Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Aisee BIG ni mchawi plus anafuga misukule ndani[emoji38][emoji38][emoji38]Yule Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida ~ 05
Tangu ujenzi wa uzio ulipoanza niliongeza zaidi umakini wangu kwenye kutazama usalama wa nje ya nyumba kwasababu geti lile dogo lililokuwa hapo sasa halikuwapo tena kwenye kingo za ukuta, badala yake lilikuwa linaegeshwa na kuondolewa, hivyo mtu asipoliegesha basi ndo tunakaa wazi kama behewa kitu ambacho kwangu kilikuwa na hatari sana maana usafiri wangu ulikuwa unakaa karibu na geti hilo. Yeye mwenye nyumba alisema anataka kuleta geti jingine, lile la zamani lisirudishwe, lakini kwa siku tatu mfululizo hakuleta geti hilo, hata mafundi wenyewe walikuwa wanalalamika hawajalipwa pesa zao, mara kadhaa walikuwa wanasaidiwa kupewa chakula na wapangaji.
Sijawahi kujua kwanini wenye nyumba wanakuwaga wagumu mno kufanya marekebisho ya mapango yao, yani mikono yao imezoea kupokea na kuchuma tu, kwenye kutoa wanaona kama vile hawastahili, yaani wanaumiaaaa.
Turudi kwenye usiku ule. Baada ya BIGI kupotelea kule kizani nilijazwa na hamu ya kwenda kutazama kule korongoni anapoenda. Nilijiuliza mara mbilimbili nikaona haitakuwa vema kwani nikitoka pale na kuacha geti dogo wazi kiasi kile nitakuwa nimejiweka matatani kiusalama, haswa wa pale nyumbani, hivyo nikaona kheri nibakie palepale kungoja lakini kwasababu sikutaka bwana yule anione kuwa namtazama nilienda zangu maeneo ya bafuni, huko kulikuwa na kiza sababu ya taa haikuwashwa, nikajibanza hapo kiubavu kutazama geti dogo.
Yani kama sekunde nne tu yule bwana akawa ametokea getini, Ilibakia kidogo tu angeniona maana ilikuwa ni upesi mno kiasi cha kunishangaza, alipoingia alitazama huku na kule, huku na kule, alafu akaufuata mlango wa grill lakini alipoufikia mlango huo, kabla hajaingia, alifanya jambo ambalo lilinifanya nihisi huenda aliniona. Alisimama hapo akitazama upande ule wa bafuni kwa kama dakika tatu pasipo kupepesa, moyo wangu ukawa unaenda mbio sana. Sikumchukulia bwana yule kama mtu wa kawaida tena bali kama dubwana lililopo mbele yangu katika mawindo yake.
Nilitulia kadiri nilivyoweza, alipotosheka akaingia ndani na kisha akaufunga mlango ule wa grill kwa funguo, kitu ambacho siku zingine huwa hakifanyi, mimi nikaachwa pale nje nisijue nini cha kufanya.
Nilikaa nikawaza niugonge mlango wa grill? Hapana, nikiugonga maana yake yule bwana atajua nilikuwa nje namfuatilia nami sikutaka kumthibitishia hilo, basi nikaona cha kufanya niendee dirisha la chumba changu, japo lipo juu, nihangaike nalo kuwaita waliomo ndani wapate kunisaidia, wakati nashuka ngazi mara nilisikia sauti ya kiume ikifoka:
"Wewe nani?"
Nilishtuka sana. Niligeuka kutazama sauti inatokea wapi nikabaini ni kwenye dirisha la yule jirani yangu mwenye duka, hapo dirishani alikuwa amesimama mtu aliyeshikilia pazia kutazama nje. Kabla sijajibu kitu, mtu huyo alinitambua akasema,
"Aah kumbe ni wewe, kaka! Vipi tena huko nje mida hii?"
Nikamdanganya nilienda maliwatoni lakini kwa bahati mbaya kurudi nikaukuta mlango umefungwa, basi kwa kunisaidia alitoka ndani kwake kuja kunifungulia.
Alinijulia hali na kidogo kwa kama dakika mbili hivi tukawa na mazungumzo mafupi. Aliniambia alisikia mtu anaufungua mlango wa grill kwenda nje, akaniuliza nilikuwa ni mimi?
Kabla sijamjibu nilitazama kwanza kwenye korido kisha nikamweleza kwa sauti yangu ya chini kuwa aliyeufungua mlango huo ni BIGI, mimi nilitoka hapo baadae kwenda maliwatoni ndipo nikaukuta tayari ameshaufunga. Sikutaka kumwambia kuhusu yale ya korongoni wala ya kujificha bafuni.
Nilipomjibu hayo naye alinieleza kuwa muda wote huo alikuwa akimshuku bwana huyo kuwa ndo' anaacha mlango wazi lakini hakuwa na uhakika, zaidi aliniambia anahisi kuna jambo haliko sawa kumhusu bwana yule kwani kuna mambo ambayo amemshuhudia yakamwacha mdomo wazi.
Hakutaka kunieleza mengi kwasababu wasaa haukuwa unaruhusu, tulikubaliana tutakapoonana na tukiwa na muda basi tutayajenga. Aliniaga akaenda zake na mimi nikaenda zangu.
Wiki iliyokuja nilipata safari ya siku tatu ya kwenda Tabora, wilaya ya Igunga, kwasababu ya msiba wa mmoja wa jamaa yetu wa kazini ambaye alifiwa na mama yake mzazi. Safari hiyo ndefu ilikomea kwenye kijiji fulani ambacho sikikumbuki jina ila ninachokumbuka nyumba ambayo tulifikia haikuwa mbali sana na shule moja ya sekondari inayoitwa Mwamashiga, huko hapakuwa na mtandao wa simu wala umeme, ni nyumba chache chache ndo' zilikuwa na taa zinazotumia nishati ya jua kwahiyo sehemu kubwa ilikuwa kizani nyakati za usiku.
