Jinsi ya kufanya miujiza (Education is power)

Jinsi ya kufanya miujiza (Education is power)

Mkuu swala zima la kuwepo au kutokuwepo Kwa mungu Ni swala la kumezeshwa tangu ukiwa mtoto
Kwanza inabidi ujue maana ya mungu unaweza kukuta mungu Ni wewe Mwenyewe so mtu akisema mungu hayupo Ila yupo huyo mungu unakuta hajakosea
Pia inabidi uwe free thinker coz ukibase Kwa upande mmoja tu utakuwa unalazimisha logic zote zije kwako
Jaribu kuchunguza vitu bila kuwa na bias then philosophy ndio huanzia hapo
Pia kuna vitabu mbalimbali mfano soma encyclopedia britanica mada ya Christianity kuna vitu vingi vya kujifunza kuhusu asili ya neno mungu na pia kuna kitabu cha dr Adolf mihanjo kinaeleza vizuri asili ya kuanza kutumika Kwa neno mungu
So usipinge direct hivo au kujaribu kucheza sana na maneno coz utazidi kwenda mbali na ukweli
Thanks

Tatizo kila mtu anamuona mwenzie ndiyo kamezesheswha halafu yeye ndiyo ana mawazo huru,sasa uwanja huu ndiyo ungeamua ni yupi kamezeshwa na yupi hajamezeshwa.
 
Nimekupata. Kumbe wewe ni mfuasi wa biblia!. Mimi naongelea fikra huru isiyo kwenye kifungo cha dini. Nilazima tufunguliwe kutoka kwenye vifungo vya dini.

Kwa mantiki hiyo wewe ni yote katika yote?

Huna aliyekuumba wala anayekupa pumzi ya kila siku?

Unaposema fikra huru una maana gani? Je hayo mawazo/fikra itakayokupa ku-conclude usahihi wa jambo fulani unaipata toka kwa nani?
 
ww ntakujibu...!!!!

NDICHO tunachosema, HIYO SIJUI KUFUFULIWA, sijui kuponywa, sijui kuokoka, sijui lazima UWE NA YESU...ndio KUKARIRISHWA....so once ukisha kuwa BRAINWASHED AND FEEDED WITH THT FAITH...utaongea na kufanya haya UNAYOSEMA....

So ww UKO MBALI SANA NA UHALISIA...sbb ur enslaved already with that FAITH....ww ulishaona MTU AMEFUFUKA AU KUFUFULIWA...!!? Taja hata mmoja tu...ww unafuata ULICHOJAZWA KICHWANI TU..HUNA PROOF ya dunia nzima...umebakia KUFUATA USICHOKIJUA...taja sehemu yeyote umesikia mtu kafufuliwa au baada ya kufa eti tutafufuliwa...HUU NDIO UGONJWA WA AKILI...ushatekwa...so ur a slave, hujui hata UNAENDA WAPI ..so you will remain tht way all ur life...AND NOTHING U CAN SEE KWA YOOOOTE UNAYOAMBIWA....

Kwanza kabisa mie sio mkristo,na huwa najiuliza sana kwanini wakanaji mungu wengi wa humu wanaonekana walikuwa wakristo!

Ujue tatizo humu ni kwamba wanaokana mungu wanajiona ndiyo wenye mawazo huru kwa huko kukana mungu,yani kupinga kile wanachokiamini wenzenu ndiyo hali hiyo mnaona mna uhuru wa mawazo. Suala la Mungu ni suala linalohitaji kuamini kwa sababu haonekani, hivyo suala la wewe au nyie kukana mungu si jambo la ajabu hapa kwa sababu haonekani huyo huyo mungu.

Kwahiyo suala hapa ni kuangalia ni ishara na hoja zipi kuonesha uwepo wake mungu na hoja zipi za kuonesha kuwa hakuna mungu,lakini tatizo lenu nyie muda wote mnapinga tu. Sie hatuwezi kuwalazimisha nyie muamini tunavyoamini sie na wala nyie hamuwezi kulazimisha tuamini mnavyoamini nyie,hivyo mmoja anapomwambia mwenziye imani yake si sahihi basi anapaswa aeleze pia usahihi wa imani yake ni upi sio kuishia kuponda imani ya mwenzio.
 
