Just Imagine Umepokea SMS hii "Mimi Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nakukaribisha ...."- Ungemjibu nini?

Unakipendekeza tu
Kwanza aliyetuma siyo Samia
Hii ni SMS kama za promotion kwenye mitandao ya simu
 
Update
Mtu mwingine aliyefurahia kupokea ujumbe huu ni huyu
View attachment 2332646
Zitto ahesabiwa ampa tano mama Samia.
Zitto Kabwe kamaliza kuhesabiwa ana furaha kubwa Sana baada ya kupokea ujumbe wa simu kutoka kwa rais Samia ambapo naye aliuforward kwa m/kiti Mbowe incase Kama hakupata wake,
Jee na yeye mtamparura, kumbeza na kumtukana kama mlivyo nifanya mimi?.
P
 
Kama sensa ingefanyika mwaka kati ya 2016 na 2020 unategemea sms ingesomekaje
 
"Mimi Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nakukaribisha kushiriki Sensa tarehe 23 Agosti,2022. Nakusihi utoe taarifa sahihi"
Mimi nimepokea na nyingine kutoka Kiembembuzi na Kiembesamaki ikisema Mimi Dr.
 
Mimi nimepokea ujumbe wa Mh. Samia na baadaye kidogo nikapokea huu hapa
"Mimi Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar naungana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kukuomba kushiriki Sensa na kutoa taarifa sahihi". Tayari nimeshahesabiwa.
 
SMS ile ya Mama kuhusu sensa ilikuwa inajibika na majibu yalikuwa yanaenda na unapata kabisa na DELIVERY REPORT. Ile ya Rais wa SMZ nayo pia ilikuwa inajibika isipokuwa yenyewe ilikuwa haileti DELIVERY REPORT
WABARIKIWE NA BWANA
 
Hata aibu hana!!!
 
Yani wewe jamaa kadiri siku zinavyosogea unashuka standards.
Mkuu Matrix19 watu hatulingani uelewa na hatufanani, sisi wengine ni washamba Sana!
Yani push messages ndio unadanganya watu zimetoka moja kwa moja kwa rais?
Wangapi wanajua mambo ya push SMS?, nimepokea SMS ya Samia, inasema "Mimi Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nakukaribisha.. " mtu asiye na uelewa na hayo mambo ya push SMS, atajuaje?. Mimi nimepokea SMS ya Rais wangu, kwa nini nisifurahi?.
This is embarrassing and too low from you.
Kwa sisi wengine, it's not embarrassing kuwa mashamba, Mimi ni mshamba fulani tuu, na mtu kuwa mshamba sio kosa!.
P
 
Paschal,hakuna cha kufurahisha kwenye hizo sms.Mimi niliamka asubuhi na kuzikuta,nikazifuta hata bila kizisoma.Nina hasira mno na double taxation wanayofanya rais na wapambe wake kina mwigulu.Nakatwa PAYE,nikienda tena kutoa pesa nakatwa tena.Ni mtu katili tu ndiye anaweza kuwatendea hivyo raia wake.
 
meseji hizo mbona za kawaida yeye anampamba kwenye hamna na mimi nimepata ya mwinyi raisi wa zanzibar na nimeona ya kawaida paschal tupo kwenye tozo meseji hizo haziwezi kumaliza kero kuhusiana na tozo zinazoendelea
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…