Joseph Musukuma: Kikokotoo kinawaumiza wananchi, tunatengeneza taifa la wezi

Joseph Musukuma: Kikokotoo kinawaumiza wananchi, tunatengeneza taifa la wezi

Kiongozi embu tuwe wa kweli

Mtu anaishi nyumba ya serikali rent mtaani nyumba anayoishi tena sio prime area labda laki 5-7 kwa mwezi. Ndani ya mwaka anaokoa million sita mpaka nane. Mafuta gari ya kazini kwa mwezi labda matumizi yake binafsi ni łąki mbili mpaka tatu, anaokoa millioni mbili mpaka tatu ukijumlisha ndani ya mwaka, mshahara million tatu plus kwa mwezi.

Kwa mwaka anaokoa kama 8-10 million kwenye mshahara wake. Halafu unakuta mtu private na mshahara wa millioni nne au tano kabla ya 40 years ana nyumba yake bila hizo ‘benefits-in-kind’ za watumishi na wenyewe wana ndugu hao hao wakuwasaidia na kusomesha.

Ifike wakati watu waambizane ukweli, uwezi kufanya kazi zaidi ya miaka 20 serikalini huku ukipokea benefits zote hizo usiwe na nyumba hata kama hukua mpiga deal.
Hizi ndio shida za kuwapa dhamana watu wasiojua wanaowaongoza. Eti unasave laki 5 Hadi 7 kwa mwezi. Unajua mshahara wa daktari, nesi, mfamasia, walimu?

Nyumba ya laki 6 wakati wengine hawapati hata take home ya laki 6.
 
Aijalishi unafanya shughuli gani jukumu la ‘personal finance’ ni lako. Kila mtu kwa situation yake anatakiwa kupanga goals za mbeleni especially watu walioelimika kama waajiriwa wa serikalini.

Hawa watu wanakuwa na advantages nyingi during their working life isipokuwa they make poor financial decisions or live reckless lives wakitegemea pension kama mwokozi ndio maana wanataka rules zao kwenye malipo badala ya kujipanga mapema.

Pension inatakiwa ikusaidie usipate tabu wakati wa kustaafu hiyo withdrawal ya 33% ndio muda wa kwenda mbugani au hata kwenda Kenya na mkewe/mume mtu anawaza kujengea au kuanzishia biashara.
Inaonekana wewe ni mnufaika wa kikokotoo. Haiwezekani pesa ya mtu ikuume kupewa yote.

Yaani una roho mbaya zaidi ya mchawi.
 
Yaani anmtetea mtu ambae amekaa nyumba ya serikali miaka 30 bure kashindwa kujenga ndani ya muda huo. Watanzania inabidi tujifunze wengine wanavyoishi huko.

Nchi zilizoendelea ukipata benefits zifuatazo bure, kama nyumba, gari full time, mafuta, furnishing, matunzo ya nyumba. Tax man atakwambia hizo ni ‘benefits in kind’.

Nyumba itaangaliwa thamani yake ya kukodisha sokoni utalipa percentage fulani ya market rent value kama kodi, mafuta utapigiwa bei ya mwezi unayogharamiwa utalipa kama kodi, furniture za nyumba zikizidi kiwango kinachoruhusiwa excess utalipa kama kodi.

Hakuna vya bure bure huko na bado mtu anastaafu na nyumba nzuri tu kwa sababu akiwa kwenye benefits za taasisi anaokoa hela nyingi tu. Yaani Tanzania mtu anataka kumuhurumia mtu alieishi miaka 20-30 kwa benefits luluki ambazo free.

Anahitajika mtu wa kuwabadili fikra watanzania.
Vya bure kivipi wakati ni hela yake?
 
Katibu Mkuu wa CCM Dr. Nchimbi kalisemea vizuri sana hili la kikokotoo, kuwa ni kilio kikubwa cha watumishi wote, hivyo atalibeba na kulipeleka kwa Mh. Rais wetu Mama Samia, na Mama yetu alivyomsikivu na uhakika atarudisha kama zamani kikokotoo cha PSPF..!!
 
Wafanyakazi wanalipwa kwa kodi za wananchi

Wapi wananchi walishirikishwa huo mkataba?

