Job Ndugai: Ipo siku Tanzania itapigwa mnada, Watu tukishakopa tunapiga makofi kujipongeza. Deni la Taifa ni 70 Trilioni

Huyu ndugai ndo alikuwa mstari wa mbele kutufokea kuhusu tozo akimsaidia chifu na madelu huku akitunanga kwamba kama hatutaki tozo tutafute vyanzo mbadala.........halafu anakuja kulialia hapa wakati bunge la mazuzu ndo wenye mamlaka ya kuibana serikali.......
 
Dah! Hapo ndiyo mimi nachoka kabisa na viongozi wetu, Mh Spika kasema hivyo kweli! Sheria zote zinatungwa pale kwenye Bunge letu tukufu na yeye ndiye kiongozi wa huo mhimili……. this is it.
Yes it is it
 
Nafikiri Ndugai kapata karipio/vitisho baada ya malalamiko yake ya awali.
 
Next time tunahitaji Magufuli aingie bungeni sasa ili kuondoa upuuzi! Naimani Bunge likiwa na mtu strong hata raisi kufanya upuuzi ni ngumu
Ngumu, hawezi kwenda kinyume na matakwa ya atakayemuweka (m/kiti wa chama chake).
 
Kipindi hayo yote yanafanyika ndungai alikuwa Bado hajawa spika wa bunge? Ccm ni wanafiki wazandiki maguluguja.uzuli ni kwamba bunge lote ni kijani wananchi tunajua Kila kitu.
Sawa ni bora kuwa Mnafiki ambaye mara moja moja unasema ukweli kuliko Wanafiki wanaopiga makofi tu mpaka wanakufa ili hali Nchi inaangamia.
 
Wewe spika washughulikie ndani ya bunge mimi nitawashughulikia nje ya Bunge. Ndipo akawa anawafukuza bungeni yule mwenzie anawatandika nje ya bunge. Anadhani tumesahau. Huyu akae kimya tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…