Juice na unga wa ngano kutoka viwanda vya Kenya vitaingia Tanzania bila vikwazo na sementi kutoka viwanda vya Tanzania vitaingia Kenya bila vikwazo

Huku ni kukosa akili(sorry) yaani unaambiwa ukauze nje unalalamika, mwenzako pia akija kuuza unalalamika. Kama siyo kukosa akili ni nini? Yaani unataka tusiuze saruji nje kisa itapanda bei!!!? Hutaki soko la nje?

Hii hangover ya ujamaa sijui tuinywee msapuo gani?
 
Azam juice haiwezi tamba kama del monte kenya itaruhusiwa kuingia .
Delmonte ipo kwenye level za Ceres
Endelea kujidanganya. Mimi naishi Mashariki ya mbali huku na Juice za Azam zinauzwa hadi huku, sembuse Kenya? Kipindi Kikwete anatoka Azam walishaanza kuuza Juice zao Kenya ila mahusiano ya kinchi yaliharibika kipindi cha JPM ndio maana mauzo yalipungua. Haya makubaliano ni neema kwetu. Tatizo watu tumezidi woga. Wakenya ni watu wa kawaida tu.
 
𝚗𝚊 𝚗𝚍𝚘 𝚔𝚒𝚙𝚒𝚗𝚍𝚒 𝚊𝚖𝚋𝚊𝚌𝚑𝚘 𝚊𝚝𝚊 𝚓𝚞𝚒𝚌𝚎 𝚣𝚊 𝚔𝚒𝚝𝚊𝚗𝚣𝚊𝚗𝚒𝚊 𝚔𝚞𝚣𝚒𝚔𝚞𝚝𝚊 𝚔𝚠𝚎𝚗𝚢𝚎 𝚗𝚍𝚎𝚐𝚎 𝚒𝚕𝚒𝚔𝚞𝚠𝚊 𝚒𝚜𝚜𝚞𝚎 𝚊𝚝𝚊 𝚖𝚊𝚓𝚒 𝚠𝚊𝚔𝚒𝚊𝚐𝚒𝚣𝚊 𝚢𝚊 𝚗𝚓𝚎.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hamna kitu .kila mtu atajikuna anapojipatia ,na yote ni furaha kwa mlaji ambae ndie mlipa kodi mkuu,vita vya panzi furaha kwa kunguru.Hata juice za ulaya mafanta na makoka yanayotoka nje si yapo ,hata bangi yetu ni nzuri ila CCM wanaikandia.
 
Naona jamaa anapenda sana Del Monte juice ila kwa kukusaidia ni kwamba Del mounte Iko kiwanda Kenya na Tanzania pia kipo ila asili yake ni USA na kuwekezwa mara ya kwanza South Africa

Ila ninachoweza kusema zote nimewahi kunywa lakini bado Azam naikubali ( Tropical [emoji484] Azam)
So vitu vikae sokoni tujichagulie
Offcorse mimi ni Mzalendo wa bidhaa za ndani Sitaacha Azam tropical kwa kweli sijaona mbadala wake.

Kwenye maziwa fresh yakiruhusiwa Azam ataumizwa na Brookside milk kwa sababu ya bei
Brookside 2000 ubora uko juu
Azam 3500 sina uhakika sana

Ushauri wangu tuunge mkono bidhaa zetu za ndani zile ambazo kwa kweli zina ubora.
Kwa sababu Kenya wanaweza kuamua kutengeneza bidhaa fake za kuja huku wakijua mtanunua kisa hamtaki vya kwenu.
 
Viwanda vyetu vimekatazwa kutumia hii gesi?
 
acha woga we ni mtoto wa kiume,na hizi point zako za history form 3,unajichoresha tu kwenye profile yako miwani mikuubwa lakini roho ya kike.
 
Delmonte foods ni kampuni ya kimarekani yenye makao makuu California; siyo ya Kenya.
... ni sawa na Dangote yenye makao makuu Nigeria(?) lakini imewekeza Tanzania.
 
[emoji44][emoji44][emoji44] manufacturing industry, assemble industry

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu kuishi madhariki ya mbali sio kujua kila kitu,
Juice za Azam zote ni chemicals syrups na zimeongezwa sukari,
Ceres na del monte ni natural juice , no preservatives na hazijaongezwa sukari , hawa jamaa kabla hawajaanza kutengeneza juice , waliwekeza kwanza kwenye kilimo cha matunda , ndo maana hata bei ya juice hizo hazifanani
 
Juice za Del Monte (hasa pinnnaple) ni nzuri kwa ajili imetengezwa na mananasi fresh ambayo kampuni inazalisha yenyewe Thika.Ubora wa brookside bila shaka upo juu ,yametengezwa na maziwa fresh(siyo reconstituted).
 
Ukiwa mtu hasi mwenye akili hasi, daima utapata maendeleo hasi. Fikra hasi za marehemu, ziliangusha ukuaji wa kila sekta ya uchumi. Tunahitaji fikra chanya kuleta positive economic growth.

Hakuna nchi hata moja Duniani, iliyokuwa maskini, halafu ilipata maendeleo, iliyoegemea eti kulinda viwanda vya ndani kwa kuzuia bidhaa toka nje. China walishindwa, Urusi walishindwa, India walishindwa, Ujerumani Mashariki walishindwa. Dubai waliweka milango wazi, wakapata maendeleo makubwa kwa kiwango cha ajabu, ndani ya miaka 15.

Mama Samia, ni akili kubwa, wengi hawataamini kwenye ukuaji wa uchumi ndani ya muda mfupi.
 
Wa Tanzania Kitendo cha Jiwe kuwabatiza Jina Wanyonge na kulikubali kumedumaza sana akili zenu, yaani Kila kitu mnahisi Mnahujumiwa, covid-19 vaccine mnahisi mnatafutwa nyie, sasa imefikia hatua mnawaogopa hata wa Kenya.
Mungu ametutendea Jambo jema sana Kumchukua Jiwe, Miaka Mitano mbele 80% ya wabongo wangekuwa Ma Zezeta
 
JPM mwondoe. Hakuna mchango wake wa maana kwenye sekta ya viwanda.
 
Yaani Watanzania sijui kwa nini hata wasomi wanapenda kuendelea kujishikamanisha na ujinga kuliko maarifa na werevu.

Yaani wajinga hawajui faida ya ushindani.
 
Unaongelea mambo usiyoyafahamu wala hujawi fanya kazi Katika sekta hizo

Wewe hujui kitu, unalalamika bila takwimu

Mpaka sasa, Bidhaa za Kenya ndio zimejaa sokoni

Ni kitu gani cha Kenya hakipo sokoni Tanzania

Huwezi kwepa Dunia ya ushindani wewe ni wale malofa wanaoamini Katika Command economy yaani serikali imiliki viwanda na kuviongoza

Wewe umepitwa na wakati, Jaribu kuwa flexible na kujifunza

Maduka makubwa mengi Tanzania yanachukua Bidhaa Kenya wanakwepa bandari ya Dar

Wewe unatokea mapori ya wapi?

Sent from my INE-LX2 using JamiiForums mobile app
 
Wewe unatumia umeme wa wapi huo mbona bei juu sana.?
Wakati sisi watumiaji wa majumbani ndo tunanunua umeme bei juu ni tsh288 kuliko wenye viwanda.!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…