Jogoo anajuaje kama asubuhi imefika aanze kuwika?

Jogoo anajuaje kama asubuhi imefika aanze kuwika?

Majogoo wana mfumo wa android kwenye seli zao uitwa antroposcipne. Mfumo huu huwa unasense kiasi cha mwanga kwenye hewa. Sensor hizo zipo kwenye kile kidude cha juu ya kicwa cha jogoo na baadhi zipo kwenye manyoya ya mkiani...
Kwani ili kuwika Jogoo hutegemea Mwanga? Kwani ili kujua kwamba kumekucha maeneo yote na nyakati zote mwanga ndiyo hutegemewa?
Halafu hiyo ya Jogoo kuwa na antroposcipne cell sijui android naona umeamua kujifanya na wewe ni RPC Mallya wa Dodoma. Umeshawaona wenzako wote humu kama vile wote ni wa Dovya.
 
Wapi huko Jike anawika....Haya ni Maajabu
Fuga kuku mkuu. hii hutokea mara moja moja sana pia huhusishwa na ushrikina ndio maana huchinjwa muda huo huo

Baba niliwahi muuliza akanijibu jike likiwika huwa ni ishara ya kuwa hapo kwenuye familia kuna mchawi
au mwanmke ndo atakuja kutawala mji au anautawala tiyari au ni Alert ya kifo nk .
hii ni imani hasa huku kanda ya ziwa
 
Majogoo wana mfumo wa android kwenye seli zao uitwa antroposcipne. Mfumo huu huwa unasense kiasi cha mwanga kwenye hewa. Sensor hizo zipo kwenye kile kidude cha juu ya kicwa cha jogoo na baadhi zipo kwenye manyoya ya mkiani...
Bro,

Mbona kama hii unatuokota!!?

Android hiii hii ya kwenye simu na jogoo anayo? Sawa sawa.
 
Majogoo wana mfumo wa android kwenye seli zao uitwa antroposcipne. Mfumo huu huwa unasense kiasi cha mwanga kwenye hewa. Sensor hizo zipo kwenye kile kidude cha juu ya kicwa cha jogoo na baadhi zipo kwenye manyoya ya mkiani...
Mkuu,wewe ndio yule Profesa Janabi?

Naona mnafanana katika utoaji wa maelezo.
 
Kwani ili kuwika Jogoo hutegemea Mwanga? Kwani ili kujua kwamba kumekucha maeneo yote na nyakati zote mwanga ndiyo hutegemewa?
Halafu hiyo ya Jogoo kuwa na antroposcipne cell sijui android naona umeamua kujifanya na wewe ni RPC Mallya wa Dodoma. Umeshawaona wenzako wote humu kama vile wote ni wa Dovya.
Just for fun, nothing serious. Uzi upo chit chat so nikaamua kutia chumvi kuchangamsha genge kidogo... 😀 :BLUBBERS:
 
Back
Top Bottom