ya miaka 10, ipigwe kura ya maoni kuwauliza Wanzibari na Watanzania kama bado wanautaka Muungano!.
  4. Tarehe 25/04/1964, Karume akatua pale Karimjee Hall na kukabidhiwa sheria ya Muungano "iliyosharekebishwa!" kuyaondoa mauza uza yote!, Baba wa watu elimu yake ngumbaro!, hakujua alisaini nini tarehe 22, wala kujua amekabidhiwa nini hiyo tarehe 25.
  5. Kiukweli Karume alikuwani mshughulikiaji mzuri wa wapinzania wake!, Nyerere alimnusu Okello, Karume akavumilia, akamshgughulikia Shamte, Nyerere hakupenda, akaamua kuwanusuru Abrahman Mohamed Babu, na Col. Mahfudha, Karume akamind, akaanza kuhubiri kuwa muungano ka koti, likikubana unalivua!
  6. Ilidhaniwa Karume aliamua kusubiri 1974 ile trial period, ili hilo koti livuliwe!, for whataver the reasons, Karume had to go!.
  7. Jumbe alivyotaka kuuchokoa, he was lucky to be spared!.
  8. Naamini kilichofanya hati hizo zipotezewe ni kuizuia kura ya maoni Zanzibar!, ndio maana Zanzibar inaogofwa na kuacha ifanye kila inachotaka but sio kura ya maoni.
  9. Katiba impya ikipita, hati za muungano zinakuwa redundant, na kubaki kuwa historical documents tuu!
  10. Katiba mpya ya serikali mbili itakaliwa Zanzibar, hivyo katiba ya zamani itaendelea, na Wanzanzibari sasa watapiga kura yao ya maoni kuhusu Muungano!, amini usiamini, utavunjiliwa mbali!.
Pasco.
 
Mbunge Lissu atoke Bungeni maana Ubunge wake ni "BATILI!!"

Sio Lissu pekee yake. Wabunge wote ni batili watoke Bungeni na hata Rais wenu n Batili atoke Ikulu. Kila kitu ni batili tuanze upya kama ilivyokuwa prior to 1964
 
Buchanan,

Nadhani mnawekeza juhudi kubomoa hata future yenu wenyewe kwa ushabiki tu. Hoja yako ni nyepesi sana kuijibu, na sioni Lissu akishindwa kuijibu vile vile.

Kinachotazamwa hapa is our desire:

1. For a constitutional government and a fair administration ambayo inatawala kwa mujibu wa, na kufuatana na sheria.

2. For the laws themselves kuwa JUST, FAIR and EQUITABLE.

Hoja yetu (mkipenda tuite wachache) ni kwamba TANU na baadae CCM has breached both conditions above. Katika hili, Shivji nae analizungumzia in "let the people speak: Tanzania Down the road to neo-liberalism(1995, page 95) kwamba:

If one is to judge by the standards of constitutionality, which are proclaimed today, our union has hardly had a constitutional government for the last thirty years. there were so many major breaches - including surreptitious manipulations of the constitution - that in reality we did not live by our constitution. We even forgot to swear by it. We, at the Hill, stopped teaching Constitutional Law in 1971 o 1972!

Kuna haja pia ukaelewa kwamba katiba isn't simply a legal document, bali its also a political document. Kimsingi, its a political document than a legal document. Lazima kwanza iwe na political legitimacy kabla ya kuwa enacted into law. Lakini kabla haijapata political legitimacy na kustahili obedience and loyalty ya watawala na watawaliwa, lazima ipatikane kwa consensus ndani ya jamii. That's what a constitution is all about, umuhimu wake wa kuwa na "political legitimacy", sio legalities and technicalities as the primary motive.

Pamoja na Katiba ya sasa kukosa sifa zote hizi,lakini haina maana kwamba serikali ya TANU na CCM ilikosa uhalali wa kutawala. Uhalali ulikuwepo lakini chanzo chake hakikuwa Katiba ya nchi bali:

1. Charisma and integrity ya Mwalimu.

2. Azimio la Arusha lililolenga kumwinua mwananchi.

3. Na mafanikio ya TANU katika kupigania wanyonge ndani na nje ya nchi.

Hizi ndio factors au sources zilizoipa CCM uhalali wa kutawala, kuunda serikali, kukamata dola, na kuendesha shughuli zote za kijamii, kisiasa na kiuchumi. Lakini kwa bahati mbaya, all these sources of legitimacy zimeporomoka, CCM imeziua yenyewe, ndio maana sasa katika mazingira ya leo, the only source of legitimacy kwa ccm au chama chochote kutawala ni Katiba ya nchi itayo tokana na maoni ya wengi. Period.

