Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa kawaida

Yule Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa Kawaida - 11


"Baba fulani, mtoto wa BIGI amefariki."

Kusikia hizo habari ikabidi ninyanyuke kuketi, nikawaza ina maana lile swala la Bembela lilikuwa ndio hilo? Yaani amemuua yule mtoto? Ndicho nilichofikiria, nilinyanyuka upesi maana usingizi na mang'amung'amu yake yote yalikuwa yamekata, nikaenda kuoga na kuketi mahali kwanza ili nipate kuandika ujumbe wa 'excuse' kwenda kazini maana tayari 'enyewe nilikuwa n'shachelewa kwenda huko, ni saa nne kasoro ya asubuhi sasa, alafu baada ya hapo ndo' nikamtafuta Bembela kwa kumtumia ujumbe, niliona hiyo ni njia bora zaidi kwangu kuliko kumpigia simu kwasababu ya madhila yangu ya mdomo, nilipotuma ujumbe huo nikakaa kungoja.

Ni baadae, kama nusu saa mbele, nikiwa napata kifungua kinywa kwa tabu yangu ya mdomo ndipo nikasikia ujumbe umeingia kwenye simu, kutazama upesi nikakuta ni ujumbe kutoka kazini, kinyume kabisa na matarajio yangu, basi nikang'aka kwa hasira, nikaona sasa bora nipige simu huenda mhusika wangu yu mbali na kifaa chake cha mawasiliano, simu nayo ikaita lakini haikujibiwa.

Nilipopiga mara mbili, nikaachana nayo nikiamini zile 'missed calls' zilikuwa zinatosha, mhusika atakapoziona basi atanitafuta kwa muda wake, mimi nikaendelea na mambo yangu.

Baadae majira ya mchana, nikiwa hapohapo nyumbani, sijatoka kwenda mahali popote pale, nikaonana na mama yangu ambaye tangu naamka sikupata kuonana naye, alikuwa amerejea kutoka mahali fulani, na punde baada ya kufika na kunitazama usoni, kwa huruma ya mama, akaanza kunipa nasaha za janga lile lililonikumba.

Alinisihi sana niende hospitali na tayari alishamweleza baba kuhusu hali yangu hiyo, hata na hivyo alishangaa sana mpaka muda huo sikuwa nimejigusa kwenda kutafuta tiba, alisema nina roho ngumu kweli, lakini kitu ambacho hakujua mimi mwenzake tayari nilishaogea ile dawa nlopewa na Bembela tangu asubuhi, dawa ya kuondoa mabaki yote yalotupwa na wabaya wangu kwa mujibu wa maneno yake, nikawa naamini dawa hiyo huenda ikanisaidia, niwe tu mvumilivu.

Basi masaa ya siku hiyo yakazidi kusogea, bado nipo hapo nyumbani na bado sijapokea ujumbe wowote toka kwa Bembela, kila nilipopata nafasi nilitazama simu yangu lakini sikuambulia kitu, sio 'call' wala 'message', mwanamke yule hakunitafuta kabisa, mpaka giza jepesi linaingia, kimya tu.

Nikajaribu kuongea na mke wangu ampigie simu Mama Tarimo kumuulizia Bembela kwani nina shida naye, nilimweleza ni shida ya dawa ya ugonjwa wangu ili kupunguza maswali yake mengi, mwanamke huyo akaridhia na punde akapiga simu ambayo aliiweka 'loudspeaker', kidogo simu kuita ikapokelewa na Mama Tarimo, mke wangu akamwelezea shida yangu, mama huyo akamjibu: "nimetoka nyumbani majira ya mchana mpaka sasa bado sijarejea, nilienda hospitali kumwona mgonjwa wangu, walakini niko njiani narudi, ningoje kidogo nikifika nitamtazama."

Baada ya hapo kazi ikawa ni kungoja. Kichwani najiuliza kwanini Bembela alifanya kile kitendo? Kwanini mtoto? Sasa kwa kufanya hivyo tofauti yetu na BIGI itakuwa nini kama wote ni wauaji? Yani nilikuwa na hamu kweli ya kuongea naye, nilihisi maswali yangu yananikaba kooni nashindwa kuhema, naona kama muda hauendi.

Kweli baadae, kama lisaa hivi kupita, Mama Tarimo akatimiza ahadi yake kwa kupiga simu, nilimwona mke wangu akinijia upesi huku simu ameiweka 'loudspeaker', aliponikaribia nikasikia Mama Tarimo akisema, "Nimefika lakini Bembela hayuko nyumbani, sio yeye wala shoga yake niliyemwona, nadhani wametoka, wakirejea nikafanikiwa kuwaona basi ntakujuza."

