Joseph Musukuma: Kikokotoo kinawaumiza wananchi, tunatengeneza taifa la wezi

Joseph Musukuma: Kikokotoo kinawaumiza wananchi, tunatengeneza taifa la wezi

Yaani anmtetea mtu ambae amekaa nyumba ya serikali miaka 30 bure kashindwa kujenga ndani ya muda huo. Watanzania inabidi tujifunze wengine wanavyoishi huko.

Nchi zilizoendelea ukipata benefits zifuatazo bure, kama nyumba, gari full time, mafuta, furnishing, matunzo ya nyumba. Tax man atakwambia hizo ni ‘benefits in kind’.

Nyumba itaangaliwa thamani yake ya kukodisha sokoni utalipa percentage fulani ya market rent value kama kodi, mafuta utapigiwa bei ya mwezi unayogharamiwa utalipa kama kodi, furniture za nyumba zikizidi kiwango kinachoruhusiwa excess utalipa kama kodi.

Hakuna vya bure bure huko na bado mtu anastaafu na nyumba nzuri tu kwa sababu akiwa kwenye benefits za taasisi anaokoa hela nyingi tu. Yaani Tanzania mtu anataka kumuhurumia mtu alieishi miaka 20-30 kwa benefits luluki ambazo free.

Anahitajika mtu wa kuwabadili fikra watanzania.
Nani alikuambia wafanyakazi wa serikali ukiacha wa vyombo vya ulinzi na usalama wanaishi ktk nyumba za serikali bure?. Hata hao wengine tunao wanaishi huku mitaani wamepanga. Walio ktk nyumba za serikali waliobakia hulipa 10%:ya mishahara kulipia kodi. Barua zao zote za ajira hazina kipengele cha kupewa nyumba ya serikali. Wanaobahatika kupewa nyumba ni wale wakuu wa wizra, vitengo ambao ni wachache sana na mara nyingi wanatokea ktk nyumba za kupanga kabla ya UTEUZI.

Hawa huwa hawana uwezo wa kujenga nyumba ktk miaka 30 wanayifanyakazi mpaka wanapostaafu. Vitu muhimu ni kuwa na familia kuikuza kiafya na elimu kwa mishahara midogo wanayopata.

Wanapostaafu ndio hupata pesa ya kujenga kajumba. Ndio sababu wanalalamika kulipwa 33% ya kiinua mgongo halafu ile pesa ya pensheni ya kila mwezi wanapata mwisho miaka 72. Hapo unaachwa ufe. Wakubwa wanaendelea kulipwa mpaka wafe kwa kikotoo cha zamani. UMEELEWA?
 
Mkuu, kwa nini unashangaa?

Unaishi nchi gani kwani wewe, nchi yetu sisi, inawatu masikini mno mkuu

Huku kwetu familia moja inaweza kuwa na mmoja tu aliyejaliwa kuwa mfanyakazi anayelipwa, na malipo menyewe pengine ni miatano elfu tu,

Jamii yake nayo inamwangalia huyo huyo, akiigawagawa haiwezi hata kumfikisha mwezi mwingine, sasa kama ni hivyo, ataanzaje kujenga mkuu

Nchini kaenu naona mko vizuri mkuu, hadi unatushangaa sisi bongo?
Kiongozi embu tuwe wa kweli

Mtu anaishi nyumba ya serikali rent mtaani nyumba anayoishi tena sio prime area labda laki 5-7 kwa mwezi. Ndani ya mwaka anaokoa million sita mpaka nane. Mafuta gari ya kazini kwa mwezi labda matumizi yake binafsi ni łąki mbili mpaka tatu, anaokoa millioni mbili mpaka tatu ukijumlisha ndani ya mwaka, mshahara million tatu plus kwa mwezi.

Kwa mwaka anaokoa kama 8-10 million kwenye mshahara wake. Halafu unakuta mtu private na mshahara wa millioni nne au tano kabla ya 40 years ana nyumba yake bila hizo ‘benefits-in-kind’ za watumishi na wenyewe wana ndugu hao hao wakuwasaidia na kusomesha.