Muda wote nikiwa huko sikuweza kutumia simu yangu kwaajili ya mawasiliano, simu iligeuka kuwa 'toy' la kuchezea game ama kukokotoa hesabu. Nilikuja kupata mawasiliano siku tulipotoka huko kijijini njiani kuelekea Igunga mjini, kitu kilichonifanya nikajua kuwa mtandao umerudi ni ujumbe ulioingia kwenye simu yangu; ujumbe kutoka Airtel kuwa kifurushi changu kimeisha, baada ya ujumbe huo nilipokea ujumbe mwingine toka kwenye namba ngeni ukisema (nanukuu):
"Kaka ukirudi nyumbani fanya tuonane upesi, nimejaribu kukutafuta kwa simu sikupati. Tarimo."
Nilijiuliza ujumbe huo umetokea wapi lakini baada ya punde ya kuwaza na kuunganisha matukio nilipata jibu langu, aliyetuma ujumbe ule alikuwa ni jirani yangu mwenye duka, yeye ndiye Tarimo na mara ya mwisho mimi kuonana naye alitaka tuongee tukipata nafasi.
Nilijaribu kumtafuta hewani pasipo mafanikio, si kwamba alikuwa hapatikani, lah, mimi sikuwa na salio. Nilicheki pia kwenye AirtelMoney lakini napo hola, hapakuwa na kiasi cha kunitosha kumpigia, ilinilazimu niwe mpole mpaka nitakapopata sehemu rafiki ya kununua vocha.
Wakati huo nilikuwa nawaza sana kuwa ni nini ambacho Tarimo alikuwa anataka kuniambia kwa dharura hiyo lakini pia nikajikuta nayakumbuka na kuyawaza yale ya kule nyumbani, kwa muda huo nikawa katika ulimwengu wangu wa pekee, nilikaa na watu lakini nilijihisi niko mwenyewe kabisa.
Tulipofika Igunga mjini gari lilisimama ili tupate mahitaji muhimu mathalani maji maana kuna watu walishindwa kunywa maji ya kule kijijini, maji yao ni ya kuchimba chini na kuyahifadhi kwenye ndoo, maji hayo ukiyatazama kwa haraka unaweza dhani ni chai nyepesi ya maziwa na ladha yake si kama maji uloyazoea, hapo ndipo na mimi nilipata mwanya wa kununua vocha nikapiga simu kwa Tarimo huku nikiomba apokee upesi maana simu yangu ilikuwa taabani kwa kuishiwa na charge, muda wote ambao nilikuwa kule sikuwahi kuicharge na kama matumizi yangekuwa makubwa basi bila shaka ingeshalizima muda mrefu sana.
Kidogo Tarimo alipokea simu nikamsalimu na kumweleza kuwa nimepata ujumbe wake na nilikuwa mbali mahali ambapo mtandao unasumbua, basi akanipa pole na kunitaka nikifika Dar Es Salaam nionane naye mara moja kwani kuna jambo alitaka kunishirikisha kabla hajachukua hatua zingine. Nakumbuka kauli yake moja akisema,
"Kaka, tufanye juu chini huyu jamaa aondoke hapa nyumbani kama tunataka kuwa salama."
Basi kwasababu tulishapangiana kuonana, nilikata simu na kuwatafuta watu wangu wengine wa karibu ili nipate kuwajulia hali maana sikuwa hewani kwa kitambo kidogo na sikutaka simu izime kabla sijateta nao, baada ya hapo haikupita muda mrefu simu ikazima nikabaki mpweke, wengi niliokuwa nao ndani ya gari sikuwa nafahamiana nao zaidi tu ya mfiwa na majamaa wawili wa kutoka kazini, nao walikuwa wameketi mbali na mimi.
Sikudumu muda mrefu nikapitiwa na usingizi mzito kwelikweli kwani kwa muda niliokuwa kule kijijini sikupata kulala vema, mahali pa kulala hapakuwapo, ni mara chache ndo' ningejibanza sebuleni majira ya mchana pale kwenye kochi nikalala huku nimeshika tama, usingizi wa mlinzi, hivyo nilivyotulia kwenye kiti cha basi na huku upepo unanipuliza sikuweza kuvumilia kabisa, macho yalinishinda vita.
Nilifika Dar majira ya jioni, kabla ya kunyookea nyumbani nilipitia kazini ili niuchukue usafiri wangu ambao niliuacha huko kwasababu ni salama zaidi kuliko kule nyumbani ambapo niliacha bado ujenzi unaendelea, baada ya hapo nilinyookea nyumbani na nilichokifanya baada ya kufika tu nilimpigia simu bwana Tarimo kumwambia kwamba nimewasili, bwana huyo akaniambia yuko mbali kidogo kuna mtu alimpelekea mzigo maeneo ya Mbweni lakini akitoka huko atanipigia na kunipa muafaka, basi nikangoja, wakati huo nikautumia kwenye mambo yangu mengine ya hapa na pale.
Mpaka inafikia saa nne usiku bwana Tarimo hakuwa amenitafuta, si kwa ujumbe wala kupiga, na mimi sikuona haja ya kumtafuta maana aliniambia atanijuza yeye hivyo nikatulia kungoja nikiamini atakuwa ametingwa na mambo yake ya kikazi, muda ukaenda na kuenda.
Kwenye majira ya saa tano ya usiku, nikiwa nimepumzika sebuleni, ndipo nilisikia watu wakiwa wanazungumzazungumza huko nje, haswa wanawake, katika mtindo wa zogo fulani hivi na mimi sikuwa nayasikia maneno yao wanayoyasema.
