Jumuiya kama za Kikatoliki zinapaswa kuigwa na jamii zote na taifa kiujumla

Jumuiya kama za Kikatoliki zinapaswa kuigwa na jamii zote na taifa kiujumla

John Gregory

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2019
Posts
1,137
Reaction score
2,147
hq720.jpg

Huu utaratibu wa waumini wa kanisa katoliki kukutana kila Jumamosi kwa ajili ya taratibu zao za Jumuiya nadhani linapaswa kuigwa na liwe jambo la kila Mtanzania.Jumuiya hizi hujengwa na familia kadhaa zisizopungua tano hadi kumi na tano zilizo jirani.Familia hizi hushirikiana katika mambo yote ikiwa ni pamoja na kusali pamoja,kusoma na kushirikishana katika kutafakari Neno la Mungu, kufarijiana,kulea watoto,kusaidia wenye shida,kupanga maendeleo yao,nk.

Mbali na faida za kiimani wanazopata waumini hao kwa kusali pale wanapokutana, Hilo nisingependa kulizungumzia sana, Lakini pia kuna manufaa mengine ya kijamii.

1- Ni chachu ya ushirikiano na umoja kwa wanajamii.

2- Ni sehemu ya kufarijiana na kusaidiana katika changamoto mbalimbali kama za kiafya nk.

3- Husaidia kulea vijana na watoto katika miito na maadili sahihi ili kuwa watumishi bora kwa jamii na taifa.

4- Sehemu rahisi ambayo kila mwanajamii anaweza kutoa maoni, ushauri na mapendekezo yanayohusu masuala mbalimbali.

5- Hutumika kutatua migogoro mbalimbali kama ya wanandoa kwa utaratibu sahihi.

6- Inakuza imani na maadili kwa familia (kaya); hasa baba, mama, watoto na ndugu wanaoishi pamoja wakishiriki kikamilifu.

7- Jumuiya hutoa misaada mbalimbali kwa jamii inayoizunguka.

8- Pia, jumuiya hutumika kujengana kiroho kwa kurekebishana pale mmoja anapoyumba kimaadili.

Kwa hayo machache, nadhani kukutana mara kwa mara, hususan kwa majirani au wanajamii kwa ujumla, Kuzungumza mambo kadhaa, mfano changamoto kadhaa zilizopo katika jamii, kutambulisha wageni, kujuliana hali, kusaidiana katika changamoto na shida mbalimbali kama maradhi, magonjwa nk. ni jambo jema, Ikishindikana kukutana mara moja kwa wiki, basi angalau kila mwezi au kila baada ya muda fulani kwa utaratibu maalum ambao jamii itajiwekea.
 
Waanzillishi hiyo kitu wala sio wakatoliki ni walokole walianza miaka mingi sana kitu kinaitwa ibada za nyumba kwa nyumba miaka mingi kabla hata katoliki hawajagundua hilo

Na ilianza kipindi cha mitume walikuwa wakisali nyumba kwa nyumba na kumega mkate na baadaye ikaendelea kwenye maeneo ambayo kanisa lilikuwa halikubaliki kama nchi za kikomunisti nk ambako ukristo ulikuwa haukubaliki na unapigwa vita

Baadaye kanisa katoliki likaona linapoteza waumini wakaiga na kuanzisha ulokole wa karismatiki ili na katoliki wajisikie nao walokole wakati huku wakiendelea kusali na kuomba bikira Maria nk na hizo jumuiya zilianzishwa kudhibiti waumini wao katoliki wasihame katoliki kwa vitisho vya ohhh kama huhudhurii jumuiya huzikwi au kupewa sacramenti ya ndoa nk na pia kuwa sehemu ya majungu ya nani kaenda kwa Mwamposa nk na pia jumuiya inatumika kama sehemu ya kukusanya pesa za sadaka nje ya zile za kanisani tofauti na ibada za nyumba kwa nyumba za walokole ambao hadi kesho hukutana tu kwa lengo la kusali tu,na kutiana moyo
 
Waanzillishi hiyo kitu wala sio wakatoliki ni walokole wal8anza miaka mingi sana kitu kinaitwa ibada za nyumba kwa nyumba miaka mingi kabla hata katoliki hawajagundua hilo

Na ilianza kipindi cha mitume walikuwa wakisali nyumba kwa nyumba na kumega mkate na baadaye ikaendelea kwenye maeneo ambayo kanisa lilikuwa halikubaliki kama nchi za kikomunisti nk ambako ukristo ulikuwa haukubaliki na unapigwa vita