Huo wizi kabisa ni mkataba wa kifisadi wa kuiba pesa za walipa kodi.Haiwezekani mtu alipwe mshahara halafu umwambie nitakulipia pia Pension asilimia 15 wewe utachanga asilimia tano tu.Huo mkataba ni wa kifisadi kati ya serikali na wafanyakazi wake ufutwe upesi na kwenye kikokotoo hiki kipyac iondolewe hiyo asilimia 15.Walipwe kwa hizo asilimia 5 zao tu walizochangia

Kama serikali imeamua kulipia pension wananchi wake kwanini ibague wananchi mbona serikali haiwalipii pension hata asilimia moja tu kila mwezi wanaozalisha mazao yanayoingiza pato la pesa za kigeni na za ndani wanaopinda migongo kila siku ?
Hawa wakulima miaka 55 wanakuwa wamechoka sana wanastahili kudtaafu kilimo nao kwa nini serikali haichangii pension huko?

Wizi huo mkataba utenguliwe haraka ni wa kifisadi.Serikali na wafanyakazi wameamua kukubaliana kuibia wananchi
Mbunge anavuta 250M unaona kawaida?

Mke wa Rais mstaafu analipwa unaona kawaida? Rais mstaafu analipwa 70% na kujengewa nyumba.

Halafu unaongea upuuzi hapa. Halafu hizo hela ni za wafanyakazi, kinachofanyika hapo ni kubadili jina tu.

Ni sawa simu ya 700,000 ukaambiwa inauzwa laki 800,000 na vocha ya 100,000 BURE

Hizo ni kanuni tu za kuonekana serikali unafanya kitu kumbe hamna kitu kipya.
 
Fuatilia kinachojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 15, Kikao cha 8, leo Aprili 17, 2024.


Mbunge wa Geita vijijini (CCM) Joseph Musukuma amesema Watanzania wanaliamini Bunge, na kuna vitu vimekuwa vinazungumzwa lakini havichukuliwi kwa uzito wake na kwamba Serikali na Wizara husika zikae chini kutafakari upya suala la kikokotoo kwani linawaumiza watanzania na linatengeneza taifa la wezi.

Amesema Wabunge na Serikali isiweke pamba masikioni kwani imekuwa ni ajenda inayojadiliwa kila siku, na Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Nchimbi amesisitiza suala hili lishughulikiwe.

"Nimebakiza miaka 3 na watoto wangu, natakiwa nistaafu nikajitegemee, sina nyumba nipo kwenye nyumba ya Serikali, halafu naenda kupata asilimia 30, lazima niondoke na mzigo liwalo na liwe. Kwahiyo ni vizuri tusijiwekee pamba masikioni, tuone namna ya kuwasikiliza, na kama kuna uwezekano wa kutatua hilo tatizo tulitatue" amesema Musukuma.

HAKUNA WATU WANAFIKI KM CCM NA WABUNGE WAKE, MAANA HAWA HAWA NDO WALIPITISHA KIKOKOTOO KWA BWEMBWE NA KEJELI WAMEONA UCJAGUZI UMEKARIBIA WANAANZS SARAKASI
 
Msiwafanye wananchi wajinga nyie wafanyakazi wa serikali

Wananchi inabidi tuingie mitaani kupinga asilimia 15 serikali iliyowachangia michango ya pension kila mwezi kutokana na kodi zetu iondolewe kwenye kikokotoo h8cho kioya haraka

Haiwezekani mnalipwa mishahara wengine hata ajira hawana mnachangia mifuko ya pension asilimia 5 tu halafu serikali inakamua tena walipa kodi inawachangia asilimia 15 kila mwezi mifuko ya pension Huo ni wizi .Hizo asilimia 15 kama zimo humo.kwenye kikotoo zitolewe zirudi hazina zipelekwe kwa vijana wasio na ajira wakajiajiri nyie chukueni pension asilimia tano tu mlizochangia

Kodi zetu hizo asilimia 15 tunazitaka wananchi ..Mnalipwa mara mbili nyie wafanyakazu wa serikali kwanza mnalipwa mishahara halafu tena mnalipiwa asilimia 15 ya michango ya pension .Hilo haliko sawa .Hizo asilimia 15 ziende kwenye mfuko wa kusaidia wasio na ajira wakiwa naxo nao watachangia asimia tano

