Joseph Musukuma: Kikokotoo kinawaumiza wananchi, tunatengeneza taifa la wezi

Joseph Musukuma: Kikokotoo kinawaumiza wananchi, tunatengeneza taifa la wezi

I get it kuna struggle in the beginning but then salary inapanda over the years. Unapostaafu bado una faida pension ina-calculate mshahara wako wa mwisho sio mwanzo.

So automatic unafaidika maana michango ya mwanzo ni kidogo na ndio miaka mingi, wakati calculations za malipo zinaangalia miaka ya mwisho hiyo hela pension fund lazima wajue wanaitoa wapi.

Halafu kwenye jamii walau watumishi wana-pension, si ajabu wote mke na mume ya uzeeni.

Huku kuna watanzania wengi sana with degree qualifications hawana ajira, zikitangazwa kuna wakati walijaribu kufanya usaili uwanja wa Mkapa nusu ulijaa vijana.

Ili watumishi wapate hiyo pension yao serikali inatumia resources nyingi sana, bado kuna changamoto za pension investments to how they work hadi ulipwe average ya miaka ya mwisho na changamoto zao za ‘cash-flow’.

Sasa sudhani kama serikali ime set hiyo withdrawal ya 33% kwa intentions za kuonea watu ni kwa sababu ya uhalisia wa cash-flow za mfuko na available liquidity ya kila mwaka ili waweze kukidhi kulipa (story ni ndefu to how they increase their assets).

Jaribu kufikiria kwa mwaka kama kuna wastaafu laki moja tu huo mzigo wa malipo sio mdogo na kila mtu analipwa kwa average ya mshahara wake wa mwisho. Kila mtu akichukua 50% ya lump-sum withdrawal sidhani kama watabaki na kitu. Na uwekezaji wao mara nyingi pension funds ni kwenye bonds za miaka mingi hizi taasisi kawaida hazina liquid assets banks wana value tu za bonds na interest earned.

Ni hivi kuna changamoto na CAG anazielezea mara kwa mara kwenye report yake, serikali imekuja na utaratibu ambao wanadhani wanaweza mudu watu hawataki kuelewa, halafu anatokea huyo msukuma anataka mpaka mijitu iliyokuwa na uwezo wa kujenga katika muda wao (wale ambao wameishi nyumba za serikali waibe kama serikali aiwezi wapa 50%).

Binafsi naona watumishi ni ungrateful
Ili uelewe vizuri, tafuta salary scale za watumishi! huyo mwenye degree uliza ana staafu akiwa na level gani ya mshahara hapo ndio utajua kuwa watumishi wa umma wanapitia magumu.

Naamini hapo utakuwa katika position nzuri sana ya ku argue basing on reality!

Haya unayoyasema ni mtazamo tu, kama motivation speakers wanavyo motivate watu without regarding reality ya kipato cha mtanzania au watumishi wa umma.

Sio rahisi mtumishi aache kulipia ada watoto, au kuhudumia familia, aanzishe project itakayo mcost lot of money wakati cash in-flow ni kiduchu, atafungwa au kufilisiwa hata hicho kidogo alichinacho.

Waulize waajiri kuhusu madeni waliyonayo, watumishi wao, ndio utajua uhalisia wa hichi tunacho jadili hapa.
 
Wafanyakazi wanalipwa kwa kodi za wananchi

Wapi wananchi walishirikishwa huo mkataba?

Huo wizi kabisa ni mkataba wa kifisadi wa kuiba pesa za walipa kodi.Haiwezekani mtu alipwe mshahara halafu umwambie nitakulipia pia Pension asilimia 15 wewe utachanga asilimia tano tu.Huo mkataba ni wa kifisadi kati ya serikali na wafanyakazi wake ufutwe upesi na kwenye kikokotoo hiki kipyac iondolewe hiyo asilimia 15.Walipwe kwa hizo asilimia 5 zao tu walizochangia

Kama serikali imeamua kulipia pension wananchi wake kwanini ibague wananchi mbona serikali haiwalipii pension hata asilimia moja tu kila mwezi wanaozalisha mazao yanayoingiza pato la pesa za kigeni na za ndani wanaopinda migongo kila siku ?
Hawa wakulima miaka 55 wanakuwa wamechoka sana wanastahili kudtaafu kilimo nao kwa nini serikali haichangii pension huko?

