Jinsi ya kupika ndizi mzuzu mbivu za nazi

Aaliyyah

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2022
Posts
19,041
Reaction score
46,239
Natumaini mkopoa
Wapenz wa ndizi ,Ndizi mzuzu zikiiva msitupe
Leo nimewaletea recipe hii ya kupika ndizi mzuzu zilizoiva za Nazi

MAHITAJI
Naz
Ndiz zilizoiva
Iriki iliyosagwa ama nzima
Sukari kama hupendi tumia chumvi

Hatua ya kwanza
Menya ndizi kata vipande vinne
Kama unatumia Nazi ya kawaida chuja tui la kwanza zito (bubu)na tui la pili weka pekeyake
Kama unatumia ya pakti bas andaa Nazi Yako weka maji kidogo kwakuwa huwa nzito sana

Hatua ya pili
Bandika sufuria ama pan weka ndiz zako Kisha weka tui la Nazi
La pili lile jepes kama unatumia Nazi ya pakti weka maji(maji yasiwe mengi)Kisha weka iriki funika acha ichemke had maji yakikauka

Hatua ya Tatu
Maji yakikauka weka sukari kma hupendi weka chumvi Kisha mimina tui la lile zito tikisa sufuria taratibu had vichanganyike usikoroge koroge na mwiko vitapondeka acha vichemke Kwa dakika 5 zitakuwa tayari
 
haiwekwi walau nyanya, kitungu wala chumvi
 
Zinaonekana tamu sana. Hongera sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…