JUBILEE protests IEBC's move on spoilt votes

JUBILEE protests IEBC's move on spoilt votes

Sasa kwa nini jubilee walalamije?wanaogopa nini?kama tume ya uchaguzi imeamuo wao kwa nini waogope?kama sio kujiamini ni nini.
 
Butola hao 377000 walikuwa wapiga kura? Kama jibu ni ndiyo kama hawakuona mgombea anayefaa unataka kura yake isihesabiwe?

...Sina tatizo na hilo, tatizo langu ni uwezekano wa mgombea yeyote kutopata 50%+1 ata kwenye uchaguzi wa marudio, sasa je uchaguzi utarudiwa mara ngapi?

...hapa ndipo ilipo hekima ya kuchukua tu "Jumla ya Idadi ya Kura Halali", ukizichukua tu "kura halali" basi ni lazima round ya pili itatoa mshindi, lakini bila hivyo, mtarudia uchaguzi mara ngapi?hapa ndipo palipo na tatizo...
 
swali la kizushi:
Tuseme zimepigwa 100,kura 20 zikaenda kwa Raila,kura 25 zikaenda kwa Uhuru na kura 55 zikaharibika,hivi Uhuru atatangazwa kuwa ni Rais wa Kenya?

...Ebu tuangalie pia kwa muktadha huu, kama ukiziweka "kura zilizoharibika" kama factor, na "kura Zilizoharibika" zikashinda kama hapo 55/95, zaidi ya 50%+1, sasa je kwenye uchaguzi utakaofuata wa marudio(kwa sababu hakuna kati yao aliyepata 50%+1), je watarudiana tena hao hao Kenyatta na Odinga?na je mtaurudia mpambano huo mara ngapi ndio tuseme sasa hapa basi, haturudii tena?...
 
Sasa kwa nini jubilee walalamije?wanaogopa nini?kama tume ya uchaguzi imeamuo wao kwa nini waogope?kama sio kujiamini ni nini.

...Kwa sababu wanaamini kuwa katiba iliposema 50%+1 of All Votes ilimaanisha 50%+1 ya "Kura Halali", na tayari kigezo hicho wanaamini wamekifikia...

...By the way, tume mpaka sasa ndivyo ilivyodefine, so ndivyo nao walivyokuwa wanaamini...
 
Kuna maneno haya ya Ruto “Jubilee Coalition is concerned over the sudden change of rules by IEBC which to us is meant to deny us a first round win,” halafu kuna taarifa hii "IEBC Chairman Ahmed Issack Hassan last evening announced that the percentages would now be worked out using total votes cast (including rejected and disputed votes)."

Hapa kunahitajika explanation of NOW. Je, unamaanisha mwanzoni kulikuwa na makubaliano mengine kama jinsi Ruto alivyoashiria?
 
Butola wewe unang'angania "simple majority" ambayo ni sheria ya Tanzania wao sheria ya 50% + 1. Sijui kwa nini unaogopga wale 377,000 kwamba uchaguzi ukirudiwa wataendelea kuharibu kura? Na zile za Keneth na wenzake si zitaongeza kura za mshindi?
 
Last edited by a moderator:
Butola Agatany8I IEBC wako sahihi kimahesabu. Watu wa HGL mnaweza msielewe; Ili mgombea atangazwe mshindi wa uraisi anatakiwa kupa zaidi ya 50% ya kura zilizopigwa na majimbo 24 kati ya majimbo 47. "Variable" hapa ni kura zilizopigwa na idadi ya majimbo mgombea aliyoshinda (kukubalika kitaifa).

Kura zilizopigwa (X) = kura walizopata wagombea wote + kura zilizoharibika.

Ili mgombea "A" atangazwe mshindi kura alizopata A/X lazima ziwe zaidi ya 50%.

Wakifanya kama Jubilee Coalition wanavyotaka maana yake hata kama wagombea wote wangekataliwa na wapiga kura (kura za maruhani) bado tume ingetangaza mshindi kati ya wale waliopigiwa kura

Huu tunaita ufafanuzi ulioenda shule, ila kama alikimbia Mathematics hapo kwenye A/X patamkimbiza vibaya, ila hakika umeeleweka vema nadhani hata yeye na hao Jubilee wakisoma hawatauliza tena.
 
...Kwa sababu wanaamini kuwa katiba iliposema 50%+1 of All Votes ilimaanisha 50%+1 ya "Kura Halali", na tayari kigezo hicho wanaamini wamekifikia...

...By the way, tume mpaka sasa ndivyo ilivyodefine, so ndivyo nao walivyokuwa wanaamini...
Butola define "All votes"
 
Last edited by a moderator:
226451_10200730299200318_1537057947_n.jpg

How did you get this copy?????
 
By Vitalis Kimutai and Peter Opiyo

Nairobi, Kenya: The Jubilee Coalition has contested the move by the electoral commission to include spoilt votes in calculating the presidential tally.

They objected the decision to count invalid votes along with the valid ones as part of the overall tally that would define whether any candidate has secured the 50 per cent plus one constitutional threshold.

