Mathayo Fungo
JF-Expert Member
- Nov 13, 2018
- 319
- 511
HUJUMA ALIZOFANYIWA HECHE NI AIBU KWA CHAMA KINACHOJIITA CHA DEMOKRASIA:
Uchaguzi wa Mwenyekiti Kanda ya Serengeti umetamatika huku Heche akifanyiwa hujuma, rafu na figisu za kila namna kuhakikisha kuwa anaangushwa na Esther Matiko.
Ni bahati mbaya sana kuwa chaguzi hizi za Kanda zimetawaliwa na hujuma za kila aina, rushwa za kila aina kuanzia za pesa hadi zile za ngono. Naamini Msajili wa Vyama vya Siasa nchini atashirikisha vyombo husika kuchunguza hujuma hizi.
Watu wananiuliza imekuwaje shujaa Heche aangushwe? Bahati nzuri Mimi niko jikoni na leo nitawaeleza peupe, Heche hajaangushwa kidemokrasia iko hivi:
1. Urafiki wa Heche na wapinzani wa Mbowe:
Kwa wale msiojua ni kwamba Heche ni rafiki mkubwa wa Cecil Mwambe, Joseph Selasini Saed Kubenea na Anthony Komu. Mbowe amekuwa akimuona Heche kama kitisho (threat) katika utawala wake hususani kutokana na misimamo mikali isiyoyumba ya Heche ambapo amekuwa akimkosoa Mbowe kwenye vikao vya chama bila woga. Mbowe akaamuru kuwa wajumbe na Msimamizi wa uchaguzi kuwa wahakikishe Heche aangushwe kwa gharama yoyote ile.
2. Ni Kuhusu uhusiano nyeti sana wa kimapenzi baina ya Matiko na Salum Mwalimu. Hili naliweka kiporo ila figisu zikiendelea nitapasua mbarika. Ila kiufupi tu ni kwamba Mwalimu ana Mtoto na Matiko waliozaa naye. Hivyo licha ya Mwalimu kupewa maagizo mazito na Mbowe ili aende Serengeti kuhakikisha Heche anachinjiwa baharini ni kwamba pia Mwalimu ambaye ni NKM-Zanzibar alitumia mwanya huo kuhakikisha mpenzi wake au ukipenda kimada kinapata ulaji. It was a win win situation kutwkeleza maagizo ya Mbowe ya kumchinjia mbali Heche lakini wakati huo huo akihakikisha anatumia fursa hiyo kuhakikisha anamfurahisha Matiko.
Na tayari Mbowe alishatoa amri kuhakikisha kuwa endapo Heche atajaribu kugombea uenyekiti wa CHADEMA Taifa adhibitiwe mapema hata kabla ya Uchaguzi wenyewe.
Hivyo urafiki wa Heche na mahasimu wa Mbowe ndani ya chama ndio uliomponza na kupelekea kuadhibiwa kwa amri ya Mwenyekiti.
Heche ni miongoni mwa Wabunge wanaomuunga mkono Cecil Mwambe kugombea uenyekiti wa CHADEMA Taifa na hapo ndipo uhasama zaidi kati yake na Mbowe ulipoongezeka.
Na kwa taarifa tu ni kwamba tayari Mbowe ameshasuka mkakati kuhakikisha kuwa akifanikiwa kufanya uchakachuz na kuwa Mwenyekiti kwa awamu ya tano basi John Heche, Joseph Selasini, Anthony Komu, Cecil Mwambe na Saed Kubenea watakatwa kwenye mchakato wa Kura za maoni.
Hii inasikitisha sana, sijawahi kuona Uchaguzi wa kipumbavu na kijinga kama huu. Yani hata CCM kwa sasa wana ahueni ya kidemokrasia kuliko sisi CHADEMA.
Misingi ya demokrasia haipo tena ndani ya CHADEMA, Mbowe ndiye amri, yeye ndiye Katiba na lolote atakalo anahakikisha linafanyika. Watu waejeruhiwa ndani ya CHADEMA wengine wameamua kunyamaza tu.