Baada ya hapo hata mimi binafsi nilipojaribu kumpigia Bembela sikumpata, sio tena hapokei simu bali hapatikani hewani kabisa. Hata yule shoga yake mke wangu alipojaribu kumtafuta kwa namba alonayo, naye hakumpata hewani! Sikujua nini kiliwakuta? Nilijipata najawa na hofu kifuani mwangu nikiomba yote yawe salama maana mpaka hapo sikuwa na lingine la kufanya zaidi ya hilo.

Kama utani, usiku ule ukapita kimya, kesho yake asubuhi niliamka mapema majira ya saa kumi na mbili, bado taya yangu inasumbua na imegoma kurejea kwenye hali yake ya kawaida, ile dawa ninayotumia bado haijanisaidia, mara kidogo nikiwa najiandaa ndipo simu yangu ikapokea ujumbe kutoka namba niliyoitambua upesi kuwa ni ya Bembela, ujumbe huo ulisomeka hivi:

"Habari yako shemeji, nimeona ulinitafuta tunaweza tukaongea saa hii kama una muda."

Haraka nikamrudishia majibu kwamba ni vema tukachat maana mimi bado siwezi kuongea vizuri, basi baada ya hapo tukalowea kwenye 'messages'. Nilimuuliza yuko wapi, hakutaka kuniambia, alichosema yeye yuko mbali ila salama, huko ameongozana na shangazi na shoga yake kwasababu fulani ambayo nayo pia hakutaka kuniambia.

Nikamuuliza kuhusu kifo cha mtoto wa BIGI, hapo kidogo akakwama, nadhani aliogopa kujibu swala hilo kwa njia ya ujumbe ama aliona hatoweza kulielezea vema vile anavyotaka yeye basi muda kidogo akaamua kunipigia simu kwaajili ya kuniweka sawa. Mwanamke huyo, kwa sauti ya chini, alinambia hafahamu chochote kuhusu kifo cha yule mtoto, yeye alichokifanya usiku ule ni kilekile alichoelekezwa na mtaalam kwaajili ya kumwadabisha BIGI na si vinginevyo.

Kwa maneno yake alisema, "mtaalam aliniambia nikikamilisha zoezi la kunuwia, kukoga na kumwaga dawa kisha nikamwita nikiwa nimeshikilia kitu ambacho ni mali yake binafsi basi bwana huyo atapoteza nguvu zake zote, na tena nitamkuta pale kibarazani akiwa uchi wa mnyama ili kila mtu apate kumshuhudia na kumjua kuwa ni mchawi, lakini ajabu nilipofanya hivyo asubuhi yake saa kumi na moja, nilimkuta yule mtoto, akiwa uchi wa mnyama, ameshikilia nguzo ya kibarazani, mwili wake hauna hata tone la pumzi. Mikononi mwake na miguu pake pana sarafu zile za hamsini hamsini!"

Kwakweli maelezo hayo yakaniacha mataa ya bumbuwazi. Kuna muda nilihisi nasikiliza tamthilia lakini kumbe ndo uhalisia wenyewe, nikaamini kweli ya dunia ni mengi sana!

Mwanamke huyo aliendelea kuniambia ya kwamba wakati mwili wa mtoto huyo ukiwa hapo kibarazani pasipo uhai, shangazi yake alimshuhudia BIGI kwa macho yake mwenyewe akiwa amesimama mwisho wa korido, amesimama hapo akiwa anamtazama kama paka aliyefura kwa kipigo, bila kufanya jambo akajiondokea zake na hapo ndipo wakakata shauri kuyeya hapo nyumbani baada ya shangazi yake kumsihi.

Hivyo mpaka wanaondoka, yeye, shangazi yake na shoga yake kwenda huko waliko, mwili wa yule mtoto ulikuwa palepale, hawakujua tena nini kilichofuatia baada ya hapo na hawakuwasiliana na mtu yoyote wa pale nyumbani mpaka asubuhi ya siku hiyo ambapo kabla hajawasiliana na mimi alipata kuongea na mwenye nyumba kwanza.

Baada ya kuhitimisha maongezi hayo, mimi niliendelea na maandalizi yangu, nilipokamilisha nikapitia hospitali kucheki tatizo langu maana niliona ni vema pia nikafanya hivyo, lakini huko kote hamna nilichofanya zaidi ya kupoteza tu pesa maana hamna chochote nilichoambwa na daktari, nikarejea zangu nyumbani, Afrikana.

Baadae majira ya jioni nilipata wasaa wa kuongea na wazazi wangu nikawaeleza juu ya yale niliyoambiwa kule hospitali, tena nikiongea kwa tabu sana, kuna muda machozi yalikuwa yananilenga nilipokuwa najitazama kwenye kioo nikiona namna nilivyobadilika kuwa wa ajabu, yani nakuwa mlemavu huku najiona, lakini ndo' hivyo sikuwa na namna.

