Jipatie Nakala yako: Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania by Nyerere

Jipatie Nakala yako: Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania by Nyerere

- Mkuu naona umeongeza maneno over your original post, ni kwamba kama kweli Mwalimu alikuwa na hiyo tabia unayoisema, basi angekemea kuuzwa kwa NBC, tabia hiyo ya Mwalimu ilikuwa siku zote inaangalia sura kwanza, ndio maana alimbariki Salmin kuiba urais, can you imagine Malecela ndiye angeiba urais, ingekuwaje?

- Viongozi wengine wasingeweza kuandika vitabu kuhusu tabia za Mwalimu isingewezekana it was simply impossible you know that, tumjadili Mwalimu kama bin-adam na sio kama Mungu, na tupeni nafasi na wengine tu-present the otherside kuliko kutaka kutulazimisha wote tuimbe wimbo mmoja, wa-Tanzania tujifunze kutengniasha mapenzi yetu wka Mwalimu na Mapnezi kwa taifa, inatakiwa kuwa vitu viwili tofauti.

Respect.


FMEs!
FMES,
Najua umeshaondoka kwenye mjadala lakini kama ulifuatilia issues za Bongo hasa mwaka 1997 kila mara Mwalimu alipotembelea Watanzania alikuwa anazungumzia umuhimu wa NBC kubaki benki ya Watanzania. Ilifika wakati Mkapa alimfuata Butiama akamsihi, aache kuzungumzia suala la NBC, amwamini Mkapa. Mwalimu aliponyamaza Mkapa akageuka na kuwakabidhi Makaburu NBC. Hicho kitu kilimwuuma Mwalimu mpaka mauti ilipomfika. Inasemekana tayari Mkapa alishachukua hongo ya $300,000 kutoka kwa Makaburu. Hapa Mwalimu hana lawama hata kidogo. Kama mnaitakia Tanzania mema pambaneni na rushwa!
 
FMES,
Najua umeshaondoka kwenye mjadala lakini kama ulifuatilia issues za Bongo hasa mwaka 1997 kila mara Mwalimu alipotembelea Watanzania alikuwa anazungumzia umuhimu wa NBC kubaki benki ya Watanzania. Ilifika wakati Mkapa alimfuata Butiama akamsihi, aache kuzungumzia suala la NBC, amwamini Mkapa. Mwalimu aliponyamaza Mkapa akageuka na kuwakabidhi Makaburu NBC. Hicho kitu kilimwuuma Mwalimu mpaka mauti ilipomfika. Inasemekana tayari Mkapa alishachukua hongo ya $300,000 kutoka kwa Makaburu. Hapa Mwalimu hana lawama hata kidogo. Kama mnaitakia Tanzania mema pambaneni na rushwa!

Mkuu shutuma kuwa Mkapa alichukua hongo ya dola laki 3 zinasikitisha. Lakini kama unajua madhara ya monopoly kwenye biashara unaweza kuona kuwa uamuzi wa Mkapa kuivinja NBC ulikuwa sahihi. Kusingekuwa na fair competition kwa benki nyingine, na huenda zisingetaka hata kuja kuwekeza hapa Tanzania kama NBC ingeendelea kuwa kubwa kama ilivyokuwa. Kwa upande fulani ulikuwa ni uamuzi sahihi, kwani kuvunjwa kwake hakujapunguza huduma za Benki Tanzania, japo kumepunguza umiliki wa Benki hizo Tanzania.

Matatizo yanayotokana na monopoly ya CCM kwenye siasa, yangekuwa ni hayo hayo kwenye sekta ya Benki kama NBC ingeendelea kuwa kama ilivyokuwa. Ili kuwe na fair competition kunatakiwa kuwe na level ground, na sio wengine wawe na head start.
 
Mkuu shutuma kuwa Mkapa alichukua hongo ya dola laki 3 zinasikitisha. Lakini kama unajua madhara ya monopoly kwenye biashara unaweza kuona kuwa uamuzi wa Mkapa kuivinja NBC ulikuwa sahihi. Kusingekuwa na fair competition kwa benki nyingine, na huenda zisingetaka hata kuja kuwekeza hapa Tanzania kama NBC ingeendelea kuwa kubwa kama ilivyokuwa. Kwa upande fulani ulikuwa ni uamuzi sahihi, kwani kuvunjwa kwake hakujapunguza huduma za Benki Tanzania, japo kumepunguza umiliki wa Benki hizo Tanzania.