Lakini ghafla katika zogo hilo nilisikia ukunga uuuuuuuuuwiiiiii! Uuuuuuuuuwiii! Nikapata mshtuko. Kidogo nikiwa hapo, bado sijafanya kitu, mlango uligongwa na nilipoufungua nilikutana na mwanamke mmoja ambaye anakaa kwenye zile nyumba za nje, mwanamke huyo aliniambia kuwa amepata habari toka kwa mke wa yule jirani yangu wa dukani, yaani mke wa bwana Tarimo, ya kwamba bwana huyo amepata ajali mbaya ya pikipiki maeneo ya Kunduchi, mbuyuni, kwenye mataa.
Nikaduwaa.
Picha limeanza tayari, hebu nivute kigoda kabisa.Jirani Yangu wa kule Goba Hakuwa Mtu wa Kawaida.
Sasa ni miaka miwili imepita, nimehamia na ninaishi kwengine, lakini yale ya kule Goba nayakumbuka vema kana kwamba yametokea jana yake, na huenda mambo hayo nikayakumbuka hata na milele maana ni moja ya visa ambavyo vilinishangaza sana.
Mwaka 2020 mwanzoni, mimi na familia yangu tuilihamia Goba Kontena, eneo la Mashuka, tukitokea Mbezi Beach, Makonde, kwasababu ya kutafuta eneo kubwa zaidi kukimu ukubwa wa familia. Hapo Goba tukapata mahali pazuri, nyumba kubwa ya wastani ambapo ndani yake tulikuwa tunakaa familia tatu, kila mmoja na mlango wake japo tulikuwa tunaingilia na kutokea mlango mmoja mkubwa uloshika korido, mlango wa grill, kwa nje kulikuwa na wapangaji wengine watatu kwa ujumla ambao walikuwa wanaishi kwenye vyumba vimoja vimoja, kwasababu hiyo basi humu tulimokuwa tunaishi sisi pakawa panajulikana kwa jina la 'nyumba kubwa'.
Nyumba zote hizi zilikuwa ndani ya uzio wenye geti moja dogo na lingine kubwa ambalo kukaa kwangu kote hapo sikuwahi kuliona likifunguliwa lote kwasababu njia ilikuwa imebanwa na ujenzi mwingine, usingeweza kuingiza gari hapo labda pikipiki na baiskeli tena kwa kujibanabana.
Uzuri hakukuwa na mtu mwenye usafiri wa gari, kulikuwa na watu watatu wenye pikipiki tu, mmoja ni bodaboda ambaye alikuwa akirejea usiku mzito nyumbani, mara kadhaa akija asubuhi kabisa pamekucha, saa kumi na mbili au saa moja, wa pili alikuwa ni mfanyabiashara ambaye alikuwa anatumia pikipiki yake kwaajili ya shughuli zake za dukani na wa tatu alikuwa ni mimi mwenyewe, nilikuwa nautumia pikipiki kunipeleka na kunirejesha kazini.
Wote tulikuwa tunapaki katika uwanja mdogo wa nyumba hii, lakini tofauti na wenzangu, pikipiki yangu ilikuwa imeharibika 'lock' kwenye swichi ya funguo hivyo naliweza kuzima tu lakini sikuwa na uwezo wa kuilock pikipiki, swala hilo likawa linanipa mawazo sana juu ya kuibiwa usafiri wangu kwani nilikuwa napaki karibu na geti dogo ninaloingilia na geti hilo halikuwa madhubuti kabisa, limetenguka kwa chini na bati lake la chuma limeshikwa kutu sana, zaidi tulishakuwa na matukio mawili matatu ya wezi kuingia ndani kwasababu ya ufupi wa uzio wetu.
Wanaingia na nyie mpaka mfunguo milango hamuwakuti, wanaruka kama vyura kurukia upande wa pili na kukimbilia korongoni, huko kuna giza totoro hutaweza kuwafuata.
Kwasababu hiyo, mara kadhaa nilikuwa nikichungulia dirishani pale ninapohisi kuna jambo la kutia shaka na hivi mimi nilikuwa mgumu sana wa kupata usingizi nyakati za usiku, jambo hili nililifanya vema. Ningesikia watu wakipita huko njiani, ama wakichota maji nje ama wakienda maliwatoni, japo si kila mtu lakini ilikuwa ni mara kwa mara.
Baada ya mwezi kupita hapo, maisha yakiwa kawaida tu, ndipo tukapata jirani mpya ambaye alihamia kwenye mlango unaofuata baada yangu. Alikuwa ni bwana mmoja mnene mweusi, tulikuja kumfahamu zaidi kwa jina la 'BIGI', alikuwa mtu mwenye maneno machache, sauti yake nyembamba tofauti na mwili wake, na mkewe mfupi mwenye mwili kiasi, rangi yake maji ya kunde, pamoja na mtoto mmoja wa kiume ambaye kwa makadirio alikuwa darasa la nne hivi au la tano.
Nikaendelea kumfahamu zaidi BIG baada ya kukutana naye mara kadhaa barabarani nikiwa narejea nyumbani hivyo nikawa nalazimika kumpatia lifti mpaka home. Katika wiki basi angalau tungekutana mara mbili au tatu, hali hiyo ya kurudi nyumbani pamoja, ikafanya wapangaji wenzangu kudhania mimi na huyu bwana ni marafiki kiasi kwamba mara kadhaa wakawa wananiambia nimfikishie ujumbe kuhusu kulipia zamu za umeme au malipo ya maji, lakini ukweli ni kwamba mimi na wao hatukuwa na tofauti sana, zaidi mimi nilikuwa nakutana naye mara nyingi kuliko wao lakini kukutana naye huko hakukufanya tukawa marafiki wa huyu bwana, angenisalimu na kisha akaketi kwenye pikipiki asiongee neno lingine lolote mpaka tunafika. Ndivyo ilivyokuwa.
