labda atuambie baba wa mtoto ana maamuzi gani juu ya malezi ya mtoto wake, wakati naolewa mwanaume aliniambia kabisa kwamba ana mtoto na angependa aanze kuishi nae coz wakati huo alikuwa anaishi kwa bibi yake, tulikubaliana na sijawahi kujutia maamuzi yangu ya kumlea huyo mtoto, baba mtu hajawahi kulalamika na malezi yangu hata kidogo na raha zaidi ni kwamba binti amekuwa rafiki yangu wa karibu sana sana, kwahiyo inategemea na maamuzi ya wenye huyo mtoto (baba&mama) wana maamuzi gani juu ya malezi ya mwanao, ni watoto kama hao wetu tuliowabeba miezi tisa, wanakosea/warekebishwe kama hao wetu, tuwapende kama tunavyowapenda hao wetu, tuwapende kama tunavyowapenda baba zao(waume zetu).