Jiunge nami kusema hapana kwa udhalilishaji na ubaguzi anaoufanya mmliki wa clock tower café Iringa

Jiunge nami kusema hapana kwa udhalilishaji na ubaguzi anaoufanya mmliki wa clock tower café Iringa

Weee Siyo wa Kutulalamikia Hapa

Unakuwaje M/sheria
Una Ofisi Nzuri ila Huna Choo?
Usichukulie Poa Nyumba/Ofisi ni Choo
lazma tupze sauti, hatuwezi kukubali huu ubaguzi, waziri lazma asikie , jpm lazma asikie
 
Eti vyoo havipo kila baada ya hatua mbili...kwa hiyo kuzidiwa kunatokeaga ghafla tu ndani ya sekunde???...na ukijifanya msamaria mwema kwa kila anayezidiwa sehemu kama kariakoo na mzunguko kama ule utafanya usamaria wema kwa watu wangapi mwisho si choo chako cha biashara kitageuka public toilet....hekima gani unataka nitumie wakati hekima ya wewe kuomba kwanza kabda ya kuingia huna...aya umeingia bila kuomba unatoka unashindwa hata kuzuga ujifanye unanunua vimaji vidogo badala yake unajibu eti mimi nanunuaga chakula hapa...jifunze kuheshimu biashara za watu pale sio kwako kama kuna huduma unaiomba omba kwanza utapewa but si unatumia bila kuomba alafu ukiulizwa unaleta ujinga...ukitaka watu wakufanyie ustaarabu na ubinadamu kuwa kwanza mstaarabu wewe
unazidi kuyakuza, wewe ni mbaguzi, jiandae na TRA wanajua kukwepa kwako kodi, jiandae na watu wa Afya na OSHa, watumishi hapo hawajapima, hujakidhi vigezo, na siyo hayo tu, kuna mengi ya ukwepaji kodi tutaweka hadharani na manyanyaso ya wafanyakazi hawana mikataba, hawana nssf , unauza hutoi risiti, hatuta kuacha,
 
Hata Mimi namshangaa huyu wakili Ana tatizo Sio Siri na hafai kuwa mteja wa hiyo cafe yenye hadhi kubwa.Huyo mumiliki ana haki ya kumpiga marufuku kukanyaga hapo
siyo tatizo, ngoja siku likukute wewe, mbona wazungu na wahindi wakienda pale wanafanya watakavyo?
 
Mimi nilipe kodi ya pango na mikodi mingine kibao wewe uje unye utoke bila kununua hata maji?Hata mimi sikuelewi
ni mnunuzi wa kila siku, yaani mteja, na nlikuwa kwenye mfungo na si ajabu tumbo liliniuma kwa kula chakula kilichochacha toka kwao, wameniona sina maana, hawa hawafai kabisa
 
Mkuu jifunze kusubiri muda wakuchimba dawa kama umeshindwa kulipia choo cha stendi.

Acha mazoea na Ofisi za watu, kwanza hujasema kama ulitoa salamu ulipoingia? kwanini usiombe mwanzo kwa vile unajua ni kwa ajili ya wateja ili uruhusiwe.?

Wakili unafeli sana, swala la mistari minne unaeleza page nzima unarudia yale yale
imeandikwa kukiwa na jazba sana, huu ubaguzi niliusikia afrika kusini kumbe ndio mbaya namna hii, hpna aisee, msiombe kubaguliwa, unaweza ukajiskia si mnyonge bali zwazwa na anayekubagua anakuwa KIFUTU
 
ila mkuu unaweza ukawa na kosa kwa namna flani na pia huyo mmiliki akutumia aproach nzuri kama binadamu mwenzake any way pole sana mkuu
huyu muhindi ndivyo alivyo, anapenda sura nyeupe zinazoacha tips only, huwezi endana naye kama ngozi ni nyeusi, leo naitisha press conference kulizungumzia
 
kuna watu hapa tanzania wanajiona kama wao ndio wao, hii si mara ya kwanza

Nchi ytu lakini bafo tunyanyasike, pole kak ngoda tuko pamoja huyu awe mfano
asante , watu wanabeza kwakuwa waop hawajabaguliwa, tena na mgeni ambaye ana cheti cha NATURALISTION yaani uraia wa kuomba kwa machozi ya damu, okay tusikubali kuwa watumwa kwenye nchi huru
 
