Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Hata Mimi mkuu ninayo ila kusimulia sijui naanzia wapi

Maana moja ya vitu nilivyoshuhudia ni kumuona mtu anapita mlangoni Huku mlango ukiwa umefungwa, kuiona sura yangu kwa mtu mwingine, na aliyekuwa anafanya hayo yote ni mpangaji mwenzangu na ni binti tuu wa Makamo aliyefundishwa uchawi na mama yake mzazi

Mpaka sasa Kuna vitu bado vinanitesa walivyonitegeshea na vikanivagaa,

Pia mauzauza nyumba ambayo nilikuwa nafanya kazi maeneo ya masaki napo nilishuhudia mambo mengi sana yakutisha ingawa ktk ndoto ila kulikuwa na uhalisia, yaani humo ktk huo mjengo misukule kama yote.

Jamani hii Dunia Imeficha Siri za watu wengi sana, Kuna watu hawataki kujulikana kuwa wao ni waovu ndiyo maana wamevaa vazi la dini.
Nisimulie mimi nitauweka kwenye maandishi
 
Kaka, mimi ni binadamu na ninaishi mazingira hayohayo ambayo nyinyi mnaishi na hii story sijaiandika nikaikamilisha kiasi niweze kuituma muda wowote ninaotaka, ni kwamba naandika na kutuma, hivyo muda mwingine naweza nikalenga kutuma muda fulani lakini nikatokea kushindwa kwasababu tofauti tofauti, sasa siwezi kufupisha ama kutuma nusu, nitalazimika tena nikipata muda niendelee kuandika kisha ndo nitume.

Sio kila muda nakuwa na simu mkononi, na sio kila muda ninaotaraji kuwa na simu mkononi kwa muda wa kutosha basi inakuwa hivyo. I am not an automatic robot. Najitahidi kadiri na muda wangu kuja kumfurahisha huyo mtu anayenitukana matusi ya nguoni na hata wengine ambao hawajahi kucomment lakini wanapenda kusoma vilevile, kususa sio haiba yangu, na jambo hili nililianzisha mwenyewe, nitalimaliza mwenyewe. Muda mwingine ni aibu kusemasema kila kilichokukuta na unachopitia, unanyamaza tu then unaendelea, unawatazama watu ukiamini kilichowajaa ndicho kinachowatoka.
Nmekuelewa saaana SteveMollel shusa vitu boss
 
Yani wewe jamaa SteveMollel nakuelewa vyema sana...

Dogo zezeta kushnehi....Kanasa kwenye nguzo barazani na 50cent zake....kwa ndumba za shangazi mgeni wa bembela

BIGI amekutwa chali collapsed domo limepinda kama wewe....kwa ndumba za shangazi mgeni wa bembela

Mkewe na BIGI na yeye amsizishwa na usingizi wa ajabu mbaya kwa ndumba za shangazi mgeni wa bembela

Huu mkasa wako kijana naona ni vihoja vingi vinaenda kuibuka na patashika ni nyingi sana, Sijui kama ataachwa salama mtu mwingine hapo....Kwanza wote mliohusika na kuubeba mwili wa BIGI na MKEWE mlitoboa kweli au wewe ulipona kwakua ulipewa dawa ya Kuoga na bembela 😂😂😂
 
Taswira ya mkewe BIGI baada ya kuzinduka usingizini.....😂😂😂
55F245D4-30CF-4F87-9A13-EC32F485E8A4.jpeg
 
Take easy mkuu hulipwi hapa tuliojaa ni wapenda hadithi tu iwe uongo au ukweli.
Kulikua na hadithi za kijeba mzee ole zamani alikua mambo yake km bigi.
Ulisoma story zA Linda na Obi?
Hadithi za kina AE Musiba je
Tutarudi na roho zetu,
ama zao ama zangu.
Kuna kitabu pia hadithi ya binti mmoja wa kisingida hapo Kinondoni imesimuliwa vizuri sana nimesahau jina.
Hivyo ni baadhi vitabu nimesoma.
Kuna kingine kinaitwa Nelia au Nely binti mmoja alitolewa West Africa km mchumba akapelekwa Italy bila kujua kumbe anapelekwa kwenye ma brothel kuuzwa.
Hii ilinitoa machozi.
Maana mtiririko wa hadithi na vile visa vilivyomtokea yule binti sikuvumilia.
So relax, ukipata
muda simulia
Linda na Obi daah we kweli muhenga
 
We jamaa ni nyuzi zaidi ya mbili hivi unavamia na kuleta uharibifu, hebu balance shobo hakuna aliyekuita humu. Kuwa kama mwanamke na si ujiweke binti mwenye kupelekeshwa na kuvunja ungo. Hakuna mahali alipoandika amekuwekea wewe usome
Yeye anaona kama ni bonge la mjanja kumbe anajichoresha na ushamba wake
 
Back
Top Bottom