Joseph Musukuma: Kikokotoo kinawaumiza wananchi, tunatengeneza taifa la wezi

Joseph Musukuma: Kikokotoo kinawaumiza wananchi, tunatengeneza taifa la wezi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Fuatilia kinachojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 15, Kikao cha 8, leo Aprili 17, 2024.


Mbunge wa Geita vijijini (CCM) Joseph Musukuma amesema Watanzania wanaliamini Bunge, na kuna vitu vimekuwa vinazungumzwa lakini havichukuliwi kwa uzito wake na kwamba Serikali na Wizara husika zikae chini kutafakari upya suala la kikokotoo kwani linawaumiza watanzania na linatengeneza taifa la wezi.

Amesema Wabunge na Serikali isiweke pamba masikioni kwani imekuwa ni ajenda inayojadiliwa kila siku, na Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Nchimbi amesisitiza suala hili lishughulikiwe.

"Nimebakiza miaka 3 na watoto wangu, natakiwa nistaafu nikajitegemee, sina nyumba nipo kwenye nyumba ya Serikali, halafu naenda kupata asilimia 30, lazima niondoke na mzigo liwalo na liwe. Kwahiyo ni vizuri tusijiwekee pamba masikioni, tuone namna ya kuwasikiliza, na kama kuna uwezekano wa kutatua hilo tatizo tulitatue" amesema Musukuma.
 
HIli linaumiza sana. Wazee wengine wakifikia kustaafu wakikutana na kikokotoo, huishia kuumwa kiharusi na kisukari.

Hawachukui muda mrefu wanakufa. Labda ndio mpango uliopo wa kuwaondoa wazee hawa kwa magojwa ya moyo, kupooza na kisukari?

Hili si sawa kabisa.
 
Fuatilia kinachojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 15, Kikao cha 8, leo Aprili 17, 2024.


Mbunge wa Geita vijijini (CCM) Joseph Musukuma amesema Watanzania wanaliamini Bunge, na kuna vitu vimekuwa vinazungumzwa lakini havichukuliwi kwa uzito wake na kwamba Serikali na Wizara husika zikae chini kutafakari upya suala la kikokotoo kwani linawaumiza watanzania na linatengeneza taifa la wezi.

Amesema Wabunge na Serikali isiweke pamba masikioni kwani imekuwa ni ajenda inayojadiliwa kila siku, na Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Nchimbi amesisitiza suala hili lishughulikiwe.

"Nimebakiza miaka 3 na watoto wangu, natakiwa nistaafu nikajitegemee, sina nyumba nipo kwenye nyumba ya Serikali, halafu naenda kupata asilimia 30, lazima niondoke na mzigo liwalo na liwe. Kwahiyo ni vizuri tusijiwekee pamba masikioni, tuone namna ya kuwasikiliza, na kama kuna uwezekano wa kutatua hilo tatizo tulitatue" amesema Musukuma.

Elimu yetu imeshindwa kutusaidia, Bunge Lina watu wanaojiita wasomi ila hakuna wanachoisaidia nchi, mtu kama Msukuma mnaomwita Kilaza sio msomi ndio anaongea vitu vya kueleweka kuliko hata hao wanaojiita wasomi
 
Yaani anmtetea mtu ambae amekaa nyumba ya serikali miaka 30 bure kashindwa kujenga ndani ya muda huo. Watanzania inabidi tujifunze wengine wanavyoishi huko.

Nchi zilizoendelea ukipata benefits zifuatazo bure, kama nyumba, gari full time, mafuta, furnishing, matunzo ya nyumba. Tax man atakwambia hizo ni ‘benefits in kind’.

Nyumba itaangaliwa thamani yake ya kukodisha sokoni utalipa percentage fulani ya market rent value kama kodi, mafuta utapigiwa bei ya mwezi unayogharamiwa utalipa kama kodi, furniture za nyumba zikizidi kiwango kinachoruhusiwa excess utalipa kama kodi.

Hakuna vya bure bure huko na bado mtu anastaafu na nyumba nzuri tu kwa sababu akiwa kwenye benefits za taasisi anaokoa hela nyingi tu. Yaani Tanzania mtu anataka kumuhurumia mtu alieishi miaka 20-30 kwa benefits luluki ambazo free.

Anahitajika mtu wa kuwabadili fikra watanzania.
 
Elimu yetu imeshindwa kutusaidia, Bunge Lina watu wanaojiita wasomi ila hakuna wanachoisaidia nchi, mtu kama Msukuma mnaomwita Kilaza sio msomi ndio anaongea vitu vya kueleweka kuliko hata hao wanaojiita wasomi
Mimi naona kidogo tofauti nawewe mkuu.....
Nadhani hapa tatizo ni mfumo na chama chakavu kinavyo endesha sirikali kwa fikra zilizo zeeka.
Binafsi naona kama wasomi wetu wamegundua kwamba siasa ndio kilakitu ili kujilimbikizia mali na kuilinda mianya yao ya upigaji.
 
Mwambieni Samiah kumtoa Ndalichako kisa kikotoo haitomsaidia kabisa!!

Kikotoo kitaipa upinzani serikali 2025!!

Mimi siwezi pigia kura mbunge ,diwani na Raise aliepitisha kikotoo hata kama ni mwana CCM mwenzangu napigia upinzani kabisa Ili mtumie polisi na Dola ku foji uchaguzi!!
 
Yaani anmtetea mtu ambae amekaa nyumba ya serikali miaka 30 bure kashindwa kujenga ndani ya muda huo. Watanzania inabidi tujifunze wengine wanavyoishi huko.

