JKT waliorudishwa nyumbani watakiwa makambini

JKT waliorudishwa nyumbani watakiwa makambini

Sio wale. Hawa waliripot jkt feb wakaa kaa km week2 then wakahairishiwa sasa mambo yameiva wameitwa. Ndo wanaenda kuanza
Siku hizi naona jeshi haliko serious kivileee! Kuna privacy flani haipo tena! Yani geshi watu wanaingia ingia tu na kutoka,mara wengine wanagoma!! Sijui imekuwaje?
Au anko magu-mashi kuna taratibu aliziharibu?
Mara mnaambiwa muende home,mara rudini! Dooh
 
Wangetafuta maisha mengine nje ya mifumo ya jeshi.Tukumbuke hawa madogo walitumikishwa more than two years halafu wakafukuzwa kama wahalifu kisa walidai haki zao.
 
Tatizo hujaelewa. Kwakuwa sio muhusika.ila wahusika wameelewa
Siku hizi naona jeshi haliko serious kivileee! Kuna privacy flani haipo tena! Yani geshi watu wanaingia ingia tu na kutoka,mara wengine wanagoma!! Sijui imekuwaje?
Au anko magu-mashi kuna taratibu aliziharibu?
Mara mnaambiwa muende home,mara rudini! Doo
 
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Charles Mbuge, amewataka vijana waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa kujitolea kwa mwaka 2020/2021 na kurejeshwa nyumbani mwezi Februari mwaka huu kurejea makambini.

Kaimu mkuu wa utawala wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kanali Hassan Mabena, amewaambia wanahabari kuwa vijana hao wanatakiwa kuripoti kwenye makambi waliyopangiwa awali.

Aidha Kanali Mabena amesema kuwa kuwa JKT wameingia makubaliano na Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) kwa ajili ya vijana kupata elimu ya vitalu.

Mwezi Februari mwaka huu, Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) alitangaza kuwarejesha nyumbani zaidi ya vijana 12,000, hadi ambapo wangetangaziwa tena.
Lakini nao mazoea ya kuleta au kujifanya Wana harakati wakome ,unaletaje wanaharakati katika chombo ambacho misingi yake hakiko hivyo na wakati watafuta ajira ,hivi taifa Hili kila mtu akianza andamana kisa akaajiliwe itakuaje,
 
Huenda wakawa wanapita tu kuna mahala wanaenda,
 
Usikute ndo vibaka wa muda huu. Maana matukio ya ukwapuaji yameongeza Dar. Juzi rafiki yangu kapigwa roba na kuchukuliwa simu.
Bora warudishe huko. Pia, next time CDF afanye upembuzi kabla ya kufikia maamuzi.

Hujaelewa kitu kabisaa. ❌❌❌❌❌❌❌❌❌❌❌❌❌❌. 00%

Hawa sio wale waliofukuzwa..
 
Naona watu wanachanganya kati ya wale wahaini na, wale wengine waliorudishwa kisa upungugu wa pesa zilizopelekwa kwenye kampeni.
 
Huenda wakawa wanapita tu kuna mahala wanaenda, huenda kuna mabadiliko makubwa huko wanakoenda kutakuwa na uozo mwingi

Kitendo cha kukubali kurudi tena kambini moja ya kipimo cha Uzalendo. Napanga mizigo yangu nirudi
Wanaorudishwa ni wale walioingia kwa ajili ya kuanza kozi ya jkt kwa kujitolea mwaka huu mwezi wa pili ila wakarudishwa nyumbani bila kuanza kozi.
Tetezi zilienea kua mh. marehemu Rais alisema hana bajeti ya kuwalisha huko makambini hivyo warudishwe nyumbani.
Siyo wale waliogoma wakafukuzwa...taarifa iwekwe sawa.
 
Wanaorudishwa ni wale walioingia kwa ajili ya kuanza kozi ya jkt kwa kujitolea mwaka huu mwezi wa pili ila wakarudishwa nyumbani bila kuanza kozi.
Tetezi zilienea kua mh. marehemu Rais alisema hana bajeti ya kuwalisha huko makambini hivyo warudishwe nyumbani.
Siyo wale waliogoma wakafukuzwa...taarifa iwekwe sawa.
Hata mm sijasema waliofukuzwa. Yes unalosema uko sawa
 
Usikute ndo vibaka wa muda huu. Maana matukio ya ukwapuaji yameongeza Dar. Juzi rafiki yangu kapigwa roba na kuchukuliwa simu.
Bora warudishe huko. Pia, next time CDF afanye upembuzi kabla ya kufikia maamuzi.
Sio hao unaowasemea hawa hawajui hata kusema jambo afande fatilia vizuri habari..ngoja wakafuliwe waje wampige roba vizuri rafiki yako
 
Wangetafuta maisha mengine nje ya mifumo ya jeshi.Tukumbuke hawa madogo walitumikishwa more than two years halafu wakafukuzwa kama wahalifu kisa walidai haki zao.
Usikurupuke soma habari taratibu
 
Heheheh! Ukiona hivyo ujue kuna kazi ya kumwaga zege imepatikana sehemu.
Kule huwa hakuna ubaguzi wa elimu kazi mtashiriki wote yaani kila kitu ni sawa sawa, hakuna cha dawili wala ngorongoro wote mtafanya kazi kwa scale moja. Hiyo elimu utaiacha getini na utakutana na elimu mpya ya kijeshi ambayo inaongozwa na syllabus kuu inayoitwa NIDHAMU.

Ni experience nzuri sana kutumikia jeshi letu.
 
Kule huwa hakuna ubaguzi wa elimu kazi mtashiriki wote yaani kila kitu ni sawa sawa, hakuna cha dawili wala ngorongoro wote mtafanya kazi kwa scale moja. Hiyo elimu utaiacha getini na utakutana na elimu mpya ya kijeshi ambayo inaongozwa na syllabus kuu inayoitwa NIDHAMU.

Ni experience nzuri sana kutumikia jeshi letu.
Ikiwa hivyo, hebu tuambie kwanini wameitwa la saba na form four (failures) pekee?

Au unataka kutuambia mwanajeshi ambaye ni daktari naye anashika kwanja kufyeka?
 
Ikiwa hivyo, hebu tuambie kwanini wameitwa la saba na form four (failures) pekee?
Nafikiri tujikumbushe hotuba ya CDF wakati wa commission ya maofisa wapya, alisema wanafikiria kuja na mfumo mpya katika suala hili la kujitolea kwa vijana, nachelea kusema ni mfumo upi lakini acha wao wenyewe watakuja na ufafanuzi (Mawazo binafsi haya Mkuu)
 
Back
Top Bottom