Kwa mantiki hiyo wewe ni yote katika yote?

Huna aliyekuumba wala anayekupa pumzi ya kila siku?

Unaposema fikra huru una maana gani? Je hayo mawazo/fikra itakayokupa ku-conclude usahihi wa jambo fulani unaipata toka kwa nani?

unajua mkuu huu ulimwengu wa vitabu vya mafundisho mbalimbali unateka akili za watu kwa kasi kiasi kila mtu anataka kuwa mjasiriamali siku hizi!siyo kila elimu inaelimisha nyingine zinapotosha.
 
yote kayamaliza Yesu"hata ningekuwa na imani ya kuhamisha milima kama sinao upendo mimi si kitu kabisa"maana nafsi iliyo huru inatakiwa kujazwa na upendo wa kimungu kabla ya yote hayo,maana hiyo miujiza sijui kufufua wafu,uponyaji yanawezekana kwa mwanadamu,ila nafsi ya mwanadamu kuwa na hadhi ya kimungu siyo hiyo miujiza,ni upendo ufananao na Mungu usio na mipaka!
 
Kwa mantiki hiyo wewe ni yote katika yote?

Huna aliyekuumba wala anayekupa pumzi ya kila siku?

Unaposema fikra huru una maana gani? Je hayo mawazo/fikra itakayokupa ku-conclude usahihi wa jambo fulani unaipata toka kwa nani?
Kuna thread hapa nitaileta inaongelea kabla ya kuzaliwa hapa duniani mtu alikuwa yukoje na baada ya kufa hapa duniani anakuwa yupoje. Nadani katika hiyo thread nitajibu maswali yako yote. Maana ni somo lefu na lina practicals zake.
 
yote kayamaliza Yesu"hata ningekuwa na imani ya kuhamisha milima kama sinao upendo mimi si kitu kabisa"maana nafsi iliyo huru inatakiwa kujazwa na upendo wa kimungu kabla ya yote hayo,maana hiyo miujiza sijui kufufua wafu,uponyaji yanawezekana kwa mwanadamu,ila nafsi ya mwanadamu kuwa na hadhi ya kimungu siyo hiyo miujiza,ni upendo ufananao na Mungu usio na mipaka!
Unaongelea mungu yupi huyo mwenye upendo? mungu gani huyo unayemwongelea anawaacha watu wa africa ya kusini kuuwa wenzao. Upendo gani huo anasema eti atawahukumu watu milele wakati maisha ya kuishi duniani ni chini ya miaka mia. Huoni kuwa ni kipindi kidogo sana cha kuishi?
mungu unayemtaja hapa hayupo ni elimu uliyolishwa na waleeee ili wakutawale vizuri.
 
Nawasalimia wana JF wote.

Leo nipo hapa kuongelea swala hili la kufanya miujiza na uponyaji.
Kwanza awali ya yote ningepeda kutoa utangulizi kama ifuatavyo.

UTANGULIZI
Sisi binadamu tuko na nguvu kubwa sana ndani yetu. Ni kitendo cha kujua jinsi ya kuitumia. Nguvu tuliyonayo ni nguvu ya kiroho ambayo huwezi ukaiona kwa macho ya damu na nyama lakini unaweza ukaitumia na ikaleta matokeo katika ulimwengu wetu huu.

Nguvu tuliyonayo sisi haijui kuwa hiki chema au kibaya ni mtu tu atakavyo amua kuitumia. Wengine wanaitumia kufanya uchawi lakini wengine wanaitumia kufanya miujiza ya uponyaji. Ni wewe tu utakavyoamua kuitumia hiyo nguvu. Yenyewe ipo.

