Jumla ya ada ya kusoma degree ya udaktari katika chuo kikuu cha Kairuki kwa miaka yote mitano ni milioni 32, swali langu is it worth it ?

Hiyo model nzima ya mtoto kusomeshwa na mzazi masikini ni mbovu.

Kwa sababu mnaweza kuwa na neirodivergent genius kazaliwa katika familia masikini isiyo na elimu akakosa kusoma kwa sababu tu mzazi anaona "hailipi".

Tukakosa genius wetu kupata nafasi ya kusoma na kuvumbua mambo makubwa kwenye medicine.

Halafu tukarudia kujiuliza maswali yetu yake yake ya kila siku, kuwa "Mbona Afrika hatugundui kitu, kila kitu tunaletewa kutika nje?"

Tatizo tunalitengeneza wenyewe, halafu tunashangaa wenyewe.
 
...Bahati mbaya huyo Genius wa Satarani hajatokes, na Bei Iko hivyo hivyo !!...[emoji57][emoji57]
Genius wa saratani hajatokea kwa sababu wazazi wanawaza kulinganisha mshahara na ada. Wako stuck hapo.

Kwa sababu mfumonuna lack of inclusivity. Ukizaliwa kijijini mazingira ya kusoma mbinde automatically hata kama genius unaanza kutolewa katika mstari.

Mfumonuna low tolerance for initial failure, hapo huwezi kupata genius.

Kwa sababu jamii haijajipanga inawezaje kufaidika vizuri kabisa na ma genius wetu.

Mimi sikubali kabisa kwamba wazungu au wa Asia wanatushinda kitu chochote kiasili au kibaiolojia.

Wanachotushinda ni mambo ya kiutamaduni, kiutashi, kiuchumi, mambo ya jamii kujipanga tu.
 
Ni kweli mkuu wa ni watoto wengi wameshindwa kwa sababu hiyo, Programs za STEM ilitakiwa iwe free kwa vyuo vyote vikuu bila kujali serikali au binafsi .

Pia uwekezaji wa miradi ya tafiti kwenye vyuo vyote mfano maabara, karakana na library za kutosha hapo ndio uvumbuzi utakuwepo sasa nchi zetu za kiafrika aka shithole zina vipaumbele vingine
 
Those things will never happen here unless tubadilike tuwekeze kwenye elimu kiukweli ukweli tupunguze maneno mengi. Unaona wenzetu China na India mambo ya IT, Computer science na Engeering wapo mbali. Kwenye health science nako ndio usiseme.
 
Nani alikudanganya ile hospitali na chuo ni yeye ndiye mmiliki 100%?

Naomba niishie hapa.
 


Thamani ya kitu hutokana na nini?

1: Tathmini huru ya gharama ya kitu husika/cha aina hiyo ndani ya eneo husika. Je tuna thamani halisi ya daktari Tanzania?
Ungeweza kujua gharama hii kama inabeba thamani yake pale ambapo ungekuwa unajua gharama halisi ya daktari wa kitanzani ni kiasi gani. Hapo ndo ungesema kwa gharama hii iliyo juu au chini ya iliyotathminiwa, imebeba uhalisia kigharama?

2: Uhitaji wa kitu ndani ya eneo husika. Je uhitaji wetu wa daktari ni sawa na milioni 32?
Thamani ya pili huweza kupimwa kwa hitaji la matumizi ya kitu husika. Kwa uwepo wa daktari ambaye anatimiza majukumu yake, hiyo gharama ni ndogo. Maana kuokoa kifo kimoja tu ni zaidi ya milioni 32. Afya ndo msingi na uhai hauna thamani ya kulinganisha nao kipesa.

3: Kitendacho kitu husika/kujihudumia/kujizalisha baada ya gharama. Je wamesaidika kwa kiasi gani waliosoma pale/waliopata elimu hiyo? Hii ni subjective, kwani kila mmoja anapoingia mtaani anaitumia elimu husika pamoja na changamoto za dunia ku-excel. Hapa ni pale utakapoenda kuangalia maisha na activities za alumnus wa Kairuki zikoje huko duniani. Ingawa naamini wanaishi thamani husika au zaidi kwa kujibidisha dhidi ya changamoto mbalimbali(maisha ya jumla).

4: Kuhusu kulinganisha wahitimu wa vyuo mbalimbali. Hii bado ni subjective ya kujibidisha na uwezo wa kila mmoja. Ukienda interniship au postgraduate, kuna wakati aliyetoka MNH ataonekana kama ametoka KAIRUKI na kuna wakati wa KAIRUKI ataonekana ametoka MNH. Haiko formal kwamba kila mara au kila mmoja atafanana na syndrome zilizopo kivyuo kwa wahitimu. Hapa ni uzingativu wa kila mmoja wakati wa kusoma.

5: Pia unaweza kupima thamani kwa kulinganisha na wenzetu nje ya eneo husika. Hapo ndo utaona gharama zetu bado ni nafuu kuliko tunavyodhani, ukilinganisha logistics zote.
 
Those things will never happen here unless tubadilike tuwekeze kwenye elimu kiukweli ukweli tupunguze maneno mengi. Unaona wenzetu China na India mambo ya IT, Computer science na Engeering wapo mbali. Kwenye health science nako ndio usiseme.
Hao Wahindi walianza kujipanga tangu 1950s. Waliweka mikakati ya kuwa na elimu nzuri itakayoshindana katika dunia kuanzia miaka ya 1950s.