Baba yangu alinishauri tufanye namna ya kumwona daktari bingwa wa mifumo ya fahamu, Neurologist, ili apate kunisaidia lakini mimi sikuwa radhi kabisa na hilo kwasababu niliamini lile tatizo nililokuwa nalo lilikuwa ni la kiimani zaidi kuliko hospitali, lakini kwasababu nalimfahamu mzee wangu vema, sikumwambia kitu maana hata kama ningemwelezea basi asingeniafiki hata kidogo, si mtu anayeamini kwenye mambo ya kishirikina na mimi simlaumu maana mambo haya kama hujapata kuyaona kwa macho yako ya nyama basi hutakaa uamini,kila atakayekueleza utaona ni ngano na visasili tu, hata mimi nilikuwa vivyo hivyo lakini nilikuja kujifunza katika njia ngumu hapo mbeleni.

Nakumbuka mama yangu alikuwa akinikandika mafuta ya Mwamposa na sala kedekede, lakini tena naendelea kuogea ile dawa nlopewa na Bembela, yaani tafarani tu, sijui hata kipi kilikuja kunisaidia kuniponya kati ya hivyo viwili. Mungu mwenyewe anajua.

Baada ya siku kama tatu hivi kupita baada ya kile kikao kidofo na wazazi, nilirejea nyumbani kule Goba, na kesho yake tu baada ya kufika, alikuja mwenye nyumba akitaka kukaa kikao na sisi wote kwa pamoja, siku hiyo ilikuwa 'weekend' kama si Jumamosi basi Jumapili, na taarifa ya kikao nadhani kila mmoja alikuwa ameshaipata, mimi binafsi niliupokea ujumbe siku mbili nyuma yake, hivyo kwenye kile kikao kulikuwapo na watu karibia wote, mtu pekee mzima wa afya ambaye hakuwapo ni BIGI, na hiyo haikuwa ajabu, tulishazoea, Bembela yeye alifika wakati kikao kimeshaanza, alikuja akiongozana na shangazi yake lakini mwanamke huyo mzee hakupata kujiunga na sisi kikaoni isipokuwa Bembela pekee.

Katika kikao hicho, mwenye nyumba alieleza kuwa jambo pekee lililomleta na kutukutanisha na sisi hapo ni swala la mpangaji mwenzetu ambaye alikumbwa na ile kadhia ya mwanae kufariki katika mazingira ya kutatanisha mbele ya kibaraza, bwana huyo alisema namna alivyokuwa anapitia matatizo na vyombo vya usalama, mathalani polisi na ulinzi shirikikishi, kwasababu ya mpangaji yule ambaye alienda mbele zaidi kumwita 'mpangaji asokuwa na mkataba'.

Alituambia pia namna alivyopokea malalamiko kadha wa kadha kumhusu bwana yule kutoka kwa wapangaji, majirani na Mjumbe, hivyo basi akawa amefikia maamuzi ya kutamatisha uwepo wake hapo akiahidi kurejesha pesa yake ya miezi michache ilobakia ili aende kwa amani, habari za nyumba yake kusemwa vibaya hata na watu wanaokaa nje ya zile kuta, tena huku na kule, zilimfanya ahofie kama atapata mpangaji mwingine hivi karibuni.

Baada ya maelezo hayo, kila mtu akiwa amemwelewa na kasema ya kwake, swala likabakia huyo bwana BIGI atapatikanaje? Kila mpangaji hakuwa anakumbuka alimwona lini bwana huyo jua likiwa linawaka, mwenye nyumba akasema yeye siku hiyo atangoja mpaka amwone, hatoondoka hapo mpaka atakapotimiza adhma yake, basi na kikao kikaparangayika, mimi nikapata wasaa wa kumsalimu Bembela na hata kumkaribisha ndani kwangu tupate kuongea mambo kadhaa, Bembela akiongozana na shangazi yake, wakajumuika na sisi sebuleni.

Katika mengi waliyoongea, moja ya machache niliyopata kuyashika ni maneno fulani ya yule Shangazi. Mwanamke yule mzee, kwa muda mchache niliokaa naye na kumsikiza, nilibaini ni mtu mwenye uzoefu kamilifu na mambo haya ya gizani, kama ni wataalamu na mambo yao, walozi na vituko vyao, basi yu kwenye kina cha peke yake, na kwa namna alivyokuwa anaongea, niliiona kabisa picha kichwani mwangu kuwa yeye ndo' aliyefanya lile zoezi usiku ule, wala sio Bembela.

