Joram Kihango vs Willy Gamba

Joram Kihango vs Willy Gamba

ha ha ha! Hapo kuna Kabwe Makanika aka Jitu Kumbuka. Huyu aliwasumbua aana Mafia mob wakiwa na wakubwa wao kina Don Fredrique Gaetano, Lucy Luciano na Giovani Pambieri. Kuporana almasi kule Maganzo Shinyanga na michezo ya mashine ya Magnum 357!

Kuna mwandishi anaitwa DADI MWAWARE aliandika Operation vipusa na Maputo. Jamaa alikuwa mkali sana. Yaani nilipoona vituko vya operation tokomeza utafikiri nakisoma leo operationa vipusa. Sijui na yeye yuko wapi usikute naye ni marehemu!
 
nimeona kijana wa zamani, aya mkuu, hivi sinti bint kasri ilikuwa miaka gani vile? athena nimeicheki, nami pia naisubiria IRIS no 5.

hahahaah Tausi kipenzi changu....tukisikia huu wimbo tunawahi ITV!!!!Unafikiri mimi wa zamani sana? I'M ageing 35 lakini Mama yangu alianza kunipa vitabu nikiwa standard one. Mpaka nafika darasa la tatu nilikuwa pro kwenye kusoma maana nilikuwa nashindana naye na kwa sababu yeye alikuwa mwalimu ilikuwa ni rahisi kwake kuvipata vitabu hivyo. Naamini the same method my mom used to me inaweza sana kukuza uwezo wa watoto ndani ya familia.
 
Ulikuwa unajisikiaje unapomuona mwenzako ameshika KUFA NA KUPONA, NJAMA, KIKOSI CHA KISASI, KIKOMO ama SALAMU TOKA KUZIMU, TUTARUDI NA ROHO ZETU?, LAZIMA UFE JORAM, MIKONONI MWA NUNDA, NAJISIKIA KUUA TENA!!!HEBU KUMBUKA ULIPOKUWA UNASUBURI ZAMU YAKO NA WEWE UAZIME!!!
Nimeshangazwa kujua kwamba karibia kila mwandishi bora wa nyakati hizi amefariki. Nataka tuwakumbuke na kuwaombea. Lakini ni lazima nimpongeze mwandishi bora wa nyakati hizi HUSSEIN TUWA. kwa kweli ni mkali sana hebu kwa wale wapenzi wa riwaya tutafute riwaya zake MKIMBIZI, UTATA WA 9/12 NA MDUNGUAJU

umenikumbusha mbali sana ,me karbia nilisoma vitabu vyote.nilivutiwa sana vitabu vifuatavyo, njama na lazima afe sio lazima ufe kina part one kikielezea makamanda wetu wakiwa vitan uganda na part 2 leten Giro anaporud tz na kuachana na kaz ya jeshi na kujiingza kwenye ujambazi na kwenda kuiba benki kuu.sijui naweza pata wapi tena leo ivo vitabu.mwenye namna ya kuvipata atuambie
 
Umenikumbusha mbali sana ndugu yangu. Rider Hagard ni mwandishi maarufu sana wa zamani. Alifariki mnamo miaka ya 1920. Hadithi ya Allan Quartermain aliiandika mnamo mwaka 1898. Kabla ya hapo aliandika kitabu cha Mashimo ya Mfalme Sulemani. Ni vitabu vizuri sana... Hakika ungedhani ni habari za kweli, kwani zilihusisha baadhi ya maeneo na matukio ya kweli. Loh, sijui kama vijana wa leo wanaweza kupata vitu kama hivyo.

Mkuu, umenikumbusha mbali enzi nikiwa primary school!
Usinikumbushe characters wa King Solomon's Mines, akina: Mfalme Twala, bibi mchawi Gagula (Gagool), Umbopa, Foulata na wengine wengi nimesahau majina yao.
 
daaa nilisoma vtabu hivyo miaka ya 1989 mtwara huko yani acha tu jamani pia enzihzo sani lilikuwa toleo babu kubwa kuna mwandishi amri bawji huyu mtu wa tanga nadhani aliandika lovestory tanga nyika na unguja na kitabu flani cha pumbazo la moyo cjui viko wapi jamani.
 
Dah! nimekikumbuka lakini mwandishi wake nimemsahau. Kulikuwa na Hammie Rajabu AMA ZAO AMA ZANGU, Nadhani aliandika pia dimbwi la damu na simu ya kifo. kilichonifanya nikumbuke ni uwezo wa kuongeza kujua kusoma na kuandika ulioongezwa na matokeo ya kusoma kitabu kwa haraka kabla hujanyang'anywa. Unajua Tanzania ya sasa watoto hawasomi kabisa na hawana namna ya kujiongezea maarifa kupitia vitabu. Kwa wenzetu watoto wanasoma sana tangu wakiwa wadogo.
mkuu simu ya kifo sio faraji katalambula.wapi macarius na ray sibanda kitabu jina limenitoka.
 