Matatizo yanayotokana na monopoly ya CCM kwenye siasa, yangekuwa ni hayo hayo kwenye sekta ya Benki kama NBC ingeendelea kuwa kama ilivyokuwa. Ili kuwe na fair competition kunatakiwa kuwe na level ground, na sio wengine wawe na head start.
Bongolander,
Hata tungeendelea kuwa na NBC benki za kigeni zingekuja tu. India waliruhusu benki za kigeni lakini wamebaki na benk yao, Bank of India. Kumbuka NBC ni benki pekee iliyokuwa na matawi katika sehemu zote za Tanzania hata vijijini, halafu kinachosikitisha zaidi ni bei tuliyoiuzia. Kaburu alitengeneza faida ya 200% katika kipindi cha miaka mitano tu. Hizo zingekuwa ni hela kwenye hazina yetu.
 
Mimi nafungua hakifunguki wajameni!!! Napata internet explorer error. Nisaidieni nifungueje au ndiyo kimeshapigwa pin tena hapa jamvini??
 
Hata mi nimejaribu kukifungua lakini haiwezekani 5 times.
Pengine mtusaidie zaidi
 
Sio baraza la mawaziri kwa ujumla wake ndio linaamua ubinafsishaji wa shirika kama NBC?

Kama mwenyekiti wa baraza la mawaziri kala hongo halafu kapigia chapuo kuuza kipande cha nchi na wajumbe wa kikao wamenyweshwa chai na chapati za Ikulu wakalala kikaoni hoja ikapita basi kosa la kuuza NBC si la Mkapa.
 
FMES,
Kama kuna mtu alimlazimisha Mwinyi kumchukua Warioba kama waziri mkuu alikuwa ni Salim.
Selection ya Mwalimu kwa waziri mkuu alikuwa ni Mkapa. Wakati huo Salim alikuwa NY na aliposikia hivyo akafunga safari wangu wangu kurudi Bongo kuhakikisha Mwinyi hamchukui Mkapa.Salim akapendekeza Warioba. I know this for certain from a close source to Salim, na hata Salim akiulizwa hivi leo hatasuta ukweli huu.

Mjadala huu umenipita kidogo!

Jasusi,
Putting it this way unafanya wengine wadhani kwamba Salim aonekane alikuwa anamuwekea Mkapa kauzibe. Mimi nadhani Salim alikuwa anatoa ushauri wake kwa Rais Mwinyi kwa nia jema kabisa kwa kuelewa tabia ya Mkapa maana wote walishakuwa kwenye international diplomatic circles. Kwa tabia na hulka ya Mkapa asingeliweza kuwa Waziri Mkuu mzuri kwa Mwinyi. Bila shaka Mkapa na mbwembwe zake angejaribu kum-outshine Rais wake hasa katika international fora.

Huenda basi ndio sababu ya Mkapa kuhakikisha anapindisha utaratibu wa kumpata mgombea wa CCM ili Salim asiweze kupita!! Alikuwa analipiza kisasi?
 
Sio baraza la mawaziri kwa ujumla wake ndio linaamua ubinafsishaji wa shirika kama NBC?

Kama mwenyekiti wa baraza la mawaziri kala hongo halafu kapigia chapuo kuuza kipande cha nchi na wajumbe wa kikao wamenyweshwa chai na chapati za Ikulu wakalala kikaoni hoja ikapita basi kosa la kuuza NBC si la Mkapa.

Lets be realistic. Waziri gani anayeteuliwa na Rais anaweza kupinga matakwa ya Rais aliyempa cheo? Rais akisema nataka jambo hili analiona ni jema na akatoa sababu zake zenye 'agenda' ya kificho nyuma yake, Waziri gani anaweza kumpinga? Wanachoweza kufanya ni kuchangia mawazo yao lakini mwisho wa yote hoja itapitishwa. Tunayaona hayo Bungeni, wabunge huzungumza hadi mapovu kuwatoka lakini mwisho wa siku wanasema wanapitisha hoja kwa asilimia 100, sembuse Baraza la Mawaziri lenye wateule wa mtoa hoja?
 
kitabu hakija patikana,kipo wapi,??/*&^% nashindwa kudownload hiyo link,au ndio kimefichwa tena online??
please,weka hicho kitabu katika google book,or or online server ktk pdf.

thanks
sorrry happo juuu for my *$*T%#$(%,
mzalendo
Natafuta kitabu kilichoandikwa na J.K. Nyerere, "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania" kwa Kiswahili au Kiingereza.