"Habari?" Tukionana.
"Asante." Tukiagana.
Nami sikuona taabu wala sikujali, watu hatufanani kama vidole vya mkononi, siku zikaenda mpaka na mwezi hivi, kama sijakosea, tangu wahamie pale.
Nakumbuka baada ya mwezi huo kuisha alikuja mwenye nyumba kusalimu, bila shaka kuna mmoja wa mpangaji alikuwa anadaiwa kodi maana mwenye nyumba alikuwa hapendi kutumiwa pesa kwa njia ya simu, anapendelea cash pekee mkononi, na kwa kawaida yake akifika basi hutaka kusalimu kila mtu, atagonga kila mlango apate kuwajulia hali, mimi binafsi nilikuwa namkwepa maana huwa sipendi maneno yake mengi yasoisha na pia tabia zake za kuanza kukuongelesha mambo ya wapangaji wengine ndo' ilikuwa inan'kera zaidi, lakini siku hiyo sikuwa na namna ya kumkimbia kwani alinikuta nje natazamatazama pikipiki, akanisalimu na kuniuliza habari za hapa na pale kisha akaingia ndani ya nyumba kubwa kwenda kuwagongea wengine.
Mwenye nyumba wetu kwa kabila alikuwa ni msukuma, alikuwa hawezi kuongea taratibu, akiongea upande wa pili basi hata wewe wa ng'ambo utasikia upende usipende. Hana faragha. Hata kudai kwake kodi ndo' hivyohivyo, hata ukimvutia pembeni ni kujichosha tu.
Alipogonga huko akatoka na kusimama barazani, punde kidogo wakatoka wamama wawili kumsalimu, mama mmoja alikuwa ni mke wa yule jamaa wa dukani na mwingine alikuwa ni yule mke wa BIGI.
Wanawake hawa wote walikuwa wamevalia khanga kifuani na khanga kiunoni kila mmoja, na hapa ndo ikawa mara yangu ya pili kumwona mke wa BIGI tangu amehamia hapa, siku ya kwanza ni ile waloingia na siku ya pili ndo ikawa hiyo, sikuwahi kumwona kamwe hapo katikati, iwe weekend nikiwa nashinda nyumbani au siku ya kazi nikibahatika kurejea na mumewe.
Lakini zaidi, hii ndo' ilikuwa siku yangu pekee niiliyobahatika kumwona mwanamke huyo jua likiwa linawaka kwani siku ile waliyohamia ilikuwa ni majira ya usiku.
Kwa kumtazama harakaharaka nikabaini ana makovu makubwa ya moto mgongoni mwake na kwenye mkono wake wa kuume.
Lakini mbali na hilo, nikiendelea kuwa hapo, nikabaini mwanamke huyo ni bubu, hana uwezo wakuongea. Nilimsikia mwenye nyumba akishangaa kisukuma, "Hiii!" Akamuuliza yule jirani wa muda mrefu, "Huyu hawezi kuongea?"
Yule mama jirani akanyanyua mabega kuashiria hata yeye hajui hayo. Yule mzee akaongeaongea pale haswa na yule jirani mwingine kisha alipomaiza akanifuata na kuniuliza kama nimemeona na yule jirani mpya, yaani BIGI, nikamwambia hapana, mara yangu ya mwisho kumwona ilikuwa ni siku mbili nyuma, akaniambia basi nikimwona nimwambie amtafute mwenye nyumba ampatie mkataba wake wa makazi kwani yeye amejaribu kumtafuta kwa njia ya simu pasipo mafanikio. Ni mwezi sasa umepita anaishi kwa mkataba wa maneno tu.
Na sababu iliyomfanya akanambia mimi ilikuwa ni yule jirani mwingine, alimwambia kuwa mimi ndo' mtu ambaye nipo karibu na BIGI, na japo alimwambia mkewe lakini hakuamini kama atakuwa alimwelewa au lah.
Baada ya hapo akaenda kuwagongea na kuongea na wale wapangaji wanaokaa kwenye vyumba vimojavimoja na kisha akaenda zake. Aliponiaga alinisihi nisisahau jambo lake nami nikamwambia nitajitahidi.
Ikaja kesho na keshokutwa, sijamwona BIGI, ikapita mpaka wiki nzima nisimwone jamaa huyo kitu ambacho hakikuwa kawaida, yani nisimwone hata mara moja? Na sijabadili ratiba wala njia? ... Nikajiaminiisha kuwa huenda bwana huyo atakuwa amesafiri. Nilitamani kumuuliza mkewe lakini ningeanzia wapi?
Lakini .... Em ngoja ... Nikajiuliza.
Kama mwanamke huyo alisikia hodi ya mwenye nyumba akatoka mpaka ndani kuja kuonana naye ila hakuweza tu kuongea, inamaanisha alielewa alichoambiwa, basi nikahitimisha kuwa atamwambia mumewe mambo yao wamalizane wenyewe.
Siku hiyo usiku nikiwa nautafuta usingizi kitandani, muda mfupi tu baada ya kuzima TV, nikasikia kana kwamba kuna mtu nje, majira yalikuwa ni saa tisa hivi ya usiku, nje kumetulia sana na sasa nilikuwa na uwezo wa kusikia karibia kila kitu kwani TV iliyokuwa inatoa sauti nilikwishaizima, nikajongea dirishani kuchungulia, sikutaka kupuuzia hisia zangu.