Wizi huo mkataba utenguliwe haraka ni wa kifisadi.Serikali na wafanyakazi wameamua kukubaliana kuibia wananchi
Kwani serikali ndio nini labda mkuu?

Kwani huyo mtumishi halipi Kodi ?

Au labda unazungumzia watumishi wa wapi ?
 
Ili uelewe vizuri, tafuta salary scale za watumishi! huyo mwenye degree uliza ana staafu akiwa na level gani ya mshahara hapo ndio utajua kuwa watumishi wa umma wanapitia magumu.

Naamini hapo utakuwa katika position nzuri sana ya ku argue basing on reality!

Haya unayoyasema ni mtazamo tu, kama motivation speakers wanavyo motivate watu without regarding reality ya kipato cha mtanzania au watumishi wa umma.

Sio rahisi mtumishi aache kulipia ada watoto, au kuhudumia familia, aanzishe project itakayo mcost lot of money wakati cash in-flow ni kiduchu, atafungwa au kufilisiwa hata hicho kidogo alichinacho.

Waulize waajiri kuhusu madeni waliyinayo, watumishi wao, ndio utajua uhalisia wa hichi tunacho jadili hapa.
Ideal ungeweka hizo evidence tujadili.

Anyway jioni njema JF nayo ukiendekeza ufanyi shughuli zingine.

Ciao 👋
 
Kwani serikali ndio nini labda mkuu?

Kwani huyo mtumishi halipi Kodi ?

Au labda unazungumzia watumishi wa wapi ?
Mfanyakazi wa Serikali sawa Analipa halafu anakuwa refunded mlango wa nyuma asilimia 15 ya kuchangiwa mifuko ya pension fund bure kabisa

Kwani walipa kodi wafanyakazi wengine mfano wa sekta binafsi ambao pia hulipa kodi serikali huwa inawalipia asilimia 15 nao kwa kuwa ni wafanyakazi walipa kodi?

Kwa nini imebagua kulipia wafanyakazi walipa kodi wa serikali tu na kuacha wafanyakazi wa sekta binafsi walipa kodi kama hao wa serikali kodi ziendazo serikalini kuwachangia nao hizo asilimia 15? Ili wawe sawa na wenzao wa serikali kufaidi kodi wanalipa? Kikokotoo kinawaibia walipa kodi wengine ili kufaidisha wafanyakazi wa serikali

Kikokotoo hiki cha sasa kijizi asilimia 15 ziondolewe kwenye kulipa mafao

Walipwe kwa asilimia 5 walizochangia tu

Kikokotoo cha sasa kijizi
 
Hiyo posts inaongelea watu wanaokaa nyumba za serikali na wanaopata marupurupu tele, halafu wanastaafu bila ya kujenga. Sasa hawa kutokujenga alaumiwe serikali pia.
suala sio kujenga au kutojenga suala ni wastaafu kupewa haki yao mtu amestaafu mpe 100% zake, iyo ishu ya kujenga umechukuliwa kama mfano lakini sio hao pekee ambao wanakutana na changamoto baada ya kustaafu hata kama amejenga kwanini umpe 30%? We mpe 100% akafanye anachojua yeye mwenyewe, izo nchi unazosema hakuna cha bure na wao wakistaafu wanakutana na kikokotoo?
 
Yaani anmtetea mtu ambae amekaa nyumba ya serikali miaka 30 bure kashindwa kujenga ndani ya muda huo. Watanzania inabidi tujifunze wengine wanavyoishi huko.

Nchi zilizoendelea ukipata benefits zifuatazo bure, kama nyumba, gari full time, mafuta, furnishing, matunzo ya nyumba. Tax man atakwambia hizo ni ‘benefits in kind’.

Nyumba itaangaliwa thamani yake ya kukodisha sokoni utalipa percentage fulani ya market rent value kama kodi, mafuta utapigiwa bei ya mwezi unayogharamiwa utalipa kama kodi, furniture za nyumba zikizidi kiwango kinachoruhusiwa excess utalipa kama kodi.

Hakuna vya bure bure huko na bado mtu anastaafu na nyumba nzuri tu kwa sababu akiwa kwenye benefits za taasisi anaokoa hela nyingi tu. Yaani Tanzania mtu anataka kumuhurumia mtu alieishi miaka 20-30 kwa benefits luluki ambazo free.

