Uchaguzi 2020 John Mnyika: Hatujateua majina ya wabunge Viti Maalum. Tunafuatilia Ofisi ya Spika na tukithibitisha hujuma au usaliti hatutasita kuchukua hatua

Wafuasi wa chadema hebu wapeni viongozi wenu nafasi wafanye kazi.Mliwachagua wenyewe. Hii ni Tanzania 🇹🇿 mpya na yajayo ni neema tupu.Siku zijazo mtegemeee nafasi za uwaziri.Hakuna rais bora kama JPM, tumeamua kujenga demokrasia yenye mazingira ya kitanzania kwa manufaa ya mama Tanzania 🇹🇿, hatutaki tena demokrasia ya kiliberali na kimagharibi.Siasa za fitna hazina nafasi tena, sisi sote ni watanzania.Mabeberu ikula kwa hakuna kumwaga damu Tanzania. Hongera sana Mbowe kwa kuweka Tanzania 🇹🇿 mbele kuliko chadema.
 
Nawasubiri uongozi wa Chadema wachukue hiyo hatua, hili haliwezi kuachwa lipite hivi hivi, never.
 
Aiseeee ccm wanajua kupigana vita. Ha ha ha ha. Aliyesema wanambinu za ushindi zaidi ya 300, hakukosea.
Nakumbuka sana kauli ya mzee lowassa kua muda wa kuiondoa ccm madaraka ilikua ni 2015 tu.
 
Ni wazi kuna rafu imechezwa kwa kushirikiana na Ndugai!Sasa ili iwe fundisho napendekeza wafutwe uanachama na KM apeleke majina mengine ambayo yamo kwenye orodha ya wagombea viti maalumu!
 
Hata Halima Mdee!! Loh, kweli usimwamini mtu kwa 100%.

CHADEMA lazima isimamie inachoKiamini. Bila ya kujali kama CCM itaendelea kuvunja katiba na kuamua kuendelea kuwaweka Bungeni wanachama hawa waliokisaliti chama au vinginenvyo, ni lazima hatua madhubuti zichukuliwe. Wasaliti hawa wote wafukuzwe uanachama mara moja. Wakaongeze nguvu ya UWT.
 
Inacho Uma Mwenyekiti Amekaa Kimya Sana Kwenye Ili Swala Sijui Ana Maana Gani Na Niswala Kubwa Na Gumu Lakini Yuko Kmy Au ndio lile Biti alilopigwa Na Mdee Kua Atatoboa Siri Za Ndani so sad
Mkuu hujui au...hapo mambo ya GEAR ANGANI...kwa sasa nimeamini kuwa chadema ni utopolo...acha niwe mpinzani nisiyefungamana na chama chochote nitapinga kwa yale ninayaona yapo kinyume lkn kuamini katika falsafa za kichama rasmi nimejitenga nazo
 
Wafutwe uanachama kama wamekizunguka chama na kwenda bila baraka za chama!
 
Kwa hili kama wataacha lipite najitoa CHADEMA rasmi leo tarehe 24/11/2020 Ila siendi CCM.
 
Nadhani muda mwingine kusubiri matamko ya taasisi husika ni nzuri zaidi kuliko kurukaruka....

Mbowe anajua zaidi kinachoendelea...atatolea ufafanuzi akionelea inafaa.
Kwanini wasubiri waje kufanya damage control?Kwanini hawakuwa proactive?Kuna sababu gani ya kuwaweka wafuasi na wanachama kwenye hii sintofahamu?
 
Ni wazi kuna rafu imechezwa kwa kushirikiana na Ndugai!Sasa ili iwe fundisho napendekeza wafutwe uanachama na KM apeleke majina mengine ambayo yamo kwenye orodha ya wagombea viti maalumu!
Kwa akili yako unadhani Mdee, Bulaya, Kaboyoka. Watakuwa wameebda tu Dodoma bila kuambiwa na Chama??
 
Kwanini wasubiri waje kufanya damage control?Kwanini hawakuwa proactive?Kuna sababu gani ya kuwaweka wafuasi na wanachama kwenye hii sintofahamu?
Unadhani nina majibu ya kukupa basi mkuu....labda kama unataka niwe mropokaji nijifanye F. Mbowe...

Naamini mwenyekiti wenu wa chama ana majibu na anajua kichoendelea.
 
Wajinga Sana hawa kina mnyika..
Wanahangaika na viti vya kina mama utadhani vinawahusu..
Wanataka wakose wote.
Yani wamejizalilisha Sana very shame kuumia kisa nafasi za wanawake Hawa watu wabinafsi na wachumia tumbo, wao si waligombea waende bungeni sasa kushindwa kwao ndio wanawake eti wasiende, very shame
 
Hatua gani? Hatua ilipaswa ianze na Aida kama chama kinaheshimu principles zake.

Hapa ni muda wa kujitafakari kama Chama na kufanya maamuzi yenye maslahi mapana kwa Nchi na Chama. Ni muda wa Viongozi kuonyesha uongozi. Mbowe somehow anayumba sasa
Binafsi niliamini Chadema wameamua kutotolea uamuzi rasmi suala la Aida kutokana na jinsi alivyopata ubunge wake na kutokana pia na jinsi yeye mwenyewe alivyoonyesha shauku ya kutumikia nafasi hiyo.

Hili la viti maalum liko tofauti kwa maana kwamba tunaambiwa vikao vya chama vyenye maamuzi havikufanyika na hakuna majina yaliyowasilishwa Nec. Inavyoelekea bila shaka kuna shopping list ya BAWACHA ambayo sasa inafanyiwa kazi kwa msaada wa ofisi ya Spika na vyombo vingine.
 
Ni wazi kuna rafu imechezwa kwa kushirikiana na Ndugai!Sasa ili iwe fundisho napendekeza wafutwe uanachama na KM apeleke majina mengine ambayo yamo kwenye orodha ya wagombea viti maalumu!
Upo sahihi kabisa hao wasaliti wabaki upande wa Ndugai
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…