Jitihada za kukipata mitaa ya Dar zilishindikana baada ya kuambiwa 'udaku' kwamba kimepigwa marufuku kinamna. Madukani mwa vitabu mwote nilimopita kukiulizia waliniona juha, kana kwamba 'kila mtu anajua' kitabu kilipigwa marufuku.

Madai hayo ni ya kweli au uzushi tu wa uchaguzi?

Shida yangu ni nakala moja tu ya kitabu hicho kwa ajili ya rejea ya kitaaluma.

Natanguliza shukrani.

Mlenge

=============
UPDATE by JF Admin:


Kwa msaada wa mkuu SubiriJibu kitabu kimepatikana, nakala inaweza kupatikana chini hapa
 
- Ni kweli kabisa mkuu Mwalimu was the greatest, lakini usisahau kwamba alibariki Salmin kupora Urais kule visiwani, alikuwa ni bin-adam mwenye mengi mazuri na mapungufu, ambayo tunayalipia mpaka leo.

- Lakini haibadili ukweli kwamba hakwua mwizi wala fisadi, hilo hatukatai.

Respect.

FMEs!

Kati ya maandishi yako mengi dhidi ya mwalimu katika jukwaa hili, haya uliyoandika hapa ndiyo ya maana na hitimisho sahihi. Sasa waweza kumwacha apumzike kwa amani. Tujadili walio hai sasa. Jambo la maana ni tutampataje Rais ambaye siyo mwizi wala fisadi na wala hacheki na kutumiwa nao?

Hivi mi nashaa watu kama kina Ludovick Mwesiga wanaibuka wanakoibukia sasa kumsema vibaya Mwalimu, walikuwa wapi kipindi yupo hai na hasa baada ya kung'atuka? Nadhani wanatakiwa kunyamaza. Bora Mchungaji Mtikila alikuwa akimsema akiwa hai, kwa nini hawakutumia kipindi hicho cha uhai wake baada ya kustaafu?.
 
Mkuu naona umeandika kwa jazba kidogo na sababu inaeleweka.

Mwalimu aliipenda nchi yake na aliitumikia kwa moyo wake wote - hili halina mjadala. Lolote lile aliloamua kufanya akiwa Rais na hata baada ya kustaafu alikuwa akifanya hivyo kwa mapenzi makubwa aliyokuwanayo kwa nchi na wananchi kwa ujumla, hakuwa na agenda yoyote nyingine. Yale tunayoweza kuyaona kama ni makosa kwake yeye yalifanyika kwa nia njema kabisa.

- Mwalimu hakupenda utawala unaoheshimu sheria, ndio maana mpaka leo Tanzania hatuheshimu sheria, alipenda utaratibu hapana kiongozi akiharibu hapa alihamishiwa pengine tabia ambayo tumeirithi mpaka leo,


Utaratibu wa kuhamisha kiongozi akiharibu kumpeleka kwingine ndio kuvunja sheria, ipi? Tusisahau kwamba wakati wa awamu ya kwanza kulikuwa na wasomi wachache wenye ujuzi wa kutosha kumuwezesha Rais kufukuza huyu na kumuweka yule badala yake. Nadhani alichokuwa akikifanya Mwalimu ni kujaribu pia kumpa nafasi kiongozi aliyeharibu pale, aweze kujirekebisha mahali pengine.


alimpa Mwinyi space hapana asingemchagulia Waziri Mkuu au kumwachia katibu wake mpaka msaidizi wake wa binafsi,
,



Mie naamini kwamba Mwalimu kwa tabia yake asingeliweza katu kumchagulia Mwinyi Waziri Mkuu. Naamini alichokifanya Mwalimu ni kumshauri Mwinyi kwamba fulani anaweza kukusaidia zaidi, period. Pia yawezekana Mwinyi mwenyewe ndiye aliyemuomba Mwalimu ushauri. Kuhusu Mwinyi kuachiwa Wasaidizi wa Mwalimu pia naona yalikuwa ni makubaliano yaliyokuwa na manufaa kwa Mwinyi. Ni wazi alihitaji kupata uzoefu wa nafasi aliyonayo.

