Jinsi ya kuondoa au kupunguza mafuta tumboni kwa wanawake (Vitambi vya kike)

Jinsi ya kuondoa au kupunguza mafuta tumboni kwa wanawake (Vitambi vya kike)

mkuu, ungeweka na picha ya tumbo lako basi
tuone effect ya hii diet katika kupunguza kitambi. Au waonaje?
Halafu hilo bakuli la ndizi limenitamanisha kweli,
leo lazima nifanye mpango. Asante sana mkuu
mmmh wewe mwali una yako. Ni tumbo tu wataka kuona au?funguka mama
 
Mkuu nakupa big up saaaaana maji ya moto hapo kwangu ndio tatizo, ila ngoja nijaribu
 
maji uyanywe kila siku au kwa muda fulani maana maji ya asubuhi mzeee kama smile vile na jingine huo mtindi uwe umeondolewa mafuta au ule wenye mafuta...
 
Asante mzizimkavu, binafsi nitajaribu ila hata mimi maji ya uvuguvugu nakunywa sana lakini sioni tumbo kupungua wala nini, nitajaribu na hayo mengine, Tumbo linanikosesha raha kwakweli!
 
1. Hapo penye red ndo mzizi mkuu wa mada hiii

2. Changanya na za kwako
Hii sio ya kitaalamu bali ni mimi ninavyofanya na ndio inayonisaidia kupunguza tumbo.
Kwasababu vitu vya formula mimi huwa siwezi kuvifuata na huwa naviona vigumu sana kwahiyo huwa najaribu kuishi vile ninavyoweza.

Na kizuri zaidi ni kwamba hii sio diet ya kujinyima.
Ila unaweza usifanikiwe pia kutokana na mwili wako kwakua tumeumbwa tofauti lakini unaweza kujaribu kama itafanya kazi

Tukianza na asubuhi nikiamka mimi kama Mzizimkavu, naanza kunywa maji glass 3 ya Uvugu vugu kabla ya kupiga mswaki.
Na nikiisha amka nakunywa maji ya uvugu vugu yaliokamuliwa ndimu au limao glass zingine tatu kabla ya kunywa Chai.
Ukizoea maji ni matamu kuliko hata Bia
Kuwa Teja wa Maji kuna raha yake pia

Mimi napenda vitu vichachu kwahiyo maji saa zingine naya hisi kama yamepooza ila nikikamulia ndimu/limao kwenye maji ya uvuguvugu hata nisipoweka sukari yanaleta ladha fulani hivi
Ukiweza kunywa maji ya uvugu vugu kila wakati unapohisi kiu ya maji itakuwa vizuri au hata mara tatu kwa siku angalau

Si mpenzi sana wa Chai kwakuwa sipendi kabisa vitu vya sukari, lakini siku ninapo amua kunywa chai huwa nakunywa yenye tangazwizi nyingi sana na badala ya kutumia sukari huwa naweka asali...... Ila unaweza kutumia viungo vingine mbali mbali vya ki pwani (masala)


Asali


Kwa kifungua kinywa Sausage za kuchemsha au kama utakaanga iwe kwa mafuta yasiozidi kijiko kimoja kikubwa cha kulia (nashauri ya alizeti au olive)

Mayai ya kuchemsha si mabaya pia kwa kufungua kinywa
Kumbuka mimi huwa sifanyi diet hivi ndivyo ninavyokula na inasaidia

Badala ya kutafuna Sambusa, Popcorn na cookies au chocolate kila wakati bora muda wako uelekeze kwenye matunda, kama huwezi kupitisha lisaa bila kuweka kitu mdomoni


Mchana unaweza kupiga bakuli la mchemsho wa ndizi, ziwe Bukoba au za kule kwetu Moshi zote sawa kwakuwa mchemsho hauna mafuta kabisa unajilia kadri utakavyotosheka

Kuku Choma ni chakula kingine ambacho kinanifaa nyakati za mchana, lakini haswa hupendelea Kuku wa kienyeji ambao hawakukuzwa kwa madawa
Mara nyingi usiku naipotezea tu, pengine nalalia glass 2 za wine au beer kadhaa zisizozidi 3
Au Kuku wa kienyeji wa kuchemsha aliewekwa chumvi na ndimu na ka ndizi kamoja ka kuchemsha au kukaanga kwa mafuta kidogo sana


Ugali naupenda sana na huwa najiachia nao siku za kujiharibu
Lakini kumbuka wanga sio kitu cha kukiendekeza sana hasa unapotaka kutoa kitambi
Nikiona kinachomoza, napunguza maswala ya ugali.
Japo kwangu ni ngumu siku ipite bila Ugali, ila kumbuka miili inatofautiana... naweza nikala ugali mwaka mzima mwingine akala wiki akafumuka
So usinifatishe ila jaribu kupunguza au uepuke kama utaweza

