Jinsi ya kukokotoa Ongezeko la Asilimia Mshahara!

Jinsi ya kukokotoa Ongezeko la Asilimia Mshahara!

Barua imesema "ikiwemo kima cha chini" na sio "ni kwa kimo cha chini" maana yake ni wote, soma paragraph ya kwanzaView attachment 2224480

Tanzania haina Mapato ya kubeba ongezeko la Mishahara yote kwa asilimia 23.3%
Thread starterFumadilu Kalimanzila Start date57 minutes ago Tags asilimia kubeba mapato mishahara ongezeko tanzania
1 of 3
Next
Last
F
Fumadilu Kalimanzila
JF-Expert Member
57 minutes ago
#1
Ukisoma vizuri kitabu cha WHY NATIONS FAIL ( The Origins of Power,Prosperity & Poverty) cha DARON ACEMOGLU na JAMES A.ROBINSON utajua kwa uhakika ni kwa nini Tanzania yetu ni masikini hivi na itachukua muda mrefu kubadili hali hii.

Kwa ufupi ni kwamba tunacho kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya maendeleo katika Nchi yetu kasoro watu wenye maarifa na taasisi imara.

Hata watu wachache wenye maarifa tulionao pia wana maarifa yaliyopitwa na wakati (obsolete) au waliyo karirishwa tu! Tunaweza kusema maarifa yao hayo ni USELESS KNOWLEDGE tu.

Nchi bila uzalishaji na kuingiza Nguvu kazi kubwa katika uzalishaji ili kuongeza tija ni kazi bure tu.

Viongozi wetu na wachumi wetu waliwasoma akina Adam Smith kwenye THE WEALTH OF NATIONS kwa ajili ya kukariri kujibia mitihani tu!

Watu wetu hata wasomi wakubwa hawajui kutafsiri hata vitu basic kabisa!

Watu wanaambiwa kima cha chini la Mshahara kimeongezeka kwa asilimia 23.3% ,wao wanakimbilia Rais ameongeza Mishahara kwa asilimia 23.3% ( akili za Ki- Mwijaku Mwijaku)!

Jiulize kwanza kama Mishahara itaongezwa kwa asilimia 23.3% yote ,Wage Bill yetu itakuwa Shilingi ngapi?!

Wage Bill ikifika bilioni 900 kwa mwezi na madeni tunayolipa kwa mwezi ni bilioni 900 wakati Mapato yetu kwa mwezi Trilioni 1.5 ( bilioni 1500) Nchi itakwendaje?!

Ukitaka kujua Nchi hii ina tatizo kubwa katika Wealth Creation angalia utitiri wa tozo katika mafuta!

Kwahiyo ukifuatilia sasa mjadala ni asilimia 23.3% ya ongezeko la Mishahara ni kwa kima cha chini pekee au Mishahara yote!
 
hujui chochote kuhusu ongezeko la mishahara wewe kama hujui hesabu za range and function hapa ndo mahali pake sasa

Haya sema ongezeko la asilimia ya mshahara linakokotolewa vipi ? Mambo ya functions yanaingiaje hapa ? Hii ni simple arithmetic tu ya kukotoa asilimia, ukijua mshahara unaolipwa na ukajua asilimia uliongezwa unaweza kukokotoa kiasi ulichoongezwa kwenye mshahara wako, sasa mambo ya range yanatokea wapi ?
 
Duh, ndio nini hiki?
Kwanini unafanya mambo kuwa magumu?

Kama nyongeza ni 23% si ni rahisi tu?
Kama unalipwa
Basic Salary 1,000,000/=
Mshahara wako Mpya ni 1,230,000/= nini kuwa chosha watu?

Easy take basic salary x 0.23 then jibu jumlisha na Basic Salary! Thats will be ur new Salary if things will work as it is stated.

Kwani tofauti ya ulichoandika na nilichoandika ni ipi au labda haujasoma (vizuri) nilichoandika ?
 
Jamani kaongeza kwa wooteee. Rudieni msome vzr "Rais ameridhia ongezeko mapendekezo ya ongezeko la mshahara ikiwemo kimo cha chini kwa watumishi wa umma kwa 23.3%" so ni wote ikiwemo hao kima cha chini.
 
Tanzania imejaa vi.laza ndio maana wanasiasa wanatamba sana! Kama mshahara umeongezeka kwa asilimia 23% kwa mishahara yote, je kuna haja gani ya kusema Rais ameridhia ongezeko la 23% ya kima cha chini cha Mshahara!
Kama ni kwa wote si wangesema tu Serikali imeongeza mishahara kwa asilimia 23%.
Ngojeni akina Mrisho Mpoto na Mwijaku waje wawaeleweshe ndo mtawaelewa vizuri.
Wakiambiwa wajiendeleze kielimu wanabisha alafu kwenye discussion kama hizi wanakurupukaaa tu 🤣🤣
 
Duh, ndio nini hiki?
Kwanini unafanya mambo kuwa magumu?

Kama nyongeza ni 23% si ni rahisi tu?
Kama unalipwa
Basic Salary 1,000,000/=
Mshahara wako Mpya ni 1,230,000/= nini kuwa chosha watu?