Ifike wakati watu waambizane ukweli, uwezi kufanya kazi zaidi ya miaka 20 serikalini huku ukipokea benefits zote hizo usiwe na nyumba hata kama hukua mpiga deal.
 
Nani alikuambia wafanyakazi wa serikali ukiacha wa vyombo vya ulinzi na usalama wanaishi ktk nyumba za serikali bure?. Hata hao wengine tunao wanaishi huku mitaani wamepanga. Walio ktk nyumba za serikali waliobakia hulipa 10%:ya mishahara kulipia kodi. Barua zao zote za ajira hazina kipengele cha kupewa nyumba ya serikali. Wanaobahatika kupewa nyumba ni wale wakuu wa wizra, vitengo ambao ni wachache sana na mara nyingi wanatokea ktk nyumba za kupanga kabla ya UTEUZI. Hawa huwa hawana uwezo wa kujenga nyumba ktk miaja 30 wanayifanyakazi mopaka wanapostaafu. Vitu muhimu ni kuwa na familia kuikuza kiafya na elimu kwa mishahara midogo wanayopata. Wanapostaafu ndio hupata pesa ya kujenga kajumba. Ndio sababu wanalalamika kulipwa 33% ya kiinua mgongo halafu ile pesa ya pendheni ya kila mwezi wanapata mwisho miaka 72. Hapo unaachwa ufe. Wakubwa wanaendelea kulipwa mpaka wafe kwa kikotoo cha zamani. UMEELEWA?
Hata 10% ya kodi bado wana save kiasi kikubwa ndani ya mwaka kuweza kujenga taratibu kwa miaka 20. Iweje private kwa mishahara hiyo waweze halafu wao washindwe.
 
Kiongozi embu tuwe wa kweli

Mtu anaishi nyumba ya serikali rent mtaani nyumba anayo tena sio prime area labda laki 5-7 kwa mwaka anaokoa million sita mpaka nane. Mafuta gari ya kazini kwa mwezi labda matumizi yake łąki mbili mpaka tatu kwa matumizi binafsi anaokoa millioni mbili mpaka tatu ukijumlisha, mshahara million tatu kwa mwezi.

Kwa mwaka anaokoa kama 8-10 million kwenye mshahara wake. Halafu unakuta mtu private na mshahara wa millioni nne au tano kabla ya 40 years ana nyumba yake bila hizo ‘benefits-in-kind’ za watumishi na wenyewe wana ndugu hao hao wakuwasaidia na kusomesha.

Ifike wakati watu waambizane ukweli, uwezi kufanya kazi zaidi ya miaka 20 serikalini huku ukipokea benefits zote hizo usiwe na nyumba hata kama hukua mpiga deal.
Nilichogundua mpaka hapa, wewe ni mfanya biashara, na kanuni ya biashara, ni uchoyo uliopitiliza kiwango cha utu

Inasemekana, ili ufaulu katika biashara, umeamka na miliono 20, mpango wake ni kuongeza na kupanua biadhara, hata ikitokea mzazi wako yuko taabani anahitaji elfu kumi kutoka kwenye m.20, usitoe, labda umtafutie kwingineko, na ikitokea umekosa, bora mzazi afe ili biashara iende

Mkuu, bado tuna nchi yenye watu masikini mno, 50k ya mshahara ya mtu mmoja kwenye jamii ya watu 10 masikini hawezi kujenga mpaka mafao aisee
 
Nilichogundua mpaka hapa, wewe ni mfanya biashara, na kanuni ya biashara, ni uchoyo uliopitiliza kiwango cha utu

Inasemekana, ili ufaulu katika biashara, umeamka na miliono 20, mpango wake ni kuongeza na kupanua biadhara, hata ikitokea mzazi wako yuko taabani anahitaji elfu kumi kutoka kwenye m.20, usitoe, labda umtafutie kwingineko, na ukikosa bora mzazi afe ili biashara iende

Mkuu, bado tuna nchi yenye watu masikini mno, 50k ya mshahara ya mtu mmoja kwenye jamii ya watu 10 masikini hawezi kujenga mpaka mafao aisee
Aijalishi unafanya shughuli gani jukumu la ‘personal finance’ ni lako. Kila mtu kwa situation yake anatakiwa kupanga goals za mbeleni especially watu walioelimika kama waajiriwa wa serikalini.

