Pre GE2025 John Mnyika adai kuna hujuma za kuyumbisha harakati za 'No Reforms No Election' kufuatia pingamizi la uteuzi wa vigogo nane CHADEMA

Pre GE2025 John Mnyika adai kuna hujuma za kuyumbisha harakati za 'No Reforms No Election' kufuatia pingamizi la uteuzi wa vigogo nane CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Katibu Mkuu CHADEMA, John Mnyika, amedai kuwa kuna juhudi za kuhamisha mwelekeo kutoka kwenye kampeni ya 'No Reforms, No Election'. Kupitia ujumbe wake kwenye mtandao wa X, Mnyika amesisitiza kuwa maamuzi ya Baraza Kuu la CHADEMA yaliyofanyika tarehe 22 Januari 2025 ni halali, kwani yalihusisha wajumbe halali 234 kati ya 412, sawa na asilimia 56.8, kwa mujibu wa Katiba ya chama ibara ya 6.2.2.

Pia, Soma: Team Mbowe wajidhatiti kumkwamisha LISSU , wapinga uteuzi wa Wajumbe watano wa kamati kuu aloufanya Lissu, waandika Barua kwa msajili wa Vyama

Aidha, Mnyika ameeleza kuwa kikao hicho kilifanya uthibitishaji kwa mujibu wa Katiba ibara ya 7.7.12 (c) na (e), na hakukuwa na ajenda ya uchaguzi.

Ameeleza kuwa hatua ya kuwasilisha nakala ya barua kwa Msajili wa Vyama vya Siasa inadhihirisha kuwepo kwa nia ovu inayofanyika kwa siri dhidi ya chama hicho.

Screenshot 2025-02-19 122915.png
 
Ninyi mnapenda sana kushutumu na kutuhumu wengine. Ikitokea kwenu mnaanza kulialia eti mnahujumiwa. Mkiwa madarakani mkawa mnasemwa kama inavyosemwa CCM si mtafungia mitandao yote kama Korea Kaskazini?
 
Ameeleza kuwa hatua ya kuwasilisha nakala ya barua kwa Msajili wa Vyama vya Siasa inadhihirisha kuwepo kwa nia ovu inayofanyika kwa siri dhidi ya chama hicho.
Mnarudi kwa msajili wa vyama? Du poleni, mmekwisha. Ya CUF yaingia CHADEMA. Itawakeep busy hii, mpaka oktoba 2025 ndio mechi itakwisha.
Poleni sana CHADEMA.
 
binafsi nilisema mapema kwamba,
kwa aina ya kampeni za chuki uhasama na mgawanyiko ilivyokua kabla ya uchaguzi,

yeyote atakaeshinda uenyekiti wa Chadema uchaguzi huo, atahujumiwa vilivyo katika kila agenda na mpango mkakati wa kua relevant katika medani ya siasa ya Tanzania.

Na huo ni mwanzo tu,
kwenye uteuzi wa mgombea urais, wabunge, madiwani na viti maalumu timbwili litakua ni noma zaid 🐒
 
binafsi nilisema mapema kwamba,
kwa aina ya kampeni za chuki uhasama na mgawanyiko ilivyokua kabla ya uchaguzi,

yeyote atakaeshinda uenyekiti wa Chadema uchaguzi huo, atahujumiwa vilivyo katika kila agenda na mpango mkakati wa kua relevant katika medani ya siasa ya Tanzania.

Na huo ni mwanzo tu,
kwenye uteuzi wa mgombea urais, wabunge, madiwani na viti maalumu timbwili litakua ni noma zaid 🐒
Mbunge ukichagua wako na mimi nateua wangu nakala kwa msajili
 
Hao timu mbowe kama wanaijua sana katiba,wajiunge na ccm. Wakiwa humo ccm wahoji namna mgombea urais 2025 wa ccm alivyopatikana kama ni halali au la kwa mujibu wa katiba ya ccm. Wao walishaona wapi mgombea urais anapitishwa bila kuchukua fomu!!!,waende wakahoji haya ndani ya ccm.
 
Chama kishakufa wehuntu wamebakia mle ndani wasiteseke hameni
 
Kama wameteuliwa vikao HALALI msajili anapinga nn....
Chain n ndefu sana hii chama kife tyu
 
Hao timu mbowe kama wanaijua sana katiba,wajiunge na ccm. Wakiwa humo ccm wahoji namna mgombea urais 2025 wa ccm alivyopatikana kama ni halali au la kwa mujibu wa katiba ya ccm. Wao walishaona wapi mgombea urais anapitishwa bila kuchukua fomu!!!,waende wakahoji haya ndani ya ccm.
Lissu alimkosoa sana mbowe, sasa zamu yake
 
Katibu Mkuu CHADEMA, John Mnyika, amedai kuwa kuna juhudi za kuhamisha mwelekeo kutoka kwenye kampeni ya 'No Reforms, No Election'. Kupitia ujumbe wake kwenye mtandao wa X, Mnyika amesisitiza kuwa maamuzi ya Baraza Kuu la CHADEMA yaliyofanyika tarehe 22 Januari 2025 ni halali, kwani yalihusisha wajumbe halali 234 kati ya 412, sawa na asilimia 56.8, kwa mujibu wa Katiba ya chama ibara ya 6.2.2.

Pia, Soma: Team Mbowe wajidhatiti kumkwamisha LISSU , wapinga uteuzi wa Wajumbe watano wa kamati kuu aloufanya Lissu, waandika Barua kwa msajili wa Vyama

Aidha, Mnyika ameeleza kuwa kikao hicho kilifanya uthibitishaji kwa mujibu wa Katiba ibara ya 7.7.12 (c) na (e), na hakukuwa na ajenda ya uchaguzi.

Ameeleza kuwa hatua ya kuwasilisha nakala ya barua kwa Msajili wa Vyama vya Siasa inadhihirisha kuwepo kwa nia ovu inayofanyika kwa siri dhidi ya chama hicho.

[A​
 
Mbunge ukichagua wako na mimi nateua wangu nakala kwa msajili
naona timbwili la utekaji likirejea wakati wa uteuzi wa mgombea urais, wabunge, madiwani na viti maalumu ndani ya chadema ikiwa hata katibu mkuu ameanza kupiga mayowe ya uhujuma mapema hivi 🐒
 
Hakuna meli isiyokutana na mawimbi, CHADEMA na uongozi wao wasimame thabiti, itakuwa jambo la kushangaza kama walitegemea itakuwa a smooth run.
 
Back
Top Bottom