Mambo ya kuiga wafanyavyo Wamarekani ama nchi zingine zilizoendelea bila kupima na kuwa huru kujiamulia yanayotufaa, yana madhara yake. Kwanza kwa utamaduni wetu sisi Waafrika ni kitendo cha uungwana zaidi ya kitu chochote kingine kwa Rais anayeingia madarakani kuomba ama kuachiwa wasaidizi kwa muda hadi azoee.


ndege zilikuwa haziishi Butiama watu wake hasa Mkapa wakienda kushitaki, kuna siku Apiyo anashuka na ndege Musoma, huku Mkapa anaondoka na ndege nyingine, Mwinyi akapiga marufuku hizo safari ndio Mwalimu sasa akarudi Msasani, akawa na safari ya Angola anataka ndege ya Rais, somehow Ikulu wakagoma kumpa ile ndege akaishia kwenda na ndege za kawaida, kwa mara ya kwanza Mwinyi anamvuta Simba sharubu!


Mambo kama haya yanarudisha nyuma maendeleo yetu. Mwalimu alikuwa ni kiongozi wa nchi yetu, Baba wa Taifa letu. Alikuwa na haki zote za kutaka kujua kinachoendelea nchini mwake na alikuwa na uwezo wa kumuomba kiongozi yoyote aende Butiama ama Msasani kumueleza kinaganaga kinachoendelea maana alikuwa na uchungu na nchi yake. Kama ni kweli Ikulu (Wasaidizi wa Mwinyi) waligoma kumpa Mwalimu ndege walikuwa wanafanya mambo ya kitoto sana na ya kumvunjia heshima Mwalimu. Tusimsingizie Rais Mwinyi, wala si yeye ambaye alikuwa anapanga ndege iende kumchukua Mwalimu au la. Ni wazi kwamba waliofanya kitendo hicho walikuwa wapambe nuksi tu ambao nadhani walifanya hivyo kwa 'ulevi' tu wa kuwa Ikulu.
- Mwinyi hakuomba ushauri kwa Mwalimu, ndio maana kina Mkapa na Apiyo walikuwa hawaishi kwenda kuchongea Butiama, kama Mwinyi angekwua anaomba ushauri wa Mwalimu basi hiki kitabu kisingeandikwa mengine ni common sense tu. mengine

Mimi nahisi kilichotokea ni kwamba Mwinyi alikuwa anashauriwa vibaya ya viongozi/wasaidizi wake wa karibu (kwa sababu za kibinafsi tu). Bila shaka wapo waliokuwa wanamwambia Mwinyi kwamba yeye ndiye Rais sasa kwa hiyo asimsikilize Mwalimu, Mwalimu wakati wake umekwisha, bla bla.

- Kama Mkapa angekua anaomba ushauri basi asingeweza kuuza NBC kwa bei poa, sikumbuki mkutano wowote na wananchi ambako Mwalimu alilalamika kuhusu kuuzwa kwa NBC tena kwa hela ndogo sana, huku makaburu wakitaka sheria yetu ya ardhi ibadilishwe ikidhi matakwa yao, Mwalimu alikuwepo hakusema kitu, ingawa alilalama sana in private, lakini sio in the public sababu?

Power corrupts. Mkapa naye bila shaka alipata kiburi cha kudhani kwa kuwa yeye ni Rais hawezi kufuata ushauri wa Mwalimu. Watu wanaojali maslahi ya Taifa na kuliweka Taifa mbele hutafuta ushauri, huangalia kwanza maamuzi wanayofanya yatawasaidia/yatakuwa na madhara gani kwa wananchi. Labda Mkapa alijali zaidi faida atakazopata yeye kama kweli alipewa huo mulungula. Nahisi pia alikuwa anajitafutia sifa kwamba yeye naye anaweza kuiongoza nchi bila kufuata ushauri wa Mwalimu. Alijidanganya. matokeo tunayaona hadi leo.

