Steven Sambali
JF-Expert Member
- Jul 31, 2008
- 364
- 182
Wengi wameandika kuhusu kuangalia sayari zkuanzia jana ila hawajaweka urahisi wa jinsi ya kuziona kwa macho pale anga likiwa jeupe bila mawingu.
Nitatoa maelezo kidogo ili kuwasaidia wengi waweze kuziona.
Haya maelezo ni kwa wale wapo karibu na Ikweta zaidi. Ukiwa mbali na Ikweta basi utaona picha kidogo tofauti.
1. Tofauti ya NYOTA na SAYARI ni kwamba, mwanga wa nyota unachezacheza na kubadili rangi wakati mwanga wa sayari haubadiliki Kama ilivyo kwa Mwezi.
2. Sayari zote zinapita kwenye mstari ambapo JUA linapita. Hivyo angalia tu kwenye mstari, JUA kwa sasa linapipita. HII pia ni kwa wale ambao hawapo Ikweta.
3. Sayari kubwa au zilizopo karibu na Dunia ndiyo zinaonekana vizuri. Kwa maana hiyo Basi:
I. Sayari ya Venus ndiyo inaonekana kubwa zaidi na kung'aa kupita zote kwa sababu ipo karkbu na Dunia. Ila siyo kubwa kuzidi hizo nyingine.
Ii. Sayari ya Jupiter inafuatia kwa ukubwa kuonekana na kung'aa usiku. Jupiter pia ni moja ya sayari kubwa sana angani.
Iii. Sayari ya Saturn hazipishani na MARS kwa ukubwa. Saturn iko mbali ila ukiongeza na Pete yake, inakuwa kubwa sana na hivyo kuonekana vema usiku.
IV. Sayari ya Mars pia inaonekana vema jioni ya leo. Ukiangalia vizuri utagundua Ina wekundu fulani. Waweza kufumba macho na kufungua haraka ukiangalia utaona RED PLANET. Udongo wake ni mwekundu na hivyo unaweza kuona hiyo rangi.
Kwa kuangalia jua linatoka saa ngapi na ikifika saa fulani litakuwa wapi, nitakuwekeeni Link ili kila Mtu atafute kwa Mkoa au sehemu alipo, Sayari zitatoka saa ngapi na kuzama saa ngapi.
Kwa mfano sayari ikitoka saa 6 Mchana basi unategemea kuwa kwa watu wa Ikweta, ikifika jioni saa 12, sayari itakuwa imefika utosini yaani Kama ni jua ni saa Sita Mchana.
Sayari ikitoka saa 10 jioni basi jua linapozama, sayari inakuwa usawa wa jua la saa mbili asubuhi.
Hii itawasaidia kujua hizo sayari zitakuwa usawa gani.
Kwa kuongeza tu, waweza pia angalia zile nyota tatu zilizopangana kwa urefu Sawa na zinaitwa ORION au Muwindaji.
Hizi utaona pembeni yake kuna nyota mbili kubwa kushoto na kulia na kwa Ikweta, juu yake kuna nyota kubwa inawaka sana inaitwa SIRIUS. Hapo SIRIUS Kuna vinyota viwili vidogo na kengine kadogo zaidi ambako NASA wameshakaona. Kanyota hako ndipo Kabila la Dogoni kutoka nchi ya MALI wanadai wanatoka..
Hii ni habari nyingine ndefu zaidi...
Kujua Link ya sayari kutoka na kuzama nii hapa. Kila Mtu aandike Mkoa alipo ili iwe rahisi kupata usahihi.
Hii chini kwa Mkoa wa Dar es salaam. Kuna sehemu unaandika Mkoa na unabadilisha.
www.timeanddate.com
Nyota mbili zinazoonekana kwenye Orion, moja ni inaonekana Nyeupe inaitwa RIGEL na nyingine inaitwa BETELGEUSE. Waweza kuona ukubwa wake ukilinganisha na ukubwa wa Jua. Hizo nyota ni kubwa kuliko Sayari zote na jua letu.
Haya subirini JIONI muone.sayari..
Nitatoa maelezo kidogo ili kuwasaidia wengi waweze kuziona.
Haya maelezo ni kwa wale wapo karibu na Ikweta zaidi. Ukiwa mbali na Ikweta basi utaona picha kidogo tofauti.