Jubilee blamed foreign missions for allegedly influencing the Independent Electoral and Boundaries Commission (IEBC) to take that position in tabulating the figures which it claimed was meant to deny the coalition a win in the first round of the contest.

IEBC had earlier stated the Constitution envisages the inclusion of all votes cast in calculating the percentage of the presidential tally.

According to the Constitution, a presidential candidate must garner 50 per cent plus one vote of all votes cast to be declared the winner.

Jubilee running mate William Ruto addressed the media at Bomas last night, but also appealed to Kenyans to remain calm as they take up the matter with the IEBC.

"We are aware some foreign missions have taken a position on this matter and have been canvassing to have IEBC include the spoilt votes in calculating the per centage," Ruto said.

He added: "Jubilee Coalition is concerned over the sudden change of rules by IEBC which to us is meant to deny us a first round win," he said.

Ruto said they would move to court to challenge IEBC on the matter if it becomes necessary.

Standard Digital Mobile - Kenya :: Jubilee protests IEBC's move on spoilt votes

A standoff erupted over the exclusion of rejected and disputed votes in the Independent Electoral and Boundaries Commission's calculations of the percentages held by the candidates. IEBC has been displaying the percentage for valid votes only. However, CORD pointed out the Constitution sets the threshold for victory at 50 per cent plus one vote for "all votes cast".

IEBC Chairman Ahmed Issack Hassan last evening announced that the percentages would now be worked out using total votes cast (including rejected and disputed votes). This immediately sparked a protest from the Jubilee alliance, whose officials say he was misinterpreting the law.

Standard Digital Mobile - Kenya :: Uhuru leads in provisional results


My Take:
Nakubaliana na Jubillee, "Kura Zilizoharibika ni Kama Mgombea wa Maruhani", kuzijumlisha kura hizi kwenye kutafuta percentage ya kura za wagombea kutasababisha ata kwenye uchaguzi wa marudio, wa washindi wawili wa juu, uwepo uwezakano pia wa kutopatikana mshindi, kwa sababu japo tutawaona Uhuru na Odinga, lakini kutakuwa pia na mgombea, "Kura Zilizoharibika"..

Ikumbukwe kuwa katika matokeo ya mpaka sasa, mgombea huyu "Kura Zilizoharibika", amekamata nafasi ya tatu nyuma ya Uhuru na Odinga.

Jubelee iko mbele hata marudio yakura,,,,kwani kama hawakupendi,,sioni
vile watakavyo kupenda,,,,,,,,,,,,,,, baadae,,hata wazungu na UN,,CNN,,
AlJazeera,,,,,,,,, wakikupa msaada,,,,,,,,,wowote.

Marudio ni stress tupu,,,,lakini,,,,wembe ni ule ule.

Watu ambao wange swing votes,,,,kama Musalia Mudavadi,,,hehehe:A S shade:,,,
wameshindwa kunguruma hata katika ngome zao.


Wwwwwoyiyoyoyo,,,ako wapi Eugene Wamalwa????????????

Kolonzo Musyoka,,,,,wewewewe,,,,ni kuvio.
 
Butola Agatany8I IEBC wako sahihi kimahesabu. Watu wa HGL mnaweza msielewe; Ili mgombea atangazwe mshindi wa uraisi anatakiwa kupa zaidi ya 50% ya kura zilizopigwa na majimbo 24 kati ya majimbo 47. "Variable" hapa ni kura zilizopigwa na idadi ya majimbo mgombea aliyoshinda (kukubalika kitaifa).

Kura zilizopigwa (X) = kura walizopata wagombea wote + kura zilizoharibika.

Ili mgombea "A" atangazwe mshindi kura alizopata A/X lazima ziwe zaidi ya 50%.

Wakifanya kama Jubilee Coalition wanavyotaka maana yake hata kama wagombea wote wangekataliwa na wapiga kura (kura za maruhani) bado tume ingetangaza mshindi kati ya wale waliopigiwa kura

Mkuu unachosema hakileti maana hata kidogo, kinachotakiwa ni kuhesabu kura halali na kura zilizoharibika sio halali-mi nikichora "ZOMBIE" au "MESS" au nikiandika bongo fleva kwenye karatasi ya kura na kuitumbukiza kwenye ballot box utaiita kura halali na kuihesabu? Jubilee wana haki ya kulalamika na kama sheria ndio inataka hivyo basi ni sheria ya hovyo na ya kipumbavu!
 
Butola wewe unang'angania "simple majority" ambayo ni sheria ya Tanzania wao sheria ya 50% + 1. Sijui kwa nini unaogopga wale 377,000 kwamba uchaguzi ukirudiwa wataendelea kuharibu kura? Na zile za Keneth na wenzake si zitaongeza kura za mshindi?

...Nielewe vizuri hapa, sijasema popote kuwa 50%+1 ni mbaya, hapana, suala langu ni kama utakokotoa matokeo kwa kujumlisha "kura zilizoharibika", je exit loop ya mtego huo iko wapi kwenye marudio ya uchaguzi? kumbuka so far "kura zilizoharibika" ni nyingi kuliko Jumla za kura za Kennedy na wenzake watano kwa pamoja, by the way sheria haipaswi kubahatisha, inapaswa iwe applicable kwenye mazingira yote...