NAMNA GANI WAWEZA KUIPATA HIYO NGUVU.
Watu wengi sana duniani wamekuwa hawajui hawa watu wanaofanya miujiza au wanaofanya uchawi wanapata wapi nguvu? Je hao watu ni special one? Mimi nina sema hapa ni kwamba tumesahau au tumekataa maarifa na tukakubali kuwa tunasimuliwa na kuwa sio watendaji.
Kwa wale mnaosoma biblia (Hosea 4:6 inasema "Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa....."). Inamaana watu wamekosa maarifa ndio maana waenda tu bila kujua nini cha kufanya.

Nguvu yetu ya kufanya makubwa ipo ndani ya nafsi zetu (Consciousness). Au ninaweza kusema sisi watu tunaishi katika ulimwengu wa aina mbili(Ulimwengu wa damu na nyama pia Ulimwengu wa kiroho). Sasa ulimwengu wa kiroho ndio unaguvu na ndio chanzo za nguvu zote. Na ndio uhalisia wetu sisi na ndio reality yetu sisi.

Sasa basi kiwango cha kutumia nguvu au kuwasiliana na nafsi zetu unapungua kadri umri wetu unaposogea. Mtoto anapozaliwa asilimia kubwa sana anakuwa yupo pamoja na nafsi ya ili tatizo lake anakuwa ni mgeni duniani hajui kuongea hajui chochote kilichopo duniani. Kwamaana hiyo hawezi akafikisha ujumbe wowote. Lakini kwakuwa tumekosa maarifa mtoto anapoanza kukua tunaanza kumfundisha vitu vya dunia tu na kusahau asili ya ni nini. Jambo hilo ninamfanya huyo mtoto awe mbali na nafsi yake. Kadri anavyo zidi kukua anazidi kuwa mbali.

Njia yakuweza kuwasiliana na nafsi zetu ni kuhakikisha tunafunga milango ya fahamu ya miili yetu (macho, masikio, mawazo, ngozi nk). Tunapofunga milango hiyo ya fahamu ndio tunakuwa na uwezo wa kuanza kuwasiliana na nafsi zetu.
Kwa wale wasomaji wa biblia: (mathayo 6:6 "
Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi.")

Jambo kubwa ninalojaribu kuongea hapa ni kuwaweka sawa waumini wa dini ya kikristo waelewe ni mambo gani yameandikwa kwenye kitabu chao na kwanini hawayafuati.

Njia ili uweze kuwasilina na nafsi yako kwa ufupi ni kufanya meditation (Sina neno zuri la kiswahili). Hii ndio njia bora ya kuweza kuwasilian na nafsi. Kadir unavyozidi kufanya meditation unzidi kupata uwezo mkubwa wa kufanya mambo hapa duniani.
Asilimia zote za watu waliofanikiwa au wanaofanikiwa hapa duniani wanafanya meditation.
Joshua 1:8
This Book of the Law shall not depart from your mouth, but you shall meditate on it day and night, so that you may be careful to do according to all that is written in it. For then you will make your way prosperous, and then you will have good success.
Genesis 24:63 And Isaac went out to meditate in the field toward evening. And he lifted up his eyes and saw, and behold, there were camels coming.
Psalms 119:97 Oh how I love your law! It is my meditation all the day.

Kwa hiyo meditation ndio njia nzuri ya kuweza kuwasilina na nafsi zetu.
Unajua sisi tunauwezo wa uungu ndani yetu? Unajua tunauwezo wakufanya mambo makubwa na dunia yetu ikawa sehemu nzuri ya kuishi? Sisi ni gods na tuna nguvu ya kuitwa gods na ni kweli sisi ni gods Zaburi 82:6 "
Mimi nimesema, Ndinyi miungu, Na wana wa Aliye juu, nyote pia."

Utafanya nini ukikaa katika nchi ya watu walio na uwezo na unaona kabisa wanauwezo lakini wanalia shida? Je utawaacha tu hivyo au utawafundisha namna gani walivyo na uwezo? Ni mawili hapo. Ukiwafundisha watajitambua na utakosa watumwa kwa sababu unafurahia wao kuwa watumwa wako. Utawajaza vitu vingi vya ajabu na kuwafanya wakutegemeewewe. Jambo la pili utawafundisha ili waweze kujitambua na kuleta amani katika jamii hiyo kwa kuwa hakutakuwa na tofauti maana watu wanajitambua na wanaelewa wao ni nani.