Hawa watu wanakuwa na advantages nyingi during their working life isipokuwa they make poor financial decisions or live reckless lives wakitegemea pension kama mwokozi ndio maana wanataka rules zao kwenye malipo badala ya kujipanga mapema.

Pension inatakiwa ikusaidie usipate tabu wakati wa kustaafu hiyo withdrawal ya 33% ndio muda wa kwenda mbugani au hata kwenda Kenya na mkewe/mume mtu anawaza kujengea au kuanzishia biashara.
 
Msiwafanye wananchi wajinga nyie wafanyakazi wa serikali

Wananchi inabidi tuingie mitaani kupinga asilimia 15 serikali iliyowachangia michango ya pension kila mwezi kutokana na kodi zetu iondolewe kwenye kikokotoo h8cho kioya haraka

Haiwezekani mnalipwa mishahara wengine hata ajira hawana mnachangia mifuko ya pension asilimia 5 tu halafu serikali inakamua tena walipa kodi inawachangia asilimia 15 kila mwezi mifuko ya pension Huo ni wizi .Hizo asilimia 15 kama zimo humo.kwenye kikotoo zitolewe zirudi hazina zipelekwe kwa vijana wasio na ajira wakajiajiri nyie chukueni pension asilimia tano tu mlizochangia

Kodi zetu hizo asilimia 15 tunazitaka wananchi ..Mnalipwa mara mbili nyie wafanyakazu wa serikali kwanza mnalipwa mishahara halafu tena mnalipiwa asilimia 15 ya michango ya pension .Hilo haliko sawa .Hizo asilimia 15 ziende kwenye mfuko wa kusaidia wasio na ajira wakiwa naxo nao watachangia asimia tano

Nyie wafanyakazi wa serikali na wabunge ndio mnaokula sana keki ya nchi.Wafanyakazi tunataka asilimia 15 hiyo irudi hazina msiichukue chukueni asilimia tano yenu hiyo ndio haki yenu

Kikokoto kipya kitoe hizo asilimia 15 mtakapolipwa sio zenu hizo zenu asilimia 5 ndio zenu
Hayo uliyoandika ndio mkataba wao na serikali ulivyokuwa? Mkataba wa hao wazee na serikali ni kwamba wewe serikali changia 15% na Mimi mfanyakazi nachangia 5% na hizo Hela ni mali ya mfanyakazi.
 
Hayo uliyoandika ndio mkataba wao na serikali ulivyokuwa? Mkataba wa hao wazee na serikali ni kwamba wewe serikali changia 15% na Mimi mfanyakazi nachangia 5% na hizo Hela ni mali ya mfanyakazi....
Wafanyakazi wanalipwa kwa kodi za wananchi

Wapi wananchi walishirikishwa huo mkataba?

Huo wizi kabisa ni mkataba wa kifisadi wa kuiba pesa za walipa kodi.Haiwezekani mtu alipwe mshahara halafu umwambie nitakulipia pia Pension asilimia 15 wewe utachanga asilimia tano tu.Huo mkataba ni wa kifisadi kati ya serikali na wafanyakazi wake ufutwe upesi na kwenye kikokotoo hiki kipyac iondolewe hiyo asilimia 15.Walipwe kwa hizo asilimia 5 zao tu walizochangia

Kama serikali imeamua kulipia pension wananchi wake kwanini ibague wananchi mbona serikali haiwalipii pension hata asilimia moja tu kila mwezi wanaozalisha mazao yanayoingiza pato la pesa za kigeni na za ndani wanaopinda migongo kila siku ?
Hawa wakulima miaka 55 wanakuwa wamechoka sana wanastahili kudtaafu kilimo nao kwa nini serikali haichangii pension huko?