Uzuri ama sijui ubaya, chumba changu cha kulalia kilikuwa na madirisha mawili, moja lilikuwa linatazama kaskazini kulipo geti dogo na kibaraza cha nyumba kubwa ingali lingine lilikuwa linatazama mashariki lilipo tenki kubwa la maji ambalo halikuwa mbali sana na chemba. Huko mashariki ndiko kulikuwa na taa inayoning'inia kwenye ukuta, kule kibarazani taa yake kubwa ilikuwa hafifu, haikuwa na maisha marefu kuzima, kwahiyo taa ya mashariki ndo' ilikuwa inasaidia kumulika mpaka huku mbele kwenye geti dogo na kibaraza japo kiuhafifu.
Hivyo kwakupitia madirisha haya nilikuwa na uwezo wa kuona 'engo' mbili tofauti, kaskazini na mashariki mwa nyumba.
Nilipotazama katika dirisha hili la kaskazini mwa nyumba nikamwona kijana mmoja mfupi akiwa yu peku, amepachika kandambili zake mikononi, ananyata kuelekea magharibi mwa nyumba.
Huko magharibi kulikuwapo na stoo mbili ambazo kuna wapangaji, hususani wale wa vyumba vimojamoja, wanatumia kuwekea vitu vyao kama vile majiko na vyombo kadha wa kadha kwasababu vyumba vyao havitoshi kuhifadhi vitu vingi. Humo ndani si ajabu ukakuta hata unga, mchele, mkaa, mafuta na kadhalika.
Ukivuka stoo hizo ndipo unaenda kukutana na milango ya wapangaji hao, kila mlango ukiwa na grill yake iliyofungwa haswa kwa nyakati hizi za usiku isipokuwa kile chumba ambacho kinakaliwa na yule bodaboda. Chumba hicho huwa kinabaki na grill wazi maana haijulikani yule jamaa atarejea majira gani. Mkewe alikuwa anafanya hivyo ili kumruhusu mumewe kuingia ndani muda wowote atakaorejea, iwe ni usiku mkubwa au hata asubuhi ya mapema. Yeye akirejea ataufungua mlango kwa funguo yake ya ziada kisha atafunga ule wa grill kwa funguo pekee alonayo.
Nilipoona hivyo, nikaenda sebuleni na kufungua mlango wangu taratibu sana. Nilipotoka nikafuata korido kwa kunyata mpaka kwenye mlango wa kutoka kwenye hii nyumba kubwa, hapo nikafungua mlango mdogo kisha nikaanza kutekenya taratibu mlango wa grill ili nipate kwenda nje.
Mpaka hapo sikuwa namwona tena yule jamaa niliyemshuhudia dirishani, niliamini kabisa atakuwa upande ule wa vyumba ambavyo mimi sikuwa na uwezo wa kuviona kwani dirisha langu na hapa mlangoni palikuwa panaishia kuona kwenye stoo tu, huko kwengine ni kona iliyo mbali na macho yangu.
Na shaka langu likawa kwenye ile nyumba ambayo grill yake iko wazi. Mule ndani kuna mwanamke na mtoto mdogo wa miaka michache.
Nilipomaliza kufungua grill ile, kabla sijaisukuma kwanguvu ili niende nje, nikasikia sauti kali ya kike, "mwiziiiiii!" Kufumba na kufumbua nikamwona mtu akipitia kwa kasi kubwa, alikuwa ni yule bwana niliyemshuhudia dirishani, nikasukuma grill na kutoka ndani kwa kasi lakini kabla sijafanya chochote bwana yule akawa ameshauruka ukuta na kuyoyoma kuelekea kule korongoni.
Sikuelewa aliurukaje ule ukuta kwa kile kimo chake, ni kama vile alikuwa na 'spring' kwenye miguu, nilijaribu kufanya kama yeye lakini niliishia kujiumiza tumbo na kurudi chini nikiwa na michubuko ya kutosha mkononi.
Kazi ikabaki tu kusema, "weweee! Wewee! Utakufa mbwa wewe!" Huku nikiwa sina lingine la kufanya.
Muda kidogo karibia kila mtu akawa ametoka kwenye chumba chake kuja kuuliza nini kimejiri kwasababu sauti ya mwizi mwizi iliwashtua toka usingizini, hivyo hapa kukawa na zogo kiasi, kila mtu akisema maoni yake lakini kubwa ni hali imezidi, inabidi mwenye nyumba aongeze hata mistari miwili ya tofali kwenye uzio ili kuongeza urefu wake na pia achomelee lile geti dogo kwa chini kama sio kuweka jipya kabisa.
Wakati hayo yanaendelea, mimi nikafanya kutazama kule kwenye nyumba kubwa, hamaki, nikaona mtu amesimama koridoni karibu na mlango.
Kwasababu ya uhafifu wa ile taa ya barazani, na mtu yule alikuwa amesimama kwa ndani kidogo, hakuwa anaonekana vema, lakini kwa kile kimo chake nikahisi huenda mtu huyo ni yule mke wa BIGI, kwa kujihakikishia nikasogea karibu ili nipate kumwona mtu huyo lakini ajabu aliponiona najongea akakimbia upesi kama mwizi!
Kha! Nikabaki nimehamaki. Akijikwaa je?
Nikadhani nimeona vya kutosha, lakini kumbe ule ndo' ulikuwa mwanzo kabisa wa mengi yajayo, mwanzo wa kuamini mwanamke yule ama tuseme familia ile haikuwa ya kawaida kabisa.
***
Bwana Bigi tena😃Kwahiyo tivu kule kwengine inakuwaje eti
TuendeleeNdiyo nimeanza kuisoma leo majira ya saa 9 alfajiri.