Je hili jambo la pili linafanyika sasa. La hasha hawataki kabisa wanatufundisha makanisani kuhusu utoaji wa sadaka na kuwa waadilifu ilituweze kwenda mbiguni. Jambo ambalo ni tofauti lkabisa na inavyotakiwa.

Ninayo mengi sana ya kuweza kuongea nanyi rafiki zangu. Lakini hebu niweke kalamu yangu chini na niwaache nanyie muweze kuusoma waraka huu na kuniuliza maswali. Na mimi nitakuwa tayari kujibu inaweza kuwa siyo yote nitajimbu maswali yaliyo ya msingi.

By Annael
EDUCATION IS POWER


Hakuna cha meditation, muujiza huitaji imani yako kwa yule aliyekuahidi kuutenda.
Miujiza huonyesha yenye unayemtumikia anaishi, na yupo katika utawala, ni muhimu kwa kumthibitisha mpakwa mafuta wa Mungu, kikubwa ni lazima itanguliwe na habari njema ya Kristo, angalizo :sikusema neno la Mungu, kwa sababu huwezi hubiri torati ya Musa unategemea miujiza, utakesha.
Luka 7: 19 aliwatuma kwa Bwana wamwulize: "Wewe ndiye yule
ajaye, au tumtazamie mwingine?" 20 Wale wanafunzi walipomfikia
Yesu wakamwambia, "Yohane Mbatizaji ametutuma kwako
tukuulize: Wewe ndiye yule ajaye, au tumtazamie mwingine?"
21 Wakati huohuo, Yesu alikuwa anawaponya watu wengi
waliokuwa wanateseka kwa magonjwa na waliopagawa na pepo
wabaya, akawawezesha vipofu wengi kuona tena. 22 Basi, Yesu
akawajibu, "Nendeni mkamwambie Yohane yale mliyojionea na
kuyasikia: vipofu wanaona, viwete wanatembea, wenye ukoma
wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, na maskini
wanahubiriwa Habari njema. 23 Heri mtu yule ambaye hana
mashaka nami!"
 
Ninaheshimu dini ya mtu yeyote. Lakini ukweli lazima tuuseme (Hakuna kitu kinachoitwa mungu wala shetani).
Unajua kifungo cha dini ni kibaya sana kuliko vifungo vyote. Ningekuomba uwe na fikra huru.

Mkuu unataka kusema hufaham chochote kuhusu shetani?
Jini jee?
 
Kuna thread hapa nitaileta inaongelea kabla ya kuzaliwa hapa duniani mtu alikuwa yukoje na baada ya kufa hapa duniani anakuwa yupoje. Nadani katika hiyo thread nitajibu maswali yako yote. Maana ni somo lefu na lina practicals zake.


Uniite plz utaitoa lini?
 
Unaongelea mungu yupi huyo mwenye upendo? mungu gani huyo unayemwongelea anawaacha watu wa africa ya kusini kuuwa wenzao. Upendo gani huo anasema eti atawahukumu watu milele wakati maisha ya kuishi duniani ni chini ya miaka mia. Huoni kuwa ni kipindi kidogo sana cha kuishi?
mungu unayemtaja hapa hayupo ni elimu uliyolishwa na waleeee ili wakutawale vizuri.