Tumbo liko hapa sasa!!!!!
Hili ndio tatizo lililonikuta mpaka mkaona ile ishu imechomoka siku ya Birthday yangu


Kwakweli chips ni tamu hasa kwa sisi tunaofanya kazi za usiku ukirudi umejichokea unavamia tu



Unakuta unafululiza hata mwezi unazila kisha unaenda kulala
Japo tunapenda chips vumbi ila tuwe na kipimo isizidi, isiwe kila siku
Ukijumlisha na bia, daaah!! dah!!!!!! dah!!!!! shughuli imeisha



No. 1 enemy kwa vitambi vya wanawake ni hii kitu
Kula angalau mara moja kwa wiki tafadhali kama huwezi kuacha kabisa




Wenye kuweza kufanya sit ups pia fanyeni japo najua mazoezi ni magumu sana na yanatia uvivu hasa unapokuwa na kazi nyingi



Maji ni kitu cha lazima na cha kila siku
Ukiweza kunywa maji ya uvuguvugu Asubuhi, Mchana na Usiku utafanikiwa japo kidogo



Narudia hii sio Diet ya kitaalam ni jinsi ninavyo ishi mimi, jaribu kama utaweza kufanikiwa kwa wale walioniomba ushauri.
Ila kama mwili wako ni mkubwa sana pia jaribu kupunguza kipimo cha chakula unachokula kila siku, ila usijinyime sana.

Mboga mboga kibao kila siku ukiamua mchana na jioni. Ni muhimu sana

Lady Jay Dee: JINSI YA KUUTUNZA MWILI KUPUNGUZA TUMBO NA KUPUNGUZA MAFUTA.........KUNAHITAJI VITU VINGI TOFAUTI NA VYA ZIADA ILI KUPATA SHAPE UNAYOIPENDA





 
nashukuru nimeweza kuacha chips,
ila maji ya uvuguvugu yananipa uvivu kunywa, nitaanza sasa........i hope sitakatisha......
 
Je kuna tatizo mtu akinywa tangawizi kwa wingi? Mie napenda sana tangawizi iliyochanganywa na asali, naweza kunywa mugs nne kwa siku. Je naweza kudhurika?
 
Ahsante mkuu kwa ushauri bomba

Matunda yanasaidia sana chakula kusambazwa katika sehemu zote za mwili taratibu na kwa ufanisi pamoja na kusafiri na chakula ambacho hakijameng'enywa kwa njia ya haja kubwa hivyo kupunguza uwezekano wa kupata kitambi. Chakula jamii ya mikunde mikunde inasaidia sana. .(Search Dietary Fiber)

Ila hapo kaka kwenye mayai, yasiwe mengi kwakuwa yana cholesterol na avidin(husababisha vitamin B7 isisambazwe mwilini) hivyo unaweza sababisha matatizo mengine. Mafuta ni muhimu kwakuwa yanasaidia kazi za cell na kulipumzisha ini kutengeneza mafuta mwilini.

Big up mkuu, nina jamaa hapa yeye ulaji wake sio kivile sana sana anapenda mabiscuit, chocolate kwa ufupi kwake kula sio issue lakini tumbo hilo...
 
sasa mzizi umewagusa wanene na wenye vitambi,je na sisi wembamba tule nini tuwe wanene jamani yaan huu mwili hauna shukrani nakula kitu lakin sinenepi kwann?
 
Ukishindwa kunywa Maji ya Uvuguvugu na Asali kijiko kimoja na limau moja kubwa wakati wa asubuhi unapo amka kunywa Glasi moja ya Mtindi kila asubuhi mchana na usiku kwa muda wa miezi 6 utapunguwa huo unene.

Mkuu ahsante kwa darasa lako zuri,
Binafsi nahitaji saana kupungua hususan kitambi, maji kwa asubuhi huweza kunywa isizidi glass moja na hukojoa mara kwa mara. Mtindi nikinywa tumbo hunivuruga haraka saana ambapo hupelekea mchafuko na kuharisha si zaidi ya saa moja tangu nimekunywa mtindi. Muongozo wako inshallah.
 
Mkuu ahsante kwa darasa lako zuri,
Binafsi nahitaji saana kupungua hususan kitambi, maji kwa asubuhi huweza kunywa isizidi glass moja na hukojoa mara kwa mara. Mtindi nikinywa tumbo hunivuruga haraka saana ambapo hupelekea mchafuko na kuharisha si zaidi ya saa moja tangu nimekunywa mtindi. Muongozo wako inshallah.
Kama Mtindi unakufanya uende haja kubwa basi kunywa maji glasi moja ya ya Uvuguvugu yaliyochanganywa na Asali safi kijiko kimoja kikubwa cha kulia wali na ukamulie juu yake limau kubwa moja fanya hivyo kila siku mwili wako utakuwa na Afya na kitambi kitakutoka na unene pia utakutoka utakuwa upo fresh fanya kila siku katika maisha yako.
 
Back
Top Bottom