Mwanamke huyo alisema hivi, kwa nadhiri ile waliyoifanya siku ile alafu matokeo yake wakajikuta dhahama inamwangukia yule mtoto badala ya mwenyewe bwana BIGI, anaamini kabisa kilikuwa ni kiashiria kuwa mtoto yule ni sehemu ya ndani ya yule bwana ama ni bwana yule kabisa aliyegawanyika katika maumbo mawili, moja la mkewe na jingine la mtoto, kila umbo likiwa na kazi yake maalum, mtoto yule kazi yake kukusanya pesa na ndo maana alikuwa hakaukiwi na sarafu na mwanamke yule kazi yake ilikuwa kulinda usalama wa BIGI na pesa hizo.

Kwasababu hiyo, wale viumbe wawili, yaani mtoto na yule mwanamke, hawawezi wakawa binadamu walokamilika kamwe, wote watabakiwa kuwa nusu inayokamilisha mwili mmoja wa BIGI, na jukumu la BIGI kwao ni moja tu, kuwalisha na kuwahudumia viumbe hivyo kwa hali na mali.

Alisema: "ukihangaika na BIGI hutakaa ufanikiwe kamwe, hata ukitumia silaha gani, lakini ukicheza na ile mikono yake miwili, utamshinda kama ubua. Laiti tungepata chochote kinachomilikiwa na yule mwanamke kama vile tulivyopata sarafu zilizokuwa zinamilikiwa na yule mtoto, basi naye tungemwangamiza bwana BIGI akabakia mpweke kama binadamu wengine."

Hapo nikajikuta nakumbuka zile nywele kwenye viroba, nikawaza hazikuwa za mwanamke yule kweli? ... maana siku ile namwona kichwa chake kilikuwa cheupe peh, kimenyolewa, kitu ambacho sikuwahi kuelewa ni namna gani nywele hizo zilivyokuwa zinamea na kunyolewa mara kwa mara. Lakini pia nikakumbuka yale matone yake ya damu aliyoyachuruza siku ile wakati akipelekwa na bwana BIGI maliwatoni, nikabaki mwenyewe na hizo fikra nisithubutu kuunyanyua mdomo.

Kwani,

Binafsi niliyachukulia maneno ya yule mama kama nadharia tu, ya kwamba anajaribu kuoanisha mawazo yake kichwani na matukio yanayotokea ili kupata uhalisia ila hamna kitu cha uhakika ndani yake hivyo sikuyapa mazingatio sana, ila kilichofuata kesho yake kikanifanya nimkumbuke mama huyo na maneno ya kinywa chake.

Baada ya siku ile Baba mwenye nyumba kukaa mpaka usiku mkubwa akimngoja BIGI pasipo mafanikio, aliondoka akarejea kesho yake katika majira ya mchana akiwa ameongozana na mjumbe na wanaume wawili ambao niliwatambua kama ulinzi shirikishi.

Alipofika alitusalimu kama kawaida yake kisha akaulizia kama bwana yule ameonekana, kila mtu akasema hakumwona. Alipopata majibu hayo, akiwa ameongozana na mjumbe, aliufungua mlango wa BIGI kwa kutumia funguo yake ya ziada kisha wakazama humo ndani.

Baada ya muda kidogo, mara tukaitwa wanaume wengine wawili kwaajili ya kutoa msaada, mimi nikiwa mmojawapo, kuingia tu ndani pale chini sakafuni namwona BIGI amejilaza chali anatazama dari, taya yake ya chini imeelekea kushoto kama ilivyokuwa kwangu, pembeni yake amelala yule mke wake akiwa amefumba macho kama mtu aliyepotelea usingizini, wote wamevalia kaniki nyeusi.

Nikiwa bado nashangaa nikamsikia Mjumbe anasema,

"Haya, huyu amepooza, tumbebe tumpeleke kwenye gari la mzee ...(hapa alitaja jina la baba mwenye nyumba)."

Nakwambia sijui ni nini kilitokea hata leo hii sielewi, lakini nilijikuta akili yangu inanikumbusha upesi taswira ya yule shangazi yake Bembela.

Nilijiuliza hivi yule mwanamke alikuwa kweli ni shangazi yake kama alivyosema ama ndiye ........
@Analyse
 
Usicheze na bembele wewe... [emoji23][emoji23]
Sema big ni nyox sana. Bado ninapata uoga hata usiku. Big mshenz sana. Sasa baba mwenye nyumba alijuaje wamekata moto? Maana nilijua anaongozana na mjumbe kama ushahidi kutoa viti vya big nje kumbe wanaenda kutoa wagonjwa. Huyo mke na mtoto watakua misukule si bure.
 