😃 unakesha kumbe mamiiTuendelee
Jirani Yangu wa kule Goba Hakuwa Mtu wa Kawaida.
Sasa ni miaka miwili imepita, nimehamia na ninaishi kwengine, lakini yale ya kule Goba nayakumbuka vema kana kwamba yametokea jana yake, na huenda mambo hayo nikayakumbuka hata na milele maana ni moja ya visa ambavyo vilinishangaza sana.
Mwaka 2020 mwanzoni, mimi na familia yangu tuilihamia Goba Kontena, eneo la Mashuka, tukitokea Mbezi Beach, Makonde, kwasababu ya kutafuta eneo kubwa zaidi kukimu ukubwa wa familia. Hapo Goba tukapata mahali pazuri, nyumba kubwa ya wastani ambapo ndani yake tulikuwa tunakaa familia tatu, kila mmoja na mlango wake japo tulikuwa tunaingilia na kutokea mlango mmoja mkubwa uloshika korido, mlango wa grill, kwa nje kulikuwa na wapangaji wengine watatu kwa ujumla ambao walikuwa wanaishi kwenye vyumba vimoja vimoja, kwasababu hiyo basi humu tulimokuwa tunaishi sisi pakawa panajulikana kwa jina la 'nyumba kubwa'.
Nyumba zote hizi zilikuwa ndani ya uzio wenye geti moja dogo na lingine kubwa ambalo kukaa kwangu kote hapo sikuwahi kuliona likifunguliwa lote kwasababu njia ilikuwa imebanwa na ujenzi mwingine, usingeweza kuingiza gari hapo labda pikipiki na baiskeli tena kwa kujibanabana.
Uzuri hakukuwa na mtu mwenye usafiri wa gari, kulikuwa na watu watatu wenye pikipiki tu, mmoja ni bodaboda ambaye alikuwa akirejea usiku mzito nyumbani, mara kadhaa akija asubuhi kabisa pamekucha, saa kumi na mbili au saa moja, wa pili alikuwa ni mfanyabiashara ambaye alikuwa anatumia pikipiki yake kwaajili ya shughuli zake za dukani na wa tatu alikuwa ni mimi mwenyewe, nilikuwa nautumia pikipiki kunipeleka na kunirejesha kazini.
Wote tulikuwa tunapaki katika uwanja mdogo wa nyumba hii, lakini tofauti na wenzangu, pikipiki yangu ilikuwa imeharibika 'lock' kwenye swichi ya funguo hivyo naliweza kuzima tu lakini sikuwa na uwezo wa kuilock pikipiki, swala hilo likawa linanipa mawazo sana juu ya kuibiwa usafiri wangu kwani nilikuwa napaki karibu na geti dogo ninaloingilia na geti hilo halikuwa madhubuti kabisa, limetenguka kwa chini na bati lake la chuma limeshikwa kutu sana, zaidi tulishakuwa na matukio mawili matatu ya wezi kuingia ndani kwasababu ya ufupi wa uzio wetu.
Wanaingia na nyie mpaka mfunguo milango hamuwakuti, wanaruka kama vyura kurukia upande wa pili na kukimbilia korongoni, huko kuna giza totoro hutaweza kuwafuata.
Kwasababu hiyo, mara kadhaa nilikuwa nikichungulia dirishani pale ninapohisi kuna jambo la kutia shaka na hivi mimi nilikuwa mgumu sana wa kupata usingizi nyakati za usiku, jambo hili nililifanya vema. Ningesikia watu wakipita huko njiani, ama wakichota maji nje ama wakienda maliwatoni, japo si kila mtu lakini ilikuwa ni mara kwa mara.
Baada ya mwezi kupita hapo, maisha yakiwa kawaida tu, ndipo tukapata jirani mpya ambaye alihamia kwenye mlango unaofuata baada yangu. Alikuwa ni bwana mmoja mnene mweusi, tulikuja kumfahamu zaidi kwa jina la 'BIGI', alikuwa mtu mwenye maneno machache, sauti yake nyembamba tofauti na mwili wake, na mkewe mfupi mwenye mwili kiasi, rangi yake maji ya kunde, pamoja na mtoto mmoja wa kiume ambaye kwa makadirio alikuwa darasa la nne hivi au la tano.
Nikaendelea kumfahamu zaidi BIG baada ya kukutana naye mara kadhaa barabarani nikiwa narejea nyumbani hivyo nikawa nalazimika kumpatia lifti mpaka home. Katika wiki basi angalau tungekutana mara mbili au tatu, hali hiyo ya kurudi nyumbani pamoja, ikafanya wapangaji wenzangu kudhania mimi na huyu bwana ni marafiki kiasi kwamba mara kadhaa wakawa wananiambia nimfikishie ujumbe kuhusu kulipia zamu za umeme au malipo ya maji, lakini ukweli ni kwamba mimi na wao hatukuwa na tofauti sana, zaidi mimi nilikuwa nakutana naye mara nyingi kuliko wao lakini kukutana naye huko hakukufanya tukawa marafiki wa huyu bwana, angenisalimu na kisha akaketi kwenye pikipiki asiongee neno lingine lolote mpaka tunafika. Ndivyo ilivyokuwa.
"Habari?" Tukionana.
"Asante." Tukiagana.
Nami sikuona taabu wala sikujali, watu hatufanani kama vidole vya mkononi, siku zikaenda mpaka na mwezi hivi, kama sijakosea, tangu wahamie pale.
