John Butler Walden (1939 - 2002) a.K.a ''Black Mamba''- A legend in the Tanzanian army (author unknown)

John Butler Walden (1939 - 2002) a.K.a ''Black Mamba''- A legend in the Tanzanian army (author unknown)

Hii makala inagusa moyo sana na inafungua ufahamu mkubwa kabisa juu ya changamoto za maisha, uadilifu, malengo, uvumilivu lakini pia masuala ya uzazi na ulezi wa watoto, na changamoto mbali mbali ambazo binadamu zinamkuta na namna ambavyo hatakiwi kukatishwa tamaa.

Major General Walden, pengnie maisha ya kutengwa na wazazi akiwa mtoto mdogo, yalimjgengea tabia ya kujitegemea akiwa katika umri mdogo na kufahamu kwamba ili mtu apate anachokihitaji katika maisha ni lazima afight. Bila hivyo, kitendo cha kubaguliwa na kutiliwa mashaka uzalendo na uaminifu wake kwa jeshi, kulingana na rangi yake au tabia za mzee wake, tayari kungemvujna moyo na pengine hata angeamua kufuta mkondo mwingine wa maisha. Huyu kijana anafundisha mengi mno kwa jina za matendo.

Hata hivo, ninatamani sana habari kama hizi, zingefuatiliwa na kuandikwa kabla hajafariki ili kumsikia kwa upande wake anasema nini. Yako masuala mengi sana ya kujinfunza kutoka kwa atu kama hawa. Si kwa Watanzania ama binadamu wa kawaida, bali pia upande wa serikali namna ya kuwaenzi kwa dhati badla ya kisiasa.

Major General nimeongea naye mara kadhaa nyumbani kwake Iwambi. Nilikuwa nikipitia nyumbani kwake mara nyingi nikitokea Lusaka kwa gari na alikuwa mkarimu na mwenye ushirikiano na watu sana. Penginge historia yake hii ndiyo imepelekea kumfanya awe mtu wa kuthamini watu, asiyejibagua na mwenye upendo.

Kuna mengi ambayo kama yangeandikwa pia kwa kumhoji yeye, hii habari ingelikuwa na upande wa pili ambapo pengine umma ungelifahamu Serikali yetu inawaenzi vipi mashujaa wetu wanapokuwa hai baada ya kumaliza majukumu yao. Kwa kugusa mioyo na fikira, ninahakika maisha ya Major General huyu, yangetoa mwelekeo mpya na makini juu ya kuenzi wataafu wetu wanaoishi maisha ya majuto.

Ahsante kwa makala nzuri. Karibu na zingine utushirikishe.
Tabby,
Ahsante sana.
Mimi nataka kupata jina la mtu aliyeandika taazia/makala hii lakini bado sijafanikiwa.
 
Tabby,
Ahsante sana.
Mimi nataka kupata jina la mtu aliyeandika taazia/makala hii lakini bado sijafanikiwa.

Ninaona ameauma kuwa anonymous mkuu!. Pengine aliyeileta hapa anaweza kuwa anajua chanzo chake.
 
Ninaona ameauma kuwa anonymous mkuu!. Pengine aliyeileta hapa anaweza kuwa anajua chanzo chake.
Tabby,
Mimi ndiye niliyeiweka hapa.

Nimeipata kwenye group letu moja na cha ajabu nilipoomba
picha nikawekewa ila jina sikupewa ingawa nililiomba,
 
Jamaa rangi tu ndo ilimfanya asipewe ukuu majeshi badala yake akapewa R.MBOMA
 
Huyu shujaa aenziwe kwa vita ya kagera......ilikuwa na tija gani kwe2
Ni kweli,urafiki wa watu wawili ukatuingiza katika matatizo mpaka hivi leo.Kama Milton angehamia Zambia au Zimbabwe mara baada ya kupinduliwa tusingeingia vitani hata siku moja.
 
Tabby,
Mimi ndiye niliyeiweka hapa.

Nimeipata kwenye group letu moja na cha ajabu nilipoomba
picha nikawekewa ila jina sikupewa ingawa nililiomba,

Sijajua kwa nini anahofu. Ila hii habari haijakamilika. Nilitamani sana kama tungepata upande wa Major General wakati hajatangulia, ndipo tungeelewa nilichotamani tukipate.
 