Mfano, kwenye IT, wameweka mkakati wa kujenga vyuo vyao vya vipanga wao kwenye teknolojia , vinaitwa IIT, Indian Institute for Technology. Nimeona mwaka jana wameanzisha kimoja hapo Zanzibar.


Matokeo yake tumeanza kuyaona miaka ya 1990s.

Sisi bado tunaogopa ada ya milioni sita saba kwa mwaka.

Hiyo ada ya kwenda medical school kwa Kairuki ni ndogo kuliko ya kwenda IIT Zanzibar kusoma mambo ya IT Security. Ukisoma IT Security IIT Zanzibar unaweza kufanya kazi sehemu yoyote duniani, dunia nzima inaelewa brand ya IIT ni nini. Kampuni zote za wahindi zinazofanya kazi dunia nzima zikiona umesoma IIT zinajua wewe ni "hot cake". Utafanya kazi Marekani, US, Canada, India, Australia etc, utachagua mwenyewe.

Sasa hapo napo utasema ada ni tatizo? Ada ni gharama tu, si tatizo.

Sisemi kwamba hiyo ada ni ndogo sana kwa maisha ya Mtanzania wa kawaida wa GDP per capita ya US dollar 1200.

Nasema kwamba kama jamii tunashindwa kujipanga kuangalia jambo hili beyond ada.

Kuna binamu yangu mmoja alikuwa ananiambia kuwa, matatizo halisi ya dunia hii hayatatuliwi na pesa. Mambo ya matatizo halisi ya mapenzi (si udangaji), matatizo ya uvumbuzi wa kisayansi, etc, hayo unaweza kuyarahisisha kwa pesa lakini ufumbuzi unataka akili zaidi ya pesa.

Yani Alan Turing alipokuwa anahangaika kuvunja encryption za Wajerumani katika vita vikuu vya pili vya dunia (angalia movie "The Imitation Game") pale hata ungempa hela zote za dunia kuvunja encryption kulitaka akili zaidi ya hela.

Binamu alisema kwamba ukiona tatizo linatatuliwa kwa pesa tu, hilo si tatizo, hiyo ni gharama tu.

Matatizo ya kweli hayatatuliwi kwa pesa tu.

Sasa sisi kwetu watu masikini wengi wanakwamishwa na kikwazo cha pesa mpaka wanashindwa kutambua tofauti ya tatizo na gharama.
 
Kwa maana hiyo udaktari Ni Kama tu ualimu, wote wanatembea Kwny kaul mbiu ya wito[emoji2]
 
Nani alikudanganya ile hospitali na chuo ni yeye ndiye mmiliki 100%?

Naomba niishie hapa.
Wapi nimesema ni mmiliki 100%.
Hao wauza chips mahoteli au vyuo wanavyomiliki 100% ni kina nani na viko wapi.

Hata top 10 ya matajiri duniani huwezi taja tajiri mmoja mwenye umiliki 100% wa biashara au kampuni inayomfanya awe billionaire.
 
Wewe unalia hiyo kwa chuo kikuu wakati kuna watu wanalipa hiyo hela kwenye shule za chekechea!
 
Mkuu umenikumbusha Clip moja Hivi..
Your browser is not able to display this video.
 
Hapo anachoongelea ni academic quality, ambapo kinachoangaliwa sio tu facilities, bali walimu wa kutosha wenye qualifications stahiki, i.e, professors wa kutosha, PhDs za kutosha, nk.
 
Kwa maana hiyo udaktari Ni Kama tu ualimu, wote wanatembea Kwny kaul mbiu ya wito[emoji2]
Mkuu,

Hii habari ya udaktari ni kazi ya kujitolea kwa wito bila mafanikio ya kipato au udaktari ni ajira yenye faida kiuchumi ni logical fallacy inaitwa "false dichotomy".

Yani false dichotomy maana yake ni kwamba unatengeneza njia panda ambayo haina ulazima wa kuwepo.

Yani unaweka uchaguzi wa "either or" kwamba ama udaktari ni wito, unafanya kazi kwa faida ndogo ilimradi uokoe maisha ya watu, ama udaktari ni ajira yenye kioato kikubwa, na ukielekea kuangakia faida hiyo ya kuliuchumi tu, unaondoka kwenye kuhudunia watu.

Kimsingi, hakuna sababu ya kufanya udaktari usifanye vyote viwili kwa pamoja.

Hakuna sababu udaktari usiwe wito wa kusaidia kutatua matatizo ya afya ya watu, halafu hapo hapo udaktari usiwe kazi yenye faida nzuri tu ya kiuchumi.

Ni suala la kujipanga vizuri tu ku balance hiyo equation.
 
Kwa maana hiyo udaktari Ni Kama tu ualimu, wote wanatembea Kwny kaul mbiu ya wito[emoji2]
Wito Maana yake Unatakiwa kuweka maslahi ya Umma kwanza na sio ya mfuko kulingana na Hippocroatic Oath (Kiapo)..
Cha kwanza kinaanza ni Mgonjwa cha Pili ni Hayo maslahi mengine so Bila kuitwa Kaa ajili ya kazi hiyo ni vigumu sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…