Nyie wafanyakazi wa serikali na wabunge ndio mnaokula sana keki ya nchi.Wafanyakazi tunataka asilimia 15 hiyo irudi hazina msiichukue chukueni asilimia tano yenu hiyo ndio haki yenu

Kikokoto kipya kitoe hizo asilimia 15 mtakapolipwa sio zenu hizo zenu asilimia 5 ndio zenu

Kikokotoo cha sasa kijizi kinaibia kodi za wananchi asilimia 15 wanazochangiwa na serikali mifuko ya pension .Hiyo asilimia 15 iondolewe kwenye kikokotoo

Hujui maana ya haki za watumishi, sio Tz tu hata duniani kote hujui maana ya haki zao, ni sheria hiyo dunia nzima, sbb wewe huna ajira ndio unataka watu wasilipwe mchango wa mwajiri? Kisa huna ajira unataka watumishi wasichangiwe na mwajiri? Akili huna hata nukta, unajua maana ya uwizi? Sheria za haki za watumishi unazijua? Nosense
 
Wafanyakazi wengi wa serikali hawaelewi financial planning na ndiyo maana wanalaumu kikokotoo. Na huu mkanganyiko unatokana na kutokutolewa elimu ya fedha na uwekezaji awali kabisa kwenye maisha ya watumishi. Kinachotokea ni kuwa watumishi wengi wanadhani wakipata hiyo hela zote eti maisha yao yatakuwa bora hapana kabisa tena wengi wataishia kufa na kupotea kabisa. Mfano mtu anayepata mashahara wa makadirio ya mil 1.2, mkupuo tuseme ni mil 90, kikokotoo atapata mfano mil 30, akiwekeza anapata kama laki 2.6, na ile ya mwezi kama laki 6, ukijumlisha ni kama laki nane ila angepata yote mil 90 akiwekeza atapata laki 7, na mara zote mtumishi hawezi wekeza zaidi ya kufanya miradi isiyolipa. Nadhani serikali ijikite kutoa elimu zaidi kwa watumishi
Tapeli mwengine.

Inaonekana upo mbali na biashara ndio maana unaanza kupiga hesabu za kwenye makaratasi.
 
You are stupid, hujui maana ya haki za watumishi, sio Tz tu hata duniani kote hujui maana ya haki zao, ni sheria hiyo dunia nzima, sbb wewe huna ajira ndio unataka watu wasilipwe mchango wa mwajiri? Wewe pumbaf mkubwa, kisa huna ajira unataka watumishi wasichangiwe na mwajiri? Akili huna hata nukta, unajua maana ya uwizi? Sheria za haki za watumishi unazijua? Nosense
Kifupi wafanyakazi wa serikali mumewaasha wananchi kupinga hiki kikokotoo kipya cha nyie hiki cha kulipwa ikiwemo asilimia 15 mnachangiwe na serikali you will be loosers timu za nawakili zimeshaanza kujipanga kuiburuza serikali mahakamani kwa niaba ya wananchi kupinga serikali kulipa wastaafu kwa kikokotoo kipya kama malipo yatahusisha na asilimia 15 ya serikali imechangia itakuwemo kwenye kikokotoo

Kuwa asiwepo wa kulipwa ikihusika hiyo asilimia hadi kesi ya msingi iamuliwe

Nyie wafanyakazi wa serikali ndio mliolianzisha mjiandae kulinywa kama lilivyo

Wajinga nyie serikali inawapendelea bado mnajitia ujuaji .Mtaliipwa asilimia 5 tu za mafao yenu ya mlichochangia kinachobaki subirini maamuzi ya mahakama
 
Hizi ndio shida za kuwapa dhamana watu wasiojua wanaowaongoza


Eti unasave laki 5 Hadi 7 kwa mwezi

Unajua mshahara wa daktari, nesi, mfamasia, walimu?


Nyumba ya laki 6 wakati wengine hawapati hata take home ya laki 6
Main post ya mada imeelezea msukuma kasema nini ndio kinachojibiwa. Sasa wewe unakurupuka tu, unasoma posts za watu with bias reading ukiona statement zisizokufurahisha unatoa povu.

