Jioni moja miaka mingi iliyopita na Subhash Patel

Jioni moja miaka mingi iliyopita na Subhash Patel

Kwa nini Waasia wanafanikiwa zaidi kuliko sisi Watanzania weusi ? Halafu hawaachi utamaduni wao ingawaje wala hawaishi India/Pakistani , ...
Mzee Mohammed Said naomba utusaidie kujibu swali hili kwa kadri ya ufahamu wako katika hili swala la waasia kufanikiwa Sanaa hapa nchini na Africa kwa ujumla kuliko wenyeji
 

Subash Patel nilimjua katika miaka ya mwishoni 1970 au mwanzoni 1980 kupitia rafiki yake Said Ibrahim ambaye mimi pia ni rafiki ndugu.

Said ndiye alinipeleka nyumbani kwake.

Miaka hiyo alikuwa anaishi nyuma ya Zanzibar Guest House Mtaa wa Zanaki na Libya Street sehemu za Kisutu. Siku hizo Subash hakuwa tajiri lakini mfanyabiashara kijana anaeinukia. Ninachokumbuka kila nilipokuwa nasoma jina la Subash katika magazeti au kumuona katika TV ni kuwa ilikuwa nyumbani kwake ndipo nilipoiona movie mashuhuri, "The Message," kwa mara ya kwanza.

Hii ilikuwa sinema maarufu sana kuhusu maisha ya Mtume Muhammad (SAW). Sinema hii tukiisoma sifa na "reviews," zake kwenye magazeti tu kwani enzi hizo Tanzania ilikuwa hoi na taaban kwa kila kitu.

Sinema za Holywood zilikuwa haziingii nchini. Waagizaji wa filamu Tanzania Film Company (TFC) kazi iliwashinda kabla hata hawajaianza. Kwangu Mimi kupata nafasi ya kuangalia sInema hii halikuwa jambo dogo.

Iko siku Subash alikuja ofisini kwetu alikuwa na miadi na Mkurugenzi wa Idara tukaonana na kusalimiana lakini hakunikumbuka. Ilikuwa miaka mingi imepita na ilikuwa tumeonana mara moja tu.

Kina nani hao wajenzi huru? Maana kuna dalili zikijikusanya tu, unaweza kuhisi nini kinaendelea
 
Mtu...
Uzee mbona ninao siku nyingi tu.
Sasa nina miaka 68.

Jamani Subash nimekwenda kwake na kukutananae siku moja tu.

Siwezi kuwa na mengi.
Toshekeni na hayo ndugu zanguni.
Hahaaa mzee saidi watu washazoea unaandikaga vitu ambavyo vinazuz mjadala sasa hapa wanaona km umewadisappoint.....yaani tunataka jinsi akina patel walivyosaidia uhuru wa waislamu, au kujenga msikiti wa manyema, au walivyomsaidia baba wa taifa hahaaaaaa sisi tunataka kubanguana bongo mzeee....hapo tunaona kama umeandika vitu vyepesi
 
hahaaa mzee saidi watu washazoea unaandikaga vitu ambavyo vinazuz mjadala sasa hapa wanaona km umewadisappoint.....yaani tunataka jinsi akina patel walivyosaidia uhuru wa waislamu, au kujenga msikiti wa manyema, au walivyomsaidia baba wa taifa hahaaaaaa sisi tunataka kubanguana bongo mzeee....hapo tunaona kama umeandika vitu vyepesi
Kweli huyu dingi leo hajatutendea haki. Huenda sio yeye kaandika. Inakuwaje uzi wake hauna jina la SYKES?
 
Mtu...
Uzee mbona ninao siku nyingi tu.
Sasa nina miaka 68.

Jamani Subash nimekwenda kwake na kukutananae siku moja tu.