Nakumbuka baada ya mwezi huo kuisha alikuja mwenye nyumba kusalimu, bila shaka kuna mmoja wa mpangaji alikuwa anadaiwa kodi maana mwenye nyumba alikuwa hapendi kutumiwa pesa kwa njia ya simu, anapendelea cash pekee mkononi, na kwa kawaida yake akifika basi hutaka kusalimu kila mtu, atagonga kila mlango apate kuwajulia hali, mimi binafsi nilikuwa namkwepa maana huwa sipendi maneno yake mengi yasoisha na pia tabia zake za kuanza kukuongelesha mambo ya wapangaji wengine ndo' ilikuwa inan'kera zaidi, lakini siku hiyo sikuwa na namna ya kumkimbia kwani alinikuta nje natazamatazama pikipiki, akanisalimu na kuniuliza habari za hapa na pale kisha akaingia ndani ya nyumba kubwa kwenda kuwagongea wengine.
Mwenye nyumba wetu kwa kabila alikuwa ni Msukuma, alikuwa hawezi kuongea taratibu, akiongea upande wa pili basi hata wewe wa ng'ambo utasikia upende usipende. Hana faragha. Hata kudai kwake kodi ndo' hivyohivyo, hata ukimvutia pembeni ni kujichosha tu.
Alipogonga huko akatoka na kusimama barazani, punde kidogo wakatoka wamama wawili kumsalimu, mama mmoja alikuwa ni mke wa yule jamaa wa dukani na mwingine alikuwa ni yule mke wa BIGI.
Wanawake hawa wote walikuwa wamevalia khanga kifuani na khanga kiunoni kila mmoja, na hapa ndo ikawa mara yangu ya pili kumwona mke wa BIGI tangu amehamia hapa, siku ya kwanza ni ile waloingia na siku ya pili ndo ikawa hiyo, sikuwahi kumwona kamwe hapo katikati, iwe weekend nikiwa nashinda nyumbani au siku ya kazi nikibahatika kurejea na mumewe.
Lakini zaidi, hii ndo' ilikuwa siku yangu pekee niiliyobahatika kumwona mwanamke huyo jua likiwa linawaka kwani siku ile waliyohamia ilikuwa ni majira ya usiku.
Kwa kumtazama harakaharaka nikabaini ana makovu makubwa ya moto mgongoni mwake na kwenye mkono wake wa kuume.
Lakini mbali na hilo, nikiendelea kuwa hapo, nikabaini mwanamke huyo ni bubu, hana uwezo wakuongea. Nilimsikia mwenye nyumba akishangaa kisukuma, "Hiii!" Akamuuliza yule jirani wa muda mrefu, "Huyu hawezi kuongea?"
Yule mama jirani akanyanyua mabega kuashiria hata yeye hajui hayo. Yule mzee akaongeaongea pale haswa na yule jirani mwingine kisha alipomaiza akanifuata na kuniuliza kama nimemeona na yule jirani mpya, yaani BIGI, nikamwambia hapana, mara yangu ya mwisho kumwona ilikuwa ni siku mbili nyuma, akaniambia basi nikimwona nimwambie amtafute mwenye nyumba ampatie mkataba wake wa makazi kwani yeye amejaribu kumtafuta kwa njia ya simu pasipo mafanikio. Ni mwezi sasa umepita anaishi kwa mkataba wa maneno tu.
Na sababu iliyomfanya akanambia mimi ilikuwa ni yule jirani mwingine, alimwambia kuwa mimi ndo' mtu ambaye nipo karibu na BIGI, na japo alimwambia mkewe lakini hakuamini kama atakuwa alimwelewa au lah.
Baada ya hapo akaenda kuwagongea na kuongea na wale wapangaji wanaokaa kwenye vyumba vimojavimoja na kisha akaenda zake. Aliponiaga alinisihi nisisahau jambo lake nami nikamwambia nitajitahidi.
Ikaja kesho na keshokutwa, sijamwona BIGI, ikapita mpaka wiki nzima nisimwone jamaa huyo kitu ambacho hakikuwa kawaida, yani nisimwone hata mara moja? Na sijabadili ratiba wala njia? ... Nikajiaminiisha kuwa huenda bwana huyo atakuwa amesafiri. Nilitamani kumuuliza mkewe lakini ningeanzia wapi?
Lakini .... Em ngoja ... Nikajiuliza.
Kama mwanamke huyo alisikia hodi ya mwenye nyumba akatoka mpaka ndani kuja kuonana naye ila hakuweza tu kuongea, inamaanisha alielewa alichoambiwa, basi nikahitimisha kuwa atamwambia mumewe mambo yao wamalizane wenyewe.
Siku hiyo usiku nikiwa nautafuta usingizi kitandani, muda mfupi tu baada ya kuzima TV, nikasikia kana kwamba kuna mtu nje, majira yalikuwa ni saa tisa hivi ya usiku, nje kumetulia sana na sasa nilikuwa na uwezo wa kusikia karibia kila kitu kwani TV iliyokuwa inatoa sauti nilikwishaizima, nikajongea dirishani kuchungulia, sikutaka kupuuzia hisia zangu.
Uzuri ama sijui ubaya, chumba changu cha kulalia kilikuwa na madirisha mawili, moja lilikuwa linatazama kaskazini kulipo geti dogo na kibaraza cha nyumba kubwa ingali lingine lilikuwa linatazama mashariki lilipo tenki kubwa la maji ambalo halikuwa mbali sana na chemba. Huko mashariki ndiko kulikuwa na taa inayoning'inia kwenye ukuta, kule kibarazani taa yake kubwa ilikuwa hafifu, haikuwa na maisha marefu kuzima, kwahiyo taa ya mashariki ndo' ilikuwa inasaidia kumulika mpaka huku mbele kwenye geti dogo na kibaraza japo kiuhafifu.
Hivyo kwakupitia madirisha haya nilikuwa na uwezo wa kuona 'engo' mbili tofauti, kaskazini na mashariki mwa nyumba.
