Uchaguzi 2020 John Mnyika: Hatujateua majina ya wabunge Viti Maalum. Tunafuatilia Ofisi ya Spika na tukithibitisha hujuma au usaliti hatutasita kuchukua hatua

Ajiuzulu kwakua CHADEMA ni yako wewe nyumbu au🤔?
 
Hafukuxwi mtu . Chadema ni chombo cha umma acheni uhuni.
 
Nyie chadema hao akina mama kuingia huko bungeni hakuwazuii kuendelea na harakati zenu za kisiasa, acheni malumbano.
 
Mmeanza kuleta utetezi wa kiboya siyo!

Hoja hapa ni je, imekuwaje watu kama Mdee kujipeleka huko ilhali wanajua msimamo wa chama chao? Tena jana tu Lisu kautangaza rasmi.

Yote uliyoyaandika kiini chake ni hao wanawake kujipeleka huko,(Labda utuambie CCM/Mahakama/Ndugai kawapeleka kwa nguvu)

Wasingeenda hakuna mtu angewafuata kwao kuwaapisha na baada ya vikao vitatu mfululizo wangepoteza sifa automatically.

BTW:Mbona hizi porojo hazikutumika kuwalinda wanachama wengine mliowafukuza?
 
tunaambiwa vikao vya chama vyenye maamuzi havikufanyika na hakuna majina yaliyowasilishwa Nec. Inavyoelekea bila shaka kuna shopping list ya BAWACHA ambayo sasa inafanyiwa kazi kwa msaada wa ofisi ya Spika na vyombo vingine.
Hii ni technique ya kitoto ya kujaribu kuzuia “taharuki” na mihemuko ya wafia chama waliokuwa wanaapa na kujiapiza kwamba haendi mtu Bungeni. Dada Aida sasa watu wakamuombe msamaha!

Kama tulivyosema mwanzo, hili nalo litapita kimya kwa sababu lina baraka zote za viongozi. Lissu atulie zake tu huko na ale posho za mabeberu taratibu. Huku watu wapo wanaangalia maslahi yao zaidi.

Kukaa 5 years bila mshahara wala ruzuku anaweza Maalimu Seif peke yake ingawa na yeye atasurrender muda sio mrefu. Huku bara hakuna cha Mwamba wala nini.
 
Mtawafukuza kwenye chama tu laknii ubunge imeisha hiyooo na wivu wenu kama.
 
Hapa swala sio Spika na Tume swala inakuwaje hao wanachama wenu waendee kuapishwa kama ni uongo?

Msitudanganye bwana. Inamaana hawa Viti maalumu wa chadema walitekwa mpaka bungeni.

Watanzania sio WAJINGA
 
Chadema wana kiti kimoja tu cha kuchaguliwa bungeni,lakini wana viti maalum 19.Je ccm ambayo ina vita zaidi ya 200,wanatakiwa wawe na wabunge wa viti maalum wangapi?naomba wanaojua watufahamishe.
 
Siasa za Tanzania usipozijua utapata tabu Sana ...ni Kama dabi ya yanga na Simba vilabu vyote nchini ....... wote ni washabiki wa Simba ama yanga pamoja na makocha wao......
 
Tanzanian politics inahitaji watu sio viongozi
Bobby wine wa Uganda amekamatwa muda huo huo maandamano na watu zaidi ya 30 wakafa
Halima mdee alikaa jela na kuteswa sana hatukyfanya kitu
Ni jambo jema. Ungefanya kitu pengine familia yako ingekuwa kwenye shida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…