Easy take basic salary x 0.23 then jibu jumlisha na Basic Salary! Thats will be ur new Salary if things will work as it is stated.
Hapana sio hivyo ndugu. Kadri mshahara unavyozidi kuongezeka kutoka kima cha chini, percent inapungua.
 
Kwa wale waliokuwa na kima Cha chini wewe tulia kwanza 🤣🤣🤣
... nadhani ni kwa wote ila sio flate rate kwa wote; ita-range. Kwa mfano inaweza kuwa 23.3% (kima cha chini) hadi 5% (kima cha juu). Wanaweza kufanya kama ifuatavyo;
  • TZS 270,000 hadi 350,000 ongezeko 23.3%
  • Zaidi ya 350,000 hadi 800,000 - 12%
  • Zaidi ya 800,000 hadi 1,500,000 - 10%
  • Zaidi ya 1,500,000 - 5%
Nadhani huwa wanaangalia ni wapi penye group kubwa in terms of grand total gross salaries na kujaribu kupaminya zaidi ili kutoathiri mapato ya serikali kwa kiasi kikubwa.

Kwa mfano gross kubwa most likely itakuwa kati ya 350,000 hadi 800,000 ambapo ndipo watumishi wengi wanaangukia (walimu, polisi, n.k.) utaona gap la % kutoka min. increase ni kubwa kuliko ma-gap mengine. Unaweza kukuta hili kundi linachota zaidi ya 70% ya mishahara; ukiruhusu na lenyewe lipate 23.3% hazina itakauka.
 
Huo mshahara huwa unaongezeka kwa formula ya reducing balance yaani kadri daraja la mshahara linavyopanda kwenda asilimia ya nyongeza hupungua na kadri daraja linavyopanda dogo asilimia ya nyongeza huongezeka kwa hiyo asilimia 23.3 siyo ya wenye TGTS G,H,I nk hiyo siyo yao asilimia yao inaweza kuwa hata 12%tu
 
Hapo chukua mshahara wa kima cha chini 300,000 × 23% =69,000
Kwa hiyo hapo watumishi wote wataongezewa 69,000 kwenye mishahara yao
Tafuta 23.3 ya mshahara wako, baada ya hapo jibu lako utaongeza na mshahara wako wa awali.

Eg. (300,000/- msh.) = 100%

X = 23.3

X. = 69,900/- ongezeko

:°• (300,000/- )+( 69,900) = 369900/-


369900 ndio mshahara baada ya ongezeko.
 
Nimeona wengi wanauliza nikaona nianzishe uzi labda kusaidia, ni hivi chukua asilimia ya kilichoongezwa mf. 28% gawanya kwa 100 yaani 28:100 halafu zidisha na Mshahara wako, yaani 0.28*(mshahar wako kabla ya kodi)= halafu jibu lake jumlisha tena na Mshahara wako, jibu lake ndiyo kiwango ulichoongezwa.

Huo mshahara kabla ya Kodi ndio ukokotoe!

Njia rahisi la kupata mshahara mpya kwa wale wa Mshahara wa Kima cha Chini ni kuzidisha Mshahara wako kwa 1.233 unapata jibu
 
Watumidhi wa secta binafsi mbona hawajapewa muongozo au haiwahisu hii?
 
Nimeona wengi wanauliza nikaona nianzishe uzi labda kusaidia, ni hivi chukua asilimia ya kilichoongezwa mf. 28% gawanya kwa 100 yaani 28:100 halafu zidisha na Mshahara wako, yaani 0.28*(mshahar wako kabla ya kodi)= halafu jibu lake jumlisha tena na Mshahara wako, jibu lake ndiyo kiwango ulichoongezwa.

Huo mshahara kabla ya Kodi ndio ukokotoe!
Hivi hili ongezeko ni kwa wa kima cha chini pekee!?
 
Hii ni siri ya watumishi wetu!, calculation ya mshahara wao watajua pindi wakiiupokea, usishangae kuna watu wataongezewa elfu 10
Ni kweli lakini formula inabaki kuwa hiyo. Unaweka tu hiyo percentage increment accordingly
 
Tafuta 23.3 ya mshahara wako, baada ya hapo jibu lako utaongeza na mshahara wako wa awali.

Eg. (300,000/- msh.) = 100%

X = 23.3

X. = 69,900/- ongezeko

:°• (300,000/- )+( 69,900) = 369900/-


369900 ndio mshahara baada ya ongezeko.
Mkuu
Kama ni hivyo
KWA wenye basic ya
940000=100%
X=23.3%
X=219020
Then
940000+219020=1159020/=
Impossible
Another approach
LABDA
 
Naona watu wanapoteza tu muda kubashiri mshahara mpya.. tuusubili mwezi julai tarehe 15 tutajua hali halisi..so tuwe wavumilivu kubashiri ni kupoteza muda
 
Mkuu
ACHA uongo
Yaani iwe hivi!!?
23/100=0.233
0.233×940000/= =219020/= ?
HALAFU
940000+219020= 1,159,020/= ?
KWA wale wenye TGTS E?
Haiwezekani we Jamaa!!??
Kwa mtu wa mshahara huo net Ongezeko ni around Tsh. 102,000/=
Kama una Deni la Hslb na mengine Yale ya kasaida Kama bima.
 
Back
Top Bottom