Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,872
- 34,363
Upishi wa Visheti
Vipimo
1.Unga 2 Vikombe
2.Samli au shortening ya mboga 2 Vijiko vya supu
3.Maziwa ¾ Kikombe
4.Iliki Kiasi
5.Mafuta ya kukarangia Kiasi
6.Shira
7.Sukari 1 Kikombe
8.Maji ¾ Kikombe
9.Vanila ½ Kijiko cha chai
10.Zafarani (ukipenda) Kiasi

Namna ya kutayarisha na kupika
Katika kisufuria pasha moto maziwa na wakati huo huo chemsha Samli katika kisufuria kengine.
1. Tia unga katika bakuli na iliki, kisha mimina samli iliyochemka na huku unachanganya, kisha tia maziwa na uwendele kuchanganya vizuri isiwe na madonge, ikiwa maziwa haitoshi ongeza maji kidogo.
2. Kisha uwache unga ukae mahali pa joto kwa muda wa dakika 10 hivi.
3. Halafu fanya viduara vidogo vidogo, kisha finyiza kwenye greta yenye vishimo vidogo ili upate umbo kama kwenye picha.
4. Kisha karanga kwenye mafuta yaliyopata moto hadi vibadilike rangi ya dhahabu, kisha viepue vichuje mafuta.
5. Chemsha shira, ikiwa tayari mimina visheti na upepete na kuzichanganya zipate shira kote.
6. Weka kwenye sahani na zitakuwa tayari kwa kuliwa na kahawa.