Baadaye kanisa katoliki likaona linapoteza waumini wakaiga na kuanzisha ulokole wa karismatiki ili na katoliki wajisikie nao walokole wakati huku wakiendelea kusali na kuomba bikira Maria nk na hizo jumuiya zilianzishwa kudhibiti waumini wao katoliki wasihame katoliki kwa vitisho vya ohhh kama huhudhurii jumuiya huzikwi au kupewa sacramenti ya ndoa nk na pia kuwa sehemunya majungu ya nani kaenda kwa Mwamposa nk na pia jumuiya inatumika kama sehemu ya kukusanya pesa za sadaka nje ya zile za kanisani tofauti na ibada za nyumba kwa nyumba za walokole ambao hadi kesho hukutana tu kwa lengo la kusali tu,na kutiana moyo
Miaka mingi lin mkuu. Waanzilishi ni catholic bana mpeni mtu maua yake anaPostahili. Wewe jumuiya umeziona mjin sisi tumezaliwa tunazikuta vijijin ndio zilizotukuza.
 
Ni jambo jema sana kuiga, ila kamwe msiige content, How is the World unaweza bariki ndoa ya jinsia moja?
 
Ni njia ya kutongozana na kugongana, ziko kesi kadhaa nazifahamu chanzo ni kukutana kila jmos jumuiya, mwenyekiti anawala waumini, mhasibu anajipigia na wanaanzisha mpaka watsaap group wanaishia kupigana
 
Kanisa langu tawi la mtaani tumeanza kuiga huu mtindo wa wakatoliki, kila jumamosi tunakutana kwa ibada na kupanga mambo muhimu katika mtaa wetu. Ngazi za juu kuanzia parishi, misheni, jimbo na taifa hawajui kama tawi letu tumeanzisha utaratibu kama wa wakatoliki mitaani. Jumuiya zetu tunaziita zone
 
Miaka mingi lin mkuu. Waanzilishi ni catholic bana mpeni mtu maua yake anaPostahili. Wewe jumuiya umeziona mjin sisi tumezaliwa tunazikuta vijijin ndio zilizotukuza.
Soma Biblia wewe hayo ya sala ya nyumba kwa nyumba za jumuiya yalianza kipindi cha mitume uwe unasoma Biblia sio tu kushindia misale ya waaumini na kusikiliza padre tu au unacholishwa matango pori seminary

Tatizo wakatoliki hamsomi Biblia ndio masna huwa mnaamini kanisa la Kikristo lilianzia Roma Italia mnasahau kuwa Kristo mwanzillishi wa Ukristo alizaliwa Israel sio Roma Italia mnalishwa ujinga

Ukiristo ulianzishwa uyahudi na Kristo mwenyewe anayeitwa Kristo sio Petro au yeyote


Ukristo ulianza uyahudi na Kristo ndio maana tunaitwa wakristo wafuasi qa Kristo myahudi wa uyahudi sio wa Petro wafuasi wa Petro papa wa kwanza wa wa Roman Catholic wabaojitia kanisa la kwanza lilianzia Roma kwa Petro

Sisi hatuhiji Roma na hatuna mpango tunatambua kanisa la kwanza lilianzishwa Uyahudi na Kristo mwenyewe alipozaiwa,kuhubiri kuteswa ,kufa na kufufuka

Hilo kanisa lenu mnaita la kwanza aliloanzisha Petro bakini nalo wenyewe na utapeli wenu

Kanisa la kwanza mwanzilshi Kristo hakuna cha Petro ,wakoritntho wala nani

Ni Yesu Kristo tu
 
Waanzillishi hiyo kitu wala sio wakatoliki ni walokole walianza miaka mingi sana kitu kinaitwa ibada za nyumba kwa nyumba miaka mingi kabla hata katoliki hawajagundua hilo

Na ilianza kipindi cha mitume walikuwa wakisali nyumba kwa nyumba na kumega mkate na baadaye ikaendelea kwenye maeneo ambayo kanisa lilikuwa halikubaliki kama nchi za kikomunisti nk ambako ukristo ulikuwa haukubaliki na unapigwa vita

Baadaye kanisa katoliki likaona linapoteza waumini wakaiga na kuanzisha ulokole wa karismatiki ili na katoliki wajisikie nao walokole wakati huku wakiendelea kusali na kuomba bikira Maria nk na hizo jumuiya zilianzishwa kudhibiti waumini wao katoliki wasihame katoliki kwa vitisho vya ohhh kama huhudhurii jumuiya huzikwi au kupewa sacramenti ya ndoa nk na pia kuwa sehemunya majungu ya nani kaenda kwa Mwamposa nk na pia jumuiya inatumika kama sehemu ya kukusanya pesa za sadaka nje ya zile za kanisani tofauti na ibada za nyumba kwa nyumba za walokole ambao hadi kesho hukutana tu kwa lengo la kusali tu,na kutiana moyo
Walokole na RC nani alianza kuwepo?Mitume?Unazungumzia mitume wepi hao?
 
