Mm nina mawazo sawa na Spika pia.. Ni hivi, ingekuwa Mh. Lissu bado yuko hospitalini, au karudi nchini kwa wananchi waliomchagua anapaswa kulipwa mshahara na stahiki zake zote kama kawaida, ila sababu ni muda sasa katoka hospitali na yuko huko nje ya nchi anaitwa kila kituo cha TV duniani na kupata kusema anachojisikia, na ku attack bunge na serikali, mm nadhani hastahili kulipwa mshahara hadi arudi nchini na kama hajapona kwanini anatembea nchi zote hizo ktk media mbalimbali na kuchafua nchi yake..? Hatuungi mkono kabisa na tunalaani kwa vikali kitendo cha kushambuliwa kwa risasi alichofanyiwa Mh. Lissu hilo lieleweke wazi, that is our position, ila mgonjwa gani anazunguka duniani ktk TV mbali mbali na kuichafua nchi yake? Mgonjwa hawi hivyo hata kidogo..!!