Savings zinazoongelewa ni kwa watu wanaokaa rent free nyumba za serikali. Wewe unaniletea mambo ambayo mimi sijasema kabisa.
 
suala sio kujenga au kutojenga suala ni wastaafu kupewa haki yao mtu amestaafu mpe 100% zake, iyo ishu ya kujenga umechukuliwa kama mfano lakini sio hao pekee ambao wanakutana na changamoto baada ya kustaafu hata kama amejenga kwanini umpe 30%? We mpe 100% akafanye anachojua yeye mwenyewe, izo nchi unazosema hakuna cha bure na wao wakistaafu wanakutana na kikokotoo?
Hiyo hela inabidi izungushwe, binafsi sioni shida kwenye hiyo 33%.

Ningewaelewa watumishi wangekuwa wanalalamikia ‘replacement rate’ ya 1/580 ni ndogo mno. Hiyo rate airudishi hata 20% ya mchango wa mwezi malipo ya wastaafu ni kama 10.3% (kabla ya withdrawal) kwa mwezi kwa mtu aliefanya kazi miaka 30, inaendeshwa hovyo sana hiyo mifuko.

Replacement rate inatakiwa kuwa walau between 1 of 100 to 200 kwenye calculations, tena for life. Hiyo mifuko itakuwa na hali mbaya sana.
 
Kama ni hivyo kwa nini kuna double standard.? Mawazir na wabunge watumie Kikokotoo hicho hicho kama ni kizuri
Mawaziri wengi wakistaafu au hao wabunge wanakuwa masikini sana, sababu ni poor financial planning. Amini nakuambia elimu ya uwekezaji na fedha ya wachaga na wakinga ni muhimu sana kila mtanzania aipate. Bila elimu hata kama serikali itatoa hela yote ya kustaafu hakuna unafuu utakaopatikana kwa mtumishi zaidi ya kusababisha msongo zaidi wa mawazo na kuwafanya wafe mapema. Nasisitiza serikali isikurupuke kabisa iendeshe elimu ya fedha na financial planning in masses.
 
Serikali sijui kwanini haisikilizi wananchi ,kama hadi wabunge wa CCM wanaona kikokotoo kibaya kwanini bado tu wanaendelea kukitumia? Kodi 30% mmelamba na bado mnaichukua 20% yake huu si WIZI?
 
Kifupi wafanyakazi wa serikali mumewaasha wananchi kupinga hiki kikokotoo kipya cha nyie hiki cha kulipwa ikiwemo asilimia 15 mnachangiwe na serikali you will be loosers timu za nawakili zimeshaanza kujipanga kuiburuza serikali mahakamani kwa niaba ya wananchi kupinga serikali kulipa wastaafu kwa kikokotoo kipya kama malipo yatahusisha na asilimia 15 ya serikali imechangia itakuwemo kwenye kikokotoo

Kuwa asiwepo wa kulipwa ikihusika hiyo asilimia hadi kesi ya msingi iamuliwe

Nyie wafanyakazi wa serikali ndio mliolianzisha mjiandae kulinywa kama lilivyo

Wajinga nyie serikali inawapendelea bado mnajitia ujuaji .Mtaliipwa asilimia 5 tu za mafao yenu ya mlichochangia kinachobaki subirini maamuzi ya mahakama
KUTOKA 22:18

Mithali 26:4-5
 
Hiyo hela inabidi izungushwe, binafsi sioni shida kwenye hiyo 33%.
Basi na hao wapitisha sheria(wabunge) na wao kwenye mafao yao kama yale ya kiinua mgongo baada ya miaka mitano ya ubunge wachukue 30% inayobaki izungushwe, hapa ndipo unaona hakuna usawa, mtu kamaliza muda wake mpe 100% zake akajambe mbele
Ningewaelewa watumishi wangekuwa wanalalamikia ‘replacement rate’ ya 1/580 ni ndogo mno. Hiyo rate airudishi hata 20% ya mchango wa mwezi malipo ya wastaafu ni kama 10.3% (kabla ya withdrawal) kwa mwezi kwa mtu aliefanya kazi miaka 30 inaendeshwa hovyo sana hiyo mifuko.

Replacement rate inatakiwa kuwa walau between 1 of 100 to 200 kwenye calculations, tena for life. Hiyo mifuko itakuwa na hali mbaya sana.
Hapa nakubaliana na wewe
 
Back
Top Bottom