Shotocan elekeza watu wasome biblia sehemu gani ili waone ulichoeleza.
Soma Biblia wewe hayo ya sala ya nyumba kwa nyumba za jumuiya yalianza kipindi cha mitume uwe unasoma Biblia sio tu kushindia misale ya waaumini na kusikiliza padre tu au unacholishwa matango pori seminary

Tatizo wakatoliki hamsomi Biblia ndio masna huwa mnaamini kanisa la Kikristo lilianzia Roma Italia mnasahau kuwa Kristo mwanzillishi wa Ukristo alizaliwa Israel sio Roma Italia mnalishwa ujinga

Ukiristo ulianzishwa uyahudi na Kristo mwenyewe anayeitwa Kristo sio Petro au yeyote


Ukristo ulianza uyahudi na Kristo ndio maana tunaitwa wakristo wafuasi qa Kristo myahudi wa uyahudi sio wa Petro wafuasi wa Petro papa wa kwanza wa wa Roman Catholic wabaojitia kanisa la kwanza lilianzia Roma kwa Petro

Sisi hatuhiji Roma na hatuna mpango tunatambua kanisa la kwanza lilianzishwa Uyahudi na Kristo mwenyewe alipozaiwa,kuhubiri kuteswa ,kufa na kufufuka

Hilo kanisa lenu mnaita la kwanza aliloanzisha Petro bakini nalo wenyewe na utapeli wenu

Kanisa la kwanza mwanzilshi Kristo hakuna cha Petro ,wakoritntho wala nani

Ni Yesu Kristo tu
 
Walokole na RC nani alianza kuwepo?Mitume?Unazungumzia mitume wepi hao?
Mitume Wa Yesu aliokuwa nao Israel Yesu Kristo alikoanzisha Ukristo yeye akiwa Kristo mwenyewe

Dini zote hutambua mwanzilishi wa dini husika alipozaiwa, kuhubiri na kufa ndipo dini ilanzia wawe waislamu nk

Wakristo wa kweli pia tunaamini hivyo kasoro wakatoliki ndio wapiga chenga

Mwanzillishi wa Ukristo Yesu Kristo kazaliwa uyahudi, kahubiri uyahudi, kateswa uyahudi kafa uyahudi kafufuka uyahudi halafu matapeli katoliki wanasema ooh kanisa la kwanza alianzisha Petro roma Italia mmmmmmm

Danganyaneni wenyewe huko kanisani kwenu sio kwa watu wasoma Biblia na kuielewa

Kanisa la kwanza Petro hajawahi lianzisha Yesu myahudi ndie alianzisha uyahudi
 
Jumuiya za haya madhehebu sio tu katoliki na wenzake zimekua ni msaada wa kijamii tu lakini kiroho na kiimani zimepoa sana. imebaki kuwa kama desturi tu sasa hivi za kufanikishia malengo ya kanisa. 😏
 
Mitume Wa Yesu aliokuwa nao Israel Yesu Kristo aliloanzisha Ukristo yeye akiwa Kristo

Dini zote hutambua mwanzilishi wa dini husika alipozaiwa, kuhubiri na kufa ndipo dini ilanzia wawe waislamu nk

Wakristo wa kweli pia tunaamini hivyo kasoro wakatoliki ndio wapiga chenga

Mwanzillishi wa Ukristo Yesu Kristo kazaliwa uyahudi, kahubiri uyahudi, kateswa uyahudi kafa uyahudi kafufuka uyahudi halafu matapeli katoliki wanasema ooh kanisa la kwanza alianzisha Petro roma Italia mmmmmmm

Danganyaneni wenyewe huko kanisani kwenu sio kwa watu wasoma Biblia na kuielewa

Kanisa la kwanza Petro hajawahi lianzisha Yesu myahudi ndie alianzisha uyahudi
Changamoto yako:Unaandika mambo mengi kwa emotions bila ushahidi.Wewe ni kulalama tu.
 
Changamoto yako:Unaandika mambo mengi kwa emotions bila ushahidi.Wewe ni kulalama tu.
Soma Biblia wewe dini zote huamini kuwa alipozaiwa mwanzilishi, kuhubiri na kufa ndio chanzo cha dini husika katoliki ndio matapeli pekee wasioamini hilo kuwa dini ya Kikristo haikuanzia Israel ilianzia Roma Italia

Waprotestanti wote tunaamini Ukristo ulianzia uyahudi kwa mwanzilishi Kristo mwanzillishi wa Ukristo yeye mwenyewe akiwa Kristo
 
Back
Top Bottom