Jose Mourinho ni kocha mbovu anayebebwa na pesa za usajili

Morinho anachezea sana hela ya watu , ule mshahara wa Alexis Sanchoka ni halali kweli ?
 
Uchambuzi wako ni mzuri sana.

ila Mou aondoke tuu man u.
 
Morinho anachezea sana hela ya watu , ule mshahara wa Alexis Sanchoka ni halali kweli ?
Yaani tumemnunua Sanchez na hela yake ya mshahara, ni kumuonesha PEP kuwa tunauwezo wa kuwashinda kwenye kununua wachezaji na kuwalipa.....

Msimu wa tatu huu, hakuna improvement MUFC ya chochote.... ndio vile vile kama msimu ulopita.

MOU akitaka abaki MUFC abadilishe mfumo wake wa uchezaji na kuishi na wachezaji na ajifunze kuwapa motivation.... EPL ya sasa sio ya Zamani!

Mi hanishughulishi akicheza defence, lakini mchezji wetu akishika mpira hajui afanye nini ndio kinanikereketa.... Yaani Juzi Pogba ametoa pasi kwa invisible man ivi ivi kiwepesi!!!!!

MOU pesa anaichezea haswa!
 
Wewe unajua mpira sana
MTOA MADA HAJUI MPIRA KABISA NA HILI NI TATIZO KUBWA SANA
 
Naomba kuuliza tu kama hutojali

a) Kama fedha za usajili ndio zinambeba Jose, kule Porto alipewa mamilioni mangapi mpaka akafanikiwa kuchukua kombe la UCL? Inter Milan alipewa bilioni ngapi zikasababisha achukue UCL?

b) Pellegrin alipata mafanikio gani makubwa kupitia mamilioni aliyopewa na mwarabu wa Man City? Vipi kuhusu Unai Arsenal yeye alichukua kombe gani la maana ulaya baada ya kusaini mchezaji mmoja kwa fedha inayoweza kununua timu nzima ya Arsenal?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anayelalamika kukosa hela ya kuingia sokoni ni Morinho mwenyewe .
 
Anayelalamika kukosa hela ya kuingia sokoni ni Morinho mwenyewe .
Ana haki ya kulalamika

Kumbuka, yeye ndio kocha na anayajua mapungufu ya timu yake

Sasa anapoomba fedha ya Ku address tatizo kwenye timu yake, inakuwa kosa?

Amekuwa akitaka fedha anunue beki wa kati na winger lakini bahiri Glazer hayupo tayari kutoa hela (yeye anachoangalia ni mapato yanayomtajirisha yeye bila kuangalia furaha ya mashabiki)

Guardiola moja kati ya makocha bora duniani amepewa Tsh ngapi tangu awe kocha wa city? Zaidi ya milioni £ 350. Beki wa pembeni amenunua wawili, Mendy na Walker kila mmoja zaidi ya £ 50+ milioni (hapa naongelea beki wa pembeni, sio foward, ama kiungo ama beki wa kati)

Halafu baadae unataka aje ashindane na Pep, au Klop ambao wanapewa hela wanayotaka ili kujenga vikosi vyao. Kumbuka Klop amevunja rekodi ya usajili wa beki wa kati Van Dijk kwa zaidi ya £75 milion, akaja kuvunja rekodi ya kipa Alison kwa zaidi ya £ milioni 60, hii ilikuwa kabla Chelsea nao hawajaivunja rekodi hiyo ya kipa.

Mourinho ana haki ya kutaka hela zaidi. Kama wamiliki (kupitia Ed Woodward) wanataka mafanikio ya Man Utd ya kisoka watoe hela.

Utake, usitake mpira wa sasa ni hela.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa jibu hili, sijasema nimekudharau

Sent using Jamii Forums mobile app
huwa sipendi malumbano yasiyo na tija , sijawahi kuogopa kudharauliwa na asiyenifahamu , kama wewe ni mtu wa soka unaelewa kwamba kila mwezi epl inatoa kocha bora ambaye kiwango chake baada ya matokeo ya mechi za mwezi husika kimewazidi wengine , kwa hiyo kumbe kila kipindi fulani katika soka kunakuwa na aliye wazidi wenzake kiwango bila kujali makombe waliyobeba miaka 20 iliyopita.

Hata Moore ambaye ni kocha wa WBA iliyoshuka daraja alikuwa kocha bora mwishoni kabisa mwa msimu baada ya matokeo mazuri ya timu yake kwa mwezi ule.

NB : Hii ndio post yangu ya mwisho kujibizana na wewe .
 
Okay sasa nimekupata. Kumbe una judge mkimbiaji mzuri wa mbio za marathoni kwa mita 100 za kwanza alizokimbia. Na mimi hili ni jibu langu la mwisho kwako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…