Job Ndugai: Ipo siku Tanzania itapigwa mnada, Watu tukishakopa tunapiga makofi kujipongeza. Deni la Taifa ni 70 Trilioni

Job Ndugai: Ipo siku Tanzania itapigwa mnada, Watu tukishakopa tunapiga makofi kujipongeza. Deni la Taifa ni 70 Trilioni

"Wapinzani walituchelewesha sana." Alisikika yule shujaa.
Mkuu kumbe huko ng'ambo ya pili hali siyo shwari kabisa. Mimi nilikuwa naona tetesi hapa nikadharu lakini hili jiwe lililotupwa na Ndugai linaonekana kumlenga mtu kabisa. There should be something behind the scene! Kuna kitu Ndugai amenusa. Asingeweza kujilipua namna hii bila kunyaka mipango kabambe against him.
 
Hela ipo ila usimamizi sio mzuri! Tatizo linalotukwamisha ni usimamiz wa rasilimali zetu tumewapa madaraka watu wa hovyo!
Mkuu Extrovert,

Magufuli alisimamia nidhamu ya matumizi alipigwa vita hadi leo hii ambapo hayupo nasi na wengine wanasema afukuliwe azikwe upya kilomita 1 chini ya ardhi (kaburi ambalo litakuwa limevunja rekodi ya dunia) ili asije kuleta hata ndoto. Leo hii Zenji inakuwa Dubai kwa gharama za JMT na SMZ wakati Magufuli alipojenga ushoroba wa Kaskazini (Northern Economic Corridor) aliambiwa anapoteza ela kupendelea Chato, si bora Chato iko Tanganyika. Nawaambia in 10 yrs time now on... Zanzibar itakuwa Dubai ya Afrika, ndipo majuto yatakuwa mjukuu kwa Watanganyika.

Introvert.
 
Spika wa bunge la jamhuri ya muungano JOB NDUGAI amedai kuwa kulingana na mwenendo wa deni la taifa kufikia trilion 70 ipo siku nchi ya Tanzania itapigwa mnada amenena maneno hayo baada ya kusema kwamba tozo zote zamiamala ya simu zilizopitishwa na bunge zilipitishwa kwa lazima kwani wananchi hawakuridhia kama inavyosema na baadhi ya wanasiasa.

Kwa maneno hayo naona kuna mambo yanaendelea huko Lumumba yapo mambo hayajakaa sawa ukiona spika anaanza kulalamikalalamika! Alianza kuhusiana na serikali kuhamia Dodoma kuwa kwa sasa kazi zote za serikali na makongamano zimerudishwa Dar-es-Salaam.

Mheshimiwa Ndugai popote ulipo nakwambia hivi wewe na viongozi wako mnaifanyia nini hii nchi mbona mnakaa mnalalamika lalamika wakati chama ni cha kwenu na chama chenu ndicho kimeunda serikali.?

=====

UPDATES;

=====

=> Watu wengi wanatulaumu sana, ninyi ndio Wasomi. Hebu fikiria, Juzi mama kaenda kukopa 1.3 Trilioni deni.

=> Na tuna majengo hivi sasa ya Madarasa, ya Vituo vya afya, ambayo yanajengwa kwa tozo. Hivi ipi bora? Sisi Watanzania wa miaka 60 ya Uhuru tuendelee kukopa na Madeni au tubanane banane hapa tujenge wenyewe bila madeni Makubwa yasiyoeleweka? Ni lini tutajenga wenyewe?

=> Tutembeze bakuri ndo heshima? na tukishakopa tunapiga makofi! Sisi wa kukopa kila siku?

=> Tukasema pitisha Tozo, anayetaka asiyetaka, pitisha Tozo. Lazima tuanze kujenga wenyewe. Nani atatufanyia? Yupo wapi huyo Mjomba? Tukapitisha Tozo.

=> Sasa 2025 itaamua. Mkitoa waliopo sawa. Waje watakaokuwa kazi yao kwenda kukopa endepo hiyo ndo namna ya kuendesha Nchi.

