Jumuiya ya Afrika Mashariki bila uongozi wa mzungu itakuwa ni genge la maigizo yasiyo na tija

Jumuiya ya Afrika Mashariki bila uongozi wa mzungu itakuwa ni genge la maigizo yasiyo na tija

Tindo

JF-Expert Member
Joined
Sep 28, 2011
Posts
63,730
Reaction score
111,542
Leo na kesho kutakuwa na mkutano wa wakuu wa nchi za jumuiya ya Afrika mashariki huko Arusha. Kwa mtazamo wangu mkutano huo ni wa upotevu wa muda, fedha za wananchi kwani hakuna lolote la maana linajadiliwa na kufikia hatua ya utekelezaji.

Mengi ya makubaliano ya jumuiya hii huishia kwenye makabati, huku kila nchi ikifanya kwa ubinafsi. Jumuiya hii ya Afrika Mashariki ilikuwa na ufanisi wakati wa utawala wa mzungu, lakini sisi waafrika kwenye hili tumekwama.

Ushauri wangu kwa viongozi wa nchi za Afrika Mashariki, acheni kupoteza muda na fedha za wananchi kwa mikutano isiyo na tija.
 
wameongeza Sudan, Congo, Burundi, Rwanda wakati ya awali ilikuwa haijawa integrated vizuri

Jumuiya za maana kama EU hawaongezi wanachama hovyo hovyo tu

Wanaungana ukubwa wa kieneo, lakini tabia zinabaki za kinchi binafsi. Ukipita mipakani maofisa wa nchi hizo hawajui hata umoja ni nini, na unafanyaje kazi! Umebaki ni umoja wa viongozi, nao uko midomoni na kwenye mikutano zaidi.

Kuna hiyo porojo ya sarafu ya pamoja ni muda sasa, lakini haianzi wala dalili! Kuna ushuru wa forodha ni porojo kama porojo nyingine. Kwa sasa ni rahisi kufanya biashara na nchi za ulaya, Amerika na Asia kuliko baina ya Afrika mashariki. Ili jumuiya hiyo iwe na tija ni lazima isimamiwe na mzungu na sio zaidi ya hapo.
 
Real hili li kitu limebaki just kuonyesha mataifa mengine kuwa jamaa wapo pamoja na wana jambo lao although there's nothing.

Toka tukiwa mataifa matatu akiwepo late mzee Moi, Mkapa na huyu alistata Kaguta hakuna kubwa linalofanyika zaidi ya matumizi ya pesa kwa troupes zao.

Kinachoenda kufanyika now ni kumkaribisha DRC na kuhairisha mkutano mh!.
 
Uwepo wa haya mashirikisho bila kuwa na uwezo wa kiuchumi ni maigizo tu, kujidanganya, kunafikiana, na uongo mwingine. Mwisho wa siku hakuna cha maana zaidi ya camera, matamko, over.

Naamini hakuna hata taifa moja kati ya hayo yanayounda hiyo jumuia yasiyotaka kupata fursa mapema kabla ya mwenzake, hata kama wakisema wanagawana nusu kwa nusu, bado ni maigizo tu.

Zaidi nikikumbuka juzi Samia alivyokwenda Uganda kwenye ile ziara yake, naona mikataba yote aliyosaini kule aliwanufaisha waganda tu, wala sikuona chochote cha maana sisi tulichoambulia.
 
Bila shaka familia yako umeiweka chini ya management ya mzungu.
 
Naunga mkono hoja!

Kati ya jumuiya za hovyo duniani hii inaongoza!

Toka mdogo naskia tu mara sarafu ya pamoja, mara shirikisho la kisiasa, mara umoja wa forodha.. mara kiswahili nininini sjui lakn hadi leo haieleweki utekelezaji zaidi ya kula pesa tu
 
Bila shaka familia yako umeiweka chini ya management ya mzungu.