Kwako inaweza isiwe na tija...kwn nyie si ndo mnataka sanamu ya askari pale posta itolewe na iwekwe ya diamond.. hvyo sikushangai
Nasema haikuwa na tija sababu haikuwa na sababu za msingi na zaulazima ss kupigana zaidi ya kuturudisha nyuma na kutugawa....rejea nyuma tafuta historia ya Nyamagana
 
Tabby,
Ahsante sana.
Mimi nataka kupata jina la mtu aliyeandika taazia/makala hii lakini bado sijafanikiwa.
Mzee Mohamed Said,

Mwandishi wa hii historia ni Prof. Azaria C. Mbughuni. Ni mtanzania anayeishi na kufundisha Copenhagen, Denmark. Ninaweza kukupatia akaunti yake ya Facebook kama utahitaji. Imekua posted mara ya kwanza katika mtandao wa Wanazuoni Yahoo Group. Na aliiweka yeye mwenyewe.
 
Mzee Mohamed Said,

Mwandishi wa hii historia ni Prof. Azaria C. Mbughuni. Ni mtanzania anayeishi na kufundisha Copenhagen, Denmark. Ninaweza kukupatia akaunti yake ya Facebook kama utahitaji. Imekua posted mara ya kwanza katika mtandao wa Wanazuoni Yahoo Group. Na aliiweka yeye mwenyewe.
Yaka,
Ahsante sana.
Nitashukuru kupata akaunti yake ya Facebook.
 
Jamaa rangi tu ndo ilimfanya asipewe ukuu majeshi badala yake akapewa R.MBOMA

Mkuu Geofrey Maseta wapo wengi waliostahili ukuu wa majeshi lakini walifanyiwa mizengwe kwasababu mbali mbali.
General Tumain Kiwelu ndiye five star General ambaye hakuwahi kuwa mkuu wa majeshi.Ikumbukwe wakati wa vita ya Uganda tayari General Kiwelu alikuwa Chief of Staff na ndiye aliyeandaa mipango ya kivita ya kuyaondoa majeshi ya Uganda katika ardhi ya Tanzania.Baada ya kufanikiwa kuyatimua majeshi ya Uganda katika ardhi ya Tanzania akarejea makao makuu ya jeshi kuendelea na kazi yake ya mkuu wa utawala jeshini (Chief of Staff).

Baada ya kumalizika kwa vita na ushindi mkubwa dhidi ya majeshi ya Idd Amin.General Kiwelu akaondolewa jeshini na kupelekwa Mkoa wa Tanga kuwa mkuu wa mkoa huo.Wakati General Musuguri anastaafu akaibuliwa General Kyaro na General Kiwelu akarejeshwa tena TPDF kama chief of staff kwa mara ya pili.Utashangaa General Kiwelu alimfundisha General Waitara pale Monduli Arusha TMA baadae akaja kupewa ukuu wa majeshi na kumweka kando General Kiwelu.
 
Huwa nashindwa kujua ni kwnn huyu LT genal T.Kiwelu hakupewa ukuu wa majeshi..meja general Walden...daah

Mkuu Geofrey Maseta ufuatilia historia ya JWTZ utakuta maafisa walikuwa katika makundi mawili.Kundi la maofisa wasomi waliochukua mafunzo UK & Canada kabla chuo cha kijeshi Monduli TMA hakijaanzishwa mfano General Mboma,General Kiwelu,General Sarakikya,Major General Lupogo,Lt General Mwakalindile....Halafu walikuwepo maofisa walipanda vyeo kuanzia chini hadi kufikia ngazi za juu kabisa,mfano General Musuguri,General Kyaro,Major General Marwa.....

General Kiwelu nadhani aliponzwa na kundi lilotaka kumpindua Mwl Nyerere wengi walitokea kaskazini waliondolewa jeshini na kupelekwa kuongoza mashirika ya umma eg Fiberboard,Kamata,Mkonge.......General Kiwelu alitokea kaskazini tena alisomea UK & Canada.

NB: General Kiwelu ni full General pekee ambaye hakuwahi kushika madaraka ya ukuu wa majeshi CDF.
 
Back
Top Bottom