Mtoa mada kama mwishoni ameshauri watu 'wasizushe' lakini amesahau kwamba kulikuwa kuna 'ombwe' la taarifa sahihi kwa sababu yeye muhusika hakuaga rasmi hatokuwa jukwaani kwa muda fulani
Jukwaa (Jamii) ina haki kufikiria vyovyote kama muhusika hakusema sababu ya kutokuwa 'active' na pia ukizingatia nafasi ya muhusika jukwaani
Na kwa upande mwingine inaonyesha tunaishi katika 'hofu' kama jamii ndo maana kuna hizo issue za kutekana ziliibuka hapa kuna kitu hakipo sawa
Pia ni dalili ya watu ambao tupo 'hasi' katika namna zetu za kufikiri tunawaza mabaya muda mwingi hasa kwa wenzi wetu
Lakini pia kulikuwa na some jokes tu