Nilipotazama katika dirisha hili la kaskazini mwa nyumba nikamwona kijana mmoja mfupi akiwa yu peku, amepachika kandambili zake mikononi, ananyata kuelekea magharibi mwa nyumba.
Huko magharibi kulikuwapo na stoo mbili ambazo kuna wapangaji, hususani wale wa vyumba vimojamoja, wanatumia kuwekea vitu vyao kama vile majiko na vyombo kadha wa kadha kwasababu vyumba vyao havitoshi kuhifadhi vitu vingi. Humo ndani si ajabu ukakuta hata unga, mchele, mkaa, mafuta na kadhalika.
Ukivuka stoo hizo ndipo unaenda kukutana na milango ya wapangaji hao, kila mlango ukiwa na grill yake iliyofungwa haswa kwa nyakati hizi za usiku isipokuwa kile chumba ambacho kinakaliwa na yule bodaboda. Chumba hicho huwa kinabaki na grill wazi maana haijulikani yule jamaa atarejea majira gani. Mkewe alikuwa anafanya hivyo ili kumruhusu mumewe kuingia ndani muda wowote atakaorejea, iwe ni usiku mkubwa au hata asubuhi ya mapema. Yeye akirejea ataufungua mlango kwa funguo yake ya ziada kisha atafunga ule wa grill kwa funguo pekee alonayo.
Nilipoona hivyo, nikaenda sebuleni na kufungua mlango wangu taratibu sana. Nilipotoka nikafuata korido kwa kunyata mpaka kwenye mlango wa kutoka kwenye hii nyumba kubwa, hapo nikafungua mlango mdogo kisha nikaanza kutekenya taratibu mlango wa grill ili nipate kwenda nje.
Mpaka hapo sikuwa namwona tena yule jamaa niliyemshuhudia dirishani, niliamini kabisa atakuwa upande ule wa vyumba ambavyo mimi sikuwa na uwezo wa kuviona kwani dirisha langu na hapa mlangoni palikuwa panaishia kuona kwenye stoo tu, huko kwengine ni kona iliyo mbali na macho yangu.
Na shaka langu likawa kwenye ile nyumba ambayo grill yake iko wazi. Mule ndani kuna mwanamke na mtoto mdogo wa miaka michache.
Nilipomaliza kufungua grill ile, kabla sijaisukuma kwanguvu ili niende nje, nikasikia sauti kali ya kike, "mwiziiiiii!" Kufumba na kufumbua nikamwona mtu akipitia kwa kasi kubwa, alikuwa ni yule bwana niliyemshuhudia dirishani, nikasukuma grill na kutoka ndani kwa kasi lakini kabla sijafanya chochote bwana yule akawa ameshauruka ukuta na kuyoyoma kuelekea kule korongoni.
Sikuelewa aliurukaje ule ukuta kwa kile kimo chake, ni kama vile alikuwa na 'spring' kwenye miguu, nilijaribu kufanya kama yeye lakini niliishia kujiumiza tumbo na kurudi chini nikiwa na michubuko ya kutosha mkononi.
Kazi ikabaki tu kusema, "weweee! Wewee! Utakufa mbwa wewe!" Huku nikiwa sina lingine la kufanya.
Muda kidogo karibia kila mtu akawa ametoka kwenye chumba chake kuja kuuliza nini kimejiri kwasababu sauti ya mwizi mwizi iliwashtua toka usingizini, hivyo hapa kukawa na zogo kiasi, kila mtu akisema maoni yake lakini kubwa ni hali imezidi, inabidi mwenye nyumba aongeze hata mistari miwili ya tofali kwenye uzio ili kuongeza urefu wake na pia achomelee lile geti dogo kwa chini kama sio kuweka jipya kabisa.
Wakati hayo yanaendelea, mimi nikafanya kutazama kule kwenye nyumba kubwa, hamaki, nikaona mtu amesimama koridoni karibu na mlango.
Kwasababu ya uhafifu wa ile taa ya barazani, na mtu yule alikuwa amesimama kwa ndani kidogo, hakuwa anaonekana vema, lakini kwa kile kimo chake nikahisi huenda mtu huyo ni yule mke wa BIGI, kwa kujihakikishia nikasogea karibu ili nipate kumwona mtu huyo lakini ajabu aliponiona najongea akakimbia upesi kama mwizi!
Kha! Nikabaki nimehamaki. Akijikwaa je?
Nikadhani nimeona vya kutosha, lakini kumbe ule ndo' ulikuwa mwanzo kabisa wa mengi yajayo, mwanzo wa kuamini mwanamke yule ama tuseme familia ile haikuwa ya kawaida kabisa.
***
Maandishi yakiwa marefu sana, yanachosha pia. Alaf pia raha ya simulizi, ikupe muda wa kutafakari na mshawasha wa yajayo.Nikionaga hizi mambo za ITAENDELEA basi mi huwa naishia hapohapo na hiyo story.
Kwanini hawawezi kuandika kisa kimoja kwenye post mara moja...???
To yeye Akimaliza naomba summary.
Huyo BIGI ni mchawi au mwizi?
#YNWA
Hii story haitakiwi kusomwa usiku kwa sisi waoga sema tu ni ubishi wetu masikini tarimoNgoja nifunge dirisha kwanza namuogopa BIGI
Mkuu Analyse rudisha avatar ya mwanzo jamani mpaka tuizoee hiiKwanini amuige DeepPond? Kila mmoja anafanya mambo kwa namna anayoona yeye inafaa. Badala ya kutaka watu wote wawe kwa namna unayoona ww inafaa, jifunze kuwapokea kwa jinsi walivyo.