Siwezi kuwa na mengi.
Toshekeni na hayo ndugu zanguni.
Mzee Said mimi nakuomba tu uwe unawasamehe hawa vijana na kama kuna lolote la ziada kuhusu Marehem Patel tusaidie sie tunaopenda kujifunza
 
Kwa nini Waasia wanafanikiwa zaidi kuliko sisi Watanzania weusi ? Halafu hawaachi utamaduni wao ingawaje wala hawaishi India/Pakistani , ...
Ndio maana ya kujitambua Mkuu sisi ni kama watoto wadogo kila kitu tunadandia na kutaka kujifunza matokeo yake tunapotea
 
hahaaa mzee saidi watu washazoea unaandikaga vitu ambavyo vinazuz mjadala sasa hapa wanaona km umewadisappoint.....yaani tunataka jinsi akina patel walivyosaidia uhuru wa waislamu, au kujenga msikiti wa manyema, au walivyomsaidia baba wa taifa hahaaaaaa sisi tunataka kubanguana bongo mzeee....hapo tunaona kama umeandika vitu vyepesi
James...
Nacheka peke yangu.

Watu hawataki kusikia kuwa African Association (1929) na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika (1933) iliasisiwa na Kleist Abdallah Sykes Mzulu na Mzee bin Sudi Mmanyema.

Wanataka historia ya TANU na uhuru ianze na Julius Nyerere mwaka wa 1954.

Hawataki kusikia Earle Seaton na Abdul Sykes kadi ya TANU No. 3 ndiyo walipanga kwanza safari ya Nyerere UNO na hotuba alikuwanayo Abdul Sykes toka 1950.

Yaani nikishusha vitu hivi ndiyo barza inachangamka kila muuza kahawa akipita anaambiwa apige round kote na agawe kashata hata wale jamaa walio pembeni ya barza wauza vocha na kupiga rangi viatu.
 

Subash Patel nilimjua katika miaka ya mwishoni 1970 au mwanzoni 1980 kupitia rafiki yake Said Ibrahim ambaye mimi pia ni rafiki ndugu.

Said ndiye alinipeleka nyumbani kwake.

Miaka hiyo alikuwa anaishi nyuma ya Zanzibar Guest House Mtaa wa Zanaki na Libya Street sehemu za Kisutu. Siku hizo Subash hakuwa tajiri lakini mfanyabiashara kijana anaeinukia. Ninachokumbuka kila nilipokuwa nasoma jina la Subash katika magazeti au kumuona katika TV ni kuwa ilikuwa nyumbani kwake ndipo nilipoiona movie mashuhuri, "The Message," kwa mara ya kwanza.

Hii ilikuwa sinema maarufu sana kuhusu maisha ya Mtume Muhammad (SAW). Sinema hii tukiisoma sifa na "reviews," zake kwenye magazeti tu kwani enzi hizo Tanzania ilikuwa hoi na taaban kwa kila kitu.

Sinema za Holywood zilikuwa haziingii nchini. Waagizaji wa filamu Tanzania Film Company (TFC) kazi iliwashinda kabla hata hawajaianza. Kwangu Mimi kupata nafasi ya kuangalia sInema hii halikuwa jambo dogo.

Iko siku Subash alikuja ofisini kwetu alikuwa na miadi na Mkurugenzi wa Idara tukaonana na kusalimiana lakini hakunikumbuka. Ilikuwa miaka mingi imepita na ilikuwa tumeonana mara moja tu.
Nadhani mwandishi aliambiwa na Subhash amwandike ili tumuone humu JF, sasa mwandishi hakuwa na la kuandika, ndiyo kafikia hapo ila kafanikiwa kuweka picha ya Subhash au ilikuwa ni sehemu ya hako kamkataba ka kumuandika Subhash humu JF ili tumjue au ni mwanzo wa hadithi ndefu IJAYO!? TUSUBIRI.
 
Aliiyelewa anisimulie kidogo maana sijaelewa kabisa
 
Umri nao unachangia, huyu mzee smartpone kajifunza juzi tu unataka aandike ese?
Nasononeka sana nikiona kejeli na mzaha kwa mtu kmaa Mohamed Said.
Nimesoma kitabu chake cha Wakati na Maisha ya Abdulwahid Sykes na ni mtu anayejua anachokiandika.Kitabu kimeandikwa baada ya utafiti mkubwa (kupitia nyaraka katika maktaba za CCM/TANu,kuongea na watu mbalimbali )Si mwandishi wa hadithi.
Tafuta hicho kitabu kisome na utakuja kushangaa kuwa unafanya mzaha kwa mtu ambaye hata akiondoka ataacha kumbukumbu kubwa.
 
Back
Top Bottom