Ngongo
Platinum Member
- Sep 20, 2008
- 20,654
- 35,887
Mrema apelekwa India kwa matibabu, Kalembo akimbizwa hospitali
*MKUU WA MKOA TANGA AISHIWA NGUVU NA KUKIMBIZWA HOSPITALI
Mashaka Kibaya, Korogwe na Boniface Meena
WAKATI mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema yuko nchini India kwa matibabu ya ugonjwa wa kisukari, mkuu wa mkoa wa Tanga, Meja Jenerali Said kalembo aliishiwa nguvu akiwa ziarani na kukimbizwa hospitalini.
Mrema, ambaye aliondoka wiki iliyopita, atakuwa akitibiwa Hospitali ya Appollo iliyo jijini Bambay.
Kaimu katibu mkuu wa TLP, Hamad Tao alisema Mrema amekwenda India ili kukutana na wataalam wa ugonjwa huo.
"Amekwenda tangu wiki iliyopita na atakaa huko kwa wiki tatu ili wataalam waweze kumpatia matibabu,"alisema Tao.
Alisema kuwa huo umekuwa ni utaratibu wa Mrema, ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, kwenda India kutibiwaugonjwa huo ambao umekuwa ukimsumbua kwa muda sasa.
Alisema kuwa Mrema anagharimia mwenyewe matibabu yake na kwamba hatumii fedha za TLP.
"Amejigharimia mwenyewe na si TLP iliyomgharimia... amebakiza wiki mbili za matibabu kabla hajarejea nchini," alisema Tao.
Wakati huo huo, mkuu wa mkoa wa Tanga, Meja Jenerali Said Kalembo jana alikatiza ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo kwenye Halmashauri ya Korogwe baada ya kuugua ghafla.
Kalembo alijisikia vibaya akiwa ukumbi wa halmashauri majira ya saa 3:00 asubuhi na alionekana kuhisi kizunguzungu na hivyo kuinamia meza kwa muda, lakini baadaye alipata nafuu na kuendelea kuzungumza na watendaji wa halmashauri hiyo.
Kalembo aliendelea na ratiba na kuelekea kwenye mradi wa maji ambako hali yake ilionekana kubadilika na akaanza kupepesuka na hivyo kusaidiwa kuingia kwenye gari lake na mkuu wa wilaya ya Korogwe na baadaye akarudishwa hoteli ya Motel White Parot alipofikia kwa mapumziko.
Mganga mkuu wa wilaya ya Korogwe, Dk Rashidi Said na mwenzake walifika hotelini hapo kumpatia huduma ya kwanza na kuongezewa maji.
Baadaye Kalembo alitolewa hotelini hapo akiwa ametundikiwa dripu na kuingizwa kwenye gari lake kupelekwa Hospitali ya Bombo, Tanga. Tukio hilo lilionekana kuwachanganya viongozi wa wilaya hiyo.
Chanzo Mwananchi.
Hii sasa kali tumwamini Bwana Tao au kiranja.Wakati mwingine kudandia maneno ya mitaani si vizuri tafadhali Mkuu kiranja omba radhi jamvi kwa kuleta habari za mitaani
Mashaka Kibaya, Korogwe na Boniface Meena
WAKATI mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema yuko nchini India kwa matibabu ya ugonjwa wa kisukari, mkuu wa mkoa wa Tanga, Meja Jenerali Said kalembo aliishiwa nguvu akiwa ziarani na kukimbizwa hospitalini.
Mrema, ambaye aliondoka wiki iliyopita, atakuwa akitibiwa Hospitali ya Appollo iliyo jijini Bambay.
Kaimu katibu mkuu wa TLP, Hamad Tao alisema Mrema amekwenda India ili kukutana na wataalam wa ugonjwa huo.
"Amekwenda tangu wiki iliyopita na atakaa huko kwa wiki tatu ili wataalam waweze kumpatia matibabu,"alisema Tao.
Alisema kuwa huo umekuwa ni utaratibu wa Mrema, ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, kwenda India kutibiwaugonjwa huo ambao umekuwa ukimsumbua kwa muda sasa.
Alisema kuwa Mrema anagharimia mwenyewe matibabu yake na kwamba hatumii fedha za TLP.
"Amejigharimia mwenyewe na si TLP iliyomgharimia... amebakiza wiki mbili za matibabu kabla hajarejea nchini," alisema Tao.
Wakati huo huo, mkuu wa mkoa wa Tanga, Meja Jenerali Said Kalembo jana alikatiza ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo kwenye Halmashauri ya Korogwe baada ya kuugua ghafla.
Kalembo alijisikia vibaya akiwa ukumbi wa halmashauri majira ya saa 3:00 asubuhi na alionekana kuhisi kizunguzungu na hivyo kuinamia meza kwa muda, lakini baadaye alipata nafuu na kuendelea kuzungumza na watendaji wa halmashauri hiyo.
Kalembo aliendelea na ratiba na kuelekea kwenye mradi wa maji ambako hali yake ilionekana kubadilika na akaanza kupepesuka na hivyo kusaidiwa kuingia kwenye gari lake na mkuu wa wilaya ya Korogwe na baadaye akarudishwa hoteli ya Motel White Parot alipofikia kwa mapumziko.
Mganga mkuu wa wilaya ya Korogwe, Dk Rashidi Said na mwenzake walifika hotelini hapo kumpatia huduma ya kwanza na kuongezewa maji.
Baadaye Kalembo alitolewa hotelini hapo akiwa ametundikiwa dripu na kuingizwa kwenye gari lake kupelekwa Hospitali ya Bombo, Tanga. Tukio hilo lilionekana kuwachanganya viongozi wa wilaya hiyo.
Chanzo Mwananchi.
Hii sasa kali tumwamini Bwana Tao au kiranja.Wakati mwingine kudandia maneno ya mitaani si vizuri tafadhali Mkuu kiranja omba radhi jamvi kwa kuleta habari za mitaani