Yule Jirani yangu wa kule Goba hakuwa mtu wa Kawaida - 11


"Baba fulani, mtoto wa BIGI amefariki."

Kusikia hizo habari ikabidi ninyanyuke kuketi, nikawaza ina maana lile swala la Bembela lilikuwa ndio hilo? Yaani amemuua yule mtoto? Ndicho nilichofikiria, nilinyanyuka upesi maana usingizi na mang'amung'amu yake yote yalikuwa yamekata, nikaenda kuoga na kuketi mahali kwanza ili nipate kuandika ujumbe wa 'excuse' kwenda kazini maana tayari 'enyewe nilikuwa n'shachelewa kwenda huko, ni saa nne kasoro ya asubuhi sasa, alafu baada ya hapo ndo' nikamtafuta Bembela kwa kumtumia ujumbe, niliona hiyo ni njia bora zaidi kwangu kuliko kumpigia simu kwasababu ya madhila yangu ya mdomo, nilipotuma ujumbe huo nikakaa kungoja.

Ni baadae, kama nusu saa mbele, nikiwa napata kifungua kinywa kwa tabu yangu ya mdomo ndipo nikasikia ujumbe umeingia kwenye simu, kutazama upesi nikakuta ni ujumbe kutoka kazini, kinyume kabisa na matarajio yangu, basi nikang'aka kwa hasira, nikaona sasa bora nipige simu huenda mhusika wangu yu mbali na kifaa chake cha mawasiliano, simu nayo ikaita lakini haikujibiwa.

Nilipopiga mara mbili, nikaachana nayo nikiamini zile 'missed calls' zilikuwa zinatosha, mhusika atakapoziona basi atanitafuta kwa muda wake, mimi nikaendelea na mambo yangu.

Baadae majira ya mchana, nikiwa hapohapo nyumbani, sijatoka kwenda mahali popote pale, nikaonana na mama yangu ambaye tangu naamka sikupata kuonana naye, alikuwa amerejea kutoka mahali fulani, na punde baada ya kufika na kunitazama usoni, kwa huruma ya mama, akaanza kunipa nasaha za janga lile lililonikumba.

Alinisihi sana niende hospitali na tayari alishamweleza baba kuhusu hali yangu hiyo, hata na hivyo alishangaa sana mpaka muda huo sikuwa nimejigusa kwenda kutafuta tiba, alisema nina roho ngumu kweli, lakini kitu ambacho hakujua mimi mwenzake tayari nilishaogea ile dawa nlopewa na Bembela tangu asubuhi, dawa ya kuondoa mabaki yote yalotupwa na wabaya wangu kwa mujibu wa maneno yake, nikawa naamini dawa hiyo huenda ikanisaidia, niwe tu mvumilivu.

Basi masaa ya siku hiyo yakazidi kusogea, bado nipo hapo nyumbani na bado sijapokea ujumbe wowote toka kwa Bembela, kila nilipopata nafasi nilitazama simu yangu lakini sikuambulia kitu, sio 'call' wala 'message', mwanamke yule hakunitafuta kabisa, mpaka giza jepesi linaingia, kimya tu.

Nikajaribu kuongea na mke wangu ampigie simu Mama Tarimo kumuulizia Bembela kwani nina shida naye, nilimweleza ni shida ya dawa ya ugonjwa wangu ili kupunguza maswali yake mengi, mwanamke huyo akaridhia na punde akapiga simu ambayo aliiweka 'loudspeaker', kidogo simu kuita ikapokelewa na Mama Tarimo, mke wangu akamwelezea shida yangu, mama huyo akamjibu: "nimetoka nyumbani majira ya mchana mpaka sasa bado sijarejea, nilienda hospitali kumwona mgonjwa wangu, walakini niko njiani narudi, ningoje kidogo nikifika nitamtazama."

Baada ya hapo kazi ikawa ni kungoja. Kichwani najiuliza kwanini Bembela alifanya kile kitendo? Kwanini mtoto? Sasa kwa kufanya hivyo tofauti yetu na BIGI itakuwa nini kama wote ni wauaji? Yani nilikuwa na hamu kweli ya kuongea naye, nilihisi maswali yangu yananikaba kooni nashindwa kuhema, naona kama muda hauendi.

Kweli baadae, kama lisaa hivi kupita, Mama Tarimo akatimiza ahadi yake kwa kupiga simu, nilimwona mke wangu akinijia upesi huku simu ameiweka 'loudspeaker', aliponikaribia nikasikia Mama Tarimo akisema, "Nimefika lakini Bembela hayuko nyumbani, sio yeye wala shoga yake niliyemwona, nadhani wametoka, wakirejea nikafanikiwa kuwaona basi ntakujuza."