aiseee chalii yangu endeleeni kulima tu na mdhulumiwe mazao yenu
wakulima si mmerudishiwa korosho zenu mkazipande tena?huna habari?
mmeambiwa mazao tani moja yasilipiwe ushuru, akawafundisha ujanja, unabeba fuso tani moja toka mbeya mpaka dar, unarudi tena mbeya unabeba nyingine mpaka zifike 10, na kumbuka fuso moja unakwepa ushuru wa elfu 3, za kuambiwa changanya na zaako
 
ni mnunuzi wa kila siku, yaani mteja, na nlikuwa kwenye mfungo na si ajabu tumbo liliniuma kwa kula chakula kilichochacha toka kwao, wameniona sina maana, hawa hawafai kabisa
Pale cafe na hospital Sio mbali ungekimbilia vyoo vya hospital
siyo tatizo, ngoja siku likukute wewe, mbona wazungu na wahindi wakienda pale wanafanya watakavyo?
Na nyie mumezidi kuunga mkono watu weupe so ukale kwa waswahili wenzie uwaungishe riziki? Wao huwa hawali hoteli za waswahili wewe Nini kinakupeleka kwa watu weupe? Ulishawahi ona mhindi anakula hoteli ya mswahili au kwa mama ntilie mswahili ? Wewe msomi wawezeshe waswahili wenzio kwa kula hoteli na cafe za waswahili wenzio
 
Kiukweli hiyo cafe naifaham vizuri tuu...tena inatoa huduma nzuri sana na customer care yake ipo vizur kiujumla....pale huwa tunakutana watu wa jamii tofauti lakin sijawahi shuhudia ubaguzi ulio nenwa na huyu wakili kanjanja....ni wivu tuu kwa kweli pale wapo viongoz wakubwa tu wa mkoa na bei za vyakula vyao ni nafuu sana....cjui huyu mtu anasema anabaguliwa kwa kipi....nadhan kuna ustarabu hakuufuta...mmilik wa cafe..ni mtu poa sana tena ni wakujishusha kweli kweli...he z very smart kwa kweli...tujaribu kutunza brand za watu...mods naombeni futen huu uzi..upo kwa ajili ya kuharibu biashara za watu..
Hayo ni maoni yako, acha na wengine watoe maoni yao. Usitake uzi ufutwe
 
Mkuu mimi sikubaliani na wewe na ninahisi wewe ndo ulikuwa na makosa...choo ni kwa ajili ya watu wanaopata huduma hapo na si kwa ajili ya nyi wapita njia...eti kwa sababu tu ushawahi pata huduma hapo so unaona ndo sehemu ya kwenda kumaliza haja zako mda wowote ukijiskia katika mizunguko yako...choo ni kwa ajili ya watu wanaopata huduma kwa mda ule pale
Hata mimi naungana na wewe
 
Duuuh!!
Mwezi mtukufu huu(kwa mujibu wenu) ni mwezi wa kutenda mema, sasa nashindwa kuelewa hili unalolitenda ni jema au la!!
Anyway mie naona makosa kwenu nyote, na hapa tumesikia upande wako tu hatuujui huo upande mwingine.
 
Wakili mbumbumbu kabisaaa, unazalilisha taaluma yetu we mbururaa, yaani unaandika maneni elf moja kwa kitu ambacho ungekisema tu kwa maneno matatu? Alafu vitu personal usivifanye vya jamii nzima, mwisho umetoa mawasiliano yako sasa ili iweje watu wakupe pole kwa mawasiliano hayo au? Hahahaaha akili ndogo sanaa.
 
Kikubwa usizoee sana ofisi za watu ,,choo kipo kwa ajili ya wateja tu na sio wapita njia ,Iringa vyoo ni vingi tu ,toa 200 acha kuzoea


Kuna hichi choo cha stand kimetazamana na mahala wamachinga wamepanga vitu ,,ukiwa mteja wa kila siku unatoa 100 tu.
Hili ndo tatizo LA watanzania kwahiyo ukiizoea tu sehemu unaanza kuhitaji mtelemko!!!? Na hicho ndo kilichomponza jamaa.
 
Ukome na wewe kutwaa kwa vyoo vya watu tengenwza chako au ukome kufturu alfajiri.
 
We wakili km ulivyosema,unashindwa vipi kumshughulikia huyo fala,unamwogopa sababu gabacholi?ulitakiwa ww ndo uwe mfano umtengeneze maana ashazoea huyu.fikiria wakulima je wakija hapo inakuaje?
Mi naweza kuja nikakojoa akiniletea ufala huo ni vibao tu no excuse pumbavu
 
Back
Top Bottom