Kabisa, na ukweli ni kuwa hiyo jumuiya ya Afrika mashariki ilikuwa na tija wakati iko chini ya Mkoloni. Kwa sasa chini ya weusi wenzetu ni porojo baada ya porojo.
 
Leo na kesho kutakuwa na mkutano wa wakuu wa nchi za jumuiya ya Afrika mashariki huko Arusha. Kwa mtazamo wangu mkutano huo ni wa upotevu wa muda, fedha za wananchi kwani hakuna lolote la maana linajadiliwa na kufikia hatua ya utekelezaji.

Mengi ya makubaliano ya jumuiya hii huishia kwenye makabati, huku kila nchi ikifanya kwa ubinafsi. Jumuiya hii ya Afrika Mashariki ilikuwa na ufanisi wakati wa utawala wa mzungu, lakini sisi waafrika kwenye hili tumekwama.

Ushauri wangu kwa viongozi wa nchi za Afrika Mashariki, acheni kupoteza muda na fedha za wananchi kwa mikutano isiyo na tija.
Wamekwenda kukutana na kula pesa za wavuja jasho tu.
 
Naunga mkono hoja!

Kati ya jumuiya za hovyo duniani hii inaongoza!

Toka mdogo naskia tu mara sarafu ya pamoja, mara shirikisho la kisiasa, mara umoja wa forodha.. mara kiswahili nininini sjui lakn hadi leo haieleweki utekelezaji zaidi ya kula pesa tu
Majumuia yote ya afrika hakuna hata moja lenye nguvu. Wako kwa ajiri ya kutengeneza ajira za watoto wao na wajomba zao kwenye hizo ofisi. Au na SADEC hadi leo wameshindwa kutoa msaada japo kidogo tu kule Cabo Delgado Msumbiji ambapo Magaidi wanasumbua karubu mwaka wa tano sasa.

Ingekuwa ushurikiano wa kupigana na wapinzani wanaopinga watawala wenzao ungeina umoja wao ulivyo na nguvu.
 
Leo na kesho kutakuwa na mkutano wa wakuu wa nchi za jumuiya ya Afrika mashariki huko Arusha. Kwa mtazamo wangu mkutano huo ni wa upotevu wa muda, fedha za wananchi kwani hakuna lolote la maana linajadiliwa na kufikia hatua ya utekelezaji.

Mengi ya makubaliano ya jumuiya hii huishia kwenye makabati, huku kila nchi ikifanya kwa ubinafsi. Jumuiya hii ya Afrika Mashariki ilikuwa na ufanisi wakati wa utawala wa mzungu, lakini sisi waafrika kwenye hili tumekwama.

Ushauri wangu kwa viongozi wa nchi za Afrika Mashariki, acheni kupoteza muda na fedha za wananchi kwa mikutano isiyo na tija.
Dah!

Hii ni mada nzito kweli, lakini nimebaki tu nikitoa kicheko; hasa kuhusu huyo "mzungu"!

Tukiondoa hilo la mzungu, ninakubaliana nawe moja kwa moja. Angalia viongozi waliopo kwenye kundi hilo, akina M7, Kagame, Samia...

Hawa ni viongozi wa kutegemewa kuleta mabadiliko ya maana katika jumuia kama hii? Kenyatta, anaondoka, lakini hakuwa na faida yoyote katika malengo ya kuleta maendeleo, mbali ya kuiona Kenya kuwa ndiye baba na mama wa ukanda mzima; kwa hiyo walitarajia manufaa zaidi ya wengine wote katika jumuia.

Sasa watamkaribisha Somalia!

Kazi yao kwisha.
 
Dah!

Hii ni mada nzito kweli, lakini nimebaki tu nikitoa kicheko; hasa kuhusu huyo "mzungu"!

Tukiondoa hilo la mzungu, ninakubaliana nawe moja kwa moja. Angalia viongozi waliopo kwenye kundi hilo, akina M7, Kagame, Samia...