Tukirudi kwenye hoja yako ya msingi inayo hoji vyeti vya Lissu, kazi na Lissu n.k, tuchukulie mfano wa Afrika ya Kusini. Kwa miaka mingi (wakati wote wa ubaguzi wa rangi), serikali ya makaburu ilidai kwamba inatawala kwa mujibu wa katiba. In the process, kina mandela, tambo, sisulu na wengine bado walisoma, walifanya kazi za uwakili kutetea wenzao weusi chini ya katiba na sheria zile zile za makaburu, walikamatwa na kufungwa kwa sheria zile zile, na hatimaye wakaachiwa huru, katiba mpya ikaandikwa, na uhuru kupatikana. Je hali ya Lissu na wanaharakati wote hawafanani na hali hii ya Mandela? Je kina Mandela walijikaanga na mafuta yao wenyewe?

Mwalimu Nyerere alisoma chini ya sheria za mkoloni, akatumia mfumo wao kufanikisha harakati nyingi za uhuru, na akaja kupinga mfumo huo huo kwa hoja kwamba haukuwa mfumo halali, na matokeo yake, elimu, uzoefu na mafanikio ya Mwalimu chini ya mfumo na utawala wa mkoloni hayakubadilika kwa sababu tu alikuja pingana na mfumo huo, na alipoingia tu madarakani, akaibadili Katiba na pia mfumo uliomlea, mwelimisha, na kumfikisha siku ile ya uhuru wa Tanganyika. Je Mwalimu Nyerere alijikaanga na mafuta yake mwenyewe?

Turejee kwenye mfano wa Afrika ya Kusini. During apartheid, kwa makaburu, wao, a constitutional government simply meant that the government was following the letter of the constitution and the law. Na hii pia ilikuwa ni hoja ya muda mrefu ya CCM katika kupinga haja ya Katiba mpya. Lakini kwa makaburu (na pia ccm sasa), it became obvious kwamba the pre-requisite of a constitutional governmment ni kwamba the constitution and the laws themselves have to be just, fair, and equitable. Sio tu kwamba serikali ikifuata katiba na sheria bila ya kujali kama sheria ni just, fair and equitable basi serikali hiyo ijulikane kwamba ni halali kikatiba. Legitimacy inakuja iwapo katiba ni just, fair and equitable kwa maoni ya walio wengi (wananchi), ambao ndio msingi wa katiba.

Iwapo hili halikuwa a prerequisite, basi serikali ya Makaburu ingeendelea kuwa moja ya constitutional governments in the world - kwani katiba ya kikaburu followed the letter of the constitution and the law. Lakini ingekuwa ni upuuzi kuwaambia wapiganaji wa ANC kwamba they should strictly follow and respect the law. Kama ANC wangefanya hivyo, basi wasingeweza kuanzisha harakati for their right to self determination ambayo ilikuwa denied by the constitutional and legal order ya wakati ule.

Katika muktadha wa Tundu Lissu, same applies - harakati za Tanganyika zinalenga our right to self determination ambayo ipo denined by the current constitutional and legal order.

Nirudie kusema tena:
Mzee Mandela alisoma katika mfumo alioupinga, akafanya kazi za sheria katika mfumo huo huo, akakamatwa na kufungwa kwa kupinga mfumo ule, miaka 27 baadae akatolewa jela na taifa likaandika katiba mpya na kuupata uhuru. Mandela akawa rais wa kwanza mzalendo. Leo mandela ni shujaa na mfano wa kuigwa kwa kila mwanadamu duniani. Je, unataka kutuambia kwamba Mandela alijikaanga kwa mafuta yake mwenyewe? Kumbuka hata yeye alikuwa mwanasheria aliyepinga katiba na mfumo wa kikaburu, na alipata upeo huo baada ya kusoma katika mfumo ule ule na kufanya kazi katika mfumo ule ule.

Buchanan, ebu tuache masihara. Tuungane na Lissu kuinzidua Tanganyika.



Tanzania Kwanza, Tanganyika Kabla.

Cc Nguruvi3


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Tatizo langu ni kuwa wanaoamini kuwa Muungano huu ni batili na hauna uhalali hao hao walisimama na kuapa kulinda Jamhuri ya Muungano! Binafsi ningewapa umakini zaidi kama wangeamua kujitoa kwanza na kujivua nafasi zao ambazo zimeingia kwa sababu ya Muungano huu. Hatujawaona Wazanzibari wakifanya hivyo na sasa hakuna Watanganyika wenye ujasiri wa kufanya hivyo. Go figure.
 
Tatizo langu ni kuwa wanaoamini kuwa Muungano huu ni batili na hauna uhalali hao hao walisimama na kuapa kulinda Jamhuri ya Muungano! Binafsi ningewapa umakini zaidi kama wangeamua kujitoa kwanza na kujivua nafasi zao ambazo zimeingia kwa sababu ya Muungano huu. Hatujawaona Wazanzibari wakifanya hivyo na sasa hakuna Watanganyika wenye ujasiri wa kufanya hivyo. Go figure.