Umenikumbusha mbali sana,uncle wangu nowdays ni shushushu baada yakuvutiwa na kazi
za hao jamaa,nitapata wapi hivyo vitabu?
Waandishi wa siku hizi Hussein Tuwa anajitahidi,pia yupo Beka Mfaume na Innocent Ndayanse.

mbona humtaji shigongo?
 
Muhanga wa ikulu ni cha BEKA MFAUME na yeye yuko vizuri sana. Edwin Semzaba sikumsoma sana. Mimi alikuwa ni Hammie rajabu na Fred katalambuya (kama sijakosea). Nadhani hawa pia ni marehemu yaaani!!!!
Hivi waigizaji wetu hawawezi kuekti muvi kwa stori za vitabu vile? nadhani zikiigizwa muvi zitauza na kupendwa sana.
 
joram mikononi mwa nunda

kiukweli vitabu hivyo nilivisoma nikiwa STD 5-7 na nikiwa O-level. haviwekeki chini. nikikumbuka vitabu hivyo, natamani kurudisha muda nyuma

watunzi waliotangulia mbele za haki wapumzike kwa amani!
 
Dah! nimekikumbuka lakini mwandishi wake nimemsahau. Kulikuwa na Hammie Rajabu AMA ZAO AMA ZANGU, Nadhani aliandika pia dimbwi la damu na simu ya kifo. kilichonifanya nikumbuke ni uwezo wa kuongeza kujua kusoma na kuandika ulioongezwa na matokeo ya kusoma kitabu kwa haraka kabla hujanyang'anywa. Unajua Tanzania ya sasa watoto hawasomi kabisa na hawana namna ya kujiongezea maarifa kupitia vitabu. Kwa wenzetu watoto wanasoma sana tangu wakiwa wadogo.

Kama Kumbukumbu yangu ni sahihi Simu ya Kifo ni kitabu cha zamani zaidi na kiliandikwa na Hassan Hussein Katalambula kama sikosei na si Hammie Rajab.
 
Hivi waigizaji wetu hawawezi kuekti muvi kwa stori za vitabu vile? nadhani zikiigizwa muvi zitauza na kupendwa sana.
Tuna shida kubwa sana ya professionalism kwenye arts. Ukiwaona hawa wa mtaani wanapenda sana visa vya mapenzi na kwa sababu hakuna ufundi wa scripts basi wewe tafuta msichana mzuri halafu awe anakaa nusu uchi soko umepata. Wale wasomi wa bagamoyo wanakosa uhalisia inakuwa kama wanasoma. Kwa vitabu vya action kama hivi nadhani kwa Afrika bado sana maana hata Nigeria sijaona movie za action labda South Afrika.
 
mkuu simu ya kifo sio faraji katalambula.wapi macarius na ray sibanda kitabu jina limenitoka.

Wewewewe! hicho mara ya kwanza nilishindwa kukimaliza kwa kusisimkwa nacho! kinaitwa HATARI! Unaingia ndani ya Nyumba yako unasikia harufu ya sigara! Makarios yuko ndani kafuata Almasi zake halafu na wewe ndiye hakimu uliyemuhukumu! patamuje!
 
Kama Kumbukumbu yangu ni sahihi Simu ya Kifo ni kitabu cha zamani zaidi na kiliandikwa na Hassan Hussein Katalambula kama sikosei na si Hammie Rajab.
simu.jpg
 
Hivi mrembo Zabibu alikuwepo katika simulizi ya kitabu gani...? nadhani ni Njama kama sikosei (nisahihishwe tafadhali). Willy Gamba alipojibarizi naye...alimsifia sana na kumwambia "Yaani, wewe kweli ni mtamu kama zabibu"

Mrembo Zabibu anapatikana kwenye kitabu cha NJAMA wengi waliosoma vitabu hivi walivisoma miaka ya 80 -90,
mimi nilikisoma NJAMA mwaka 1989 kama sijakosea
 

Attachments

  • njama book cover.jpg
    njama book cover.jpg
    150.4 KB · Views: 182
daaa nilisoma vtabu hivyo miaka ya 1989 mtwara huko yani acha tu jamani pia enzihzo sani lilikuwa toleo babu kubwa kuna mwandishi amri bawji huyu mtu wa tanga nadhani aliandika lovestory tanga nyika na unguja na kitabu flani cha pumbazo la moyo cjui viko wapi jamani.

Tanganyika na Unguja,majina ya wahusika yakatengeneza LOVE.Mchoraji Tibasima.
 
Kikosi cha Kisasi nilisikitika sana alipokufa Koffi alipokuwa na Ozu uku Willy Gamba akishuhudia.
 
Back
Top Bottom