Baada ya hapo hata mimi binafsi nilipojaribu kumpigia Bembela sikumpata, sio tena hapokei simu bali hapatikani hewani kabisa. Hata yule shoga yake mke wangu alipojaribu kumtafuta kwa namba alonayo, naye hakumpata hewani! Sikujua nini kiliwakuta? Nilijipata najawa na hofu kifuani mwangu nikiomba yote yawe salama maana mpaka hapo sikuwa na lingine la kufanya zaidi ya hilo.

Kama utani, usiku ule ukapita kimya, kesho yake asubuhi niliamka mapema majira ya saa kumi na mbili, bado taya yangu inasumbua na imegoma kurejea kwenye hali yake ya kawaida, ile dawa ninayotumia bado haijanisaidia, mara kidogo nikiwa najiandaa ndipo simu yangu ikapokea ujumbe kutoka namba niliyoitambua upesi kuwa ni ya Bembela, ujumbe huo ulisomeka hivi:

"Habari yako shemeji, nimeona ulinitafuta tunaweza tukaongea saa hii kama una muda."

Haraka nikamrudishia majibu kwamba ni vema tukachat maana mimi bado siwezi kuongea vizuri, basi baada ya hapo tukalowea kwenye 'messages'. Nilimuuliza yuko wapi, hakutaka kuniambia, alichosema yeye yuko mbali ila salama, huko ameongozana na shangazi na shoga yake kwasababu fulani ambayo nayo pia hakutaka kuniambia.

Nikamuuliza kuhusu kifo cha mtoto wa BIGI, hapo kidogo akakwama, nadhani aliogopa kujibu swala hilo kwa njia ya ujumbe ama aliona hatoweza kulielezea vema vile anavyotaka yeye basi muda kidogo akaamua kunipigia simu kwaajili ya kuniweka sawa. Mwanamke huyo, kwa sauti ya chini, alinambia hafahamu chochote kuhusu kifo cha yule mtoto, yeye alichokifanya usiku ule ni kilekile alichoelekezwa na mtaalam kwaajili ya kumwadabisha BIGI na si vinginevyo.

Kwa maneno yake alisema, "mtaalam aliniambia nikikamilisha zoezi la kunuwia, kukoga na kumwaga dawa kisha nikamwita nikiwa nimeshikilia kitu ambacho ni mali yake binafsi basi bwana huyo atapoteza nguvu zake zote, na tena nitamkuta pale kibarazani akiwa uchi wa mnyama ili kila mtu apate kumshuhudia na kumjua kuwa ni mchawi, lakini ajabu nilipofanya hivyo asubuhi yake saa kumi na moja, nilimkuta yule mtoto, akiwa uchi wa mnyama, ameshikilia nguzo ya kibarazani, mwili wake hauna hata tone la pumzi. Mikononi mwake na miguu pake pana sarafu zile za hamsini hamsini!"

Kwakweli maelezo hayo yakaniacha mataa ya bumbuwazi. Kuna muda nilihisi nasikiliza tamthilia lakini kumbe ndo uhalisia wenyewe, nikaamini kweli ya dunia ni mengi sana!

Mwanamke huyo aliendelea kuniambia ya kwamba wakati mwili wa mtoto huyo ukiwa hapo kibarazani pasipo uhai, shangazi yake alimshuhudia BIGI kwa macho yake mwenyewe akiwa amesimama mwisho wa korido, amesimama hapo akiwa anamtazama kama paka aliyefura kwa kipigo, bila kufanya jambo akajiondokea zake na hapo ndipo wakakata shauri kuyeya hapo nyumbani baada ya shangazi yake kumsihi.

Hivyo mpaka wanaondoka, yeye, shangazi yake na shoga yake kwenda huko waliko, mwili wa yule mtoto ulikuwa palepale, hawakujua tena nini kilichofuatia baada ya hapo na hawakuwasiliana na mtu yoyote wa pale nyumbani mpaka asubuhi ya siku hiyo ambapo kabla hajawasiliana na mimi alipata kuongea na mwenye nyumba kwanza.

Baada ya kuhitimisha maongezi hayo, mimi niliendelea na maandalizi yangu, nilipokamilisha nikapitia hospitali kucheki tatizo langu maana niliona ni vema pia nikafanya hivyo, lakini huko kote hamna nilichofanya zaidi ya kupoteza tu pesa maana hamna chochote nilichoambwa na daktari, nikarejea zangu nyumbani, Afrikana.

Baadae majira ya jioni nilipata wasaa wa kuongea na wazazi wangu nikawaeleza juu ya yale niliyoambiwa kule hospitali, tena nikiongea kwa tabu sana, kuna muda machozi yalikuwa yananilenga nilipokuwa najitazama kwenye kioo nikiona namna nilivyobadilika kuwa wa ajabu, yani nakuwa mlemavu huku najiona, lakini ndo' hivyo sikuwa na namna.

