johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 97,869
- 171,716
Mbunge mstaafu wa Chadema Dkt. Joshua Nassari ameomba radhi rasmi kwa Rais Magufuli kufuatia mambo maovu aliyomfanyia kabla hajahamia CCM.
Nassari ambaye alikuwa akiongea kimasai amewaomba radhi wanaccm na wana Arusha wote kwa machukizo aliyowasababishia akiwa CHADEMA.
Nassari amewataka malaigwanan na wamasai wote na wananchi kwa ujumla kumpigia kura Dkt. Magufuli.
"Ninamshukuru sana kijana Nassari ni kijana anayejitambua, ebu mpe 'Mic' asalimu hapa na aombe kura kwa ajili ya wabunge wengine, huyu anajitambua alijua alikuwa amekosea na mimi Nassari nakuambia nitakupa kazi, ebu omba kura kwa ajili ya waheshimiwa hawa", amesema Dkt Magufuli.
Kwa upande wake Joshua Nassari akatumia nafasi hiyo kumuomba msamaha Dkt Magufuli, "Mh. Rais mtu anayeomba radhi ni anayefahamu tendo la ujasiri na mimi naomba leo niuvae ujasiri nije mbele yako na wana Meru kama kuna mahali nimewahi kukosea ninakuomba unisamehe, ninaomba radhi kwa niaba ya watu wa Meru, mwaka 2015 katika uwanja huu niliwaomba watu hawa wapeleke kura mahali pengine".
Maendeleo hayana vyama!
====
Aliyekuwa Mbunge wa Arumeru Mashariki kupitia CHADEMA, Joshua Nassari ameomba kwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli kwa kuwa upinzani
Nassari alihamia CCM akitokea CHADEMA mwezi Julai 2020, miezi kadhaa baada ya kuvuliwa ubunge kutokana na kutohudhuria vikao vitatu vya bunge
Nassari amesema mambo mengi waliyokuwa wakiyasema alipokuwa upinzani yametekelezwa na Dkt. Magufuli katika muhula wa kwanza wa uongozi wake.
Nassari ambaye alikuwa akiongea kimasai amewaomba radhi wanaccm na wana Arusha wote kwa machukizo aliyowasababishia akiwa CHADEMA.
Nassari amewataka malaigwanan na wamasai wote na wananchi kwa ujumla kumpigia kura Dkt. Magufuli.
"Ninamshukuru sana kijana Nassari ni kijana anayejitambua, ebu mpe 'Mic' asalimu hapa na aombe kura kwa ajili ya wabunge wengine, huyu anajitambua alijua alikuwa amekosea na mimi Nassari nakuambia nitakupa kazi, ebu omba kura kwa ajili ya waheshimiwa hawa", amesema Dkt Magufuli.
Kwa upande wake Joshua Nassari akatumia nafasi hiyo kumuomba msamaha Dkt Magufuli, "Mh. Rais mtu anayeomba radhi ni anayefahamu tendo la ujasiri na mimi naomba leo niuvae ujasiri nije mbele yako na wana Meru kama kuna mahali nimewahi kukosea ninakuomba unisamehe, ninaomba radhi kwa niaba ya watu wa Meru, mwaka 2015 katika uwanja huu niliwaomba watu hawa wapeleke kura mahali pengine".
Maendeleo hayana vyama!
====
Aliyekuwa Mbunge wa Arumeru Mashariki kupitia CHADEMA, Joshua Nassari ameomba kwa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli kwa kuwa upinzani
Nassari alihamia CCM akitokea CHADEMA mwezi Julai 2020, miezi kadhaa baada ya kuvuliwa ubunge kutokana na kutohudhuria vikao vitatu vya bunge
Nassari amesema mambo mengi waliyokuwa wakiyasema alipokuwa upinzani yametekelezwa na Dkt. Magufuli katika muhula wa kwanza wa uongozi wake.