Juma Nyosso amekamatwa na Polisi baada ya kumpiga shabiki hadi kuzimia

Juma Nyosso amekamatwa na Polisi baada ya kumpiga shabiki hadi kuzimia

Mkuu rudia kusoma. Aliyepigwa ni shabiki wa kagera suger na siyo shabiki wa simba. Acha kukurupuka
wewe ndo uache kuwa kama bendera. Huoni huyo shabiki kavaa jezi nyekundu tena ya simba
 
Dah ilikua ngumi jiwe hiyo hadi mtu kuzima!Ila Nyosso bana anazingua mno..si angevumilia tu ona anavyojiharibia.Chonde wasije wakampa adhabu ya kutokucheza maisha.
 
Uyo ni shabiki wa simba tena wa Dar
Nyosso wasikuzoee hao mikia
 
de5ea211b02c336d47b134de09572bc8.jpg
Mchezaji wa Kagera Sugar Juma Nyosso ashikiliwa na jeshi la polisi baada ya kutuhumiwa kumpiga Shabiki mmoja uwanjani mpaka kupoteza fahamu.

Tukio hilo limetokea muda mfupi baada ya kumalizika kwa mchezo wa ligi kuu Tanzania bara VPL kati ya Kagera Sugar dhidi ya Simba Sports Club.
Kupiga mshabiki inawezekana ila hiyo picha ya pili mbona kama haioani na tukio.

Mpira umekwisha hawa watu hapo chini mbona wamekaa kama vile mechi inaendelea nilidhani ningaliwaona wakiwa wimawima kwenye harakati za kuondoka uwanjani!!
 
Kupiga mshabiki inawezekana ila hiyo picha ya pili mbona kama haioani na tukio.

Mpira umekwisha hawa watu hapo chini mbona wamekaa kama vile mechi inaendelea nilidhani ningaliwaona wakiwa wimawima kwenye harakati za kuondoka uwanjani!!
Kuna utata kidogo. Ila wasema shabiki aliingia uwanjani punde tu mpira kwisha.
 
Mashabiki wa Simba wanaushabiki wa kishamba sana, kwa nini wamzomee Nyoso!.
 
Mashabiki wa simba ni mambumbumbu ..

Hongera nyosso umemkosa Bocco umempata shabiki wa simba ,nilitaka kushangaa nyosso awaache simba salama?
Usisome "heading" tu bali soma habari yote
 
Huyu jamaa sasa akatafute kazi nyingine tu, kipaji bila nidhamu ni bure.

Unaacha kazi inayokuletea ugali mezani unahangaika na shabiki anayepiga mayowe yake akichoka anaenda kulala kwake huko.
 
Ila washabiki wanaboa, inasemekana huyo shabiki ni wa Simba na alienda akampulizia vuvuzela Nyosso tena usoni, ebu imajini mmefungwa alafu jamaa anakuja kukupigia makelele usoni na vuvuzela.
 
Back
Top Bottom