No unachoongea hakina mashiko, unategemea upambane ukiwa nje ya uwanja wa vita ama ndani ya uwanja? Hilo haliwezekani kwa sababu ya mfumo uliopo, usipokuwa na nafasi hakuna mtu wa kukusikiliza. Unadhani kwa nini hata Yesu aliamua kuja kuungana na wenye dhambi huku aliweza tu kuwakomboa bila kujihusisha nao? Kuapa kupitia mfumo unaoupinga sio vibaya kwa sababu huwezi pigana ukiwa nje ya battle ground..kusema watesign kwanza ni fikra mbovu kabisa hasa kwa mfumo wa serikali yetu. Go Lissu, goooo
 
Mwakyembe kakana thesis yake iliyompatia udoctorate
Hahahahahaha huyo ndo mwakyembe ukimuona mwingine ujue wa kuchonga. Haya mambo yanafurahisha sana hasa unapoona mtu anajichanganya na misimamo huku akiangalia upepo unavumaje. Yaani nafikiri anatamani hayo maandiko yawe ya kufoji .
 
Buchanan,

Kumbuka Nyerere pia aliwahi kuwa mjumbe wa baraza la kutunga sheria wakati wa mkoloni, sheria ambazo zilikuwa "batili".

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Katika bandiko #71 Mchambuzi amejaribu kumjibu Buchanan vizuri sana. Niongezee katika hoja zake kwa mifano michache. Wengi wanafahamu kwa makosa kuwa Mandela alileta uhuru wa S.Africa kama wanavyoelewa Mugabe ameleta uhuru wa Zimbabwe. South Africa ilikuwa huru kilichokataliwa ni mfumo alioeleza Mchambuzi.

Zimbabwe (South Rhosesia) ilikuwa huru kilichokataliwa ni mfumo wa ubaguzi.
Askofu Abel Muzorewa alikuwa waziri mkuu wa Zimbabwe.
Alipatikana kwa njia za uchaguzi lakini je,kulikuwa na just, fair and equitable kwa uchaguzi uliofanywa chini ya sheria halali za Zimbabwe za wakati huo?


Hapa ndipo nakuja kwa swali la Mzee Mwanakijiji kuhusu watu kujitoa kwanza.
Jibu ni YES and NO.

Yes, kwasababu inapofikia katika point fulani tunaweza kwenda msituni kama Mugabe na wenzake.
Je,njia hiyo ni sahihi kwa wakati na mazingira tuliyo nayo?


Jibu lingine ni NO kwasababu, Martin Luther alipigana na mfumo wa ubaguzi akiwa Marekani.
Hakujiondoa Marekani wala kuingia msituni kupigania mfumo wa haki na usawa.


Kwa mujibu wa sheria za Marekani za wakati huo, Ubaguzi ulikuwa ni jambo halali.
Martin Luther alisoma na kushiriki katika mfumo hadi alipoamua kwa kusema enough is enough something must be done for the change. Akaendeleza harakati ndani ya mfumo ule ule uliomlea.

Mama Rosa Parker alipoambiwa akae nyuma ya basi, hakuteremka katika basi.
Alibaki akipinga kitendo hicho ndani ya basi.

Kama Rosa angeremka leo historia ingeandikwa tofauti.

Alikaa ndani ya basi na ushahidi upo na historia ikampeleka ndani ya Rotunda akiwa katika jeneza.
Historia ikamheshimu hata pale punzi ilipokoma.


Jibu ni YES kwasababu ya kiwango cha elimu na uelewa. Wapo walioona uharamu wa muungano wakakaa kimya hadi miaka 50 ambapo walizozaliwa katika mfumo huo haramu wana wajukuu na nusu ya population inajua haramu hiyo ni halali.

Jitihada za kukieleza kizazi hiki kuhusu uharamu ni ngumu kutokana na wengi kutokuwa na ufahamu. Taratibu kizazi kimeelewa, sasa watu waendelee kukaa kimya au watoe elimu kabla ya kuzima taa!
Sidhani kuzima taa ghafla kutawafanya watumiaji waelewe tatizo, nadhani kuwaeleza kwanza kwamba tatizo ni kiangazi ni nzuri zaidi.


Jibu ni NO, kwasababu mfumo huu una manufaa kwa kikundi kidogo chenye nguvu.
Kikundi hicho kimetumia uwezo wa kisheria kujenga ngome ambayo ni rahisi kumtia mtu matatani, japo basi matatani, uwezekano wa kupotea upo.

Jumbe alijaribu, Kolimba wakajaribu kila mmoja kwa njia zake, tunafahamu kilichowatokea.
Upo uwezekano wa kupigana na mfumo watu wakiwa sehemu hiyo na nadhani ni njia muafaka.
Otherwise we can 'borrow a page' from Rwanda, walijaribu short cut!
 
Uwezo wenu wa kuelewa na kufikiri ndo umeishia hapo, ndo maana mnanukuu vitu bila kujua chanzo,fuatilieni maoni yake leo
 
Kwell watz wengi elimu ilitupita kuspho!anaposema matili yupo sahihi ndiyo maana anapigania mabadiliko.nyie wawapi?
 
Nashukuru Nguruvi3 na Mchambuzi kwa kumjibu vizuri huyu mtetezi wa serikali mbili. Amethibitisha kama wenzie kule bungeni kuwa hawana hoja.

Ni matumaini yangu baada ya kusoma post zenu ataufunga huu mjadala kulinda hadhi yake kama moderator.
 
Back
Top Bottom