upishi wa tambi ndio mwenyewe,nikizipika huwa zinatoka nzuri sana,ingawa huu uzi wa zamani kidogo,bora nielezee jinsi ninavyopika mimi.
-unachukua tambi zako,unazichambua,{naongelea tambi za kukaanga}unaweka frying pan,unatia mafuta kidogo tu.tambi unazigawa mafungu mawili.fungu moja unakaanga{mafuta yanakuwa kidogo sana,zikibadilila rangi,unaweka pembeni.
-unachukua sufuria lako,unatia maji,unachanganya tambi zote,za rangi na zisizo na rangi unatia ndani ya sufuria,unazichanganya kidogo,unavyochanganya mwiko unaoutumia,unaugeuza,kwenye ile fimbo ndio unachanganyia{inasaidia hazigandani}.baada ya muda kama dakika 5,unazichuja.
unachukua sufuria lako,unaweka jikoni,hakikisha hakuna maji ndani,unachukua mafuta yako,kidogo tu,unatia ndani ya sufuria,mafuta yakipata moto,unachukua tambi zako,ambazo kwa muonekano,zinakuwa na rangi 2,unazitia kwenye sufuria.ukishatia tu,unatia sukari ya kiasi kulingana na idadi ya tambi zako,kinachofuatga ni hiliki iliyosagwa{inasaidia tambi zinakua na harufu nzuri}unachanganya kwa kutumia sehemu ya fimbo ya mwiko,kwa dakika moja tu.tambi zako zinakuwa tayari.ila kuna wengine wanapenda kuchanganya na zabibu kavu,ila sio lazima