1. Tofauti ya NYOTA na SAYARI ni kwamba, mwanga wa nyota unachezacheza na kubadili rangi wakati mwanga wa sayari haubadiliki Kama ilivyo kwa Mwezi.
2. Sayari zote zinapita kwenye mstari ambapo JUA linapita. Hivyo angalia tu kwenye mstari, JUA kwa sasa linapipita. HII pia ni kwa wale ambao hawapo Ikweta.
3. Sayari kubwa au zilizopo karibu na Dunia ndiyo zinaonekana vizuri. Kwa maana hiyo Basi:
I. Sayari ya Venus ndiyo inaonekana kubwa zaidi na kung'aa kupita zote kwa sababu ipo karkbu na Dunia. Ila siyo kubwa kuzidi hizo nyingine.
Ii. Sayari ya Jupiter inafuatia kwa ukubwa kuonekana na kung'aa usiku. Jupiter pia ni moja ya sayari kubwa sana angani.
Iii. Sayari ya Saturn hazipishani na MARS kwa ukubwa. Saturn iko mbali ila ukiongeza na Pete yake, inakuwa kubwa sana na hivyo kuonekana vema usiku.
IV. Sayari ya Mars pia inaonekana vema jioni ya leo. Ukiangalia vizuri utagundua Ina wekundu fulani. Waweza kufumba macho na kufungua haraka ukiangalia utaona RED PLANET. Udongo wake ni mwekundu na hivyo unaweza kuona hiyo rangi.
Kwa kuangalia jua linatoka saa ngapi na ikifika saa fulani litakuwa wapi, nitakuwekeeni Link ili kila Mtu atafute kwa Mkoa au sehemu alipo, Sayari zitatoka saa ngapi na kuzama saa ngapi.
Kwa mfano sayari ikitoka saa 6 Mchana basi unategemea kuwa kwa watu wa Ikweta, ikifika jioni saa 12, sayari itakuwa imefika utosini yaani Kama ni jua ni saa Sita Mchana.
Sayari ikitoka saa 10 jioni basi jua linapozama, sayari inakuwa usawa wa jua la saa mbili asubuhi.
Hii itawasaidia kujua hizo sayari zitakuwa usawa gani.
Kwa kuongeza tu, waweza pia angalia zile nyota tatu zilizopangana kwa urefu Sawa na zinaitwa ORION au Muwindaji.
Hizi utaona pembeni yake kuna nyota mbili kubwa kushoto na kulia na kwa Ikweta, juu yake kuna nyota kubwa inawaka sana inaitwa SIRIUS. Hapo SIRIUS Kuna vinyota viwili vidogo na kengine kadogo zaidi ambako NASA wameshakaona. Kanyota hako ndipo Kabila la Dogoni kutoka nchi ya MALI wanadai wanatoka..
Hii ni habari nyingine ndefu zaidi...
Kujua Link ya sayari kutoka na kuzama nii hapa. Kila Mtu aandike Mkoa alipo ili iwe rahisi kupata usahihi.
Hii chini kwa Mkoa wa Dar es salaam. Kuna sehemu unaandika Mkoa na unabadilisha.
Which Planets Can You See Tonight?
Choose tonight or another date and see which planets are shining in the sky above you or anywhere else.
Nyota mbili zinazoonekana kwenye Orion, moja ni inaonekana Nyeupe inaitwa RIGEL na nyingine inaitwa BETELGEUSE. Waweza kuona ukubwa wake ukilinganisha na ukubwa wa Jua. Hizo nyota ni kubwa kuliko Sayari zote na jua letu.
Haya subirini JIONI muone.sayari..
Attachments
-
Screenshot_2025-01-25-20-41-27-983_com.noctuasoftware.stellarium_free-edit.jpg238.8 KB · Views: 6 -
Screenshot_2025-01-25-20-26-19-469_com.noctuasoftware.stellarium_free.jpg427.5 KB · Views: 5 -
Screenshot_2025-01-26-11-53-53-106_com.whatsapp-edit.jpg374 KB · Views: 5 -
Screenshot_2025-01-26-11-54-28-604_com.whatsapp-edit.jpg486 KB · Views: 4