Anahitajika mtu wa kuwabadili fikra watanzania.
Kichekekesho ni pale viongozi waandaamizi kama Rais, waziri mkuu nk nao wakistaafu wanapewa nyumba, huku wakilipwa 80% ya mshahara apatao aliye madarakani kwa wakati huo!
 
Fuatilia kinachojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 15, Kikao cha 8, leo Aprili 17, 2024.


Mbunge wa Geita vijijini (CCM) Joseph Musukuma amesema Watanzania wanaliamini Bunge, na kuna vitu vimekuwa vinazungumzwa lakini havichukuliwi kwa uzito wake na kwamba Serikali na Wizara husika zikae chini kutafakari upya suala la kikokotoo kwani linawaumiza watanzania na linatengeneza taifa la wezi.

Amesema Wabunge na Serikali isiweke pamba masikioni kwani imekuwa ni ajenda inayojadiliwa kila siku, na Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Nchimbi amesisitiza suala hili lishughulikiwe.

"Nimebakiza miaka 3 na watoto wangu, natakiwa nistaafu nikajitegemee, sina nyumba nipo kwenye nyumba ya Serikali, halafu naenda kupata asilimia 30, lazima niondoke na mzigo liwalo na liwe. Kwahiyo ni vizuri tusijiwekee pamba masikioni, tuone namna ya kuwasikiliza, na kama kuna uwezekano wa kutatua hilo tatizo tulitatue" amesema Musukuma.

Huyu jamaa huwa anatumia hekima za standard 7 kwa kujua sasa tunahitaji kwenda majimboni tangu ajenda ya kikotoo imeanza namsikia bulaya tu msukuma ulikua wapi!
 
Mfanyakazi wa Serikali sawa Analipa halafu anakuwa refunded mlango wa nyuma asilimia 15 ya kuchangiwa mifuko ya pension fund bure kabisa

Kwani walipa kodi wafanyakazi wengine mfano wa sekta binafsi ambao pia hulipa kodi serikali huwa inawalipia asilimia 15 nao kwa kuwa ni wafanyakazi walipa kodi?

Kwa nini imebagua kulipia wafanyakazi walipa kodi wa serikali tu na kuacha wafanyakazi wa sekta binafsi walipa kodi kama hao wa serikali kodi ziendazo serikalini kuwachangia nao hizo asilimia 15? Ili wawe sawa na wenzao wa serikali kufaidi kodi wanalipa? Kikokotoo kinawaibia walipa kodi wengine ili kufaidisha wafanyakazi wa serikali

Kikokotoo hiki cha sasa kijizi asilimia 15 ziondolewe kwenye kulipa mafao

Walipwe kwa asilimia 5 walizochangia tu

Kikokotoo cha sasa kijizi
Kila Boss alipe watu wake ? Na huko sekta binafsi ni wafanyakazi gani hao wanaolipa Kodi ?


Kama unazungumzia wafanyakazi wenye taaluma zao huko sekta binafsi sawa , lakini kaangalie madaraja ya mishahara Yao alafu ulinganishe na mishahara ya watumishi wa umma.?
 
Mfanyakazi wa Serikali sawa Analipa halafu anakuwa refunded mlango wa nyuma asilimia 15 ya kuchangiwa mifuko ya pension fund bure kabisa

Kwani walipa kodi wafanyakazi wengine mfano wa sekta binafsi ambao pia hulipa kodi serikali huwa inawalipia asilimia 15 nao kwa kuwa ni wafanyakazi walipa kodi?

Kwa nini imebagua kulipia wafanyakazi walipa kodi wa serikali tu na kuacha wafanyakazi wa sekta binafsi walipa kodi kama hao wa serikali kodi ziendazo serikalini kuwachangia nao hizo asilimia 15? Ili wawe sawa na wenzao wa serikali kufaidi kodi wanalipa? Kikokotoo kinawaibia walipa kodi wengine ili kufaidisha wafanyakazi wa serikali

Kikokotoo hiki cha sasa kijizi asilimia 15 ziondolewe kwenye kulipa mafao

Walipwe kwa asilimia 5 walizochangia tu

Kikokotoo cha sasa kijizi
Mfano Engineer mwenye shahada sekta binafsi wanakunja mpaka 2M - 4M ukijumlisha na posho wakati Engineer aliyeajiriwa serikalini mwenye shahada hio 2+M labda aibe.