Wizi huo mkataba utenguliwe haraka ni wa kifisadi.Serikali na wafanyakazi wameamua kukubaliana kuibia wananchi
 
Aijalishi unafanya shughuli gani jukumu la ‘personal finance’ ni lako. Kila mtu kwa situation yake anatakiwa kupanga goals za mbeleni especially watu walioelimika kama waajiriwa wa serikalini.

Hawa watu wanakuwa na advantages nyingi during their working life isipokuwa they make poor financial decisions or live reckless lives wakitegemea pension kama mwokozi ndio maana wanataka rules zao kwenye malipo badala ya kujipanga mapema.

Pension inatakiwa ikusaidie usipate tabu wakati wa kustaafu hiyo withdrawal ya 33% ndio muda wa kwenda mbugani au hata kwenda Kenya na mkewe/mume mtu anawaza kujengea au kuanzishia biashara.
Mkuu, watu wanalalamika sababu mishahara ni midogo sana.
Kiongozi embu tuwe wa kweli

Mtu anaishi nyumba ya serikali rent mtaani nyumba anayoishi tena sio prime area labda laki 5-7 kwa mwezi. Ndani ya mwaka anaokoa million sita mpaka nane. Mafuta gari ya kazini kwa mwezi labda matumizi yake binafsi ni łąki mbili mpaka tatu, anaokoa millioni mbili mpaka tatu ukijumlisha ndani ya mwaka, mshahara million tatu plus kwa mwezi.

Kwa mwaka anaokoa kama 8-10 million kwenye mshahara wake. Halafu unakuta mtu private na mshahara wa millioni nne au tano kabla ya 40 years ana nyumba yake bila hizo ‘benefits-in-kind’ za watumishi na wenyewe wana ndugu hao hao wakuwasaidia na kusomesha.

Ifike wakati watu waambizane ukweli, uwezi kufanya kazi zaidi ya miaka 20 serikalini huku ukipokea benefits zote hizo usiwe na nyumba hata kama hukua mpiga deal.
Toka jana, nilikuambia kunauwezekano hufahamu salary scale za watumishi wengi wa serikali.

Ungekuwa unafahamu, nadhani usinge thubutu kusema watumishi ni wazembe, haiwezekan aslimia 80 ya watumishi wawe wazembe? haiwezekani!

Tatizo kubwa ni kuwa mishahara ni midogo sana, saaana! how do you save If gross ni Tsh 720K then hapo ukatwe, PAYE, PSSF,HESLB,NHIF unabaki na 500 au 400+K, how can this amount be saved??

And mostly hiyo take home is for financing chakula, ada,and rent!
 
Fuatilia kinachojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 15, Kikao cha 8, leo Aprili 17, 2024.


Mbunge wa Geita vijijini (CCM) Joseph Musukuma amesema Watanzania wanaliamini Bunge, na kuna vitu vimekuwa vinazungumzwa lakini havichukuliwi kwa uzito wake na kwamba Serikali na Wizara husika zikae chini kutafakari upya suala la kikokotoo kwani linawaumiza watanzania na linatengeneza taifa la wezi.

Amesema Wabunge na Serikali isiweke pamba masikioni kwani imekuwa ni ajenda inayojadiliwa kila siku, na Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Nchimbi amesisitiza suala hili lishughulikiwe.

"Nimebakiza miaka 3 na watoto wangu, natakiwa nistaafu nikajitegemee, sina nyumba nipo kwenye nyumba ya Serikali, halafu naenda kupata asilimia 30, lazima niondoke na mzigo liwalo na liwe. Kwahiyo ni vizuri tusijiwekee pamba masikioni, tuone namna ya kuwasikiliza, na kama kuna uwezekano wa kutatua hilo tatizo tulitatue" amesema Musukuma.