Ukiongea vizuri na watu walioamua kuondoka CHADEMA unaweza kuwaomba msamaha kama uliwatukana. Mbowe huyu ambaye baadhi ya vijana wameamua kumuabudu na kumsujudia huku wakilamba viatu vyake ili MATUMBO yao yashibishwe ndiye anaenda kuizika CHADEMA. Amini usiamini 2020 CHADEMA hii chini ya Mbowe itakuwa DHAIFU sana kuliko hata TLP ya Mrema.
Mbowe amegeuza CHADEMA kuwa mali yake. Mali za chama amegeuza ni zake. Anyway nikipata wasaa nitaeleza namna Mbowe anavyokifisadi chama na kujineemesha huku akitutumia vijana kama greda lake la umchimbia barabara ili aendelee kuneemeka.
Kama ulikuwa unajiuliza imekuwaje shujaa Heche aangushwe Serengeti basi UKWELI MCHUNGU ndio huo kuwa nguvu ya ngono na na urafiki wake na kina Selasini, Mwambe, Kubenea na Komu ndivyo vilivyo mgharimu.
Level ya udikteta wa Mbowe aliyofikia ndani ya CHADEMA hana legitimacy ya kumuita mtu yeyote yule kuwa ni Dikteta.
Kwa upuuzi huu tunaoufanya CHADEMA hatuna legitimacy ya aina yoyote ile ya kukashifu hujuma za uchaguzi wa Serikali za mitaa. Hivi kwa upumbavu huu unapata wapi ujasiri wa kumkashifu Waziri Jafo na Mwita katika uchaguzi wa SM?
Dawa chungu ndiyo inayoponesha, UKWELI MCHUNGU unauma lakini UKWELI hauna mbadala.
Baadae nitaanika hujuma alizofanyiwa Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini katika uchaguzi wa Mwenyekiti Kanda ya Kaskazini dhidi ya Godbless Lema.
Remmy Cameroon
Sauti ya wasio na sauti
Uchaguzi wa Mwenyekiti Kanda ya Serengeti umetamatika huku Heche akifanyiwa hujuma, rafu na figisu za kila namna kuhakikisha kuwa anaangushwa na Esther Matiko.
Ni bahati mbaya sana kuwa chaguzi hizi za Kanda zimetawaliwa na hujuma za kila aina, rushwa za kila aina kuanzia za pesa hadi zile za ngono. Naamini Msajili wa Vyama vya Siasa nchini atashirikisha vyombo husika kuchunguza hujuma hizi.
Watu wananiuliza imekuwaje shujaa Heche aangushwe? Bahati nzuri Mimi niko jikoni na leo nitawaeleza peupe, Heche hajaangushwa kidemokrasia iko hivi:
1. Urafiki wa Heche na wapinzani wa Mbowe:
Kwa wale msiojua ni kwamba Heche ni rafiki mkubwa wa Cecil Mwambe, Joseph Selasini Saed Kubenea na Anthony Komu. Mbowe amekuwa akimuona Heche kama kitisho (threat) katika utawala wake hususani kutokana na misimamo mikali isiyoyumba ya Heche ambapo amekuwa akimkosoa Mbowe kwenye vikao vya chama bila woga. Mbowe akaamuru kuwa wajumbe na Msimamizi wa uchaguzi kuwa wahakikishe Heche aangushwe kwa gharama yoyote ile.
2. Ni Kuhusu uhusiano nyeti sana wa kimapenzi baina ya Matiko na Salum Mwalimu. Hili naliweka kiporo ila figisu zikiendelea nitapasua mbarika. Ila kiufupi tu ni kwamba Mwalimu ana Mtoto na Matiko waliozaa naye. Hivyo licha ya Mwalimu kupewa maagizo mazito na Mbowe ili aende Serengeti kuhakikisha Heche anachinjiwa baharini ni kwamba pia Mwalimu ambaye ni NKM-Zanzibar alitumia mwanya huo kuhakikisha mpenzi wake au ukipenda kimada kinapata ulaji. It was a win win situation kutwkeleza maagizo ya Mbowe ya kumchinjia mbali Heche lakini wakati huo huo akihakikisha anatumia fursa hiyo kuhakikisha anamfurahisha Matiko.