Cha msingi kila Boss alipe watu wake.

Hizo swagger za asilimia 15 ziondolewe, huo ni uvunjifu wa amani.
 
HIli linaumiza sana. Wazee wengine wakifikia kustaafu wakikutana na kikokotoo, huishia kuumwa kiharusi na kisukari.
Hawachukui muda mrefu wanakufa.
.Labda ndio mpango uliopo wa kuwaondoa wazee hawa kwa magojwa ya moyo, kupooza na kisukari?
Hili si sawa kabisa.
Wafanyakazi wengi wa serikali hawaelewi financial planning na ndiyo maana wanalaumu kikokotoo. Na huu mkanganyiko unatokana na kutokutolewa elimu ya fedha na uwekezaji awali kabisa kwenye maisha ya watumishi. Kinachotokea ni kuwa watumishi wengi wanadhani wakipata hiyo hela zote eti maisha yao yatakuwa bora hapana kabisa tena wengi wataishia kufa na kupotea kabisa.

Mfano mtu anayepata mashahara wa makadirio ya mil 1.2, mkupuo tuseme ni mil 90, kikokotoo atapata mfano mil 30, akiwekeza anapata kama laki 2.6, na ile ya mwezi kama laki 6, ukijumlisha ni kama laki nane ila angepata yote mil 90 akiwekeza atapata laki 7, na mara zote mtumishi hawezi wekeza zaidi ya kufanya miradi isiyolipa. Nadhani serikali ijikite kutoa elimu zaidi kwa watumishi
 
wabunge hawataki kukubali kwa sababu wao ndo wanaoongoza kukopa kwenye hayo mashirika i.e NSSF, wastaafu wakipewa yote watakopa wapi? ndio mentality yao
 
We
Kiongozi embu tuwe wa kweli

Mtu anaishi nyumba ya serikali rent mtaani nyumba anayoishi tena sio prime area labda laki 5-7 kwa mwezi. Ndani ya mwaka anaokoa million sita mpaka nane. Mafuta gari ya kazini kwa mwezi labda matumizi yake binafsi ni łąki mbili mpaka tatu, anaokoa millioni mbili mpaka tatu ukijumlisha ndani ya mwaka, mshahara million tatu plus kwa mwezi.

Kwa mwaka anaokoa kama 8-10 million kwenye mshahara wake. Halafu unakuta mtu private na mshahara wa millioni nne au tano kabla ya 40 years ana nyumba yake bila hizo ‘benefits-in-kind’ za watumishi na wenyewe wana ndugu hao hao wakuwasaidia na kusomesha.

Ifike wakati watu waambizane ukweli, uwezi kufanya kazi zaidi ya miaka 20 serikalini huku ukipokea benefits zote hizo usiwe na nyumba hata kama hukua mpiga deal.
Inashangaza yaani unazungumza alinacha! Kama hujui jambo ni bora kukaa kimya kuliko kutunga hadithi ambazo huzijui. Andiko lako kwanza linaonyesha huna idea ya viwango vya mishahara serikalini watumishi wanavyolipwa ila na wewe kwa saba umetaka uonekane umechangia basi unaropokaropoka.

Nafasi za kazi serikalini mbona zinatangazwa mara kwa mara kama huna sifa sio sababu ya kuwachukia watumishi hawajakuzuia kuajiriwa .
 
Wafanyakazi wengi wa serikali hawaelewi financial planning na ndiyo maana wanalaumu kikokotoo. Na huu mkanganyiko unatokana na kutokutolewa elimu ya fedha na uwekezaji awali kabisa kwenye maisha ya watumishi. Kinachotokea ni kuwa watumishi wengi wanadhani wakipata hiyo hela zote eti maisha yao yatakuwa bora hapana kabisa tena wengi wataishia kufa na kupotea kabisa. Mfano mtu anayepata mashahara wa makadirio ya mil 1.2, mkupuo tuseme ni mil 90, kikokotoo atapata mfano mil 30, akiwekeza anapata kama laki 2.6, na ile ya mwezi kama laki 6, ukijumlisha ni kama laki nane ila angepata yote mil 90 akiwekeza atapata laki 7, na mara zote mtumishi hawezi wekeza zaidi ya kufanya miradi isiyolipa. Nadhani serikali ijikite kutoa elimu zaidi kwa watumishi
Kama ni hivyo kwa nini kuna double standard.? Mawazir na wabunge watumie Kikokotoo hicho hicho kama ni kizuri
 
Yaani unaongea upuuzi


Mtu analipwa pesa laki 3 Hadi 6 anastaafu


Unadhani anafanya jambo gani la maana?