Hiki kikokotoo ndicho kitakachoiondoa serikali ya kifisadi ya CCM madarakani mwaka 2025 misa ya kwanza tu. Hawa mbwa wanatusumbua sana.
 
Yaani anmtetea mtu ambae amekaa nyumba ya serikali miaka 30 bure kashindwa kujenga ndani ya muda huo. Watanzania inabidi tujifunze wengine wanavyoishi huko.

Nchi zilizoendelea ukipata benefits zifuatazo bure, kama nyumba, gari full time, mafuta, furnishing, matunzo ya nyumba. Tax man atakwambia hizo ni ‘benefits in kind’.

Nyumba itaangaliwa thamani yake ya kukodisha sokoni utalipa percentage fulani ya market rent value kama kodi, mafuta utapigiwa bei ya mwezi unayogharamiwa utalipa kama kodi, furniture za nyumba zikizidi kiwango kinachoruhusiwa excess utalipa kama kodi.

Hakuna vya bure bure huko na bado mtu anastaafu na nyumba nzuri tu kwa sababu akiwa kwenye benefits za taasisi anaokoa hela nyingi tu. Yaani Tanzania mtu anataka kumuhurumia mtu alieishi miaka 20-30 kwa benefits luluki ambazo free.

Anahitajika mtu wa kuwabadili fikra watanzania.
Vitu ratio ya hali ya maisha na kiwango cha mishahara uko nchi ulizotolea mfano ni sawa na hapa kwetu?
 
Msiwafanye wananchi wajinga nyie wafanyakazi wa serikali

Wananchi inabidi tuingie mitaani kupinga asilimia 15 serikali iliyowachangia michango ya pension kila mwezi kutokana na ko asilimia 15 wanazochangiwa na serikali mifuko ya pension .Hiyo asilimia 15 iondolewe kwenye kikokotoo
Tulia sindano ziingie wewe. Hizo 15% ni zile ambazo serikali inawaibia watumishi wa umma kwa kuwapunja mishahara yao. Sasa wanaamua kuzirejesha kwa mlango wa nyuma. Hata hizo 15% ni ndogo sana walipaswa waongeze hadi 30%. Unafurahi sana unapoona watu wakidhulumiwa haki yao. Mchawi mkubwa!
 
Elimu yetu imeshindwa kutusaidia, Bunge Lina watu wanaojiita wasomi ila hakuna wanachoisaidia nchi, mtu kama Msukuma mnaomwita Kilaza sio msomi ndio anaongea vitu vya kueleweka kuliko hata hao wanaojiita wasomi
Mkuu wasomi na usomi ni vilaza na ukilaza wenyewe , wasomi wengi wamefungwa kwenye fikra za watu wengine( vitabu).
 
Mkuu, watu wanalalamika sababu mishahara ni midogo sana.

Toka jana, nilikuambia kunauwezekano hufahamu salary scale za watumishi wengi wa serikali.

Ungekuwa unafahamu, nadhani usinge thubutu kusema watumishi ni wazembe, haiwezekan aslimia 80 ya watumishi wawe wazembe? haiwezekani!

Tatizo kubwa ni kuwa mishahara ni midogo sana, saaana! how do you save If gross ni Tsh 720K then hapo ukatwe, PAYE, PSSF,HESLB,NHIF unabaki na 500 au 400+K, how can this amount be saved??

And mostly hiyo take home is for financing chakula, ada,and rent!
I get it kuna struggle in the beginning but then salary inapanda over the years. Unapostaafu bado una faida pension inakuwa-calculate kwa kuangalia mshahara wako wa mwisho sio mwanzo.

So automatic unafaidika maana michango ya mwanzo ni kidogo na ndio miaka mingi, wakati calculations za malipo zinaangalia miaka ya mwisho hiyo hela ya nyongeza pension fund lazima wajue wanaitoa wapi.