Na tayari Mbowe alishatoa amri kuhakikisha kuwa endapo Heche atajaribu kugombea uenyekiti wa CHADEMA Taifa adhibitiwe mapema hata kabla ya Uchaguzi wenyewe.
Hivyo urafiki wa Heche na mahasimu wa Mbowe ndani ya chama ndio uliomponza na kupelekea kuadhibiwa kwa amri ya Mwenyekiti.
Heche ni miongoni mwa Wabunge wanaomuunga mkono Cecil Mwambe kugombea uenyekiti wa CHADEMA Taifa na hapo ndipo uhasama zaidi kati yake na Mbowe ulipoongezeka.
Na kwa taarifa tu ni kwamba tayari Mbowe ameshasuka mkakati kuhakikisha kuwa akifanikiwa kufanya uchakachuz na kuwa Mwenyekiti kwa awamu ya tano basi John Heche, Joseph Selasini, Anthony Komu, Cecil Mwambe na Saed Kubenea watakatwa kwenye mchakato wa Kura za maoni.
Hii inasikitisha sana, sijawahi kuona Uchaguzi wa kipumbavu na kijinga kama huu. Yani hata CCM kwa sasa wana ahueni ya kidemokrasia kuliko sisi CHADEMA.
Misingi ya demokrasia haipo tena ndani ya CHADEMA, Mbowe ndiye amri, yeye ndiye Katiba na lolote atakalo anahakikisha linafanyika. Watu waejeruhiwa ndani ya CHADEMA wengine wameamua kunyamaza tu.
Ukiongea vizuri na watu walioamua kuondoka CHADEMA unaweza kuwaomba msamaha kama uliwatukana. Mbowe huyu ambaye baadhi ya vijana wameamua kumuabudu na kumsujudia huku wakilamba viatu vyake ili MATUMBO yao yashibishwe ndiye anaenda kuizika CHADEMA. Amini usiamini 2020 CHADEMA hii chini ya Mbowe itakuwa DHAIFU sana kuliko hata TLP ya Mrema.
Mbowe amegeuza CHADEMA kuwa mali yake. Mali za chama amegeuza ni zake. Anyway nikipata wasaa nitaeleza namna Mbowe anavyokifisadi chama na kujineemesha huku akitutumia vijana kama greda lake la umchimbia barabara ili aendelee kuneemeka.
Kama ulikuwa unajiuliza imekuwaje shujaa Heche aangushwe Serengeti basi UKWELI MCHUNGU ndio huo kuwa nguvu ya ngono na na urafiki wake na kina Selasini, Mwambe, Kubenea na Komu ndivyo vilivyo mgharimu.
Level ya udikteta wa Mbowe aliyofikia ndani ya CHADEMA hana legitimacy ya kumuita mtu yeyote yule kuwa ni Dikteta.
Kwa upuuzi huu tunaoufanya CHADEMA hatuna legitimacy ya aina yoyote ile ya kukashifu hujuma za uchaguzi wa Serikali za mitaa. Hivi kwa upumbavu huu unapata wapi ujasiri wa kumkashifu Waziri Jafo na Mwita katika uchaguzi wa SM?
Dawa chungu ndiyo inayoponesha, UKWELI MCHUNGU unauma lakini UKWELI hauna mbadala.
Baadae nitaanika hujuma alizofanyiwa Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini katika uchaguzi wa Mwenyekiti Kanda ya Kaskazini dhidi ya Godbless Lema.
Remmy Cameroon
Sauti ya wasio na sauti