ingekuwa Mungu anawapangia watu ya kufanya,basi binadamu tungefanana na malaika na waovu wangeangamizwa,ila dunia ina mchanganyiko wa watu waovu na wema na wote wanaishi katika viwango vyote vya maisha(kuna waovu maskini na wanyonge pia wapo waovu matajiri,kuna wema matajiri na wapo wema hao hao maskini) mwanadamu kaumbwa kwa nafsi huru ambayo yeye mwenyewe huamua kuijaza na kipi aidha kuijaza na takataka kama hizo zako za kutenda miujiza,kujitukuzia uungu kwa kutenda makuu,au nafsi hiyo ikaamua kufungamana na Mwenyezi Mungu,kwamba taswira ya utukufu wa Mwenyezi Mungu ikaonekana katika maisha yetu hapa duniani,wananchi wa s.africa kuuana hilo ni kusudio la nafsi zao la kiburi na majivuno,Mwenyezi Mungu wa kweli siyo Mungu wa fujo,huonesha utukufu wake kwa kusudio maalum la kuwakumbusha wanadaam kuwa yeye ndiye wa kweli na wa pekee,rejea pale pote ambapo Mungu alijidhihirisha kwa wanadamu kwenye maandiko,alipowasaidia waisrael katika vita,alipowatoa utumwani misri na kwingine pote,kusudio ni kuwaonesha wanadamu kuwa ni yeye wa pekee,lakini hakumlazimisha mtu kumuabudu,bali kila mmoja kwa matashi yake amwabudu kwa upendo usiopimika,naomba niishie hapo,nachoka kuandika kwa kutumia simu.i
 
Mkuu unataka kusema hufaham chochote kuhusu shetani?
Jini jee?
Kweli kuna roho zipo katika ulimwengu wa roho. Lakini kwa jinsi vinavyotajwa hapa duniani wakati mwingine ni hadith. Nimeahidi katika thread inayokuja nitaongelea baada ya kufa mtu anaenda katika evolution ipi kulingana na sababu ambazo nitakuja kuzieleza na kutoa practical ili tuweze kujaribu.
 
Hahahahahaaaaaaa! :tape:

So unataka kusema wakiristo ni tatizo ila biblia iko sahihi?

Na ikiwa biblia ndio chanzo cha hayo matatizo kwanini unaitumia kama reference kusapoti madai yako????

Ivi unaichukuliaje biblia?

Ndugu maswali mazuri sana,mtoa mada anaweweseka hajui ganachokisema kama ulishasema kitu hakifahi iweje leo ukilink na mambo yako ya Education power link mambo yako na Wakina Plato,Alistoto and Newton.Hacha kutoana sisi hatuna uwezo wa kufikiri km meditation Wachina na Wajapani wanafanya sana lakini nothing new on it.Kama wewe si Mkristo na haupendi Ukristo kamwe huwezi ukatumia maandiko yke kutufundisha u west ur time.
 
Biblia ni kama vitabu vingine vya hadith za kale. Unajua ukitaka kuishi na kupata watu kutoka kwenye jamii fulani fanana nao kwa kitambo. Hatimaye waeleze ukweli kuwa hakuna kitu kinachoitwa mungu duniani, mungu kaumbwa na watu na sio kuwa mungu kawaumba watu. Kwa sababu watu hao wamefungwa na vifungo vya imani. Ni vyema kuwapa elimu kidogo kidogo mwisho wa siku somo litaeleweka na kuiweka dunia kuwa mahali salama kwa watu wote. Hii ndio ninayo isema NWO lazima elimu ipite kwanza na ndipo tutakapofikia kipindi cha kuweka silaha chini na kuwa kitu kimoja. Laki ni sharti mambo ya dini yafe kabisaaaaa.

Hapana hapa UMEKUFURU kabisa. The world is lead by almighty power which is God!! Kama sio hakuna binadamu angeweza kuwa na meditation power. Ulimwengu umaweza ukakuruhusu uingie kwenye ulimwengu wa kiroho kwa meditation ila huwezi fanya makuu ya kubadili maumbile au kuhamisha tungamo. unaweza kukerakera tu. HIVYO KUNA MAMLAKA ILIO JUU ZAIDI
 
Sihitaji kusubiri thread nyingine kupata majibu ya maswali madogo tu kama hayo...

Tafadhali nipatie majibu, nipo jamvini hapa 24/7...

Waiting...

Kuna thread hapa nitaileta inaongelea kabla ya kuzaliwa hapa duniani mtu alikuwa yukoje na baada ya kufa hapa duniani anakuwa yupoje. Nadani katika hiyo thread nitajibu maswali yako yote. Maana ni somo lefu na lina practicals zake.
 
Back
Top Bottom