Baba yangu alinishauri tufanye namna ya kumwona daktari bingwa wa mifumo ya fahamu, Neurologist, ili apate kunisaidia lakini mimi sikuwa radhi kabisa na hilo kwasababu niliamini lile tatizo nililokuwa nalo lilikuwa ni la kiimani zaidi kuliko hospitali, lakini kwasababu nalimfahamu mzee wangu vema, sikumwambia kitu maana hata kama ningemwelezea basi asingeniafiki hata kidogo, si mtu anayeamini kwenye mambo ya kishirikina na mimi simlaumu maana mambo haya kama hujapata kuyaona kwa macho yako ya nyama basi hutakaa uamini,kila atakayekueleza utaona ni ngano na visasili tu, hata mimi nilikuwa vivyo hivyo lakini nilikuja kujifunza katika njia ngumu hapo mbeleni.

Nakumbuka mama yangu alikuwa akinikandika mafuta ya Mwamposa na sala kedekede, lakini tena naendelea kuogea ile dawa nlopewa na Bembela, yaani tafarani tu, sijui hata kipi kilikuja kunisaidia kuniponya kati ya hivyo viwili. Mungu mwenyewe anajua.

Baada ya siku kama tatu hivi kupita baada ya kile kikao kidofo na wazazi, nilirejea nyumbani kule Goba, na kesho yake tu baada ya kufika, alikuja mwenye nyumba akitaka kukaa kikao na sisi wote kwa pamoja, siku hiyo ilikuwa 'weekend' kama si Jumamosi basi Jumapili, na taarifa ya kikao nadhani kila mmoja alikuwa ameshaipata, mimi binafsi niliupokea ujumbe siku mbili nyuma yake, hivyo kwenye kile kikao kulikuwapo na watu karibia wote, mtu pekee mzima wa afya ambaye hakuwapo ni BIGI, na hiyo haikuwa ajabu, tulishazoea, Bembela yeye alifika wakati kikao kimeshaanza, alikuja akiongozana na shangazi yake lakini mwanamke huyo mzee hakupata kujiunga na sisi kikaoni isipokuwa Bembela pekee.

Katika kikao hicho, mwenye nyumba alieleza kuwa jambo pekee lililomleta na kutukutanisha na sisi hapo ni swala la mpangaji mwenzetu ambaye alikumbwa na ile kadhia ya mwanae kufariki katika mazingira ya kutatanisha mbele ya kibaraza, bwana huyo alisema namna alivyokuwa anapitia matatizo na vyombo vya usalama, mathalani polisi na ulinzi shirikikishi, kwasababu ya mpangaji yule ambaye alienda mbele zaidi kumwita 'mpangaji asokuwa na mkataba'.

Alituambia pia namna alivyopokea malalamiko kadha wa kadha kumhusu bwana yule kutoka kwa wapangaji, majirani na Mjumbe, hivyo basi akawa amefikia maamuzi ya kutamatisha uwepo wake hapo akiahidi kurejesha pesa yake ya miezi michache ilobakia ili aende kwa amani, habari za nyumba yake kusemwa vibaya hata na watu wanaokaa nje ya zile kuta, tena huku na kule, zilimfanya ahofie kama atapata mpangaji mwingine hivi karibuni.

Baada ya maelezo hayo, kila mtu akiwa amemwelewa na kasema ya kwake, swala likabakia huyo bwana BIGI atapatikanaje? Kila mpangaji hakuwa anakumbuka alimwona lini bwana huyo jua likiwa linawaka, mwenye nyumba akasema yeye siku hiyo atangoja mpaka amwone, hatoondoka hapo mpaka atakapotimiza adhma yake, basi na kikao kikaparangayika, mimi nikapata wasaa wa kumsalimu Bembela na hata kumkaribisha ndani kwangu tupate kuongea mambo kadhaa, Bembela akiongozana na shangazi yake, wakajumuika na sisi sebuleni.

Katika mengi waliyoongea, moja ya machache niliyopata kuyashika ni maneno fulani ya yule Shangazi. Mwanamke yule mzee, kwa muda mchache niliokaa naye na kumsikiza, nilibaini ni mtu mwenye uzoefu kamilifu na mambo haya ya gizani, kama ni wataalamu na mambo yao, walozi na vituko vyao, basi yu kwenye kina cha peke yake, na kwa namna alivyokuwa anaongea, niliiona kabisa picha kichwani mwangu kuwa yeye ndo' aliyefanya lile zoezi usiku ule, wala sio Bembela.

