John Malecela: Sioni Hoja ya Wanaopinga Uwekezaji wa DP World Bandarini

John Malecela: Sioni Hoja ya Wanaopinga Uwekezaji wa DP World Bandarini

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Waziri Mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, John Malecela ametoa kauli kuhusu sakata la makubaliano ya uwekezaji wa bandari nchini na Serikali ya Dubai kupitia Kampuni ya Dubai Port World (DPW).

IMG_7732.jpeg

Malecela ametoa kauli hiyo leo Jumapili Juni 25, 2023 baada ya kuulizwa swali kuhusiana na uwekezaji huo unaohusisha Serikali hizo mbili.

Malecela amesema haoni shida ya uwekezaji huo na amewashangaa wanaopinga akisema ndio demokrasia inavyowaruhusu.

"Kwanza wako wachache wanaopinga na sioni hoja yao," amesema Malecela ambaye ni Waziri Mkuu wa saba wa Tanzania akipokea nafasi hiyo kutoka kwa Jaji Joseph Warioba.

Leo, Malecela amekutana na waandishi wa habari nyumbani kwake eneo la Kilimani jijini Dodoma akielezea kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaotanywa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Mwananchi
 
Waziri Mkuu mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, John Malecela ametoa kauli kuhusu sakata la makubaliano ya uwekezaji wa bandari nchini na Serikali ya Dubai kupitia Kampuni ya Dubai Port World (DPW).
kwake eneo la Kilimani jijini Dodoma akielezea kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaotanywa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Mwananchi
Huyu si ndo alibadil Dini kuwa muislamu Ili mradi awe Raisi...siyo wazee wote Wana busara..
HuwezI ukaenda Msoga kupata ushauri afu urudi na kitu cha Maana
 
Si ndiyo huyu Mwalimu Nyerere alikuwa akimwita na ama akitaka kumuonya alimwita, wewe John, njoo!! Ulitaka kusema nini??

Mwalimu hakutaka kumwita Mh waziri mkuu Jonh Malecela

Huyu hawezi kubadiri chochote kwa tunaoupinga huu mkataba wa kuchukua Bandari zetu zooote!
 
Huyu si ndo alibadil Dini kuwa muislamu Ili mradi awe Raisi...siyo wazee wote Wana busara..
HuwezI ukaenda Msoga kupata ushauri afuburudi na kitu cha Maana
Wengi wanaopinga huo mkataba wako katika udini na ndio maana hata wewe umemuhusisha kwenye udini mzee wa watu,udini uleta chuki mbaya sana mkuu
 
Waziri Mkuu mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, John Malecela ametoa kauli kuhusu sakata la makubaliano ya uwekezaji wa bandari nchini na Serikali ya Dubai kupitia Kampuni ya Dubai Port World (DPW).

Kwanini unamtukanisha mzee. Na atatukanwa na kudharaulika mno. Waacheni wapumzike
 
Waziri Mkuu mstaafu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, John Malecela ametoa kauli kuhusu sakata la makubaliano ya uwekezaji wa bandari nchini na Serikali ya Dubai kupitia Kampuni ya Dubai Port World (DPW).


Malecela ametoa kauli hiyo leo Jumapili Juni 25, 2023 baada ya kuulizwa swali kuhusiana na uwekezaji huo unaohusisha Serikali hizo mbili.
Malecela amesema haoni shida ya uwekezaji huo na amewashangaa wanaopinga akisema ndio demokrasia inavyowaruhusu.

"Kwanza wako wachache wanaopinga na sioni hoja yao," amesema Malecela ambaye ni Waziri Mkuu wa saba wa Tanzania akipokea nafasi hiyo kutoka kwa Jaji Joseph Warioba.

Leo, Malecela amekutana na waandishi wa habari nyumbani kwake eneo la Kilimani jijini Dodoma akielezea kuridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaotanywa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Mwananchi
Mimi mwenyewe sioni hoja yoyote kwenye maneno yake.
Sijui hata kama anajua watu wanalalamikia nini.....watu wanazungumzia vifungu tata kwenye mkataba yeye mzee wetu sijui anazungumzia kitu gani?...
Waacheni hawa wazee wapumzike.
 
Wengi wanaopinga huo mkataba wako katika udini na ndio maana hata wewe umemuhusisha kwenye udini mzee wa watu,udini uleta chuki mbaya sana mkuu
Sijahusisha udini. Najaribu kuangalia uzalendo wake naukosa....kipindi kile miaka ya 90 alitumika Vibaya sana tena na hawa hawa waarabu Hadi kumshawishi abadili dini na kashifa yake haikuwa ya kitoto.

Lakini Hata uzao wake haikuwa na faida Kwa nchi. Kumbuka mto wake RIP aliyetumbuliwa na MAGUFULI ... they're traitors

Kiufupi familia ya malecela haijawahi kuwa na faida Kwa Nchi. Simshangai kumwona anakubali jambo linaloenda kinyume na katiba ya nchi
 
Mimi mwenyewe sioni hoja yoyote kwenye maneno yake.
Sijui hata kama anajua watu wanalalamikia nini.....watu wanazungumzia vufungu tata kwenye mkataba yeye mzee wetu sijui anazungumzia kitu gani?...
Waacheni hawa wazee wapumzike.
Nashangaa Hata warioba au mwinyi siyo wa kuilizwa Jambo kama hili... Ni sawa na kumlazimisha mgonjwa mahututi kuandika wosia
 
Si ndiyo huyu Mwalimu Nyerere alikuwa akimwita na ama akitaka kumuonya alimwita, wewe John, njoo!! Ulitaka kusema nini??

Mwalimu hakutaka kumwita Mh waziri mkuu Jonh Malecela

Huyu hawezi kubadiri chochote kwa tunaoupinga huu mkataba wa kuchukua Bandari zetu zooote!
Huyo Mzee anaoneka ni tatizo toka zamani Hana jipya.... Mtu yeyote aliyekataliwa na Nyerere ni wa kuogopa kama ukoma. Si mnamwoma Kikwete anavotuyumbisha.
 
Back
Top Bottom