Joseph Kusaga: Tamasha la Fiesta kufanyika Dar es Salaam Disemba, namiliki Redio zote za vijana

Joseph Kusaga: Tamasha la Fiesta kufanyika Dar es Salaam Disemba, namiliki Redio zote za vijana

CEO wa CMG Mr. Joseph Kusaga jana kupitia mahojiano yako katika 360 ulisikika ukisema kuwa Fiesta lazima ifanyike ndani ya mwaka huu, Lakini ulienda mbali sana na kufikia kusema umeshaongea hadi na Mh Rais kwaajili ya tamasha lako la Fiesta.

Kimsingi Afisa Utamaduni wa Manispaa ya kinondoni kwenye barua yake kwenu yenye Kumb No. KMC/UT/KMO/01 ya tarehe 23/11/2018 haikupiga marufuku Tamasha la Fiesta isipokuwa eneo lalamikiwa ambalo linafanyika tamasha lenu lilikuwa na karibu na Hospital na kuwataka tamasha lenu lipelekwe Tanganyika Peakers-kawe, Ata kama musingetaka lifanyike Tanganyika Peakers labda kutokana na miundombinu basi ata Uwanja wa uhuru ungefaa pia.

Kwenda kuongea na Mh Rais kushinikiza Tamasha lenu lifanyike Leaders tena ni kuto tii mamlaka za chini sasa musije kufikia hatua mukawa munamshinikiza Mh Rais avunje utaratibu wa mamlaka zake za chini kisa uswahiba wenu.

Nakutaka Kusaga kuheshimu mamlaka kwani manispaa ya Kinondoni ishapiga marufuku kwa shughuli zozote za matamasha kufanyika hapo Leaders na usitumie mwanya wa uswahiba wako na Mh Rais kushinikiza yale unayoyataka ilimradi sheria na taratibu zivunjwe.

CEO fuata utaratibu.
Team Bashite! Pilipili usiyoila inakuwashia Nini? Hayo yaliyoandikwa kwenye hiyo barua yalijulikana masaa machache kabla ya Tamasha? Alietoa kibali hakujuwa uwepo wa hizo sababu? Kawe hamna Hospitali? Hamna Wagonjwa wa BP?
Tanzania ina wajinga wengi Sana, kibaya zaidi, asilimia kubwa Ni Vijana, mmojawapo Ni wewe!
 
Hiyo takataka (fiesta) ina faida gani kwa nchi hii? Badala ya kujikita kwenye mambo ya msingi yanayogusa jamii pana kama retirement benefits, elimu, afya, n.k. tunajadili upuuzi ufanyikie wapi? What is fiesta?
 
Team Bashite! Pilipili usiyoila inakuwashia Nini? Hayo yaliyoandikwa kwenye hiyo barua yalijulikana masaa machache kabla ya Tamasha? Alietoa kibali hakujuwa uwepo wa hizo sababu? Kawe hamna Hospitali? Hamna Wagonjwa wa BP?
Tanzania ina wajinga wengi Sana, kibaya zaidi, asilimia kubwa Ni Vijana, mmojawapo Ni wewe!
Barua ilijieleza "Kutokana na malalamiko " so kilichofanya kusitishwa ni malalamiko sio kama Manispaa ilikurupuka tu! alafu majuzi hapa wametoa taarifa nyingine kuwa kwasasa shughuli za matamasha zisifanyike tena katika viwanja hivyo.
 
Team Bashite! Pilipili usiyoila inakuwashia Nini? Hayo yaliyoandikwa kwenye hiyo barua yalijulikana masaa machache kabla ya Tamasha? Alietoa kibali hakujuwa uwepo wa hizo sababu? Kawe hamna Hospitali? Hamna Wagonjwa wa BP?
Tanzania ina wajinga wengi Sana, kibaya zaidi, asilimia kubwa Ni Vijana, mmojawapo Ni wewe!
Kimsingi Kawe inapakana na Lugalo Barracks kwa karibu sana. Kwa maana hiyo hospitali ya jeshi ya Lugalo ndio wataathirika sana. Na Massana hopitali ilyopo Mbezi Juu.
 
Kimsingi Kawe inapakana na Lugalo Barracks kwa karibu sana. Kwa maana hiyo hospitali ya jeshi ya Lugalo ndio wataathirika sana. Na Massana hopitali ilyopo Mbezi Juu.
Hawa jamaa labda wanataka kutuaminisha kuwa Wagonjwa walioko karibu na Leaders Ni wa maana Sana kuliko wale walioko Karibu na Tanganyika Packers!
 
Kaongelea kujengwa kitu.. wewe unabwatuka upupwu..
Wazo la Endorsement ndilo unalo zungumzia na alisema " Kama Mh Rais unanisikia, Mh Waziri na Mkuu wangu wa Mkoa basi watupe eneo la kujenga Endorsement yenye kuchukua ata watu 20,000 kwa kushirikiana na wadau" lakini Issue ya fiesta alishasema alimeongea na Mh Rais tayari.

Ata Issue ya Endorsement nayo itakuja kuleta malalamiko maana Diamond alishawasilisha mpaka kwa Waziri mkuu kuomba eneo la kujenga Endorsement na Juzi mkubwa Fela nae kamuomba tena Waziri wa habari, Sanaa utamaduni na Michezo kuomba eneo la kujenga Endorsement tena.
 
Kimsingi Kawe inapakana na Lugalo Barracks kwa karibu sana. Kwa maana hiyo hospitali ya jeshi ya Lugalo ndio wataathirika sana. Na Massana hopitali ilyopo Mbezi Juu.
Ile Hospital karibu na Leaders inasemeka iko mita 200 tu toka Leaders sasa jenga picha kwa sound ile alafu kuna wagonjwa! mi naona kuna hoja hapa manispaa ikae etenge eneo maalumu kwajili ya shughuli hizo na inasemekana mwenye ile Hopsital ndiye alieindikia barua Manispaa kutaka lile tamasha lisitishwe lina wabuhudhi pale kutokana na ile Sound!
 
Hospital gani iko pale readers?
Ipo pale ilipo kuwa Tazara hostel. Lakini ninavyofahamu ilifungwa kwani NSSF walichukua vifaa baada ya mwenye hospitali kushindwa kulipa deni na baadae mwenye hospitali ile kufariki.
 
Watumishi fanyeni hujuma indirect dhidi ya serikali hii onevu kwenu ni miaka mitatu hakuna ongezeko la mishahara na maslahi yenu yanazidi kukandamizwa.
 
Hiyo takataka (fiesta) ina faida gani kwa nchi hii? Badala ya kujikita kwenye mambo ya msingi yanayogusa jamii pana kama retirement benefits, elimu, afya, n.k. tunajadili upuuzi ufanyikie wapi? What is fiesta?
Kama unaona haina faida kaa kimyaa
 
Sio kosa lako ila kama ungetambua makosa ya kisarufi andishi jinsi yanavyoigharimu adhira wala usingejaribu kubisha 'ttzo la binadam ataki kurekebishwa
Ushamba wako ndio umeona point ya kuongelea hiyo helufi, acha upoyoyo wako!!
 
Sio kosa lako ila kama ungetambua makosa ya kisarufi andishi jinsi yanavyoigharimu adhira wala usingejaribu kubisha 'ttzo la binadam ataki kurekebishwa
Huna unalolijua ina maana hujawahi kusoma threads ndefu, maana siku nzima ungekuwa una edit sarufi. Usiniletee njaa umetoka kwe hoja unaingia kwenye mambo hata yasiofikilisha akili.
 
Back
Top Bottom