Mwanamke huyo alisema hivi, kwa nadhiri ile waliyoifanya siku ile alafu matokeo yake wakajikuta dhahama inamwangukia yule mtoto badala ya mwenyewe bwana BIGI, anaamini kabisa kilikuwa ni kiashiria kuwa mtoto yule ni sehemu ya ndani ya yule bwana ama ni bwana yule kabisa aliyegawanyika katika maumbo mawili, moja la mkewe na jingine la mtoto, kila umbo likiwa na kazi yake maalum, mtoto yule kazi yake kukusanya pesa na ndo maana alikuwa hakaukiwi na sarafu na mwanamke yule kazi yake ilikuwa kulinda usalama wa BIGI na pesa hizo.

Kwasababu hiyo, wale viumbe wawili, yaani mtoto na yule mwanamke, hawawezi wakawa binadamu walokamilika kamwe, wote watabakiwa kuwa nusu inayokamilisha mwili mmoja wa BIGI, na jukumu la BIGI kwao ni moja tu, kuwalisha na kuwahudumia viumbe hivyo kwa hali na mali.

Alisema: "ukihangaika na BIGI hutakaa ufanikiwe kamwe, hata ukitumia silaha gani, lakini ukicheza na ile mikono yake miwili, utamshinda kama ubua. Laiti tungepata chochote kinachomilikiwa na yule mwanamke kama vile tulivyopata sarafu zilizokuwa zinamilikiwa na yule mtoto, basi naye tungemwangamiza bwana BIGI akabakia mpweke kama binadamu wengine."

Hapo nikajikuta nakumbuka zile nywele kwenye viroba, nikawaza hazikuwa za mwanamke yule kweli? ... maana siku ile namwona kichwa chake kilikuwa cheupe peh, kimenyolewa, kitu ambacho sikuwahi kuelewa ni namna gani nywele hizo zilivyokuwa zinamea na kunyolewa mara kwa mara. Lakini pia nikakumbuka yale matone yake ya damu aliyoyachuruza siku ile wakati akipelekwa na bwana BIGI maliwatoni, nikabaki mwenyewe na hizo fikra nisithubutu kuunyanyua mdomo.

Kwani,

Binafsi niliyachukulia maneno ya yule mama kama nadharia tu, ya kwamba anajaribu kuoanisha mawazo yake kichwani na matukio yanayotokea ili kupata uhalisia ila hamna kitu cha uhakika ndani yake hivyo sikuyapa mazingatio sana, ila kilichofuata kesho yake kikanifanya nimkumbuke mama huyo na maneno ya kinywa chake.

Baada ya siku ile Baba mwenye nyumba kukaa mpaka usiku mkubwa akimngoja BIGI pasipo mafanikio, aliondoka akarejea kesho yake katika majira ya mchana akiwa ameongozana na mjumbe na wanaume wawili ambao niliwatambua kama ulinzi shirikishi.

Alipofika alitusalimu kama kawaida yake kisha akaulizia kama bwana yule ameonekana, kila mtu akasema hakumwona. Alipopata majibu hayo, akiwa ameongozana na mjumbe, aliufungua mlango wa BIGI kwa kutumia funguo yake ya ziada kisha wakazama humo ndani.

Baada ya muda kidogo, mara tukaitwa wanaume wengine wawili kwaajili ya kutoa msaada, mimi nikiwa mmojawapo, kuingia tu ndani pale chini sakafuni namwona BIGI amejilaza chali anatazama dari, taya yake ya chini imeelekea kushoto kama ilivyokuwa kwangu, pembeni yake amelala yule mke wake akiwa amefumba macho kama mtu aliyepotelea usingizini, wote wamevalia kaniki nyeusi.

Nikiwa bado nashangaa nikamsikia Mjumbe anasema,

"Haya, huyu amepooza, tumbebe tumpeleke kwenye gari la mzee ...(hapa alitaja jina la baba mwenye nyumba)."

Nakwambia sijui ni nini kilitokea hata leo hii sielewi, lakini nilijikuta akili yangu inanikumbusha upesi taswira ya yule shangazi yake Bembela.

Nilijiuliza hivi yule mwanamke alikuwa kweli ni shangazi yake kama alivyosema ama ndiye ........
[emoji419][emoji419]
 
Haya haya wale watukutu na wapiga kelele wakiongozwa na dr namugari njooni muendelee na mitkasi yenu ya uhariri

[emoji23][emoji23]
[emoji23][emoji23][emoji23] hao watu wana team yao sasa hivi wameamia kwa sodoku habari na hoja wanarudia kusoma story yake wanamwambia ole wako tukute chai jiandae na umesema story ya kweli
 
Back
Top Bottom