John Heche Muongo, eti Misri mvua hainyeshi miaka 20 lakini hakuna mgao wa maji

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
Kasema Tanzania kuna Ziwa Nyasa, Tanganyika, Ziwa Victoria lakini tunadai kuna upungufu wa maji na kuna mgao Dar na Mwanza. Eti Jangwa la Kalahari huko Botswana maji yapo hakuna mgao.

Anasema Tanzania hakuna Viongozi wenye maono sababu wananunua Magari ya Bil 500 wakati Dar Bil. 200 inamaliza tatizo la maji.

Je, anachoongea kina mashiko au ndiyo upinzani?

Tanzania kuna ombwe la uongozi.

Your browser is not able to display this video.
 
Issue ni Misri kutonyesha mvua hata miaka 20? Hicho ni sahihi. Maeneo mengi kama Cairo iko hivyo. Mtu anazaliwa hajui mvua. Mimi nimesoma miaka minne huko.
 
Sehemu kubwa ya Misri ni jangwa. Nadhani ye kaongea kwa generalize japo kuna baadhi ya sehemu hupata mvua. Pole km umekwazika kada lia lia wa Chama kilichotukwamisha maendeleo kwa miaka zaidi ya 60.
 
Umeandika kwa jazba bin gubu utadhani umenyimwa unyumba!Uwe unatuliza wenge.πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Mvua iliyonyesha Cairo majuzi. Yaani ilinyesha kishenzi hadi kuleta mafuriko. Siyo kweli kwamba mvua kule hainyeshi kwa miaka ishirini. Heche aache kusema uongo.

 
Mvua iliyonyesha Cairo majuzi. Yaani ilinyesha kishenzi hadi kuleta mafuriko. Siyo kweli kwamba mvua kule hainyeshi kwa miaka ishirini. Heche aache kusema uongo.

View attachment 2407104
Uwe muelewa.Anaposema miaka "ishirini" anamaanisha muda mrefu.Usiwe na one to one correspondence translations.Acha tafsiri sisisi!Kuna kipindi chaneli zako huwa ni chenga tupu!
 
Sijui nani alituloga tukapeleka Capital City yetu kwenye Jangwa la Wagogo,ona sasa tunavyoadhirika na Maji.
 
Kweli kabisa mm niko mwanza tunashuudia maajabu ya mgao wa maji maeneo ya kishiri ni taabu tupu mwezi hata tone la maji akuna uongozi wa hovyo kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…