Hawa ni viongozi wa kutegemewa kuleta mabadiliko ya maana katika jumuia kama hii? Kenyatta, anaondoka, lakini hakuwa na faida yoyote katika malengo ya kuleta maendeleo, mbali ya kuiona Kenya kuwa ndiye baba na mama wa ukanda mzima; kwa hiyo walitarajia manufaa zaidi ya wengine wote katika jumuia.

Sasa watamkaribisha Somalia!

Kazi yao kwisha.

Wanapanuka kwa ukubwa wa kijiografia, lakini makubaliano ya msingi hayatekelezwi. Na upanukaji mkubwa ni wa nchi zilizo desparate na vita.
 
Inasikitisha sana
Wanaungana ukubwa wa kieneo, lakini tabia zinabaki za kinchi binafsi. Ukipita mipakani maofisa wa nchi hizo hawajui hata umoja ni nini, na unafanyaje kazi! Umebaki ni umoja wa viongozi, nao uko midomoni na kwenye mikutano zaidi.

Kuna hiyo porojo ya sarafu ya pamoja ni muda sasa, lakini haianzi wala dalili! Kuna ushuru wa forodha ni porojo kama porojo nyingine. Kwa sasa ni rahisi kufanya biashara na nchi za ulaya, Amerika na Asia kuliko baina ya Afrika mashariki. Ili jumuiya hiyo iwe na tija ni lazima isimamiwe na mzungu na sio zaidi ya hapo.
 
Nikiwa Zambia najisikia huru zaidi kuliko Rwanda au Uganda!
Wanaungana ukubwa wa kieneo, lakini tabia zinabaki za kinchi binafsi. Ukipita mipakani maofisa wa nchi hizo hawajui hata umoja ni nini, na unafanyaje kazi! Umebaki ni umoja wa viongozi, nao uko midomoni na kwenye mikutano zaidi.

Kuna hiyo porojo ya sarafu ya pamoja ni muda sasa, lakini haianzi wala dalili! Kuna ushuru wa forodha ni porojo kama porojo nyingine. Kwa sasa ni rahisi kufanya biashara na nchi za ulaya, Amerika na Asia kuliko baina ya Afrika mashariki. Ili jumuiya hiyo iwe na tija ni lazima isimamiwe na mzungu na sio zaidi ya hapo.
 
Wanapanuka kwa ukubwa wa kijiografia, lakini makubaliano ya msingi hayatekelezwi. Na upanukaji mkubwa ni wa nchi zilizo desparate na vita.
Ngoja nikufahamishe kwa nini ipo hivyo kama hujalifikiria hili.

Hawa viongozi ni 'opportunists'.

Ngoja nikupe mifano:

Sudan Kusini hakuwa na sifa zilizotakiwa kujiunga ndani ya umoja huo, lakini kwa M7 na Kenyatta waliona fursa kubwa kwa nchi zao kwa Sudan Kusini kuwa mwanachama wa Jumuia.

Hali ni hiyo hiyo na DRC, msukumo na uharaka umetokana na fikra za kudhani DRC litakuwa shamba la bibi.

Panapokuwepo na urafi wa namna hiyo, maana yake maslahi ya umoja hayapo, ni maslahi ya nchi(viongozi) wanaokimbilia kunufaika.

Somalia ilicheleweshwa, kwa sababu ulikuwa ni mwiba kwa Kenya. Walijua kuingia kwa Somalia hakuwapi manufaa kama walivyotegemea na hizi nchi nyingine.

Lakini niseme, hakuna jambo lenye ubaya pekee. Hata jambo linaloonekana kwa upande mmoja kuwa baya, ukiliangalia kwa upande wa pili lina uzuri wake.
Kuingia kwa hizi nchi nyingi, kunapunguza matatizo baina ya nchi za mwanzo katika Jumuia hiyo. Kwa mfano, matatizo yaliyokuwa mengi kati ya Tanzania na Kenya, sasa yatapunguzwa nguvu kwa kufifishwa na wingi wa wanachama wa Jumuia.
 
Back
Top Bottom