Pesa wanayolipwa watumishi wengi ni ya kujaza tumbo ili wapate nguvu maana hata kula haitoshi.


Halafu hizo pesa ni zao, acha upumbavu wa kumpangia mtu namna ya kutumia pesa zake
 
Msiwafanye wananchi wajinga nyie wafanyakazi wa serikali

Wananchi inabidi tuingie mitaani kupinga asilimia 15 serikali iliyowachangia michango ya pension kila mwezi kutokana na kodi zetu iondolewe kwenye kikokotoo h8cho kioya haraka

Haiwezekani mnalipwa mishahara wengine hata ajira hawana mnachangia mifuko ya pension asilimia 5 tu halafu serikali inakamua tena walipa kodi inawachangia asilimia 15 kila mwezi mifuko ya pension Huo ni wizi .Hizo asilimia 15 kama zimo humo.kwenye kikotoo zitolewe zirudi hazina zipelekwe kwa vijana wasio na ajira wakajiajiri nyie chukueni pension asilimia tano tu mlizochangia

Kodi zetu hizo asilimia 15 tunazitaka wananchi ..Mnalipwa mara mbili nyie wafanyakazu wa serikali kwanza mnalipwa mishahara halafu tena mnalipiwa asilimia 15 ya michango ya pension .Hilo haliko sawa .Hizo asilimia 15 ziende kwenye mfuko wa kusaidia wasio na ajira wakiwa naxo nao watachangia asimia tano

Nyie wafanyakazi wa serikali na wabunge ndio mnaokula sana keki ya nchi.Wafanyakazi tunataka asilimia 15 hiyo irudi hazina msiichukue chukueni asilimia tano yenu hiyo ndio haki yenu

Kikokoto kipya kitoe hizo asilimia 15 mtakapolipwa sio zenu hizo zenu asilimia 5 ndio zenu

Kikokotoo cha sasa kijizi kinaibia kodi za wananchi asilimia 15 wanazochangiwa na serikali mifuko ya pension .Hiyo asilimia 15 iondolewe kwenye kikokotoo
Unajua kama hao wafanyakazi wanakatwa Kodi Kila mwezi?


Yaani mtu umemuajiri, umamlipa pesa kiduchu Kisha unamlipisha kodi


Halafu kuna bumunda anakuja kuongea ujinga
 
W
Kiongozi embu tuwe wa kweli

Mtu anaishi nyumba ya serikali rent mtaani nyumba anayoishi tena sio prime area labda laki 5-7 kwa mwezi. Ndani ya mwaka anaokoa million sita mpaka nane. Mafuta gari ya kazini kwa mwezi labda matumizi yake binafsi ni łąki mbili mpaka tatu, anaokoa millioni mbili mpaka tatu ukijumlisha ndani ya mwaka, mshahara million tatu plus kwa mwezi.

Kwa mwaka anaokoa kama 8-10 million kwenye mshahara wake. Halafu unakuta mtu private na mshahara wa millioni nne au tano kabla ya 40 years ana nyumba yake bila hizo ‘benefits-in-kind’ za watumishi na wenyewe wana ndugu hao hao wakuwasaidia na kusomesha.

Ifike wakati watu waambizane ukweli, uwezi kufanya kazi zaidi ya miaka 20 serikalini huku ukipokea benefits zote hizo usiwe na nyumba hata kama hukua mpiga deal.
Wewe bumunda unajua mishahara ya serikali au ili uongee?

Kuna watu wakikusanya take home mwaka mzima wanapata milioni 4 hadi 6. Wewe unakuja kuongelea habari ya milioni kadhaa kwa mwezi.

Mkae kimya kama hamjui.
 
Back
Top Bottom