Halafu kwenye jamii walau watumishi wana-pension, si ajabu wote mke na mume.

Huku kuna watanzania wengi sana with degree qualifications hawana ajira, zikitangazwa ajira kuna wakati walijaribu kufanya usaili uwanja wa Mkapa nusu ulijaa vijana.

Ili watumishi wapate hiyo pension yao serikali inatumia resources nyingi sana, bado kuna changamoto za pension investments to how they work hadi ulipwe average ya miaka ya mwisho na wao wana changamoto zao za ‘cash-flow’.

Sasa sidhani kama serikali ime set hiyo withdrawal ya 33% kwa intentions za kuonea watu ni kwa sababu ya uhalisia wa cash-flow za mfuko na available liquidity ya kila mwaka ili waweze kukidhi kulipa (story ni ndefu to how they increase their financial assets).

Jaribu kufikiria kwa mwaka kama kuna wastaafu laki moja tu huo mzigo wa malipo sio mdogo na kila mtu analipwa kwa average ya mshahara wake wa mwisho. Kila mtu akichukua 50% ya lump-sum withdrawal sidhani kama watabaki na kitu. Na uwekezaji wao mara nyingi pension funds ni kwenye bonds za miaka mingi hizi taasisi kawaida hazina liquid assets banks wana value tu za bonds na source kubwa ya hela zao interest earned.

Jumlisha na white elephants projects kibao za pension funds ambazo zimechukua hela nyingi ambazo hazirudi kwa haraka kwa hivyo mfuko financial una struggle that’s just common sense.

Ni hivi kuna changamoto na CAG anazielezea mara kwa mara kwenye report yake, serikali imekuja na utaratibu ambao wanadhani wanaweza mudu watu hawataki kuelewa, halafu anatokea huyo msukuma anataka mpaka mijitu iliyokuwa na uwezo wa kujenga katika muda wao (wale ambao wameishi nyumba za serikali waibe kama serikali aiwezi wapa 50%).

Binafsi naona watumishi ni ungrateful
 
Vitu ratio ya hali ya maisha na kiwango cha mishahara uko nchi ulizotolea mfano ni sawa na hapa kwetu?
Hiyo posts inaongelea watu wanaokaa nyumba za serikali na wanaopata marupurupu tele, halafu wanastaafu bila ya kujenga. Sasa hawa kutokujenga alaumiwe serikali pia.
 
Kwa mtazamo wako huu, wastaafu wote wa mafao walikuwa wanakaa nyumba za serikali au za bure wakiwa kazini?
Hapana labda nazungumzia hoja ya msukuma leo. sijasema watumishi wote wanakaa nyumba za seriali au ata wana-magari ya serikali.
 
Yaani anmtetea mtu ambae amekaa nyumba ya serikali miaka 30 bure kashindwa kujenga ndani ya muda huo. Watanzania inabidi tujifunze wengine wanavyoishi huko.

Nchi zilizoendelea ukipata benefits zifuatazo bure, kama nyumba, gari full time, mafuta, furnishing, matunzo ya nyumba. Tax man atakwambia hizo ni ‘benefits in kind’.

Nyumba itaangaliwa thamani yake ya kukodisha sokoni utalipa percentage fulani ya market rent value kama kodi, mafuta utapigiwa bei ya mwezi unayogharamiwa utalipa kama kodi, furniture za nyumba zikizidi kiwango kinachoruhusiwa excess utalipa kama kodi.

Hakuna vya bure bure huko na bado mtu anastaafu na nyumba nzuri tu kwa sababu akiwa kwenye benefits za taasisi anaokoa hela nyingi tu. Yaani Tanzania mtu anataka kumuhurumia mtu alieishi miaka 20-30 kwa benefits luluki ambazo free.

Anahitajika mtu wa kuwabadili fikra watanzania.
Ndio sasa akistahafu alipwe chake .........unampatia 30% halafu hiyo 70% unabaki nayo.....akifariki ndio basi tena
 
Back
Top Bottom