Nchi zilizoendelea ukipata benefits zifuatazo bure, kama nyumba, gari full time, mafuta, furnishing, matunzo ya nyumba. Tax man atakwambia hizo ni ‘benefits in kind’.

Nyumba itaangaliwa thamani yake ya kukodisha sokoni utalipa percentage fulani ya market rent value kama kodi, mafuta utapigiwa bei ya mwezi unayogharamiwa utalipa kama kodi, furniture za nyumba zikizidi kiwango kinachoruhusiwa excess utalipa kama kodi.

Hakuna vya bure bure huko na bado mtu anastaafu na nyumba nzuri tu kwa sababu akiwa kwenye benefits za taasisi anaokoa hela nyingi tu. Yaani Tanzania mtu anataka kumuhurumia mtu alieishi miaka 20-30 kwa benefits luluki ambazo free.

Anahitajika mtu wa kuwabadili fikra watanzania.
Mkuu, kwa nini unashangaa?

Unaishi nchi gani kwani wewe, nchi yetu sisi, inawatu masikini mno mkuu

Huku kwetu familia moja inaweza kuwa na mmoja tu aliyejaliwa kuwa mfanyakazi anayelipwa, na malipo menyewe pengine ni miatano elfu tu,

Jamii yake nayo inamwangalia huyo huyo, akiigawagawa haiwezi hata kumfikisha mwezi mwingine, sasa kama ni hivyo, ataanzaje kujenga mkuu

Nchini kwenu naona mko vizuri mkuu, hadi unatushangaa sisi bongo?
 
Fuatilia kinachojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 15, Kikao cha 8, leo Aprili 17, 2024.


Mbunge wa Geita vijijini (CCM) Joseph Musukuma amesema Watanzania wanaliamini Bunge, na kuna vitu vimekuwa vinazungumzwa lakini havichukuliwi kwa uzito wake na kwamba Serikali na Wizara husika zikae chini kutafakari upya suala la kikokotoo kwani linawaumiza watanzania na linatengeneza taifa la wezi.

Amesema Wabunge na Serikali isiweke pamba masikioni kwani imekuwa ni ajenda inayojadiliwa kila siku, na Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Nchimbi amesisitiza suala hili lishughulikiwe.

"Nimebakiza miaka 3 na watoto wangu, natakiwa nistaafu nikajitegemee, sina nyumba nipo kwenye nyumba ya Serikali, halafu naenda kupata asilimia 30, lazima niondoke na mzigo liwalo na liwe. Kwahiyo ni vizuri tusijiwekee pamba masikioni, tuone namna ya kuwasikiliza, na kama kuna uwezekano wa kutatua hilo tatizo tulitatue" amesema Musukuma.

jambo hili ni la kisera lakini pia ni la kisheria. Serikali sikivu ya ccm, imesikia maoni na mitazamo ya wanainchi, wadau na wafanyakazi juu ya kikokotoa cha sasa, na bila shaka kwa wakatiki muafaka itakuja na maelezo na hatua mujarabu za kimkakati, kisera na kusheria, ili hatimae kuhitimisha jambo hili kwa muafaka wa pamoja... :NoGodNo:

muhimu zaidi ni kua wastahimilivu, wangwana na wenye subra:Doits:
 
Mwambieni Samiah kumtoa Ndalichako kisa kikotoo haitomsaidia kabisa!!

Kikotoo kitaipa upinzani serikali 2025!!

Mimi siwezi pigia kura mbunge ,diwani na Raise aliepitisha kikotoo hata kama ni mwana CCM mwenzangu napigia upinzani kabisa Ili mtumie polisi na Dola ku foji uchaguz
Mkuu Ndalichako kahusikaje na lawama za sera ya kikokotoo?
 
Msiwafanye wananchi wajinga nyie wafanyakazi wa serikali

Wananchi inabidi tuingie mitaani kupinga asilimia 15 serikali iliyowachangia michango ya pension kila mwezi kutokana na kodi zetu iondolewe kwenye kikokotoo h8cho kioya haraka

Haiwezekani mnalipwa mishahara wengine hata ajira hawana mnachangia mifuko ya pension asilimia 5 tu halafu serikali inakamua tena walipa kodi inawachangia asilimia 15 kila mwezi mifuko ya pension Huo ni wizi .Hizo asilimia 15 kama zimo humo.kwenye kikotoo zitolewe zirudi hazina zipelekwe kwa vijana wasio na ajira wakajiajiri nyie chukueni pension asilimia tano tu mlizochangia

Kodi zetu hizo asilimia 15 tunazitaka wananchi ..Mnalipwa mara mbili nyie wafanyakazu wa serikali kwanza mnalipwa mishahara halafu tena mnalipiwa asilimia 15 ya michango ya pension .Hilo haliko sawa .Hizo asilimia 15 ziende kwenye mfuko wa kusaidia wasio na ajira wakiwa naxo nao watachangia asimia tano

Nyie wafanyakazi wa serikali na wabunge ndio mnaokula sana keki ya nchi.Wafanyakazi tunataka asilimia 15 hiyo irudi hazina msiichukue chukueni asilimia tano yenu hiyo ndio haki yenu

Kikokoto kipya kitoe hizo asilimia 15 mtakapolipwa sio zenu hizo zenu asilimia 5 ndio zenu

Kikokotoo cha sasa kijizi kinaibia kodi za wananchi asilimia 15 wanazochangiwa na serikali mifuko ya pension .Hiyo asilimia 15 iondolewe kwenye kikokotoo
 
Back
Top Bottom