...Kama IBEC watafanya hivyo, Jubillee ni vyema waipeleke hilo suala mahakama itoe defintion, either "kura zilizoharibika" zisikokotoa kwenye "total votes cast" waiweke basi hiyo exit loop, sio kuweka sheria isiyoweka kumaliza suala pale mambo yanapokwenda kinyume...
 
Mkuu unachosema hakileti maana hata kidogo, kinachotakiwa ni kuhesabu kura halali na kura zilizoharibika sio halali-mi nikichora "ZOMBIE" au "MESS" au nikiandika bongo fleva kwenye karatasi ya kura na kuitumbukiza kwenye ballot box utaiita kura halali na kuihesabu? Jubilee wana haki ya kulalamika na kama sheria ndio inataka hivyo basi ni sheria ya hovyo na ya kipumbavu!

...Umeweka mfano mzuri sana hapa, sasa je mtu huyu aliyechora Zombie kwenye karatasi ya kura ana tofauti gani na mtu ambaye "alijisajiri kupiga kura" lakini "hakujitokeza kupiga kura"?logically huyu nae ni kama yule ambaye hajajitokeza, kama ndivyo basi kwanini matokeo yasikokotolewe kutokana na "registered voters"?..


...Naamini IEBC hawatauingia huu mkenge, wakishindwa basi mahakama itatoa definition nzuri ya "Total Votes Cast" na Jubillee kupewa ushindi wao wa "kipindi cha kwanza"..
 
...Umeweka mfano mzuri sana hapa, sasa je mtu huyu aliyechora Zombie kwenye karatasi ya kura ana tofauti gani na mtu ambaye "alijisajiri kupiga kura" lakini "hakujitokeza kupiga kura"?logically huyu nae ni kama yule ambaye hajajitokeza, kama ndivyo basi kwanini matokeo yasikokotolewe kutokana na "registered voters"?..


...Naamini IEBC hawatauingia huu mkenge, wakishindwa basi mahakama itatoa definition nzuri ya "Total Votes Cast" na Jubillee kupewa ushindi wao wa "kipindi cha kwanza"..


Mkuu ZeMarcopolo naye ametoa observation nzuri kuhusiana na kauli ya 'NOW' toka kwa mwenyekiti wa Tume, labda Ndachuwa aje atupe ufafanuzi!!!
 
Last edited by a moderator:
Ninachomaanisha, ni maoni ya wapiga kura 49.9% hayatazingatiwa? Demokrasia iko wapi hapo? hata kama atapata 52% na mwezake 48% hakuna demokrasia hapo! Bora gepu liwe kubwa ndo mmoja apewe mamlaka ya kuendesha nchi otherwise wote waendeshe nchi pamoja kama ilivo kenya/zimbabwe kwa sasa na si mpaka manung'uniko na fujo zitokee ndio wajue wanaweza fanya kazi pamoja?
Mkuu hiyo ndio demokrasia sasa, kwa kizungu changu cha kuunga unga wanasema Democracy is the dictatorship of the majority to the minority, as long as below 50% is regarded as a minority then they should agree with the majority which is above 50%.
 
Butola said:
My Take:
Nakubaliana na Jubillee, "Kura Zilizoharibika ni Kama Mgombea wa Maruhani", kuzijumlisha kura hizi kwenye kutafuta percentage ya kura za wagombea kutasababisha ata kwenye uchaguzi wa marudio, wa washindi wawili wa juu, uwepo uwezakano pia wa kutopatikana mshindi, kwa sababu japo tutawaona Uhuru na Odinga, lakini kutakuwa pia na mgombea, "Kura Zilizoharibika"..

Ikumbukwe kuwa katika matokeo ya mpaka sasa, mgombea huyu "Kura Zilizoharibika", amekamata nafasi ya tatu nyuma ya Uhuru na Odinga.

Kama hii hapa chini ndiyo provision ya katiba yao namna ya kumpata mshindi wa kiti cha uraisi hapo IEBC hawastahili lawama hata kidogo bali kwakuwa kila mmoja angependa kupata ushindi wa moja kwa moja raundi hii ya kwanza ndio sababu wanalalamika, wala hili halihitji intervention ya foreign missions kama Ruto anavyolalamika, ni suala tu la tafsiri ya katiba na sheria. Hapo kwenye red colour hapo ndipo tafsiri sahihi ya kikatiba ilipo na kama wanadhani ama na wewe Butola unadhani kujumuisha kura zilizoharibika ni makosa basi inabidi uwashauri wakenya wairekebishe katiba yao isomeke kwamba mshindi atapatikana kwa asilimia 50 + ya kura halali.

Butola; According to the Constitution said:
of all votes cast[/COLOR] to be declared the winner.
 
Last edited by a moderator:
Butola hao 377000 walikuwa wapiga kura? Kama jibu ni ndiyo kama hawakuona mgombea anayefaa unataka kura yake isihesabiwe?

hili jambo wengi tunalichukulia kirahisirahisi lakini sio ishu nyepesi kama tunavyodhani
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom