Najua watu wengi sana macho yao yapo kwa Zidane. Lakini na yeye pia sio kocha mzuri wa kupewa kikosi kibovu akakitengeza. Zidane upande fulani ni kama Mourinho, give hi m the players he wants na sio umwambie aanze kumwagilia maji madogo wa academy. Tofauti ya Zidane na Mou, ni kwamba Z yeye wachezaji wana uhuru wa kucheza watakavyo as long as wanashirikiana na kutafuta ushindani wakati mourinho anataka ucheze anavotaka yeye hata kama ikibidi lukaku akae kipa lazima ukubali. Mou hata kama upo chini ya goli bado kupiga shuti ushinde yeye kama anataka urudishe mpira kwa jones basi uurudishe. ndio maana anakosana na wachezaji.
Tunaweza kwenda kwa pochettino, namuona kuwa ni mtu ambae kama anamwagiwa hela kama alizopewa Mouninho basi ataifikisha timu mbali. Au tunaweza kwenda kwa Simione nae pia ni kocha ambae ana uwezo, tatizo ni resources kwake ni limited kama pochetino.
MU ili panic baada ya Pep kujiunga na MC, ndio maana wakamtimua LVG na kumueka MO.
Sikatai MO anarekodi nzuri, enzi zake Chelsea ukifika Stamford unajitaarisha kuzuia usifungwe mengi, mana pale darajani hata SAF aliteswa sana na MOU, ila huyu wa sasa nawaambia watu kila siku, sio yule wa enzi zile damu inamchemka.