-
Ninachojua ni kwamba Mwinyi alipoongeza bei ya Matrekta Mwalimu alilalama sana kule Mbeya, sasa inasababisha maswali mengi sana yasiyo na majibu, kwa mfano, ipi was the worst kuuza NBC kwa bei poa, au kumshambulia Amin mpaka ndani ya Uganda ili kumrudisha Obote, na Tanzania kulipa madeni ya silaha za ile vita mpaka leo, vita ambayo alishauriwa sana kwamba iishe baada ya kumtoa Amin kwenye mipaka yetu tu ili kutuokoa na madeni? Si tunalipa yale madeni mpaka ingawa Obote wala hakudumu na Uraisi uliotugharimu sana Tanzania mpaka hii leo, au?

Respect.

FMEs!

What a comparison! Pia umechanganya issues mkuu. Sababu za kuingia ndani ya Uganda Mwalimu alizielezea wazi - kuwasaidia wananchi wa Uganda. Waganda waliomba Tanzania ifanye hivyo. Kumbuka Obote alidhulumiwa na kupokwa uongozi wa Uganda baada ya kazi aliyoifanya hadi Uganda ikawa nchi huru, so he deserved to have his country back. Kuna factors nyingi zilizosababisha Obote asimudu urais as you put it. Urais wa Obote sio uliotugharimu sana Tanzania. Kilichotugharimu ni kutetea nchi yetu dhidi ya nduli Idd Amin ambaye alianzisha vita dhidi ya Tanzania. Sidhani kwamba kuna Rais yeyote ambaye anaweza kukaa Ikulu kuendesha business as usual wakati kuna Rais kichaa anatishia usalama wa wananchi wa Tanzania!

On another issue, baadhi ya watu wamekuwa wakidai kwamba Mwalimu alikuwa anamchukia Mzee Malecela na ndio maana akaandika kitabu kumsakama. Argument hii ni hafifu. Kama kawaida yake Mwalimu alikuwa anaangalia maslahi ya taifa zaidi kuliko kitu kingine chochote. Nasikia Mzee Malecela na Mwalimu walikuwa marafiki (family friends). Kwa hiyo inadhihirisha ni kwa kiasi gani Mwalimu alikuwa anaweka maslahi ya taifa mbele kuliko kitu kingine chochote.

Kubwa zaidi, kwenye hiki controversial kitabu, Mwalimu wakati wote amezungumzia wajibu wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na si wajibu wa Mzee Malecela as a person. Angelitaka kumjadili Malecela as a person, bila shaka tungelisoma humo ule udaku usio na ukweli wowote kwamba Mzee Malecela alisilimishwa!

Respect!
 
Boramaisha,
I wasn't able to give you senks until now because I could not sign in. Good analysis.
 
Nafikiri wadau wengi hapa mnatakiwa kutumia Voltaire Principle katika kujadiliana na FMES: "I totally disagree with what you are saying, but I'll defend to death your right of saying it".

From the arguments between FMES and the rest, it looks like it is "not allowed" to provide the other side of the story, especially when discussing Nyerere. In any discussion where people resorts to name-calling, personallity attacks, instead of the issue at hand, that is a good sign of healthy discussion.

Surely we don't want "zidumu fikra" type of discussion, where everyone says "me too", do we?
 
Nafikiri wadau wengi hapa mnatakiwa kutumia Voltaire Principle katika kujadiliana na FMES: "I totally disagree with what you are saying, but I'll defend to death your right of saying it".

From the arguments between FMES and the rest, it looks like it is "not allowed" to provide the other side of the story, especially when discussing Nyerere. In any discussion where people resorts to name-calling, personallity attacks, instead of the issue at hand, that is a good sign of healthy discussion.

Surely we don't want "zidumu fikra" type of discussion, where everyone says "me too", do we?
Mlenge,
Mbona sijaona mtu kamnyima mwenziwe nafasi na haki ya kutoa maoni yake? Tumesikia maoni ya pande zote bila upande mmoja kutaka kulazimisha mwenzake kuwa upande wake ndio sahihi, au?
 
Nafikiri wadau wengi hapa mnatakiwa kutumia Voltaire Principle katika kujadiliana na FMES: "I totally disagree with what you are saying, but I'll defend to death your right of saying it".

From the arguments between FMES and the rest, it looks like it is "not allowed" to provide the other side of the story, especially when discussing Nyerere. In any discussion where people resorts to name-calling, personallity attacks, instead of the issue at hand, that is a good sign of healthy discussion.

Surely we don't want "zidumu fikra" type of discussion, where everyone says "me too", do we?