=> Hivi sasa deni letu ni 70 Trilioni. Hivi ninyi si Wasomi? Is that healthy? Kuna siku nyi itapigwa mnada hii. Madeni Madeni Madeni

=> Bajeti yetu Trilioni 30, Trilioni 10 kati ya hizo kwa Mwaka tunalipa Madeni.

=> Tumeenda Kukopa 1.3 Trilioni, Tunapiga Makofi. Tunawapa Wazungu Trilioni 10 Mariba Matupu. Wanatufanya Sisi Mazezeta. Hela yako Mwenyewe. Anachukua hela yako, halafu anakupa Kidogo Unashangilia.

=> Toza fanya hivi, tujitegemee, Tusimame wenyewe. Kuna ubaya gani? Hata msomi anatupinga.
View attachment 2060338
Wafu wanazikana wenyewe.
 
Angefanya hata comparison kabla hajafanya conclusion hata na majirani wetu kenya.

Kenya deni la taifa na uwiano na GDP ni 67% na Tanzania ni 35%.

Hata mataifa makubwa yana madeni makubwa sana kama wafanyabishara wakubwa sana cha muhimu ni kuhakikisha kunakuwa na transparency na monitoring nzuri ya hiyo mikopo.
Bado unajisifia kenya 67% kwa yetu 35% siyo? Walio jikoni wameona Kuna tatizo. Wewe unaona sana. Una mzazi au ndugu mpiga makofi mle bungeni hata spika aki ja---mba?.
 
Anaoneka kama anauchungu sana na taifa ila sasa.....
Labda ameona Bandari ya Bagamoyo imepotezewa wakati aliishakarimiwa kupitia Sino-Africa Blackmail, mimi nafikiri tupunguze matumizi ya Mhimili wa Bunge ili tulipie mikopo hiyo. Mbona Raila alimbana Kibaki hadi wabunge wakapunguziwa maslahi na serikali ikapumua.
 
Mkuu Extrovert,

Magufuli alisimamia nidhamu ya matumizi alipigwa vita hadi leo hii ambapo hayupo nasi na wengine wanasema afukuliwe azikwe upya kilomita 1 chini ya ardhi (kaburi ambalo litakuwa limevunja rekodi ya dunia) ili asije kuleta hata ndoto. Leo hii Zenji inakuwa Dubai kwa gharama za JMT na SMZ wakati Magufuli alipojenga ushoroba wa Kaskazini (Northern Economic Corridor) aliambiwa anapoteza ela kupendelea Chato, si bora Chato iko Tanganyika. Nawaambia in 10 yrs time now on... Zanzibar itakuwa Dubai ya Afrika, ndipo majuto yatakuwa mjukuu kwa Watanganyika.

Introvert.
Wacha tuendelee kusubiria
 
Inafikirisha sana nchi iliyojaariwa utajiri mkubwa inahoji kipi bora kati ya kuongeza tozo kwa wananchi wake ama kukopa pesa zitakazolipwa na wananchi wake.
Kazi kwelikweli.
 
Inafikirisha sana nchi iliyojaariwa utajiri mkubwa inahoji kipi bora kati ya kuongeza tozo kwa wananchi wake ama kukopa pesa zitakazolipwa na wananchi wake.
Kazi kwelikweli.
Yani eti wanaona tuna option mbili japokuwa tuna kila aina ya rasilimali. Yani kwao option ni either tukope au tozo
 
Tafsiri ya malalamiko ya Spika ni kwamba Mhimili wa Bunge umeshindwa kufanya kazi yake ya kuisimamia serikali (inakopa hovyo hovyo). Hivyo basi, Mhe. Ndugai kwa kauli yake anathibitisha kuingia rasmi kwenye kundi la akina Polepole, Gwajima na Silaa.
Na kama Bunge limeshindwa kuisimamia serikali bora basi livunjwe twende kwenye uchaguzi, ili tupate pia Bunge ambalo silo la Magufuli labda.
 
Back
Top Bottom