Baada ya kusoma hii comment yako Mkuu Mlenge, nimepitia tena hii thread kutoka mwanzo nione ni wapi name-calling, personality na attacks zimeelekezwa kwa FMES lakini sikufanikiwa. Nilichoona ni watu ambao wamesimama kidete kutetea kile wanachoamini ni cha kweli dhidi ya madai ya FMES. Wengine wetu kwenye huu mjadala tu watu wazima na mengi yanayoongelewa humu tumeyashuhudia na si kusimuliwa. Hatuna uhusiano wowote wa kindugu na Mwalimu Nyerere na hivyo tunasukumwa zaidi ya historia ambayo kwa namna moja ama nyingine sisi ni sehemu yake kwa sababu tulikuwapo. Bila shaka hatutakaa kimya wala hatutaona haya kumkosoa yeyote yule atakayejaribu ama kwa makusudi au kwa malengo yoyote yale kuupindisha ukweli.

Ninachoweza kusema ni kuwa haya madai hayangeweza kutolewa wakati Mwalimu yuko hai kwa sababu moja tu - hofu ya kuwakwaza wananchi walio wengi kuliko hofu ya kumkwaza Mwalimu. Wanaoyatoa hivi sasa waliwaogopa watanzania kuliko walivyomwogopa Mwalimu kwani kwa wakati huo madaraka yote yalikuwa mikononi mwao. Amini usiamini Mkuu, kila wakati Mwinyi alipokwaa kisiki, alitafuta ushauri Butiama licha ya wabaya wa Mwalimu kumshauri tofauti. Baadaye aliposalimu amri na kuanza kuwasikiliza, kama pale ndogo ndogo zilipoanza kupigwa ili aongezewe awamu ya tatu, alijikuta akishukiwa kama mwewe anavyomshukia kifaranga. Mwalimu alijali na kuheshimu utaratibu, ni hiyo ilimsukuma hadi kumshukia hata Sam Nujoma wa Namibia alipotaka kuchezea katiba ili aendelee kubaki madarakani -Katiba haibadilishwi kama shati !
 
Sidhani viongozi wa Tanzania wa sasa wamefikia kuchukia uchambuzi wa Mwalimu wa Hatma ya Tanzania, kiasi cha kukipiga marufuku kitabu cha Baba wa Taifa.Mimi nadhani, kutokana na hali ya uchumi na upatikanaji wa printing facilities wakati ule Mwalimu akitaka kuchapisha kitabu hiki, ilikuwa ni lazima akichapishe nje ya nchi. Sasa hali ya Zimbabwe imeharibika zaidi, na hata kama kuna demand ya hicho kitabu, Mchapishaji wake hawezi kukichapisha.Labda Mzee MwanaKijiji angefanya mpango akaomba kichapishwe hapa Tanzania, basi hao wanaotaka kukisoma wangepata "new edition".

Hakikuchapishwa nje si kwa sababu ya kutokuwapo printing facilities nchini mwetu wakati ule, zilikuwepo. Nadhani Oxford University Printing Press wamekuwepo nchini kwa muda mrefu, pia Government Printer's wangeliweza kuombwa na kukubali kuifanya kazi hiyo kwa ajili ya Mwalimu. Kwa vyovyote vile Mwalimu angelipenda zaidi kutumia facilities za nchini badala ya nchi za nje (Zimbabwe). Kilichapishwa nje kutokana na unyeti wa suala lenyewe. Kuchapisha nje ilikuwa ni kwa ajili ya kuhakikisha kwamba habari za kitabu hicho haziwezi ku-leak.

Kama wazo la kukipiga marufuku kitabu hicho lipo basi halijatangazwa rasmi. Naamini kitabu bado kipo ofisi za Taasisi ya Mwalimu Nyerere kwa yeyote anayetaka kukinunua. Hivi sasa wamehamia kwenye jengo refu lililopo mkabala na hospitali ya Dr. Khan. Bila shaka kinaweza kuuzwa kwenye Kongamano la Kumbukumbu ya Kuzaliwa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere linaloanza kesho tarehe 12/4/2010 Chuo Kikuu Dar es Salaam, Mlimani.
 
Toleo jipya.. liko mbioni.. likiwa na commentary. Naomba anayekumbuka mlolongo wa viongozi wote wakuu wahusika wa sakata la Tanganyika na OIC... anisaidie..
 
Back
Top Bottom